Karibuni wanaohitaji ushauri wa kiafya na maswali kuhusu afya

Dr. Wansegamila

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2012
Posts
2,968
Reaction score
8,139
Kuanzia leo nitakuwa natoa ushauri wa kiafya kwa wenye shida na matatizo mbalimbali ya kiafya kupitia uzi huu kwa kadri ntakavyokuwa napata nafasi. Karibuni sana
 
safi mkuu,
swali:
mimi nina approach 40 yrs, nimekutana na rafiki zangu niliosoma nao na kufanya kazi miaka ya 25-36 kwakweli nimestaajabu baadhi wameanza kuchoka; vitambi, sura inazeeka, wengine pombe sana sura zimeisha, wengine mara waseme miguu imevimba, wengine wanachagua vyakula.(ila sio wote maana ilikuwa msibani). sasa daktari kupitia uzi huu naomba utupe njia ya kuishi ili kwa kula nini na kuishi mfumo upi ili tusizeeke. wenzetu china na western europe wanaishi sana kwanini???
 
Ahsante sana kwa swali lako. Its a very broad question, but i will try my best.
-Pata mlo uliokamilika yaani uwe na virutubisho vyote kama wanga,protini,mafuta,vitamins na madini kwa uwiano sahihi... Na hii wala si gharama kama wengi tunavyodhani;katika mlo wako hakiksha unapata mboga za majani na matunda kwa wingi kuliko vyakula vya wanga(wali/ugali)!! kwa wabongo wengi tunakula kinyume na inavyoshauriwa kiafya, i.e ugali mkubwa mboga kidogo;unatakiwa ule kwa mfano ugali robo sahani-robo tatu iliyobaki ujazie mboga za majani, nyama/samaki/dagaa/maharage, na
matunda.
-Pia tuepuke nafaka iliyokobolewa(sembe) na badala yake tupendelee dona zaidi.
-Wakati wa asubuhi(kifungua kinywa) ndo kinatakiwa kiwe kizito zaidi,halafu mchana unapunguza kidogo, na jioni unakula kidogo zaidi(usile chakula baada ya saa moja usiku!!)
-Tuepuke kabisa pombe,sigara,vinywaji vya makopo kama soda na juice za viwandani. Badala yake tunywe zaidi maziwa,juice za matunda(sio za viwandani).
-Chakula tunachopika tuepuke sana kuweka mafuta mengi ya kupikia(kwa siku moja kiafya unatakiwa usizidishe kijiko kimoja cha chakula cha mafuta ya kupikia!!!!) Ni vizuri pia kupikia kwa mafuta ya mimea(kama alizeti) kulikoya wanyama;pia tupendelee zaidi vyakula vya kuchemsha na kupunguza vyakula vya kuunga.
-Tuepuke vyakula vya kukaanga kwa mafuta.
-MAZOEZI- Ni muhimu sana kuhakikisha kila siku tumepata angalau dakika 30-45 za kufanya mazoezi ya viungo mpaka kutoa jasho!!
 
Nina shida ya keroid masikioni na nimekata mara 4 ktk hospt na madkt tofautitofauti ambapo kila m1 alikuwa akiniaidi kuwa yeye atamaliza ila tatizo bado linajirudia. Nimeshaenda k.c.m.c, drk Gullet yupo Ar kwa dkt Mohamed nk. Jee nini dawa yake au maisha yangu yoye itakuwa ni kila mwaka kukata na kurudia baada ya miezi michachee??
 
nilipokuwa mdogo nilianguka na kuvunjika meno kipande... mwanzoni haikua shida but now days naanza kupata shida kwa mfano siwezi kunywa kitu cha baridi au hewa ikiingia kwenye meno sehemu ile iliyovunjika nasikia maumivu flan hivi........
shida inaweza kuwa nini na nifanye nini.......
 
Jina sahihi la ugonjwa unaokusumbua ni KELOIDS.
Keloids ni a very challenging disorder kuitibu; kwa sababu ina recurrence rate(uwezekano wa tatizo kurudi baada ya matibabu) kubwa mno. Inasisitizwa kuwa the best option ni PREVENTION yaani kuzuia keloids zisitokee kuliko kutibu. Kwa mfano wewe love more than100 nimeona thread yako ambayo inaonyesha tangu mdogo kuwa una tatizo hilo; lakini pengine kwa kutokujua au kutopata ushauri sahihi bado ulienda kutoboa masikio tena kuongeza tundu la pili!! Huwa wenye tatizo la keloids wanashauriwa sana kuavoid surgeries au procedure ambazo si za muhimu ili kupunguza tatizo hili(the best option ilikuwa wewe kutotoboa masikio yako for the second time!!)
Keloids hata ukizifanyia upasuaji(excision), recurrence yake ni up to 100%(surgery alone); na bado hata ukifanya surgery+radiation, recurrence rate(uwezekano wa tatizo kurudi ni 60%)!! Hata hiyo laser therapy ambayo pia ulieleza ulifanyiwa(kwenye ile thread yako nyingine), recurrence rate yake ni up to 90%!!
Kwa wenzetu wana options zaidi kama vile use of intralesion interferons therapy(hizi interferons ni kama vichocheo hivi ambapo vinachomwa kwenye hizo keloids)-hizi zinasaidia kupunguza keloids(ukubwa) kwa karibu 50%. Pia kuna dawa zinaweza kuchomwa kwenye hizo keloids kama 5 Fluorouracil kwa wiki kadhaa. Hizi options mbili za mwisho(na zipo nyingine nyingi) ndo among the best options kwa mtu kama wewe ambae umeshafanyiwa surgery pamoja na radiations lakini bado zimerudi tena. Kwa bahati mbaya sana hivyo vitu havipo nchini kwetu kwa sasa(to the best of my knowledge-a dermatologist might give more insights kama kuna center hapa bongo hivyo vitu vipo)
Ushauri wangu1)Nenda kwa hao ma dermatologist unaowaona waulize je hapa bongo hakuna options nyingine zaidi ya kukata na radiations? waambie kuwa umesoma soma kwenye internet umeona kuna vitu kama interferons,5 fluorouracil, je kama vinapatikana bongo haviwezi kukusaidia? Waulize kistaarabu tuu na mdiscuss kuhusu options ambazo zipo kwa hilo tatizo,
2) Kama una uwezo wa kutosha unaweza kufanya mpango wa kwenda india au south africa kwa ajili ya hizo options ambazo hapa bongo hamna.
Ahsante sana na pole sana kwa matatizo haya.
 
