Zanzibar 2020 Kamwe Joni hawezi Kusafiri na Hussein kwenda nae Zanzibar, ila atasafiri na Makame ambaye si tu amemzoea bali pia anammudu sana

Zanzibar 2020 Kamwe Joni hawezi Kusafiri na Hussein kwenda nae Zanzibar, ila atasafiri na Makame ambaye si tu amemzoea bali pia anammudu sana

Mzukulu

JF-Expert Member
Joined
Feb 14, 2020
Posts
1,401
Reaction score
2,641
Kuna Mzee Mmoja ( Jina Kapuni ) japo alishawahi Kuniongoza Kikatiba huko nyuma taratibu sasa naanza kuona jinsi ambavyo huenda Ugonjwa wa Moyo utakavyoanza Kumuathiri na pengine hata Israeli anaweza Kuamua Kuondoka nae mapema tu kwenda katika Mapumziko yake ya Milele.

Sababu kubwa ni kwamba kama kuna Mzee ambaye si tu alikuwa anajikomba bali bado pia anajikomba kwa Joni huku akijiaminisha kabisa kuwa iwe isiwe Mwanae Mpendwa aliyeyazoea Maisha ya kuishi na Wanajeshi kwa miaka mingi atakuja nae Kuirithi Kazi yake huko kwa Waunguja na Wapemba ila kwa upepo unavyoenda sasa Mwanae huyo hiyo Kazi ataisikia tu katika Bomba.

Si tu kwamba Joni hataki Kuongozana na Hussein katika Safari yake ya kwenda Kisiwani Zanzibar ila anaogopa kuwa huenda huko mbeleni akaja Kumsumbua hasa ukizingatia Hussein kaanza kuwa katika Mfumo kabla yake na ana Mtandao mkubwa ulioratibiwa vyema na Baba yake alipokuwa Kazini hivyo anaona bora tu asafiri na Makame ambaye amemzoea na anammudu vilivyo kabisa.

Na kinachosikitisha na hata kutia Huruma kabisa ni kuwa tayari Hussein alishaanza Kuuvaa uhusika wa hiyo Kazi anayoenda Kuikosa na Kuijutia.
 
Kuna Mzee Mmoja ( Jina Kapuni ) japo alishawahi Kuniongoza Kikatiba huko nyuma taratibu sasa naanza kuona jinsi ambavyo huenda Ugonjwa wa Moyo utakavyoanza Kumuathiri na pengine hata Israeli anaweza Kuamua Kuondoka nae mapema tu kwenda katika Mapumziko yake ya Milele.

Sababu kubwa ni kwamba kama kuna Mzee ambaye si tu alikuwa anajikomba bali bado pia anajikomba kwa Joni huku akijiaminisha kabisa kuwa iwe isiwe Mwanae Mpendwa aliyeyazoea Maisha ya kuishi na Wanajeshi kwa miaka mingi atakuja nae Kuirithi Kazi yake huko kwa Waunguja na Wapemba ila kwa upepo unavyoenda sasa Mwanae huyo hiyo Kazi ataisikia tu katika Bomba.

Si tu kwamba Joni hataki Kuongozana na Hussein katika Safari yake ya kwenda Kisiwani Zanzibar ila anaogopa kuwa huenda huko mbeleni akaja Kumsumbua hasa ukizingatia Hussein kaanza kuwa katika Mfumo kabla yake na ana Mtandao mkubwa ulioratibiwa vyema na Baba yake alipokuwa Kazini hivyo anaona bora tu asafiri na Makame ambaye amemzoea na anammudu vilivyo kabisa.

Na kinachosikitisha na hata kutia Huruma kabisa ni kuwa tayari Hussein alishaanza Kuuvaa uhusika wa hiyo Kazi anayoenda Kuikosa na Kuijutia.
Wewe jidanganye kwa kudhani usiyoyajua. Hiyo ya Hoseni ilishakuwa muda mrefu toka enzi na enzi. Yako macho yaache kodo, ukishindwa basi masikio yako weka waz
 
Dr. John Pombe Magufuli
Hussein Mwinyi
Makame Mbarawa
halafu utamu zaidi hawa wote hawajawahi kuhudumu kabisa kwa ukamilifu katika SMZ

Huyu Makame ndo hata jimbo alishindwa kulipata kule kwao ni Ngangari tupu. Labda akaanzie na uwakilishi kwanza

ila siasa za mwaka 2020 zitakua na mengi mapya kama tuliyoyashuhudia yakitokea miaka hii 5 yote. Yale yasiyowezekana yamewezeshwa kuwezekana. Tunapata new "NORMALS"
 
Joni hataki Kuongozana na Hussein katika Safari yake ya kwenda Kisiwani Zanzibar ila anaogopa kuwa huenda akaja Kumsumbua hasa ukizingatia Hussein kaanza kuwa katika Mfumo kabla yake na ana Mtandao mkubwa hivyo anaona bora tu asafiri na Makame ambaye amemzoea na anammudu vilivyo kabisa.
Duh...!.
Hoja za bandiko hili ni hoja za uongo mkubwa na za kubaini!.
1. Joni sio mtu muoga na asiejiamini kama unavyomuelezea hapa kumuonyeshea ni mtu muoga, hana confidence na anasumbuliwa na tatizo la insecurity ya kuogopa watu kitu ambacho sii kweli!.
2. Hussein hana mtandao wowote, ni mtu simple, humble and down to earth, anasimama mwenyewe with his own merits, hategemei mbeleko ya yeyote!
3. Kitu pekee ulichopatia kwenye bandiko hili ni Makame kwa sababu ni presidential material kama nilivyo muelezea hapa
Prof. Mbarawa ni Presidential material! Tuwaspot na kuwagroom Presidential materials au tumwache tu yeyote awe?
P
 
halafu utamu zaidi hawa wote hawajawahi kuhudumu kabisa kwa ukamilifu katika SMZ

Huyu Makame ndo hata jimbo alishindwa kulipata kule kwao ni Ngangari tupu. Labda akaanzie na uwakilishi kwanza

ila siasa za mwaka 2020 zitakua na mengi mapya kama tuliyoyashuhudia yakitokea miaka hii 5 yote. Yale yasiyowezekana yamewezeshwa kuwezekana. Tunapata new "NORMALS"
Kwani aliyepo alishawahi kuwa wa jumbo lipi?

Tukumbushane basii?
 
Back
Top Bottom