Karume hakusaini hati ya muungano

Karume hakusaini hati ya muungano

palalisote

JF-Expert Member
Joined
Aug 4, 2010
Posts
8,335
Reaction score
1,459
10151410_4228453164959_6813253786322445256_n.jpg


10174958_4228392603445_8754754751771851547_n.jpg


1977132_4228452644946_8149743562807800466_n.jpg


1978880_579267468838322_8421878849491764009_n.jpg
 
Naomba kufahamu hizo document mbili za secret na confidential ni za vyombo vya nje ya nchi au vya hapa, nani alikuwa anataalifiwa?
 
dah hii movie tamu sana,kila siku nawambia wnajamvi kuwa dunia imekuwa ndogo,sasa hili gazeti ni la mwaka wa 1964
hehehehe na wewe nawe mmbea...

unajua kuna vitu viwili vinawachanganya watu. Moja ni articles of union na union order. Articles of union hizo hazina shida na hizo ndizo zinafahamika na hapo juu kwenye picha ndiyo zinasainiwa lakini hiyo union order haifahamiki ilipo ndiyo inatafutwa
 
unajua kuna vitu viwili vinawachanganya watu. Moja ni articles of union na union order. Articles of union hizo hazina shida na hizo ndizo zinafahamika na hapo juu kwenye picha ndiyo zinasainiwa lakini hiyo union order haifahamiki ilipo ndiyo inatafutwa

Union Order naona Karume alizifungia samaki.....kwa bahati mbaya bila ya kujua 🙂,Sasa tuseme hawa wanasiasa wetu hawalijui hili au wanalijua isipokuwa wanawafanya watanzania wajinga....,,Kama huyu Nahodha ameshawahi kuwa waziri kiongozi Zanzibar mbona anaongea utumbo
 
4.jpg


1.jpg



2.jpg



3.jpg
 

Attachments

  • kalume 2.jpg
    kalume 2.jpg
    71.2 KB · Views: 481
Wanabodi,

Wakati sintofahamu kuhusu Hati Halisi za Muungano, ikiendelea, nawaomba Watanzania wenzangu tufike mahali tuambiane ukweli halisi kuwa Hati Halisi za Muungano", hazipo popote!, nakala iliyowasilishwa kwenye Bunge Maalum la Katiba, yenye saini ya Nyerere na Pius Msekwa!, ile sio hati ya muungano (Articles of The Union" bali ile ni Sheria ya Muungano!, "The Act Of Union!" iliyotungwa na Bunge la Tanganyika, ku ratify the "Artcles of Union", ambayo imesainiwa na Nyerere, Speker wa Bunge na Msekwa kama Katibu wa Bunge wa Wakati Huo!.

Msekwa was never a signatory kwenye Artcles of The Union!".

Signatories kwenye "Artcles of The Union" ni
  1. Mwalimu Julius Nyerere-Rais wa Jamhuri ya Tanganyika
  2. Sheikh Abedi Amani Karume- Rais wa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
  3. Mwanasheria Mkuu wa Tanganyika -Fifthfoot
  4. Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar (Wolfgang Dourado-Alipewa likizo ya lazima nje ya nchi, Akaletwa mwanasheria wa Ghana kuusimamia muungano, ukasainiwa na Mwanasheria Mkuu wa Tanganyika pekee!)
Hati Hizi hazipo Idara ya Nyaraka na kumbukumbu za Taifa Nimezungumza na Mtanzania wa Kwanza kuwa mkuu wa Idara ya Kumbukumbu, Mzee Mongela, hakuwahi kuziona hati hizo wala hata copy yake!.
Nikazungumza na Mkurugenzi wa Nyaraka aliyepita Bwana Mlyansi, pia amekiri kutoziona hati hizi!. Nikazungumza na Mkurugenzi wa Nyaraka aliyeko sasa Bw. Magai!, hati hizo hazipo!.

Ule uongo wa kuwa eti hati ziko UN, nimewahi kuzifuatilia mpaka huko UN hati hizo hazipo!.

