mcshonde
Member
- Jul 15, 2022
- 66
- 154
Kitu kingine ukiachana na kuongea ukweli kuhusu wayahudi, Kanye amedai kuwa wasanii wengi walio Marekani ni waoga sana kiasi kwamba hawana sauti juu ya haya makampuni makubwa. Miaka miwili iliyopita alieleza kuwa kuna wamarekani weusi wamepelekwa gerezani na vielelezo vyote vinaonyesha hawana makosa. Lakini wasanii/celebrities walichofanya ni kupost tu mtandaoni bila kuchukua hatua yoyote. Kanye akauliza endapo wapo tayari kusimamisha michezo/basketball walau kwa siku moja ili waishinikize serikali iwaachie huru. Kanye anasema hawawezi..hawawezi kwa sababu wao pia wako jela...jela ya uoga..jela ya fikra.