House4Sale Kariakoo: 4 Bdrm Apartment For Sale - Dar

Kasri Homes Tz

JF-Expert Member
Joined
Dec 12, 2016
Posts
501
Reaction score
694
• Direction: Uhuru Road/China Plaza
• Facilities: 4 bedrooms, 3 washrooms
• Floor Area: 180 sqm
• Document: Title deed
• Price: TSH 150 million
• Viewing charge: TSH 30,000
.
✓ Imetazama Uhuru Road
✓ Ipo floor ya 9
✓ Lift yenye inverter ipo
✓ Vyumba viwili self & viwili vya kawaida, public washroom, sebule, jiko na balkoni zenye grili
✓ Ina finishing ya malumalu sakafuni, feni za juu na makabati jikoni
✓ Inauzwa bila samani za ndani (unfurnished)
✓ Hakuna parking ila kuna eneo maalum la parking ya kulipia jirani
.
• In Real Estate We Connect
☎💬 +255767157788
• Jiunge nasi Facebook, Instagram, X na Telegram: BongoLocate
 

HIYO PARKING ITAKUWA NI NDANI YA BENJAMINI MKAPA. all in all maeneo hayo ni mazuri sana kwa mtu anayependa sehemu zilizochangamka sana na za kelele kelele
 
Hivi ukinunua apartment inakuwa yako kwa muda gani, na vipi ghorofa ikivunjwa?
 
Hivi ukinunua apartment inakuwa yako kwa muda gani, na vipi ghorofa ikivunjwa?
Inakuwa yako kwa muda wote mpaka utakapoigawa bure au kwa pesa…
Inategemea na sababu ya kuvunjwa. Wote wanaomiliki apartment kwenye jengo hilo lazima washirikishwe. Kwa mfano ametokea developer anataka kujenga jengo la kisasa zaidi, wenye apartment watapisha, ujenzi ukikamilika watagawiwa apartment zao.
Kama kuna mabadiliko ya matumizi basi wenye apartment watalipwa stahiki zao
 
Mwachiluwi
 
Naomba kuelimishwa juu ya ununuzi wa appartments viwanja vinasomekaje
 
Shida ya hizi appointment za maghorofani ni kama unakuwa mpangaji tu maana utilities bills ni kila mwezi
Aprtments ya ghorofa ni kama kijiji.zile ni kaya nyingi sana zilizopo mahali pamoja.kinakuwa ni kijiji chenye ustarabu flan hiv kwa sababu pako organised maswala ya ulinzi,usafi ,umeme,maji na mambo yoyote ya kijamii.na kuna mtu yuko responsible a kwa kila kaya kulipa ada ya mwezi. Sema tu huwezi kuwa na ile privacy kama unayokuwa nayo ukiwa ktk nyumba yako ya peke yako kwenye fence
 
Shida ya hizi appointment za maghorofani ni kama unakuwa mpangaji tu maana utilities bills ni kila mwezi
Yes!
Sababu utahitaji huduma kama ulinzi, ukusanyaji taka (maana huna eneo la kutupa taka unazozalisha kwenye apartment yako), msafisha ngazi na mazigira ya jengo, lift (kwa majengo ya ghorofa 6 na kuendelea).
Kwa maghorofa makubwa (viwanja viwili) na marefu, tozo ya mwezi hutumika sana kwenye umeme wa lift pia jenereta kipindi cha adha ya umeme na hivyo kufanya majengo haya kuwa na gharama sana mpaka kufikia $ 200 kwa mwezi
 
Hata ukiwa na nyumba yako, bills ziko palepale
Huwezi kunifungia geti langu nisipite ati kwa kuwa sijalipa bill za kuzoa taka, kwenye hayo ma apartment ya maghorofani wanaweza kukuzuia kuingia nyumbani kwako tu kwasababu hujalipa bill za matengenezo ya lift.
 
Huwezi kunifungia geti langu nisipite ati kwa kuwa sijalipa bill za kuzoa taka, kwenye hayo ma apartment ya maghorofani wanaweza kukuzuia kuingia nyumbani kwako tu kwasababu hujalipa bill za matengenezo ya lift.
Kumbe, basi hatari.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…