Kipindi hiki cha Bunge Maalum sasa ndicho kipindi muafaka tuelezane ukweli bayana kuwa hati hizo are no where to be seen!, tuelezwe vizuri tuu kuwa kwa bahati mbaya zililiwa na mchwa hivyo zimetoweka zote kwa pamoja!.
  1. Nakala halisi ya Serikali ya Tanganyika, imetoweka!
  2. Nakala halisi ya SMZ, imetoweka!
  3. Nakala halisi ya Bunge la Tanganyika-imetoweka!
  4. Nakala halisi ya BLW nayo imetoweka!
  5. Nakala halisi ya Mwanasheria Mkuu -imetoweka!.
  6. Nakala halisi ya Nyerere-imetoweka
  7. Nakala halisi ya Karume -imetoweka!
Hili suala la hati halisi za Muungano nimelizungumza
Hapa-Swali: Hivi Muungano Tanzania Upo Kweli?! au ni Dhana Tuu?!. (Ufuatiliaji Muungano Sehemu ya I) - JamiiForums

Na Hapa-Jee Wajua Kuwa Tanzania Hatuna Mkataba wa Muungano?. Kilichopo ni Makubaliano Tuu ya Muungano?!. - JamiiForums

Na Hapa-Je, wajua kuwa Zanzibar haikuridhia Muungano? Ina Maana Gani? - JamiiForums

Na Hapa-[h=3]Je, wajua kuwa kuna uwezekano Tanzania sio nchi halali Kisheria (De Jure) Bali ni De Factor?! - JamiiForums

Kwa kuanzia jee Nakala Halisi za Muungano ziko wapi?.

Pasco
 
Halafu tunaambiwa muungano ulifanywa kwa maslahi ya wananchi. Jamani tuachiani tuamue sasa kipi kizuri kwetu na sio kwa faida ya viongozi waliopita!
 
unapomfukuza ngiri atakimbia wee ila akifika mbele atajiuliza hivi ninakimbilia nini?atageuka na kuanza kukukimbiza wewe mkimbizaji,ndio yanayotokea kwenye suala hili la muungano.Wametukimbiza wee sasa tumegutuka wao sasa ndio wakimbizwaji.
 
Likes Given39021


[h=2]
icon1.png
Swali: Hivi Muungano Tanzania Upo Kweli?! au ni Dhana Tuu?!. (Ufuatiliaji Muungano Sehemu ya I)[/h]
Wanabodi,

Wakati tukiendelea na mjadala wa serikali 3 kuelekea kwenye katiba mpya, uoga mkuu kuhusu uwepo wa serikali 3, ni tishio la serikali tatu kuudhoofisha muungano hatimaye kurisk kuuvunja!. Watanzania bado hatujaruhusiwa kuhoji au kujadili kuhusu uwepo wa muungano, still it's a toboo topic!.

Wakati hayo yakiendelea, nina swali moja la msingi, ambalo jibu lake linahitaji kajiutafiti kadogo na kupata uthibitisho wa kimaandishi kuwa "Hivi Kweli Huu Muungano uliounganisha Tanganyika na Zanzibar ni Kweli Upo?!... au ni Dhana Tuu?!.

1. Kwa vile Tanganyika huru yenye kiti kule UN, na Zanzibar nayo ni nchi huru, yenye kiti kule UN, muungano wowote wa nchi mbili hizi, ulipaswa kwanza kutanguliwa na "Instruments" za Kimataifa za Union!. Instruments hizo, zilibidi ziridhiwe kwanza (Ratified) na Mabunge ya nchi hizo mbili kisha zile ratified instruments zipelekwe UN na kuwa filed kwanza ndipo viti vya Tanganyika na Zanzibar vingekuwa merged na kiti cha nchi mpya Tanzania kingepandishwa!.

2. Instuments za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar zilikuwa drafted as local treaty wakati zilipaswa ziwe ni an International Instruments na (Hati za Muungano), zikasainiwa na Nyerere na Karume haste haste bila wananchi wa nchi husika hizo kuulizwa!. Baada ya kusainiwa zilibidi ziwe ratified na Bunge la Tanganyika na BLM kule Zanzibar. Inaelezwa kuwa Bunge la Tanganyika lili ratify!, Jee kuna yeyote aliyewahi kuzisoma hizo hansard za bunge la Tanganyika likiratify Union Instruments?!.

3. Kwa upande wa Zanzibar, hakuna ratification yoyote iliyofanyika!, bali Abedi Karume aliwaita Wanabalozi waliokuwepo Zanzibar na kuwaeleza kwa kauli kuwa BLM limeridhia kuratify zile Instruments. Hakuna andiko lolote la ratification kutoka Zanzibar!. Ratification is a process na kufanyika kwa maandishi!, na sio kwa kauli!.

