Kamwe Mfugaji hawezi kuishi pamoja na Mkulima. Maisha hayawaruhusu

Kamwe Mfugaji hawezi kuishi pamoja na Mkulima. Maisha hayawaruhusu

G-Mdadisi

Senior Member
Joined
Feb 15, 2018
Posts
165
Reaction score
100

✍#GMdadisi
Sijui ni lini WAFUGAJI na WAKULIMA watakuja kuelewana na waishi pamoja bila kuwa na migogoro wala chuki. Nadhani hii yaweza kuwa ni ndoto nzuri ambayo haitakuja kushudiwa katika kizazi hiki.

Bahati mbaya sana ukimsikiliza mfugaji analalamika kuonewa na mkulima. Vivo hivyo mkulima analalamika kuonewa na mfugaji. Kiufupi kila mmoja anajiona mwenye haki mbele ya mwenzake.

Yaaan popote alipo mkulima, mfugaji hawezi kuishi kwa amani. Na alipo mfugaji mkulima ataishi kwa wasiwasi tu siku zote labda akishavuna.🤭

Kuna haja hawa watu wawekewe mazingira ya kutoingiliana kwani kila mmoja anatafta kukidhi malengo yake ambayo kukaa karibu karibu haiwezekani.

Mkulima anathamini zaidi mazao yake na kuona mifugo si lolote kwenye maisha, huku mfugaji akiamini katika mifugo yake na kumuona mkulima ni mpotezaji tu wakati wote na hata thamani yoyote mbele ya mifugo yake.

Mkulima wa kule Kasato, Ruganzu, Ntungamo, Runazi na hata Katunguru mawazo yake ni sawa sawa na mkulimà wa Kinowe,Micheweni, na mfugaji wa Micheweni ana mawazo sawa na mfugaji wa Rukoke, Nyakahura..nk.

Hivyo ili kuepusha migogoro kama hii, ni muhimu wafugaji wachangamane na wafugaji wenzao, huku wakulima pia wakae na wakulima wenzao.

Vinginevyo hata wale wamasai waliopelekwa kule MSOMERA, Tanga kama wataingiliana na wakulima tutakuwa tumeongeza idadi ya migogoro ambayo hata kama si leo basi kesho au keshokutwa utaibuka tu.
 
Wamasai nux anapitisha vifugo kwenye shamba lako anakimbilia police kuoga
 
Ungeleta taarifa tu, hata ufanyaje dunia hii yoteee. Wakulima hawakai meza moja na wafugaji na haiwezekani maaana wote wanamatumizi ya ardhi
 
KIlimo na ufugaji vyote ni duni lazima pawe na migogoro.. Haswa ufugaji wa kuchunga wanyama ni hatari sana
 
Mafuta na maji haitokaa itokee ikachanganyikana
 
Unajua kwa nini kanda ya ziwa hamna migogoro ya wakulima na wafugaji?
 
View attachment 2964183
✍#GMdadisi
Sijui ni lini WAFUGAJI na WAKULIMA watakuja kuelewana na waishi pamoja bila kuwa na migogoro wala chuki. Nadhani hii yaweza kuwa ni ndoto nzuri ambayo haitakuja kushudiwa katika kizazi hiki.

Bahati mbaya sana ukimsikiliza mfugaji analalamika kuonewa na mkulima. Vivo hivyo mkulima analalamika kuonewa na mfugaji. Kiufupi kila mmoja anajiona mwenye haki mbele ya mwenzake.

Yaaan popote alipo mkulima, mfugaji hawezi kuishi kwa amani. Na alipo mfugaji mkulima ataishi kwa wasiwasi tu siku zote labda akishavuna.🤭

Kuna haja hawa watu wawekewe mazingira ya kutoingiliana kwani kila mmoja anatafta kukidhi malengo yake ambayo kukaa karibu karibu haiwezekani.

Mkulima anathamini zaidi mazao yake na kuona mifugo si lolote kwenye maisha, huku mfugaji akiamini katika mifugo yake na kumuona mkulima ni mpotezaji tu wakati wote na hata thamani yoyote mbele ya mifugo yake.

Mkulima wa kule Kasato, Ruganzu, Ntungamo, Runazi na hata Katunguru mawazo yake ni sawa sawa na mkulimà wa Kinowe,Micheweni, na mfugaji wa Micheweni ana mawazo sawa na mfugaji wa Rukoke, Nyakahura..nk.

Hivyo ili kuepusha migogoro kama hii, ni muhimu wafugaji wachangamane na wafugaji wenzao, huku wakulima pia wakae na wakulima wenzao.

Vinginevyo hata wale wamasai waliopelekwa kule MSOMERA, Tanga kama wataingiliana na wakulima tutakuwa tumeongeza idadi ya migogoro ambayo hata kama si leo basi kesho au keshokutwa utaibuka tu.
Umeongea Kweli kbs,

Hayo yangewezekana ikiwa wanyama wangekuwa na akili ya kutofautisha mazao ya mkulima, na majani Yao ya asili Kwa chakula.
 
Back
Top Bottom