Kanuna eti kisa hajapishwa siti ya daladala akae na mwanae

Kanuna eti kisa hajapishwa siti ya daladala akae na mwanae

Nyamwage

JF-Expert Member
Joined
Oct 16, 2020
Posts
712
Reaction score
1,748
Gari ya kutoka T/chang'ombe kwenda Makumbusho iliingia Makumbusho stendi na abiria wakiwa level seat lakini hakuna abiria alieshuka ikimaanisha kuwa hao abiria wamegeuka na gari ili wasisimame wamelipa nauli ya go and return abiria tuliokuepo stendi tukapanda tukasimama chuma ikaamsha.

Tumefika Mwananyamala kuna dada kapanda na mtoto wake kama wa miaka miwili akitarajia kuwa atapishwa seat akae lakini wapi abiria wamegeuzia shingo pembeni wanaangalia nje.

Kaona kama vile abiria hawajamuona ili wampishe akae sijui alimfanya nini mtoto wake sijui alimfinya maana mtoto aliangua kilio cha ghafla tu lakini wapi abiria wamekaza hawakujali chochote.

Tumeendelea na safari chuma kimefika Buguruni abiria wakashuka wengi tu karibia wote gari lika baki na seat kibao mzee mmoja kamwambia binti kaa umbembeleze mwanao maana safari ya huyo dada bado ilikuwa inaendelea dada kugoma kukaa bwana kasema eti sina shida ya kukaa.
 
Alivyo kuwa kubwa jinga kajua akinuna kuna mtu atamuweza. Cha ajabu kakuweza wewe utamfikiria we mpaka utamuota leo usikun mwisho utajutia. .
 
😅😂 mimi sikuhiz sipishi ng'ombe yoyote seat, yaaan labda uwe na mguu mmoja... Mjamzito Mzee Mlemavu wa kawaida tu au Mama mwenye mtoto I don't care utasimama mbele yangu mwanzo wa kituo hadi mwsho wa safar na sipepesi macho pembeni
 
Hao abiria kwann wasimpakate huyo mtoto wa miaka miwili wakachana huyo mama
 
Kuwapa tu watu dhambi ndogo ndogo, siku moja yalinikuta nimepanda coaster alafu nyumba kuna kama coaster nne ivi zimepaki zinasubiriana kupakia. Ile niliyopanda ikajaa ikawa inataka kuondoka stand akaja mdada na mwanae mdogo mgongoni akapanda ile coaster akasimama pembeni yangu ilhali anaona kabisa zile zingine zilizokuwa chini pale jirani niliyekaa naye akamwambia mbona utateseka sana na mtoto zile pia zinaenda hajajibu. Mie kimya nikainamia siti kabisa earphone maskioni kidogo ananiamsha dada nisaidie kupakata mtoto nikamwambia mlete mtoto akaanza kilio hataki watu nilimpisha akakaa na mwanae ila alinikera mnoo.
 
hao abiria kwann wasimpakate huyo mtoto wa miaka miwili wakachana huyo mama
Weee kuna watoto wengine huwa wanagoma kupakatwa na mtu mwingine, kuna siku tumepanda Mbagala eti naye kaingia na mtoto wa miaka 2 na zaidi aligoma kupakatwa na mtu halafu wanashukia mwananyamala nani asimame, tuliwaacha wacheze bamping na Mama yake mpaka wanashuka.
 
Kuwapa tu watu dhambi ndogo ndogo, siku moja yalinikuta nimepanda coaster alafu nyumba kuna kama coaster nne ivi zimepaki zinasubiriana kupakia. Ile niliyopanda ikajaa ikawa inataka kuondoka stand akaja mdada na mwanae mdogo mgongoni akapanda ile coaster akasimama pembeni yangu ilhali anaona kabisa zile zingine zilizokuwa chini pale jirani niliyekaa naye akamwambia mbona utateseka sana na mtoto zile pia zinaenda hajajibu. Mie kimya nikainamia siti kabisa earphone maskioni kidogo ananiamsha dada nisaidie kupakata mtoto nikamwambia mlete mtoto akaanza kilio hataki watu nilimpisha akakaa na mwanae ila anilikera sana.
Ungemwambia uliambiwa gari zipo zinawasubilia abilia kama nyie, mpe konda au dereva akusaidie kumpakata.
 
[emoji28][emoji23] mimi sikuhiz sipishi ng'ombe yoyote seat, yaaan labda uwe na mguu mmoja... Mjamzito Mzee Mlemavu wa kawaida tu au Mama mwenye mtoto I don't care utasimama mbele yangu mwanzo wa kituo hadi mwsho wa safar na sipepesi macho pembeni
Toka nimpishe mzee tandika akaniibia elf 60 yangu ya ada niliweka mfuko wa nyuma wa suruali,na nimetoka kuomba kwa ndugu maana wazazi walishatangulia mbele ya haki mwaka 2009 hiyo nakaribia kupiga pepa ya form 6, niliapa sitkuja kumpisha kiumbe yoyote kwenye daladala labda mke wangu akiwa na mtoto wangu
 
Gari ya kutoka T/chang'ombe kwenda makumbusho iliingia makumbusho stendi na abilia wakiwa level seat lakini hakuna abiria alieshuka ikimaanisha kuwa hao abiria wamegeuka na gari ili wasisimame wamelipa nauli ya go and return abiria tuliokuepo stendi tukapanda tukasimama chuma ikaamsha.

Tumefika Mwananyamala kuna dada kapanda na mtoto wake kama wa miaka miwili akitalajia kuwa atapishwa seat akae lakini wapi abiria wamegeuzia shingo pembeni wanaangalia nje.

Kaona kama vile abiria hawajamuona ili wampishe akae sijui alimfanya nini mtoto wake sijui alimfinya maana mtoto aliangua kilio cha ghafla tu lakini wapi abiria wamekaza hawakujali chochote.

Tumeendelea na safari chuma kimefika Buguruni abiria wakashuka wengi tu karibia wote gari lika baki na seat kibao mzee mmoja kamwambia binti kaa umbembeleze mwanao maana safari ya huyo dada bado ilikuwa inaendelea dada kugoma kukaa bwana kasema eti sina shida ya kukaa.

Mbona niko stendi sijakuona[emoji3064]
 
Ungemwambia uliambiwa gari zipo zinawasubilia abilia kama nyie, mpe konda au dereva akusaidie kumpakata.
Alinikera sana aisee na wakati jirani niliyekaa naye anamwambia alivyo jeuri akanyamaza basi tu nikasema ngoja nimpishe kwa ajili ya mwanae.
 
Toka nimpishe mzee tandika akaniibia elf 60 yangu ya ada niliweka mfuko wa nyuma wa suruali,na nimetoka kuomba kwa ndugu maana wazazi walishatangulia mbele ya haki mwaka 2009 hiyo nakaribia kupiga pepa ya form 6, niliapa sitkuja kumpisha kiumbe yoyote kwenye daladala labda mke wangu akiwa na mtoto wangu
Aiseeee, nimecheka ila pole sana
 
Hali ya maisha ilivyokuwa ngumu tutaona mengi 😀😀😀
 
Back
Top Bottom