Kariakoo na Dar es Salaam: Wanahistoria tendeeni haki Historia za majina hayo

Kariakoo na Dar es Salaam: Wanahistoria tendeeni haki Historia za majina hayo

FaizaFoxy

Platinum Member
Joined
Apr 13, 2011
Posts
100,246
Reaction score
123,145
Tafiti ndogo tu, yangu binafsi na isiyo na shaka kabisa niliyoifanya kuhusu jina la jiji letu kuu "Dar Es Salaam" na jina la soko letu kuu "Kariakoo" ninaihitimisha kwa ufupi (summary) hapa chini kwa kusema wanahistoria hususan wa hapa Tanzania hawayatendei haki hayo majina kwa kutuaminisha maana ya majina hayo isiyo halisi na isiyo ya kweli.

Dar Es Salaam

Kila ninapokutana na maana ya jina Dar Es Salaam naona makosa ya wazi kabisa au ya wanaotoa maana kutokufanya tafiti japo kidogo au kuwaamini sana wanahistoria ambao au wao kuwaamini waliowafundisha au waliyoyasoma bila kuyafanyia tafiti na kuiamini tu maana inayotolewa. Au ni makusudi inafanyika ili kuifuta maana halisi ya jina hilo na lilipoanzia kihistoria.

Mara nyingi, kama si zote, tumeaminishwa kuwa maana ya neno Dar Es Salaa ni "bandari ya Salama", na wanatuaminisha kuwa historia yake ni Waarabu waliotoa jina hilo kutokana na kuwepo bandari hapo Dar Es Salaam. Huo tunaoaminishwa sio ukweli.

Ukweli ni kuwa neno Bandari halimaanishi bandari kwa Kiarabu bali neno Bandar ni neno la Kiajemi (Persia) linalomaanisha bandari. Na ipo miji maarufu ya Kiajemi (Persia) yenye jina hilo.

Jina Dar Es Salaam halina neno "Bandar" la Persia au Kiarabu hata maana yake iwe ni "Bandari". Jina hilo lina neno la Kiarabu"Dar" linalomaanisha Nyumba au "dari" kwa maana "haven". Kwa akirefu chake ni Dar Es Salaam ni Nyumba ya Amani au vile vile Dar Es Salaam ni "haven of Peace". Ambayo ni maana halisi ya jina la lililokuja kuwa jiji letu pendwa.

Neno Dar Es Salaam linatokana na neno la Kiarabu fasaha "Dar Us Salaam" linalopatikana ndani ya Qur'an Tukufu, utalipata katika sura ya 10 aya ya 25 na sura ya 6 aya ya 127 likimaanisha jina la pepo (Abode or Haven of Peace).

Kwa maana hizo, jina la jiji letu la Dar Es Salaam lilianzia kilipojengwa chuo cha kwanza cha Kiislam (Madrassa) hapo ilipo sasa Ikulu ya Dar na jengo hilo la la chuo hicho ndio likaitwa Dar Us Salaam (Nyumba ya amani) na ilipo Hospitali ya Ocean Road ndipo palikuwa mabweni ya chuo hicho. Mjerumani ndiye akja kukifanya chuo hicho kuwa nyumba ya gavana baada ya kukitengeneza upya lakini aliacha mjengo ule ule wa asili kwa kiwango kikubwa. Athari za majengo ya Kiarabu na Kiislaam kwenye Ikulu yetu ipo mpaka leo. Haipingiki kwa aijuae Ikulu hiyo.

Kama hiyo haitoshi, pia kuna nchi, Brunei, jina la jiji lake linaitwa Dar us salaam kama jiji letu Dar Es Salaam, lakini kwenye jiji hilo hilo bandari yake inatwa Bandar Seri Begawan. Hiyo inaonessha tofauti iliyopo katika maana ya maneno "Bandar" na "Dar".

Baadhi ya miji yenye jina hilo na maana yake ikielezewa Kiingereza...


From Wikipedia, the free encyclopedia

Darussalam (Arabic: دار السلام) is an Arabic word which means "abode of peace" and is the name of one of the layers of Jannah (Paradise in Islam). It may refer to:

Post ijayo ntawaletea maana ya jina Kariakoo.
 
Kariakoo

Hili nalo ni jina maarufu sana la soko letu kuu la Tanzania (kwa sasa naamini ni soko kuu Afrika Mashariki na Kati), Kariakoo.

Hili nalo kwa tafiti yangu binafsi niliyoifanya ni dhahiri wanahistoria wetu wengi au takriban wote, hawatupi maana yake halisi. Hata nguli wa historia ya Tanzania, kaka yangu Mohamed Said kuna sehemu nadhani amewahi kuandika maana aliyoikuta shule au aliyoaminishwa na Waalimu wake bila kufanya tafiti akaiamini na kuitumia.

Wanasema "uongo ukisemwa sana hugeuka ukaoneka ni ukweli".

Jina la Kariakoo tumeaminishwa kuwa linatokana na lugha ya Kiingereza "Carrier Corps" kama alivyoandika mwana JF mmoja: ASILI YA NENO "KARIAKOO"

Wengine nimewasoma wanasema ni "Courrier court".

Wote wakimaanisha linatokana na Kingereza ndipo kwa Kiswahili kushindwa kutamka sawa hicho Kingereza pakajulikana kama panavyoitwa sasa Kariakoo". Ukitazama kijuujuu bila kuwa mdadisi utaamini hivyo ndio sahihi. Mimi napingana na maana zote hizo.

Maana ya ukweli wa jina hilo ni maneno ya Kiarabu, "Qaria: au "Garia" kwa Waarabu wa Hadhramout, inamaanisha ni "kijiji" na neno "Koo" linaweza kuwa linatokana na Kibantu "Kuu" au Kiarabu "Kulu" ikimaanisha wote,
Qaria Kulu, kijiji cha wote.

Tayari Mjerumani alipokuja Kariakoo ilikuwepo na ikiitwa Qaria Kuu kwa maana kijiji kikuu kupita vypote vinavyoizunguka. Kariakoo tayari ilikuwa ina wakazi 24,00 katika miaka 1900s.

Ukweli ni huo, hakuna zaidi ya huo. Kuamini kuwa Kariakoo limetokana na neno la Kingereza ni "kulishana matango pori" tu.

Leo umeyajuwa mapya mawili yanayohusu historia ya nchi yako kutoka Darsa la FaizaFoxy.
 
Kariakoo

Hili nalo ni jina maarufu sana la soko letu kuu la Tanzania (kwa sasa naamini ni soko kuu Afrika Mashariki na Kati), Kariakoo.

Hili nalo kwa tafiti yangu binafsi niliyoifanya ni dhahiri wanahistoria wetu wengi au takriban wote, hawatupi maana yake halisi. Hata nguli wa historia ya Tanzania, kaka yangu Mohamed Said kuna sehemu nadhani amewahi kuandika maana aliyoikuta shule au aliyoaminishwa na Waalimu wake bila kufanya tafiti akaiamini na kuitumia.

Wanasema "uongo ukisemwa sana hugeuka ukaoneka ni ukweli".

Jina la Kariakoo tumeaminishwa kuwa linatokana na lugha ya Kiingereza "Carrier Corps" kama alivyoandika mwana JF mmoja: ASILI YA NENO "KARIAKOO"

Wengine nimewasoma wanasema ni "Courrier court".

Wote wakimaanisha linatokana na Kingereza ndipo kwa Kiswahili kushindwa kutamka swa hicho Kingereza pakajulikana kama panavyoitwa sasa Kariakoo". Ukitazama kijuujuu bila kuwa mdadisi utaamini hivyo ndio sahihi. Mimi napingana na maana zote hizo.

Maana ya ukweli wa jina hilo ni maneno ya Kiarabu, "Qaria: au "Garia" kwa Waarabu wa Hadhramout, inamaanisha ni "kijiji" na neno "Koo" linaweza kuwa linatokana na Kibantu "Kuu" au Kiarabu "Kulu" ikimaanisha wote,
Qaria Kulu, kijiji cha wote.

Tayari Mjerumani alipokuja Kariakoo ilikuwepo na ikiitwa Qaria Kuu kwa maana kijiji kikuu kupita vypote vinavyoizunguka. Kariakoo tayari ilikuwa ina wakazi 24,00 katika miaka 1900s.


Ukweli ni huo, hakuna zaidi ya huo. Kuamini kuwa Kariakoo limetokana na neno la Kingereza ni "kulishana matango pori "tu.


Leo umeyajuwa mapya mawili yanayohusu histori ya nchi yako kutoka Darsa la FaizaFoxy.
We bibi hujambo!?

Nasikia wewe ndio Samia Suluhu?
 
Mwanangu una akili sana. Umetoa historia bila upendeleo. Nakubaliana nawe. Wahafidhina wanataka kila kitu kizuri kitokane na waarabu na siyo wengine. Kumbe Dar Us Salaam ni tamu hivyo! Basi nayo tuifanye eneo takatifu kama Makka maana jina lake liko kwenye Quran. Unasemaje mwanangu nasi kuanza kupata utakatifu ambao wageni walijirundikia sisi tukionekana makafiri wa kawaida?
 
Shukrani, kwa upeo wangu binafsi hoja yako ni ya msingi ukizingatia na kiarabu unakifahamu. Labda binafsi najiuliza kwanini walipotosha tafsiri ya hilo jina?!! Hawakuwa na uelewa wake?!
 
Mwanangu una akili sana. Umetoa historia bila upendeleo. Nakubaliana nawe. Wahafidhina wanataka kila kitu kizuri kitokane na waarabu na siyo wengine. Kumbe Dar Us Salaam ni tamu hivyo! Basi nayo tuifanye eneo takatifu kama Makka maana jina lake liko kwenye Quran. Unasemaje mwanangu nasi kuanza kupata utakatifu ambao wageni walijirundikia sisi tukionekana makafiri wa kawaida?
Ardhi yote ni takatifu Kiislaam. Bila kujalisha jina.

Kwa kukujuza tu, hata Jerusalem ni derivative ya Dar Es Salaam.

Tafiti yangu, ambayo hapa nimei "summarize" tu inakwenda ndani (deeper) zaidi ya hayo mawili yaliyopotoshwa na yanayoendelezwa kupotoshwa uhalisia wa asili yake. Au kwa kujazwa ujinga kwa makusudi au kwa watu kujazwa ujinga bila kujielewa kuwa wamejazwa ujinga.

Yangu ni tafiti ya majina ya miji mingi duniani na pia pia ni tafiti ya maneno mengi ya Kiswahili na Kingereza yanayotokana na Kiarabu. (Anthropology).

Corona imenifanya nikae ndani kwa muda mrefu sana na nikaona nisikae bure nifanye hii tafiti ya ki "anthropology".
 
Shukrani, kwa upeo wangu binafsi hoja yako ni ya msingi ukizingatia na kiarabu unakifahamu. Labda binafsi najiuliza kwanini walipotosha tafsiri ya hilo jina?!! Hawakuwa na uelewa wake?!
Kila kinachohusiana na Uislam kinapotoshwa kwa makusudi kwenye historia Hata Kiswahili sanifu ni zao la chuki hizo. Kiswahili fasaha kinabadilishwa mbele ya macho yetu.

Hata Historia ya utumwa imepotoshwa kuonesha kuwa mzungu ndio bingwa aliyekuja kuondosha utumwa wakati ni kinyume chake.

Ni mengi sana, tafiti yangu ndoo imelenga sana yaliopotoshwa kihistoria, kimaana na kiuhalisia inayaibua. Mengine ni kuwa hayajaandikwa tu maana yake na si kuwa yote yanapotoshwa kwa makusudi.Mpaka sasa sijaiweka kikamilifu kwani kuna topics nyingi sana. In shaa Allah nikipata wasaa nitaingia deeper kwenye kila topic.
 
Back
Top Bottom