Kamwe usiolewe na mwanaume asiyeweza kukulipia mahari

Kiranga jamani.
Mahari ni utamaduni unaomba ridhaa kwa wakwe zako kuwa unaoa na utamtunza mke na watoto wote watakaopatikana kwenye nyumba yenu.

Kamwe mahari haiwezi kumfanya mwanamke awe bidhaa
Sijakataa kwamba ni utamaduni.

Kuwa utamaduni hakuondoi ukweli kwamba ni utamaduni unaomfanya mwanamke kuwa bidhaa.

Na kuna watu wakiona bidhaa haifai, wakimpa mwanamke talaka, wanadai sehemu ya mahari waliyolipa.

Huko Africa hususan, kitu kuwa utamaduni haimaanishi ni kizuri.

Kuna sehemu nyingi bado wanawake wanakatwa visimi kwa minajili ya utamaduni. Huu ni utamaduni, lakini si mzuri.

Ukisoma tamaduni za Africa, kihistoria, mwanamke na mtoto ni kama mali za mwanamme tu.

Na ndiyo maana machifu walikuwa na wake wengi, watoto wengi. Ni alama ya utajiri.

Na kwa kuwa mwanamke ni bidhaa kwa tamaduni hizi, basi anawekewa bei rasmi.

Na bei hiyo inaitwa mahari.

Jamii yenye mahari haiwezi kuwa na usawa wa watu.

Anayelipa mahari, ceteris paribus, atajiona yuko juu kwenye ndoa.

Ukikubali mahari na kusema mwanamke ni mtumwa wa mwanamme, sina tatizo nawe.

Ukikubali mahari na kusema mwanamke ni sawa na mwanamme kiutu, hapo naona kuna uongo.

Kwa sababu kama mahari ni utamaduni wa zawadi tu, kwa nini familia ya mwanamme haipewi zawadi ikawa mwanamme anatoa mahari kwa mwanamke na mwanamke anatoa mahari kwa mwanamme? Mahari iwe exchange of gifts tu?

After all, reciprocity is the height of diplomacy and love.

Mahari ni bei ya kununua mke.

Inawezekana ni kitu muhimu katika jamii masikini, kuzuia watu masikini wasioweza ku maintain family kuoa.

Lakini, kwenye jamii zilizovuka mto huo, boti hilo halihitajiki.

Ndiyo maana jamii zilizoendelea kielimu na kiuchumi zimeondokana na utamaduni huu.

Lakini labda huko Africa tunauhitaji bado.

Hayo yote hayabadilishi ukweli kwamba mahari ni bei ya kununua mke kama bidhaa.
 
Kiranga jamani.
Mahari ni utamaduni unaomba ridhaa kwa wakwe zako kuwa unaoa na utamtunza mke na watoto wote watakaopatikana kwenye nyumba yenu.

Kamwe mahari haiwezi kumfanya mwanamke awe bidhaa
Bidhaa ni nini na ina sifa gani?
 
Hakuna pesa inayoweza mnunua mwanadamu
 
Definition ya mahari katika jamii zetu siyo hiyo uliyoiweka wewe hapo
Unaweza kuyaita mavi jina lolote.

Lakini, ukiyaita mavi maua, hiyo definition yako haitayabadilisha mavi.

I don't care how you define mahari.

It is called "brideprice" for a reason.
 
Unaweza kuyaita mavi jina lolote.

Lakini, ukiyaita mavi maua, hiyo definition yako haitayabadilisha mavi.

I don't care how you define mahari.

It is called "brideprice" for a reason.
Mahari ni akhsante kwa wazazi kwa kumlea binti.
 
Lakini mahari inanunua mke. Kwa sababu katika tamaduni zenye mahari hii, mwanamke si mwanadamu, ni bidhaa.
Hivi utamlinganishaje mwanamke na bidhaa??
Ng'ombe na mwanamke wapo sawa??
 
Kwa nini akhsante itolewe kwa wazazi wa binti tu?

Wazazi wa mume hawastahili akhsante kutoka upande wa binti kwa kumlea mume?
Kwa sababu binti anaenda kukuza ukoo wa mume.
Na Ndiyo maana kuna mwanaume na mwanamke[emoji4]
 
Kwa sababu binti anaenda kukuza ukoo wa mume.
Na Ndiyo maana kuna mwanaume na mwanamke[emoji4]
Kwa nini binti aende kukuza ukoo wa mume wakati watoto wanapatikana kwa kushirikiana wote?

Jibu lako linaonesha kwamba mwanamke si tu ni bidhaa.

Jibu linaonesha mwanamke ni bidhaa inayotumika kuzidisha ukoo wa mwanamme.

Kwa nini mwanamke azidishe ukoo wa mwanamme na si ukoo wake mwanamke?

Mpaka hapo jibu lako linakubaliana na hoja yangu kwamba mwanamke ni bidhaa ya mwanamme tu katika tamaduni hizi zinazotoa mahari.

Ndiyo maana anaolewa, haoi.

Ndiyo maana anabadili jina na kuchukua juna la ukoo wa mwanamme.

Ndiyo maana watoto anaozaa wanakuwa rasmi katika ubini wa ukoo wa mwanamme.

Jibu lako halikanushi hoja yangu.

Jibu lako linaiongezea nguvu hoja yangu.
 
Wewe unaona wapo sawa?
Suala si mimi.

Suala ni mwanamke mwenyewe.

Mwanamke anayekubali mahari, amejifanya kuwa sawa na bidhaa nyingine yoyote.

Whether mimi naona hivyo au sioni hivyo is immaterial.
 
Suala si mimi.

Suala ni mwanamke mwenyewe.

Mwanamke anayekubali mahari, amejifanya kuwa sawa na bidhaa nyingine yoyote.

Whether mimi naona hivyo au sioni hivyo is immaterial.
Mimi nimekuuliza wewe,je!um unaona wapo sawa??

Mkuu mahari lazima itolewe na bila mahari hatuolewi,na ni utamaduni utakaoendelea kuwepo.

Huo usasa usikufanye udharau tamaduni zetu
 
Hiyo ni asili inataka hivyo
Na tangu kuumbwa kwa ulimwengu ..wote tumechukua ubin wa Adam..bin_adamu

Hiyo ya bidhaa sijui hata umeitoa wapi.
Hata ukisoma kwenye Biblia utakuta mahari imeongelewa.
 
Mimi nimekuuliza wewe,je!um unaona wapo sawa??

Mkuu mahari lazima itolewe na bila mahari hatuolewi,na ni utamaduni utakaoendelea kuwepo.

Huo usasa usikufanye udharau tamaduni zetu
Mimi naamini katika haki za binadamu, mtu akijiweka kuwa bidhaa, hiyo pia ni haki yake.

Hujakatazwa kujifanya bidhaa yenye bei.

Ni haki yako.

Lakini, hilo haliondoi ukweli kwamba umejifanya bidhaa yenye bei.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…