Kaniambia nisome Zaburi 109. Naomba mnisaidie kunifafanulia

Kaniambia nisome Zaburi 109. Naomba mnisaidie kunifafanulia

Kavunja ahadi waliyokubaliana ndo mana kammaindi kwann amsimulie dada ake sjui mama ake kama ameathirika
Kweli naweza kukiri nilikosea lakini kabla sijamwambia dada yake yy alinambia kwamba kamwambia dadake matokeo ya vipimo!
Kwa mshutuko ule nahisi alikuwa hajawaweka wazi ndugu zake! Mama wa watu alikuwa anahaha vibaya sana kwenye simu nimweleze kimetokea nn mbona hali ya ndugu yao si hali anashindwa hata kulala amenunuliwa hadi Dawa za usingizi lakini halali kweli ilibidi niseme ukweli wa tatizo! Basi nitamtafuta tena huyo mama niongee nae tena
 
Zaburi 109 ni sala ya kisasi kwa maadui .
Basi kama ni mabalaa yake apambane nayo maana mm sihusiki na kuathirika kwake ila hali niliyoiona baada ya majibu kutoka asikwambie mtu ilihitaji uvumilivu wa hali ya juu na sikuai
 
Achana naye na Zaburi zake
Nimemtafuta na kuongea nae nae amekiri kunikosea alimaanisha Zaburi 119 na sio 109! Sijui kama alimaanisha hivyo kwa sababu tulivyokuwa karibu kimawasilianosiyo kwa sasa
 
zaburi 109
1Ee Mungu, ambaye ninakusifu,
usiwe kimya,

2kwa maana watu waovu na wadanganyifu
wamefungua vinywa vyao dhidi yangu;
wasema dhidi yangu
kwa ndimi za udanganyifu.

3Wamenizunguka kwa maneno ya chuki,
wananishambulia bila sababu.

4Wanachonilipa badala ya urafiki wangu ni kunishtaki,


huyo msichana ameshapewa taarifa na huyo mama/dada kama wewe uliwapa umbea kuhusu afya yake, kwasababu hiyo amekukasirikia kwa style ya zaburi 109

mkuu endelea kumfariji sana huyo msichana bado yupo kwenye grieving stage anaitaji ukaribu na urafiki asiwaze mabaya juu yake
 
Duhh...

Huyu Manzi anaweza jichomoa uhai. Au kuuwa kabisa.

Jiweke mbali.
 
zaburi 109
1Ee Mungu, ambaye ninakusifu,
usiwe kimya,

2kwa maana watu waovu na wadanganyifu
wamefungua vinywa vyao dhidi yangu;
wasema dhidi yangu
kwa ndimi za udanganyifu.

3Wamenizunguka kwa maneno ya chuki,
wananishambulia bila sababu.

4Wanachonilipa badala ya urafiki wangu ni kunishtaki,


huyo msichana ameshapewa taarifa na huyo mama/dada kama wewe uliwapa umbea kuhusu afya yake, kwasababu hiyo amekukasirikia kwa style ya zaburi 109

mkuu endelea kumfariji sana huyo msichana bado yupo kwenye grieving stage anaitaji ukaribu na urafiki asiwaze mabaya juu yake
Hiyo mistari niliisoma mpaka nikpaniki ndo maana nikaja hapa kuomba ushauri nafikiri amaechukia kweli maana ilikuwa haipiti siku tusiwasiliane Leo sijamtafuta na hajanitafuta mpaka muda huu!
 
Hufai kupewa siri.

Mambo hizo huwezi mwambia mtu bila ridhaa ya muhusika.....hata akifa, unakaa nalo tu. Kwani ungesema hujui chochote ungepungua mini?
 
Hufai kupewa siri.

Mambo hizo huwezi mwambia mtu bila ridhaa ya muhusika.....hata akifa, unakaa nalo tu. Kwani ungesema hujui chochote ungepungua mini?
Mhusika alishasema kwamba kamwambia huyo ndugu yake! Huyo dadake nadhani alikuwa anathibitisha tu maana Kuna vitu aliniuliza nikajua ana taarifa ila huyu mgonjwa nadhani hakujua kabisa kama mm na dadake tulikuwa na mawasiliano!
 
