Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 2,060
- 5,648
Katika kata ya Qurus, Wilaya ya Karatu, hekaheka za uandikishaji wa wapiga kura kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa Novemba 27 ziliendelea, lakini hali ilikuwa ya kioja. Mussa, msimamizi wa kituo na Mratibu wa Elimu Kata, alikabiliwa na malalamiko makali kuhusu uandikishaji wa majina ya wapiga kura. Tangu siku ya kwanza, alidaiwa kuandika majina hewa kitendo ambacho kiliibua hisia kali
Raia mwema alifika kituoni na kugundua kasoro hizo ambapo alidai kila siku, idadi ya watu wanaofika vituoni imekuwa ikiongezeka kwa kasi. Katika siku moja, watu 70 walifika kituoni, lakini jioni, idadi ilipanda hadi 150. Walipopigiwa hesabu, waligundua kwamba Mussa alikuwa anaruka kurasa za daftari na kujaza majina ya wapiga kura bila kufuata taratibu. Walipomuhoji kuhusu uhalali wa majina hayo, Mussa alijibu kwa jeuri, akisema ni majina ya watumishi waliopo kwenye kazi, bila kutoa maelezo ya kutosha.
Soma, Pia:
+ CHADEMA Dodoma mjini wadai kunasa majina feki ya wapiga kura
+ Special Thread: Hali ya Vituo vya Kujiandikisha kupiga Kura Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 kwa Picha na Video
+ Shinyanga: Mwanafunzi wa miaka 16 akutwa na wakala wa CHADEMA akiwa anajiandikisha kwenye Uchaguzi wa Serikali Za Mitaa. Apigwa maswali mazito!
Raia mwema alifika kituoni na kugundua kasoro hizo ambapo alidai kila siku, idadi ya watu wanaofika vituoni imekuwa ikiongezeka kwa kasi. Katika siku moja, watu 70 walifika kituoni, lakini jioni, idadi ilipanda hadi 150. Walipopigiwa hesabu, waligundua kwamba Mussa alikuwa anaruka kurasa za daftari na kujaza majina ya wapiga kura bila kufuata taratibu. Walipomuhoji kuhusu uhalali wa majina hayo, Mussa alijibu kwa jeuri, akisema ni majina ya watumishi waliopo kwenye kazi, bila kutoa maelezo ya kutosha.
+ CHADEMA Dodoma mjini wadai kunasa majina feki ya wapiga kura
+ Special Thread: Hali ya Vituo vya Kujiandikisha kupiga Kura Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 kwa Picha na Video
+ Shinyanga: Mwanafunzi wa miaka 16 akutwa na wakala wa CHADEMA akiwa anajiandikisha kwenye Uchaguzi wa Serikali Za Mitaa. Apigwa maswali mazito!