olele
Dalili unazoanza kuzipata zinaonyesha kwamba ulipoumia, sehemu ya nje ya jino ambayo ndo huwa inalinda kiini cha jino(pulp) ililika/kumeguka, hivyo kusababisha kiini cha jino(pulp) kuathirika/kuharibika ndo maana unaanza kupata maumivu ukinywa kitu cha baridi au hewa ikiingia(kitaalamu inaitwa pulpitis).
Cha kufanya; nenda kwa dentist haraka aweze kuevaluate meno yako na aweze kukupat tiba sahihi kulingana na extent ya tatizo(kufanya root canal, au kung'oa jino, etc).
 
Last edited by a moderator:
Ndugu habari.

Mimi nnatatizo la nyayo kuwaka moto, na nimeomba ushauri katika uzi huu.

Msaada: Nyayo zangu zinawaka moto.

Hapa hapa jukwaani, kuna dawa nmezitumia kama neuro support, neurobine na multvitamins mara kadhaa.

Kitu kingine, niliwahi kuambiwa nina fungus kwenye ngozi, nilijaribu kutibu na sijaona majibu yake.

Nina uzito wa 68Kg, urefu 170cm, presha 130/90, umri 26 yrs.

Asante.
 
Dokta umekimbia..., swali la korodani moja kuuma alilouliza kinyaga linanihusu, nasubiri jibu
 
Dokta umekimbia..., swali la korodani moja kuuma alilouliza kinyaga linanihusu, nasubiri jibu

Nimsaidie Dr maana kazi zetu ni nyingi... tatizo la maumivu ya korodani ni kubwa na lina uwanja mpana wa kushughulika nalo kwa sababu maumivu hayo yanaweza kusababishwa na sababu nyingi ambazo hugawanya ktk makundi mawili...
1.Maumivu yanayoanzia katika korodani zenyewe.. mfano.. ORCHITIS NA EPIDIDYMITIS
2.Maumivu yanayoanzia nje ya korodani.. mfano kwenye figo kukiwa na stones n.k
Hivo basi ili kuondoa kabisa tatizo inapaswa tujue sababu... na nakushauri kufika kituo cha huduma ili Dr achukue hx, afanye physical examination na ddx... all the best.
 
Kuna rafikiangu ana tatizo la hethi, alijifungua tar 1/5/2014 na baada ya siku 40 kupita alianza hedhi kawaida imeenda

vizuri tuu, lakini kuanzia mwezi wa kumi mwaka jana ikakta tena na mpaka saizi hajapata hedhi tena, alienda kwa docor

akapima km ana mimba lkn hakuwa nayo lakni doctor hakusema sababu kamili ya hili tatizo, nahitaji msaada wako doctor

nini tatizo

na tiba yake ni ipi, maana mpaka sasa anaogopa asije pata mimba tena na mtoto bado mdogo na uzazi wa mpango hataki maana una madhara mengi sana.
 
Naomba msaada mana rafiki yangu anadai akiwa bleed anaumwa sana tumbo chini ya kitovu na damu hutoka kdg tena nyepesi je huenda akawa na tatizo
 
je? ninaposhika damu ya mtu alie na virus vya ukimwi nanikiwa sina mchubuko wowote mikononi kwa kujisahau hapo hapo nikajikuna mdomoni naweza kuambukizwa virus vya ukimwi?
 

Hongera kwa kupata mtoto

Hiyo huwa ni hali ya kawaida sana hasa kama mama anakua anamnyonyesha mtoto wake... kwa ufupi katika kipindi hicho vichocheo vya mwili(HORMONES) hasa sex hormones znakua HAZIJA-BALANCE... Mara nyingi huisha bila matibabu yoyote,, LAKINI ENDAPO ITAKUA NI KWA MUDA MREFU AFIKE HOSP
 
je? ninaposhika damu ya mtu alie na virus vya ukimwi nanikiwa sina mchubuko wowote mikononi kwa kujisahau hapo hapo nikajikuna mdomoni naweza kuambukizwa virus vya ukimwi?

VIPIMO TU... VIPIMO TU ndo vitathibitisha kama umeathirika au hujaathirika.

Kwa maelezo yako ni kwa kiwango kidogo sana mtu anaweza kupata maambukizi.. hii ni kwasababu mdomo una ngozi laini sana kwa ndani ambayo inaweza pelekea kuwa njia ya virusi kupita hasa kama kuna mchubuko.

Kwa USHAURI.. jaribu kutembelea kituo cha huduma kwa ushauri na vipimo.
 
Dr. Wansegamila tafadhali itendee haki jamii ya JF na post hii kwa kutoa msaada kama ulivo tarajia.. Natambua majukumu ni Mengi lakini huna budi kuwasaidia watu hawa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…