4. Kufuatia kukosekana kwa ratification ya upande mmoja wa Muungano, jee kiti cha Zanzibar, kilifutika futika vipi kule UN na nafasi yake kukaliwa na Tanzania bila hizo instuments kuwasilishwa rasmi UN?!.

5. Wakati fulani nikiwa NY, nilipata fursa kupita pale ubalozini kwetu UN, enzi hizo wife wa mwana jf mwenzetu akiwa ni receptionist, niliomba kumsalimia Balozi enzi hizo akiwa Daudi Mwakawago. Ilishindikana!. Wabongo wakimuona mbongo ambaye sio mserikali hapo ubalozini , they treat you like a shit!. Baada ya kueleza shida yangu, nilielezwa maswali yangu nilipaswa kuyaleta kitambo kwa maandishi hivyo hayakupata majibu!. Miongoni mwa mambo niliyouliza ni copy ya International Treaty ya Union btn Tanganyika and Zanzibar iliyowasilishwa UN ili kufuta Viti vya Tanganyika na Zanzibar na Kuzaa Tanzania!. Sikuonyeshwa!.

6. International Treaties zote za Kimataifa zinazofika UN, zinahifadhiwa katika Maktaba Maalum, hutolewa copy na kuwekwa kwenye UN Open Library ambapo iko wazi kwa yeyote mwenye UN Access kuiperusi na kuisoma. Hivyo nilipokwenda kwenye UN Library, hakuna any International Treaty iliyopelekwa na Serikali ya Tanganyika kukifuta kiti chake UN wala iliyopelekwa na serikali ya Zanzibar kukifuta kiti chake!. Kilichopo kule ni Note Verbale ya Tanzania mpya kuumuarifu Katibu Mkuu wa UN kuwa Tanganyika na Zanzibar zimeungana!. Hiyo Note Verbale ndio taarifa ya awali, instuments zingefuatia!. Jee kuna Yeyote aliwahi kuziona hizo instuments?!. Hivi kumbe kiti cha nchi kwenye UN kinaweza kufutwa kwa Note Verbale tuu bila instruments zozote kujustify huo muungano?!.

7.Niliwahi kwenda pale Ofisi za Nyaraka na Kumbukumbu za Taifa, nikiamini kuwa classified documents are unclassified baada ya kipindi cha miaka 30!. Nikaomba kuziona hizo classified documents!, nikaelezwa zilizopo kwenye public access ni zile mkoloni tuu!. Za Tanganyika huru na Tanzania, they are unclassified but haziko kwenye open access!, ili uzione, unapaswa kuandika barua rasmi ya kuomba kuziona, ukieleza lengo la kuziomba ni nini?!.Nikauliza tuu jee Hati za Muungano zipo mle?!. Nilijibiwa zipo!. Barua sijaandika na hati zijaziona!. Jee kuna mtu yeyote amewahi kuziona hati hizo za muungano?!.

8. Kama hati za Muungano, au Mkataba wa Muungano kama ule ulioletwa humu jf, ndio mkataba wenyewe!, Niliwahi kusema hauna sifa za kuitwa mkataba kwa sababu umekosa kipengele kiitwacho "Privity to contract" sambamba na kukosekana kipengele cha kuvunjika kwa mkataba!. Ili mkataba uwe na sifa ya mkataba, lazima kuwepo na kipengele cha itakuwaje endapo mkataba huo utavunjika!. Hati za Muungano hazikuwa na kipengele hicho hivyo huo haukuwa mkataba halali bali ni makubaliano tuu ya Muungano kati ya Nyerere na Karume, yasingefit hata kuwa filed kwenye Nyaraka na Kumbukumbu za Taifa, seuze kufika UN?!.

9. Kwa vile sasa hoja kuu ya mjadala wa katiba ni serikali tatu kwa lengo la kuulinda muungano!, swali la msingi sasa ni jee huu muungano tunaotaka kuulinda upo kiukweli kweli, au ni dhana tuu, kama wanandoa wawili wanapochukuana na kuishi pamoja kama mume na mke kwa dhana ya ndoa, baada ya kuishi miaka miwili kisheria wanakuwa ni wanandoa kabisa, ila pasipo na hati ya ndoa, wanandoa hawa wanakuwa wanaishi kwenye dhana tuu ya ndoa hata wakiishi miaka 100!. Sasa jee huu muungano wetu ni wa kweli au ni dhana tuu ya muungano?!.

