Kampuni ya kuzalisha vioo Tanzania yawasha mitambo, itatumia malighafi za Nchini kwa 80%

Kampuni ya kuzalisha vioo Tanzania yawasha mitambo, itatumia malighafi za Nchini kwa 80%

DodomaTZ

Member
Joined
May 20, 2022
Posts
84
Reaction score
118
photo_2024-08-19_21-34-50.jpg

Kampuni ya KEDA (T) Ceramics Co. Ltd imefanya uzinduzi wa awali wa kuwasha mitambo ya kiwanda hicho kilichopo Mkuranga Mkoani Pwani, leo Agosti 19, 2024.

Uzinduzi huo umefanywa na baadhi ya viongozi wa Kampuni pamoja wa Wafanyakazi wao wakiongozwa na Mkurugenzi wa Ceramics Co. Ltd, Wayne Zhong.

Akizungumza katika sherehe za uzinduzi huo, Wayne Chong amesema moja ya faida ya mradi huo ni kutoa ajira kwa Wazawa na kutumia malighafi nyingi kutoka Tanzania, akitoa mfano kwa kusema Watanzania wanaotarajiwa kuajiriwa kiwandani hapo ni zaidi ya 5000.
photo_2024-08-19_21-35-05.jpg
Wayne Zhong amesema uwashaji wa mitambo umefanyika kwa mara ya kwanza tangu walipoanza kuwekeza Mwaka 2017.

Sherehe hizo zimeendana na hatua mbalimbali za Kitamaduni zilizofanyika kabla ya kuanza kwa zoezi hilo ikiwemo kuwasha moto.

photo_2024-08-19_18-39-21.jpg

photo_2024-08-19_21-35-06.jpg
Amesema “Kutokana na uwekezaji huu tunatarajiwa kuwa na bidhaa ya Twyford Float Glass zenye ubora wa kiwango cha juu, pia tunatarajia kusambaza bidhaa zetu katika Nchi za Afrika Kusini, Kenya, Uganda, Zambia, Mashariki ya Kati na Barani Asia.

“Uwashaji huu wa mitambo utaendelea kwa majaribio na kumaanisha tupo tayari, hivyo, siku 25 zijazo tunatarajiwa kuzindua rasmi kuanza kwa kiwanda hiki.

“Tumefanikiwa pia kutokana na uwepo wa Rais Samia Suluhu Hassan na Serikali yake kwa kutupa ushirikiano, wamewezesha wawekezaji kuendelea kuja Tanzania kwa kuwa kuna fursa nyingi zinazopatikana.”

“Tunaamini tutatengeneza bidhaa bora na zitapatikana kwa bei rafiki kwa wanaohitaji.”

Upande wa Afisa Biashara na Mahusiano wa Twyford Tanzania, John Chimwejo amesema “Tunatarajia kufanya ufunguzi wa kiwanda rasmi na kioo cha kwanza kitazalishwa Septemba 2024.

“Pia malighafi nyingi ambazo tunazitegemea zinatokea hapahapa Tanzania, jambo ambalo ni fursa kwa Watanzania wenzetu kutumia nafasi hiyo kukuza biashara zao, kwani ni Asilimia 18 au 20 tu inayotoka nje.”
 
Back
Top Bottom