Kansa ya matiti inammaliza mke wangu nikiwa nashuhudia, sina la kufanya. Sijui kama naweza kusahau hili

Kansa ya matiti inammaliza mke wangu nikiwa nashuhudia, sina la kufanya. Sijui kama naweza kusahau hili

Aisee mkuu pole,,familia yetu tumewahi oata wagonjwa wawili wa saratani ya shingo ya kizazi. Wa kwanza ni dada yangu ila alifariki na wa pili akawa mtoto wake ajabu dogo alipata saratani akiwa darasa la 7 kwakweli kuuguza mgonjwa wa saratani ni gharama mno ila Mungu amejaalia yule dogo amepon na anaendelea na masomo yake.

M/Mungu akutie nguvu katika nyakati hizi ngumu.
Wewe ni muongo.

Ukipata saratani ya kizazi/uke hakuna matibabu. Huwezi kupona. Lazima ufe.
 
Pole, lakini lazima NIKUAMBIE UKWELII.

Hiyo unayoiita TIBA MBADALA ndio TIBA HALISI, Mimea ya asili yenye nguvu ya kukuponya na kuhuisha mwili dhidi ya maradhi ya aina yoyote.

Hayo MAKEMIKALI ndio yalipaswa kuwa TIBA MBADALA. Ukishafeli kutumia MIMEA SAFI (kitu ambacho hakiwezekani) sasa ndio ukajijaze MAKEMIKALI MACHAFU na MIONZI.

Mkiambiwa MNABEZA, ooohh MIMEA NI UCHAWI! Haya sasa!!!!! Umerudi kule kule!!!

Oooohh, wewe hujui sayansi, wewe mchawiii!! Sayansi yenyewe ndio hiyo, umelipa MAMILIONI ukajazwa MIONZI LUKUKI mpaka mwili ukaharibika zaidi na zaidi.

Najua kuna MAKANJANJA watanivamia hapa, lakini sijali. MIMI NAPASUA UKWELI TU, tukana, bwata, lakini HABARI IMEFIKA.
kama unatiba mbadala msaidie hayo maneno huwa yanasemwa baada ya mgonjwa kupona hapo unazidi kumchanganya mwenzio ukweli umekosea...ila nawewe huenda sio kosa lako labda upo tungi.
 
CHEMOTHERAPY haiwezi kukuponya KANSA, inakuongezea KANSA. Ni kama unajibanika kwenye TANURU LA MOTO.

Achana na CHEMOTHERAPY, angalia chakula chake cha kila siku ni chakula gani?

Kama una akili timamu, ungelima hapo bustani upande mchicha mwingi ambao hauna MAKEMIKALI, pamoja na KAROTI, hiyo iwe FIRST AID yake.

MAUCHAFU kwenye damu yake pia, SUMUU, UTANDO, MUCUS, afanye namna ya kuondoa yote hayo. DAMU CHAFU.

PAMBANA SANA, ATAPONA KAMA UNA AKILI TIMAMU.

Ukiendelea na MAKEMIKALI na hizo CHEMOTHERAPY utamuangamiza.
Mkuu BICHWA KOMWE - hujamtendea haki mleta mada. Inawezekana hujaelewa madhara ya kauli yako. Umesamehewa.

Jamaa ameshirikisha nzengo changamoto anazopitia kuhusu afya ya mke wake. Akaenda mbali Zaidi akasema Ushauri wowote anapokea. Umeshindwa nini kumpatia Ushauri kama alivyoomba?

Hakuna mkamilifu. Jifunze kuelewa hisia za wenzako.
 
Manjano mbichi
Komamanga
Kitunguu swaumu
Tangawizi
Visikosekane kwenye mlo wa kila siku.
. Tuachane na machai yenye sukari,maubwaubwa, machapati,machipsi,vitumbua,maandazi, bagia na masembe..
 