10. Kwa vile Idara ya Nyaraka ipo, barua ya kuomba kuziona hati hizo nitaiandika!, kwavile MFA ipo, barua ya kuziona hizo instuments zilizopelekwa UN pia nitaiandika, na UN kwenyewe nitarudi tena this time na barua ili nisirudi tena mikono mitupu!

My Take:
Nahisi mara tuu baada ya muungano, kwa Nyerere na Karume kutia saini kwenye hati zile mbele ya kadamnasi ya watu!, wanasheria makini, waligundua hati zile zilikuwa defective na makosa ambayo hayarekebishiki!, Hati zile zingeonekana zingeufanya mkataba wa muungano kuwa ni void contract, usiorekebishika, ambapo zingeufanya muungano usiwepo abinitio!. Naamini kilichofuatia ni mkataba ule kuchanwa chanwa kuchomwa moto au kutumbukizwa chooni tena kwenye choo cha shimo kwa matumaini, ungetengenezwa mkataba mwingine proper na kusainiwa tena kimya kimya ambao ndio ungepelekwa hata UN!, jambo ambalo halikufanyika hivyo kuufanya huu muungano wetu kuwepo kwenye dhana tuu ya muungano ndio maana tumekuwa tukiyaongeza with no reference ya hati zozote ambazo they don't exist anymore.

Mwenye kujua lolote kuhusu uhalisia hili atujuze,
vinginevyo fuatana nami kuufuatilia Muungano kwa lengo la kuudumisha! na sio kuuchokoa ili kuubomoa!.

Wasalaam

Pasco.

Update: 1Nimefanikiwa kuipata document ya ratification ya Muungano kwa bunge la Tanganyika. Document ya ratification kama hii ilipaswa kuwepo Zanzibar, ila kule haipo!. Hakuna ratification process yoyote iliyofanyika kwa Zanzibar kuuratify muungano zaidi ya kauli ya Karume kwa wanabalozi kuwa BLM limeridhia!. Rafication haifanywi kwa kauli, its a process inayofanyika kwa maandishi kama tulivyofanya Tanganyika!.
paperclip.png
Attached Files


Update: 2
Nimefanikiwa kuipata Document Tanzania iliyoiwasilisha UN kuuthibitisha muungano wetu, ila pia bado kuna maswali bila
majibu, NV hii imeandikwa inawasilishwa akiandamana na mkataba, ila kiukweli mkataba haukuwekwa!.​
paperclip.png
Attached Files


Last edited by Pasco; 31st December 2013 at 06:04.​
Tumsifu Samwel, Abunwasi, Hassan J. Mosoka and 5 others like this.


 
Mbona picha zinaonesha kuwa alisaini? Hafu Zenji nao nchi nzima haikuwa na mwanansheria hata 1 wakat wanafanya mapinduzi?
 
[h=2]
icon1.png
Jee Wajua Kuwa Kuna Uwezekano Tanzania Sii Nchi Halali Kisheria (De Jure) Bali ni De Factor?!.[/h]
Wanabodi,​

Wakati mchakato wa kelekea kwenye Katiba Mpya unakwenda vizuri na sasa ni wazi tunaelekea kwenye serikali tatu,

