Kampuni ya Telecom ya China yatoa huduma bora yenye bei rahisi ya mtandao nchini Kenya

Kampuni ya Telecom ya China yatoa huduma bora yenye bei rahisi ya mtandao nchini Kenya

ldleo

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
1,116
Reaction score
1,121
中国电信.jpg
Kampuni ya Telecom ya China ni moja ya kampuni tatu kuu ya TEHEMA nchini China. Katika miaka ya hivi karibuni kampuni hiyo pia imeanzisha shughuli katika nchi mbalimbali barani Afrika, na kutoa hoduma bora yenye bei rahisi ya mtandao katika nchi hizo.

Kila Jumamosi alasiri, Levin Chama mwenye umri wa miaka 11 huja kwenye Kituo cha Mtandao cha Konnect Hub kilicho kwenye mtaa wa 44 ya Githurai wa mji mkuu wa Kenya, Nairobi, ili kusikiliza masomo ya lugha, utamaduni, hisabadi yanayotolea na walimu wa nchi mbalimbali kupitia mtandao wa Internet.

“Napenda masomo haya, ambayo ni tofauti na yale ya shuleni. Nimejifunza lugha mpya na kujua utamaduni wa nchi nyingine” Alipoulizwa anapenda kujua zaidi mambo ya nchi gani, Levin alijibu ni China. “Kwa sababu China ni nchi yenye teknolojia nyingi za juu, naweza kujifunza mambo mengi ya kisasa."

Kituo cha Konnect Hub ni jukwaa la elimu ya mtandao lililotolewa na tawi la Kampuni ya Telecom ya China nchini Kenya kwa kushirikiana na Wachina binafsi nchini humo kwa watu wa kipato cha chini na cha kati. Katika miaka ya hivi karibuni, sekta ya mtandao wa Internet imekua haraka sana barani Afrika, lakini kiwango cha matumizi bado kiko nyuma sana ikilinganishwa na kanda nyingine duniani, kutokana na gharama kubwa. Takwimu zinaonesha kuwa, ada ya mtandao mjini Nairobi ni shilingi 3,000 kwa mwezi. Wakati huo huo asilimia 80 ya familia mjini humo zina kipato kati ya 20,000 na 50,000 tu.

Ili kusaidia watu wenye kipato cha chini na cha kati kuweza kutumia mtandao, tawi la kampuni ya Telecom ya China nchini Kenya kwa kushirikiana na Wachina binafsi walianzisha kampuni ya teknolojia ya mtandao ya Ahadi Wireless Limited, ambayo inatoa huduma ya mtandao ya bei nafuu ya shilingi 20 kwa saa, shilingi 70 kwa siku, shilingi 350 kwa wiki hadi shilingi 1,000 kwa mwezi, na kasi ya mtandao ni megabytes 8 kwa sekunde. Licha ya hayo, kampuni hoyo pia imeanzisha Vituo vya Konnect Hub, ambavyo vinatoa huduma bure ya masomo mtandaoni kwa watoto kati ya miaka 5 hadi 15. Hadi sasa, kampuni hiyo ina watumiaji 65,000 wa kusajiliwa.

Kufanikiwa kwa kampuni hiyo ni mfano mmoja tu wa ushirikiano kati ya China na nchi za Afrika katika maendeleo ya shughuli za mtandao. Katika miaka ya hivi karibuni, kutokana na Baraza la Ushirikiano kati ya China na Afrika FOCAC na pendekezo la “Ukanda Mmoja, Njia Moja”, China imechangia sana ujenzi wa “Afrika ya Kidijitali”, na kuzisaidia nchi za bara hilo kutumia mtandao kama njia ya kukabiliana na changamoto, zikiwemo kuimarisha juhudi za kupambana na janga la COVID-19, kutoa mafunzo mtandaoni, na mawasiliano ya jamii mbalimbali.
 
Wewe jamaa utakuwa mchina mwanachama WA CPC si Kwa kuisifia China Huko.
 
Wamelilenga kundi ambalo ni very fragile. Hili kundi ndiyo hasa linaloamua hatima ya kizazi kijacho. Ukishafanikiwa to brainwash this group, unakuwa umejihakikishia full dominance of the future of any nation.
Pole nyingi wa Waafrika wenzangu, maana huko watoto hawatajifunza lolote kuhusu nchi yao na tamaduni zao
vinatoa huduma bure ya masomo mtandaoni kwa watoto kati ya miaka 5 hadi 15.
 
Wamelilenga kundi ambalo ni very fragile. Hili kundi ndiyo hasa linaloamua hatima ya kizazi kijacho. Ukishafanikiwa to brainwash this group, unakuwa umejihakikishia full dominance of the future of any nation.
Pole nyingi wa Waafrika wenzangu, maana huko watoto hawatajifunza lolote kuhusu nchi yao na tamaduni zao
Waache wajifunze ya Uchina maana nafuu ya huko china kuliko tuna shuhudia sasa vijana wengi wakikimbilia Dubai na huko Dubai wana Dubaiwa mpaka watu maarufu kwenye industry ya Mziki.

So China kwa Jicho la pekee wamelibeba bara la Africa kwa kiasi kikubwaaa.
Acha tuu watoto wetu wajifunze tamaduni zao huwenda wakajua na Tech

Sent from my SM-A125F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom