Waziri mpya na machachari wa mambo ya ndani wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kangi Lugola ametoa maoni yake kuhusiana na wasanii wanaofanya vizuri nchini Diamond na Alikiba.
Katika mahojiano hayo Mh Lugola alipoulizwa kuhusu Ali Kiba na Diamond alisema yeye hawakubali wote wawili bali anawakubali Beka na Aslay. Lakini pamoja na hayo hakusita kutoa maoni yake kuhusu Alikiba na Diamond ambapo amesema Diamond hana nidhamu katika muziki tofauti na Alikiba kwa kuwa Diamond analalamikiwa kuchelewa majukwaani.