baada ya miaka hii 50 ya Muungano uliozaa Taifa la Tanzania, tufike mahali tujiulize hivi Taifa letu la Tanzania lipo kusheria (De Jure) au kimabavu tuu (De Factor)?!.
Andamana nami katika ziara hii fupi kukufanyia utambuzi wa uhalali wa Taifa la Tanzania.
  1. Ili taifa lolote liwepo kihalali kwa kisheria (de jure) au isivyo kihalali kisheria lakini lipo (de factor) taifa hilo lazima lijitambulishe Umoja na Mataifa na umoja huo ulipitishe rasmi kama Taifa.
  2. Tanzania nayo pia ilipitishwa rasmi kule UN kama Taifa huru, la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania mnamo tarehe 14 May, 1964 kufuatia kuwasilishwa kwa taarifa rasmi ya maandishi, Note Verbale toka kwa Balozi wa Tanganyika kwenye Umoja wa Mataifa, wakati huo, Chief Arasto Mang'enya na kuitambulisha United Republic of Tanganyika and Zanzibar. Wakati huo, jina la Tanzania halijaanza kutumika. Mwezi June Balozi Mang'enya aliteuliwa rasmi kuwa balozi wa kudumu wa Jamuhuri ya Tanganyika na Zanzibar, na mwezi September ndipo akawasilisha rasmi hati zake za utambulisho na jina rasmi la United Republic of Tanzania.
  3. Hii ni taarifa rasmi ya UN kuhusu kuungana kwa mataifa -MERGER OF MEMBER STATES. During the period under review the issue of the merger of Member States arose in the United Nations in connexion with the formation of the United Republic of Tanganyika and Zanzibar, later called the United Republic of Tanzania. Tanganyika and Zanzibar, which had been admitted which in the United Nations since 14 December 1961 and 16 December 1963 respectively, informed the Secretary-General by a note verbale dated 6 May 1964 of the following:
  4. Hiki ndicho kilichokuwemo ndani ya Note Verbale ile
    " . . . the Republic of Tanganyika and the People's Republic of Zanzibar were united as one Sovereign State on 26 April 1964, under the name of the United Republic of Tanganyika and Zanzi- bar and under the presidency of Mwalimu Julius K. Nyerere. A copy of the said Articles of Union is enclosed herewith.
    "The Secretary-General is asked to note that the United Republic of Tanganyika and Zanzibar declares that it is now a single Member of the United Nations bound by the provisions of the Charter, and that all international treaties and agreements in force between the Republic of Tanganyika or the People's Republic of Zanzibar and other States or international organizations will, to the extent that their implementation is con- sistent with the constitutional position established by the Articles of Union, remain in force within the regional limits prescribed on their conclusion and in accordance with the principles of international law."
  5. On 14 M a y , the Secretary-General, at the request of the Government of the United Republic of Tan- ganyika and Zanzibar, communicated the note to all States Members of the United Nations, to the principal organs of the United Nations and to the subsiding organs of the United Nations to which Tanganyika or Zanzibar had been appointed or admitted, and to the specialized agencies and to the International Atomic Energy Agency, by a note verbale which included the following statement:
  6. Hili ndilo Tamko la Katibu Mkuu wa UN wakati huo, kulitangaza rasmi taifa la Tanzania
    "The Secretary-General is taking action, within the limits of his administrative responsibilities, to give effect to the declaration in the attached note that the United Republic of Tanganyika and Zanzibar, is now a single Member of the United Nations bound by the provisions of the Charter. This action is undertaken without prejudice to and pending such action as other organs of the United Nations may take on the basis of the notification of the establishment of the United Republic of Tanganyika and Zanzibar."
  7. Hivyo msingi mkuu wa Taifa la Tanzania ni zile hati ambazo zimeelezwa kuwasilishwa na lile tangazo la Balozi, swali ni jee Hati hizo, ziliwasilishwa?, kwanini hazikuwasilishwa?, bila hati hizo Tanzania bado ni taifa?. Uhalali wa Tanzania kama Taifa bila hati ukoje?.
  8. Wakati wa Kipindi cha Rais Benjamin Mkapa nilibahatika kwenda UN, na nikaenda ubalozi wetu kunusa nusa tuu kama hizo hati zinaonekanika, nikashindwa kufuatia urasimu fulani. Wakati wa Kipindi cha JK nikaenda tena pale pale ubalozini, this time receptionist ni shemeji yetu (mke wa member mwenzetu wa jf), nikaomba appoinment kumuona balozi bila mafanikio!. Hata hivyo nilipokwenda maktaba ya UN, Note Verbale ile ipo, ila hakuna hiyo attachment ya Articles of Union!. Hivyo swali la kujiuliza jee kuna nini kuhusu hizi articles hadi zisiwepo?!.
  9. Ukweli ni kuwa au hiki kitu kinaitwa Mkataba wa Muungano, "Articles of Union" sio mkataba halali, (Contract) bali ni makubaliano tuu "agreement" ya Muungano, tofauti kati ya Mkataba (Contract) na Makubaliano (Agreement au MoU) ni kuwa mkataba uko kisheria zaidi unavipengele vya kisheria na unatawaliwa na sheria, (legal binding) wakati makubaliano yanategemea mapatano tuu na maelewano, hakuna legal binding ya mapatano japo yakisajiliwa kisheria yana legal binding ya kimapatano na sio kimkataba!. Jee kwa nini hizi "Articles of Union" naziita ni mapatano tuu na sio mkataba?!.
  10. Ili makubaliano yoyote yaitwe mkataba ni lazima yawe na sifa kuu 4 za mikataba, zinazoitwa vipengele, na kikikosekana kimoja wapo cha sifa hizo, then huo sio mkataba bali ni makubaliano tuu ambayo nayo ni halali. Makubaliano hayo ya Muungano hayana zile sifa kuu 4 za mkataba. Jee sifa hizo kuu 4 za mkataba ni zipi?!. (Hii sio thread ya contents za Hati za Muungano bali presence ya hati hizo). Ili kujua kwa nini hati za muungano sio mkataba bali ni makubaliano, then itakubidi unitembelee hapa!- Jee Wajua Kuwa Tanzania Hatuna Mkataba wa Muungano?. Kilichopo ni Makubaliano Tuu!.
  11. Kufuatia uwezekano wa Taifa la Tanzania kuwasilishwa kwa NV tuu bila Mkataba wowote wa Mungano, hivyo ile nchi ya Tanzania iliyopo UN ni Tanzania De Facto na sio Tanzania De Jure. Ila kuwa inchi, Tanzania bado ni nchi, iwe de jure au de facto bado ni nchi!. Yaani inchi yetu imekalia kiti cha UN kama De Jure, kumbe infact ni De Factor, hivyo uanachama wenu UN could be a lie!. We are existing a lie, living a lie and continue lying!.
  12. Hivyo kufuatia huu mchakato wa katiba mpya, turekebishe makosa, lets make things right kwa Tanzania kuwa na Mkataba halali kabisa wa Muungano ambao njia pekee ya kuupata ni kupitia referandum, hivyo wakati tukipiga kura ya katiba mpya, tuupigie na muungano!.
Suala hili bado linahitaji uchunguzi wa kina na uthibitisho pasipo shaka, kwa vile mwakani nitakuwa na safari binafsi ya US, this time nitafanya juhudi za makusudi kupita tena Ubalozi wetu pale UN na kutembelea tena Maktaba ya UN kuziona hizo "Hati za Muungano!