1Ee Mungu, ambaye ninakusifu,

usiwe kimya,

2kwa maana watu waovu na wadanganyifu

wamefungua vinywa vyao dhidi yangu;

wasema dhidi yangu

kwa ndimi za udanganyifu.

3Wamenizunguka kwa maneno ya chuki,

wananishambulia bila sababu.

4Wanachonilipa badala ya urafiki wangu ni kunishtaki,

lakini mimi ninawaombea.

5Wananilipiza mabaya kwa mema,

chuki badala ya urafiki wangu.



6Agiza mtu mwovu ampinge,

mshtaki asimame mkono wake wa kuume.

7Anapohukumiwa, apatikane na hatia,

nayo maombi yake yamhukumu.

8Siku zake za kuishi na ziwe chache,

nafasi yake ya uongozi ichukuliwe na mtu mwingine.

9Watoto wake na waachwe yatima,

mke wake na awe mjane.

10Watoto wake na watangetange wakiomba,

na wafukuzwe kwenye magofu ya nyumba zao.

11Mtu anayemdai na ateke vyote alivyo navyo,

matunda ya kazi yake yatekwe nyara na wageni.

12Asiwepo mtu yeyote wa kumtendea mema

wala wa kuwahurumia yatima wake.

13Uzao wake na ukatiliwe mbali,

majina yao yafutike katika kizazi kifuatacho.

14Maovu ya baba zake na yakumbukwe

mbele za Bwana,

dhambi ya mama yake

isifutwe kamwe.

15Dhambi zao na zibaki daima mbele za Bwana,

ili apate kukatilia mbali kumbukumbu lao duniani.



16Kwa maana kamwe hakuweza kutenda wema,

bali alimfukuza mnyonge na mhitaji,

aliwafanyia jeuri wahitaji na waliovunjika moyo.

17Alipenda kulaani,

nayo laana ikampata;

hakupenda kubariki,

kwa hiyo baraka na ikae mbali naye.

18Alivaa kulaani kama vazi lake,

nayo laana ikamwingia mwilini mwake kama maji,

kwenye mifupa yake kama mafuta.

19Na iwe kama joho alilozungushiwa,

kama mshipi aliofungiwa daima.

20Haya na yawe malipo ya Bwana kwa washtaki wangu,

kwa wale wanaoninenea mabaya.



21Lakini wewe, Ee Bwana Mwenyezi,

unitendee wema kwa ajili ya jina lako,

uniokoe kwa wema wa pendo lako.

22Maana mimi ni maskini na mhitaji,

moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.

23Ninafifia kama kivuli cha jioni,

nimerushwa-rushwa kama nzige.

24Magoti yangu yamelegea kwa kufunga,

mwili wangu umedhoofika na kukonda.

25Nimekuwa kitu cha kudharauliwa kwa washtaki wangu,

wanionapo, hutikisa vichwa vyao.



26Ee Bwana, Mungu wangu nisaidie,

niokoe sawasawa na upendo wako.

27Watu na wafahamu kuwa ni mkono wako,

kwamba wewe, Ee Bwana, umetenda hili.

28Wanaweza kulaani, lakini wewe utabariki,

watakaposhambulia wataaibishwa,

lakini mtumishi wako atashangilia.

29Washtaki wangu watavikwa fedheha,

na kufunikwa na aibu kama joho.



30Kwa kinywa changu nitamtukuza sana Bwana,

katika umati mkubwa nitamsifu.

31Kwa maana husimama mkono wa kuume wa mhitaji,

kuokoa maisha yake kutoka kwa wale wanaomhukumu.
 
Basi kama ni mabalaa yake apambane nayo maana mm sihusiki na kuathirika kwake ila hali niliyoiona baada ya majibu kutoka asikwambie mtu ilihitaji uvumilivu wa hali ya juu na sikuai
Aisee pole
 
Back
Top Bottom