Pre GE2025 Kanali Mtambi aonya Siasa za Majitaka Mara, TAKUKURU yakazia kupambana na Rushwa

Pre GE2025 Kanali Mtambi aonya Siasa za Majitaka Mara, TAKUKURU yakazia kupambana na Rushwa

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Mkuu wa Mkoa wa Mara, Kanali Evans Mtambi, ametoa wito kwa viongozi na wanasiasa wa mkoa huo kufanya siasa za kistaarabu badala ya siasa za chuki na zinazogawa wananchi akisema hazitavumiliwa mkoani humo.

Kanali Mtambi ametoa agizo hilo alipokuwa akizungumza na viongozi wa vyama vya siasa mkoani Mara katika kikao kilichoandaliwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru). Lengo la kikao hicho lilikuwa kuwaelimisha viongozi hao kuhusu umuhimu wa kujiepusha na vitendo vya rushwa kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu ujao.
IMG_0682.jpeg

Kanali Mtambi amesema baadhi ya viongozi wamekosa sera za maana za kunadi kwa wananchi, na badala yake wamejikita katika "siasa za majitaka" zinazochochea chuki, fitina, ukabila, na kugawa wananchi.
IMG_0679.jpeg

Amehimiza vyama kufuata kanuni na taratibu zilizopo ambazo zinaelekeza namna ya kushughulikia malalamiko yoyote yanayotokea wakati wa uchaguzi.
IMG_0681.jpeg

Amewataka wananchi kutokubali kudanganywa na siasa za namna hiyo, kwani zinaweza kuwanyima fursa ya kupata viongozi wenye sifa na uwezo.

Pia, Soma: MARA: Matukio yanayojiri kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Novemba 27, 2024

Kwa upande wake, Mkuu wa Takukuru wa Mkoa wa Mara, Mohammed Sharif, amewasihi viongozi wa kisiasa kuimarisha mikakati ya kutokomeza vitendo vya rushwa ndani ya vyama vyao. Pia amewataka kutoa elimu kwa wafuasi wao kuhusu kujiepusha na vitendo vya rushwa.

Sharif amesema taasisi hiyo imejipanga kikamilifu kudhibiti mianya yote ya rushwa katika kipindi chote cha uchaguzi.

Soma:

Kahama: TAKUKURU waonya Chawa wanaotumika kugawa fedha na zawadi ili wagombea wao wachaguliwe
TAKUKURU hawana meno kwenye rushwa ya uchaguzi wa ndani CCM?
 
Mkuu wa Mkoa wa Mara, Kanali Evans Mtambi, ametoa wito kwa viongozi na wanasiasa wa mkoa huo kufanya siasa za kistaarabu badala ya siasa za chuki na zinazogawa wananchi akisema hazitavumiliwa mkoani humo.

Kanali Mtambi ametoa agizo hilo alipokuwa akizungumza na viongozi wa vyama vya siasa mkoani Mara katika kikao kilichoandaliwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru). Lengo la kikao hicho lilikuwa kuwaelimisha viongozi hao kuhusu umuhimu wa kujiepusha na vitendo vya rushwa kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu ujao.
View attachment 3150856
Kanali Mtambi amesema baadhi ya viongozi wamekosa sera za maana za kunadi kwa wananchi, na badala yake wamejikita katika "siasa za majitaka" zinazochochea chuki, fitina, ukabila, na kugawa wananchi.
View attachment 3150857
Amehimiza vyama kufuata kanuni na taratibu zilizopo ambazo zinaelekeza namna ya kushughulikia malalamiko yoyote yanayotokea wakati wa uchaguzi.
View attachment 3150858
Amewataka wananchi kutokubali kudanganywa na siasa za namna hiyo, kwani zinaweza kuwanyima fursa ya kupata viongozi wenye sifa na uwezo.

Pia, Soma: MARA: Matukio yanayojiri kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Novemba 27, 2024

Kwa upande wake, Mkuu wa Takukuru wa Mkoa wa Mara, Mohammed Sharif, amewasihi viongozi wa kisiasa kuimarisha mikakati ya kutokomeza vitendo vya rushwa ndani ya vyama vyao. Pia amewataka kutoa elimu kwa wafuasi wao kuhusu kujiepusha na vitendo vya rushwa.

Sharif amesema taasisi hiyo imejipanga kikamilifu kudhibiti mianya yote ya rushwa katika kipindi chote cha uchaguzi.

Soma:

Kahama: TAKUKURU waonya Chawa wanaotumika kugawa fedha na zawadi ili wagombea wao wachaguliwe
TAKUKURU hawana meno kwenye rushwa ya uchaguzi wa ndani CCM?

..mbona kama washiriki hawafuatilii kikao, na wengine wamechoka, na kusinzia?
 
Back
Top Bottom