Kampuni ya OYA watoa milioni 1 kwa familia Juma Mfaume ambaye alifariki baada ya kupigwa na wafanyakazi wa kampuni hiyo

Kampuni ya OYA watoa milioni 1 kwa familia Juma Mfaume ambaye alifariki baada ya kupigwa na wafanyakazi wa kampuni hiyo

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Mwenyekiti wa Kitongoji cha Kaloleni kilichopo Kata ya Janga, Ahmed Kilindo amesema kampuni ya OYA Microcredit imetoa mchango wa shilingi milioni moja (Tsh.1,000,000/=) kwa familia ya Juma Said Mfaume ambaye alifariki baada ya kupigwa na wafanyakazi wa kampuni hiyo walioenda kudai sehemu ya mkopo waliomkopesha mke wa Juma.

Kilindo amesema kampuni hiyo imetoa fedha hizo kama sehemu ya pole kwa familia huku akieleza kuwa uongozi wa kampuni hiyo umesikitishwa na kitendo kilichofanywa na wafanyakazi wake kwani ni kinyume cha miiko na maadili ya kazi yao.

Soma Pia:
Kilindo ameeleza hayo wakati akitoa salamu za uongozi wa eneo hilo kwa familia ya Juma.

Aidha Juma amezikwa katika Makaburi ya Mtongani kwa Domo yaliyopo Mlandizi.
 
Wabadilishe mifumo ya kudai wasiende na silaha za jadi.

Mfanyakazi ukumbuke kuwa ukijifanya una uchungu sana na pesa za kampuni mpaka kudhuru au kuua basi mshahara wako unaofata utakuwa rambirambi au pesa ya matibabu huku ukipambana na kesi wewe na ndugu zako na mkurugenzi atakulaani kuwa umefanya kinyume na utaratibu wa kazi.
 
Kilindo amesema kampuni hiyo imetoa fedha hizo kama sehemu ya pole kwa familia huku akieleza kuwa uongozi wa kampuni hiyo umesikitishwa na kitendo kilichofanywa na wafanyakazi wake kwani ni kinyume cha miiko na maadili ya kazi yao.
Ila bado hadi kieleweke kwanini walichukua sheria mkononi
 
Mmeajiri watu mmewapa goals ambazo kuzifikia wanatakiwa watumie silaha na nguvu, wanafanya hivyo then wanaua alafu mnakuja kutoa rambirambi ambayo imepatikana kwa riba yenu kubwa. Mliowaajiri wanaozea jela nyie huku mko uraiani maisha yanaendelea na mnapiga riba kamakawa daah kwel ubepari nao Mavi kweli kweli.
 
Pesa ndogo sana hiyo.. Hawana hata aibu hao
Ndugu watafute njia iongezeke hat mke asiwaze mengi na deni lisamehewe walimlipie wao.
Wametoa tamko halafu
downloadfile-2.jpg
 
Back
Top Bottom