Kansela wa Austria atangaza kujiuzulu kwa tuhuma za Ubadhirifu

Kansela wa Austria atangaza kujiuzulu kwa tuhuma za Ubadhirifu

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Kansela wa Austria Sebastian Kurz amesema anapanga kujiuzulu kutokana na shinikizo la tuhuma za ubadhirifu, na nafasi yake itajazwa na waziri wa mambo ya nje.

Kurz amekuwa akikabiliwa na tuhuma kwamba chama anachokiongoza kilitumia fedha za serikali kujiunufaisha na fadhila ya vyombo vya habari.

Baada ya kukaidi miito ya kumtaka ajiuzulu, hatimaye Jumamosi usiku alisalimu amri, na kutangaza kuwa anajiengua madarakani kutokana na shutuma hizo kwamba ofisi yake ilivuja fedha za umma.

Kurz amesema ataingia bungeni kama kiongozi wa chama cha kihafidhina cha Austrian People's Party (ÖVP), na kwamba waziri wa mambo ya nje, Alexander Schallenberg atajaza nafasi yake kama kansela.

''Nchi yangu ni muhimu kwangu kuliko mimi,'' amesema Kurz katika hotuba yake kwa njia ya televisheni.
 
Ninahamu sana siku moja au mbili hili litokee na kwetu Afrika
Tayari ilishatokea tena tanzania,
Mzee ali hassan mwinyi alijiuzulu uwaziri wa mambo ya ndani enzi za nyerere, na lowasa alijuliuzulu uwaziri mkuu enzi za kikwete
 
10 Oct 2021
Austrian Chancellor Sebastian Kurz steps down but stays in power | DW News



Austrian Chancellor Sebastian Kurz has resigned. He has been under pressure over allegations he bribed a newspaper for favorable coverage prior to his election as party leader and then chancellor.

As he made that announcement on Saturday, Kurz said he wasn't involved in any criminal activity. And that he was standing aside to prevent a government crisis after his Greens coalition partner said he was unfit to lead the country. Kurz was expected to face a vote of no confidence in parliament next week

Source: DW News
 
Back
Top Bottom