Asanteni.

Pasco.
paperclip.png
Attached Files
 
[h=2]
icon1.png
Jee Wajua Kuwa Tanzania Hatuna Mkataba wa Muungano?. Kilichopo ni Makubaliano Tuu ya Muungano?!.[/h]
Wanabodi,​

Wakati tukijiandaa rasmi kuingia kwenye serikali 3, tutake tusitake, lazima tutarudi nyuma kuungazia muungano wetu, na kabla hatujaingia katika serikali tatu, lazima kwanza tuwe na Mkataba rasmi wa Muungano, ndipo zifuate hizo serikali 3. Hiki kilichopo, kinaichwa Mkataba wa Muungano, "Articles of Union", kiukweli, nasema bila kumung'unya maneno, sio Mkataba wa Muungano (contract), bali ni Makubaliano ya Muungano (Agreement) tuu.

Kuna tofauti kubwa kati ya Mkataba na Makubaliano, kila mkataba ni makubaliano, ila sio kila makubaliano ni mkataba!. Yaani "Every contract is agreement, but not every agreement is a contract!".

Ili makubaliano yaitwe mkataba, ni lazima makubaliano hayo yawe na sifa kuu nne za mkataba. Kwa bahati mbaya sana, Makubaliano ya Muungano wetu, yamekosa baadhi ya sifa hizo muhimu.

Ambatana nami katika kuyachambua haya makubaliano ya muungano kwa nini ni makubaliano tuu na sio mkataba, na niu kwa nini lazima kwanza tuwe na mkataba wa muungano ndipo tuweze kwenda kwenye serikali tatu.

Kwa wale wenye nafasi, mnaweza kuanza kuyapitia haya makubaliano ya muungano, kisha tutapelekana kidogo kidogo kwa lugha rahisi kwa kila mtu kulielewa hili.

NB. Mambo mengine, yako kisheria zaidi, ila bado I stand to be corrected na "the learned brothers and sisters"

Kwa wale ambao sio wanasheria, unaweza pia kuwa mwanasheria bila kusomea chuo chochote

kwa kuanzia jisomee mwenyewe
  1. What is a contract?
  2. What is an agreement?
  3. What are the differences between Contacts and Agreements?
  4. Why every contract is an agreement but not all agreements are contracts
  5. Baada ya kusoma hayo hapo juu, tunaweza kwenda pamoja kujua kwa nini makubaliano ya muungano sio mkataba
NB. Japo makubaliano haya ya muungano sio mkataba, na japo hayakuridhiwa rasmi Zanzibar (ratification), bado ni makubaliano halali, hivyo muungano wetu ni halali na nchi yetu Tanzania ni nchi halali (de facto) ila sio halali kisheria (de jure).

