kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 13,778
- 14,214
Nchi yetu ni kubwa sana na timu zimetawanyika sana kwenye mikoa, wilaya, tarafa, kata hata kwenye vijiji. Viwanja vyetu vingi havina dimba nzuri la kuchezea hivyo linazalisha ajali nyingi zisizozuilika kwa wachezaji.
Wachezaji wetu wengi hawakutokea kwenye sports academies hivyo wanarukiana tu bila kujali afya za wenzao na kuzalisha majeraha mengi kwa wachezaji.
Baadhi ya barabara za kwenda na kutoka kwenye mikoa, mechi zitakakochezwa ni ndefu na zina mashimo na matuta mengi, baadhi ya viwanja viko kwenye maeneo ambayo hakuna usafiri wa ndege, timu nyingi hazina fedha za kusafirisha timu kwa ndege.
Timu zetu na hospitali zetu hazina matibabu mazuri kwa wachezaji. na wachezaji wetu hawapati vyakula vizuri vya kuponyesha mwili haraka. Hivyo ndani ya masaa 72 mchezaji atakuwa hayuko fit 100% kumudu kucheza mechi nyingine.
Kanuzi ya TFF/Bodi ya Ligi, CAF na FIFA kupangia timu kucheza mechi kuazia masaa 72 baada ya mechi iliyopita inaziathiri timu nyingi kwenye ligi zetu Tanzania, hasa timu ndogo ambazo hazina vikosi vipana kutokana na hali ya uchumi wao.
Timu kucheza baada ya masaa 72 tu kunalazimisha wachezaji kucheza wakiwa na uchovu mwingi, majeraha, kukosa baadhi ya wachezaji muhimu na timu kufanya vibaya.
Mazingira yetu (jeografia, ubora wa viwanja, aina ya wachezaji na makuzi yao, huduma za afya, usafiri, uchumi na vyakula vya wachezaji) hayaruhusu utekelezwaji wa kanuni hii ya masaa 72, hivyo tusiwe kama dodoki au kasuku wa kutekeleza kila kanuni bila kuangalia hali yetu.
Yaani we have to think globally and act locally kwa kuzingatia hali yetu sisi Tanzania.
Wachezaji wetu wengi hawakutokea kwenye sports academies hivyo wanarukiana tu bila kujali afya za wenzao na kuzalisha majeraha mengi kwa wachezaji.
Baadhi ya barabara za kwenda na kutoka kwenye mikoa, mechi zitakakochezwa ni ndefu na zina mashimo na matuta mengi, baadhi ya viwanja viko kwenye maeneo ambayo hakuna usafiri wa ndege, timu nyingi hazina fedha za kusafirisha timu kwa ndege.
Timu zetu na hospitali zetu hazina matibabu mazuri kwa wachezaji. na wachezaji wetu hawapati vyakula vizuri vya kuponyesha mwili haraka. Hivyo ndani ya masaa 72 mchezaji atakuwa hayuko fit 100% kumudu kucheza mechi nyingine.
Kanuzi ya TFF/Bodi ya Ligi, CAF na FIFA kupangia timu kucheza mechi kuazia masaa 72 baada ya mechi iliyopita inaziathiri timu nyingi kwenye ligi zetu Tanzania, hasa timu ndogo ambazo hazina vikosi vipana kutokana na hali ya uchumi wao.
Timu kucheza baada ya masaa 72 tu kunalazimisha wachezaji kucheza wakiwa na uchovu mwingi, majeraha, kukosa baadhi ya wachezaji muhimu na timu kufanya vibaya.
Mazingira yetu (jeografia, ubora wa viwanja, aina ya wachezaji na makuzi yao, huduma za afya, usafiri, uchumi na vyakula vya wachezaji) hayaruhusu utekelezwaji wa kanuni hii ya masaa 72, hivyo tusiwe kama dodoki au kasuku wa kutekeleza kila kanuni bila kuangalia hali yetu.
Yaani we have to think globally and act locally kwa kuzingatia hali yetu sisi Tanzania.