Mwamuzi wa Tanzania
JF-Expert Member
- Apr 7, 2020
- 15,486
- 45,256
Tukichukulia tukio moja tu la moto uliotikisa au unaotikisa hifadhi ya Mlima Kilimanjaro tunapata jibu moja kwa moja kuwa ni vyema Jeshi la Zimamoto na Uokoaji likawa na magari na ndege za kisasa za kuzimia moto.
Tanzania tuna hifadhi nyingi, hivyo lolote linaweza kutokea kwenye hizi hifadhi zetu, helicopter za kuzimia moto na kuokoa watu wakati wa majanga ni jambo lisilokwepeka.
Mafuriko yaliyoichapa Tanzania na Afrika Mashariki mwaka jana kuna watu Kilwa walikufa kizembe. Kama tungekuwa na helicopter za uokoaji wasingekufa baadhi ya watu.
Kuna siku nilimsikia Rais akipondea ile tenda ya Lugola na Andengenya, akisema helicopter hazina kazi kwenye uzimaji moto, ikumbukwe kuwa kesho hili kazi yake si tu kuzima moto. Anayetaka kuamini aende YouTube atafute hotuba ya uuzinduzi wa Nyumba za Magereza Ukonga.
Kama kulikuwa na mistake au harufu ya ufisadi tenda ingeendelea na washukiwa wangefikishwa mahali sahihi na si kusitisha tenda ya vifaa muhimu vya kuzimia moto na uokoaji.
Tanzania tuna hifadhi nyingi, hivyo lolote linaweza kutokea kwenye hizi hifadhi zetu, helicopter za kuzimia moto na kuokoa watu wakati wa majanga ni jambo lisilokwepeka.
Mafuriko yaliyoichapa Tanzania na Afrika Mashariki mwaka jana kuna watu Kilwa walikufa kizembe. Kama tungekuwa na helicopter za uokoaji wasingekufa baadhi ya watu.
Kuna siku nilimsikia Rais akipondea ile tenda ya Lugola na Andengenya, akisema helicopter hazina kazi kwenye uzimaji moto, ikumbukwe kuwa kesho hili kazi yake si tu kuzima moto. Anayetaka kuamini aende YouTube atafute hotuba ya uuzinduzi wa Nyumba za Magereza Ukonga.
Kama kulikuwa na mistake au harufu ya ufisadi tenda ingeendelea na washukiwa wangefikishwa mahali sahihi na si kusitisha tenda ya vifaa muhimu vya kuzimia moto na uokoaji.