Karibu uandamane nami.
Pasco.

Up Date !.

Happy New Year!

Pasco.
paperclip.png
Attached Files
 
[h=2]Je, wajua kuwa Zanzibar haikuridhia Muungano? Ina Maana Gani?[/h]
Wanabodi,

Kufuatia chokochoko ya kuuchokoa Muungano ilioanzishwa na kikundi cha Uamsho huko Zanzibar, zimeanza kutolewa hoja mbalimbali ikiwemo Watanzania tupewe fursa kuujadili Muungano na ikibidi ipigwe kura ya maoni kuwauliza Watanzania na Wanzanzibari kama wanautaka muungano, jee wanataka muungano wa aina gani, na endapo hawautaki, process ya kuuvunja rasmi aianze.

Wako wengi wanaupenda muungano na wangependa uendelee ila uboreshwe!. Pia wako wanao ona sasa imetosha na muungano uvunjwe!.

Maudhui ya mada hii ni kuwaeleza wanabodi, jambo muhimu liitwalo "kuridhia" ambapo serikali zote zilipaswa kuuriidhia huo muungano kwa utaratibu unaoitwa "RATIFICATION" ambapo ni serikali ya Tanganyika pekee ndio iliyofanya process rasmi ya "ratification", Zanzibar, haikufanya process bali ilitamka tuu kwa maneno ya mdomo bila tamko lolote rasmi la maandishi, na badala yake, hati ya ratification ya Zanzibar, iliwasilishwa kwenye bunge la Tanganyika na dunia kutangaziwa muungano uliridhiwa pande zote!.

Kwa vile Zanzibar, haikuuridhia rasmi Muungano, kama ni kweli hizi chokochoko za Uamsho ni uthibitisho kuwa sasa Zanzibar inataka kujitoa katika muungano wetu huu adhimu, kisheria, mlango uko wazi, yaani wide open for Zanzibar to just walk out, with no regret and no strings attached kwa sababu hawakuuridhia ule mkataba wa muungano in then first place!, hivyo mkataba huo hauko binding kwao!.

Mada yangu hii inakuwa na sehemu zifuatazo.

1. Kuridhia ni Nini (Ratification).
2. Rafication Hufanyikaje.
3. Mikataba ya Kimaifa ni nini? na Jee Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar ni Mkataba wa Kimataifa?.
4. Muungano wa Tanganyika na Zanzibar
5. Process ya Ratification kwa Upande wa Tanganyika.Process ya Ratification kwa Upande wa Zanzibar.
6. Hadaa ya Ratification ya Zanzibar, ilipangwa na nani na kwa nini?.
7. Kukosekana kwa ratification upande wa Zanzibar kunamaanisha nini.
8. Pamoja na kutokuwepo ratification, Jee Muungano ni halali?
9. A Way Forward 1:Tudumishe Muungano?, Muungano wa Aina Gani?.
10. A Way Forward 2:Tuuvunje Muungano?. What are the Consequences?.

1. Kuridhia ni Nini (Ratification).
Kuridhia, au ratification, ni process inayofanywa kwa nchi husika kuridhia mikataba ya kimaifa ili kuipa uhalali wa kisheria kutumika katika nchi husika. Mfano mzuri ni mkataba wa Muungano baina ya Tanganyika na Zanzibar, Tanganyika ni nchi, na Zanzibar ni nchi, hivyo ule mkataba wa muungano ni mkataba wa kimataifa.

Jee kila mkataba wa kimataifa ni lazima uridhiwe?. Jibu ni hapana, sio kila mkataba wa kimataifa ni lazima uridhiwe, ili mkataba wa kimataifa uridhiwe lazima mkutaba husika uwe na kipengele kinacholazimisha mkataba huo kuridhiwa. Tukirudi kwenye mfano wetu wa mkataba wa muungano, kipengele cha VIII cha Articles of Union, kinalazimisha process ya ratification lazima ifanyike ili kuuhalalisha mkataba ule.

(viii) These Articles shall be subject to the enactment of laws by the Parliament of Tanganyika and by the Revolutionary Council of the Peoples' Republic of Zanzibar in conjunction with the Cabinet of Ministers thereof, ratifying the same and providing for the Government of the united Republic and of Zanzibar in accordance therewith.