Pole sana brother na Mungu akutie nguvu, niliwahi kusikia sehemu kuwa tunda la stafeli lina msaada mkubwa sana kwa wagonjwa wa saratani.
Majani yake achemshe anywe pia kuna Yale majani ya :mhadalati' naruhusu kurekebishwa spelling atwange achuje anywe, mkuu mfa.maji haachi kutapatapa jaribu huenda Mungu anaweza kushusha Shani yake, poleni mgonjwa na wewe muuguzaji Mungu azidi kukupa nguvu
 
Yasemekana mitaani huko Dawa inayoponya donda ndugu yaweza ponya kansa. Ila sasa sio kwa kila stge ya kansa
 
Yapata miaka miwili imepita tangu mke wangu alipogundulika ana saratani ya matiti, tulianza dozi ya CHEMOTHERAPY pale GOOD SAMARITAN CANCER HOSPITAL Ifakara, tulipatiwa jumla ya mizunguko 8 ya CHEMO, hali ilionekana kuwa nzuri ila ndani ya muda mfupi sana uvimbe ulianza tena.

Baada ya kuona uvimbe umeanza upya tulihamia Dodoma BENJAMIN MKAPA napo tulipatiwa chemo 4 kisha ukafanyika upasuaji ili kuondoa titi lililoathirika na saratani, upasuaji amefanya mwezi wa 4 mwaka huu.

Baada ya upasuaji hali ilionekana kama ipo vizuri, ila baada ya miezi ipatayo mi3 mgonjwa ameanza kusumbuliwa tena.

Anasumbuliwa na; MAUMIVU MAKALI SANA MAHALA ALIPOFANYIWA UPASUAJI
KIDONDA KISICHOPONA (kilianza kidogo sana, kama kiji upele, hatimae kikakua. Hakionyeshi dalili ya kupona.

Najua yote ni mipango ya Mungu, ila sina matumaini kama mke wangu anaweza kupona kwa sasa.

KUNA MTU ASHAWAHI KUUGUZA MGONJWA WA SARATANI naomba ushuhuda ambao unaweza nisaidia cha kufanya.

KAMA KUNA DAWA ZA TIBA MBADALA ULITUMIA ZIKASAIDIA, NAOMBA MSAADA PIA.

Kwa sasa mgonjwa yupo tu nyumbani tunasubiri neema ya Mungu

Ushauri wowote pia napokea.

======

UPDATE:
Mkuu pole sana hebu kajiunge hili group kisha omba protocol ya tiba ipi itamfaa kisha tumia me nlijiunga kwenye group hili baada ya kupoteza mzazi kwa cancer ningelijua mapema ningempa hizi dawa wanazotumia jamaa usichelewe
Screenshot_20250208_023920_Opera%20Mini.jpg
Screenshot_20250208_025315_Opera Mini.jpg
 
 
Mkuu BICHWA KOMWE - hujamtendea haki mleta mada. Inawezekana hujaelewa madhara ya kauli yako. Umesamehewa.

Jamaa ameshirikisha nzengo changamoto anazopitia kuhusu afya ya mke wake. Akaenda mbali Zaidi akasema Ushauri wowote anapokea. Umeshindwa nini kumpatia Ushauri kama alivyoomba?

Hakuna mkamilifu. Jifunze kuelewa hisia za wenzako.
Huyu jamaa yupo kwenye list ya watu niliowaignore michango yao siioni ila mkimquote naona fulani uliyemuignore. Mara nyingi nagundua niko sahihi kuwaignore baadhi wa wapuuzi ninapokuta watu mnajibizana nao kutokana na upuuzi wanaoandika.

Wapuuzi ni wengi sana na kila ninapofakiwa kuwatambua mapema huwa natembeza ignore.
 
Ila kuna watu wamepitia nyakati ngumu sana. Sote tunajua tutakufa siku moja ila kuna wenzetu ndio kama hivi anajua kabisa mke wangu atafariki miezi fulani. Imagine maumivu yake.

Kaka nimechelewa kuona huu uzi ila shukuru kwa kila jambo. Naamini shemeji alipata wakati mwingi zaidi wa kuongea na Mungu na ametangulia akiwa msafi.
 
Back
Top Bottom