Nyerere na Karume wangeweza kuamua wakishasaini makubali yale iishie hapo, ingekuwa hivyo hivyo hitaji la kuridhia lisingekuwepo!.

2. Rafication Hufanyikaje?.
Kwa vile mikataba yote ya kimataifa ni lazima iwe ni ya maandishi, vivyo hivyo, ratifikation lazima ifanyike kwa maandishi na sio kwa kauli.

Kwa bunge letu, masharti ya kuridhia hufanywa kwa mujibu wa kifungu cha 63(3)(e) cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kinachotamka kuwa, Bunge litajadili na kuridhia Mikataba yote inayohusu Jamhuri ya Muungano na ambayo kwa masharti yake inahitaji kuridhiwa na kwa mujibu wa Kanuni za Bunge, Kanuni ya 114(11) ya 2007.
1. Waziri husika huwasilisha mezani kwa spika mkataba husika
2. Spika ataipa kamati husika kupata maoni yake
3. Kambi ya upinzani itapewa fursa ya kuandaa maoni yake.
4. Mkataba huo utatangazwa rasmi kwenye order paper ya siku ya kuwasilishwa
5. Waziri atawasilisha, kisha maoni ya kamati, maoni ya kambi ya upinzani na majadiliano.
6. Bunge litakaa kama kamati kupitia kifungu kwa kifungu
7. Bunge litarudi kama bunge na kuridhia mkataba husika
8. Mkataba huo unakuwa sehemu ya sheria za nchi,
9. Unasainiwa na rais na kutangazwa katika gazeti za serikali GN.
10.Ndio unakuwa umeridhiwa, yaani ratified!.

3. Mikataba ya Kimaifa ni nini? na Jee Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar ni Mkataba wa Kimataifa?.
Mkataba wa Kimataifa, ni mkataba kati nchi moja na nchi nyingine, au mikataba yote ya jumuiza za kimataifa ambayo nchi ama hutakiwa kuridhia, au kulazimishwa kuiheshimu hata kama haikuridhia. Mikataba hii au itifaki mbalimbali (protocals), hupaswa kuridhiwa kabla haijawa sheria kwa nchi husika.

Mfano Tanzania iliridhia mkataba wa mahakama ya kimataifa ya Biashara, ICC. Dowans iliposhinda ile kesi, imepaswa kuisajili hukumu hiyo kwenye mahakama zetu (ratification), ili hukumu hiyo igeuke sheria zetu, (domestic law) na kutekelezwa. Watu humu walipiga sana kelele, nilipouangalia mkataba ule humu jf, nikawaambia wana jf wenzangu, hatuna pa kutokea, tozo ile italipwa tuu mara baada ya tozo hiyo kusajiliwa, kinachoendelea sasa ni delaying tactics ambayo nayo tutailipia dearly!.

Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar, ni mkataba halali wa kimataifa wenye sifa muhimu za mkataba, japo una mapungufu mengi kubwa likiwa ni kitu kinachoitwa "Privity of Contrac" ambapo mkataba ulikuwa kwa lugha ya Kiingereza na signatory mmoja alikuwa msomi anaejua kusoma na kuandika kiingereza, wakati signatory wa pili hakujua kusoma, kuandika wala kiingereza, hivyo alisaini kwa dole gumba!.

Ufafanuzi zaidi kuhusu Muungano kuwa ni mkataba wa kimataifa, unapatikana pia katika ukurasa wa kwanza wa andiko la
Prof. Shivji kwenye kitabu cha "The Legal Foundation of the Union in Tanzania and Zanzibar Constitution, DUP, 1990.

Kwa faida ya wasoma kimombo, tembelea
http://www.scribd.com/doc/45109599/T...A-AND-ZANZIBAR

4. Muungano wa Tanganyika na Zanzibar
Kila mtu anaelewa Mkataba wa Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar, ulitiwa saini na Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Abeid Amani Karume, Aprili 22, 1964, Mjini Zanzibar Hapa nitawapa tuu ilivyokuwa kabla na kilichofuata.
Baada ya Mapinduzi ya Zanzibar, na Nyerere kumsaidia Karume kumshughulikia Johh Okello, Karume alikuwa bado ana wasiwasi wa kudumu kwake kama Mwenyekiti wa BLM, kwa kuzingatia Karume hakushiriki mapinduzi yale, Kiongozi wa mapinduzi alikuwa ni John Okello, Karume alikimbilia bara kujificha! (Japo ilikuja kutangazwa ati alikuwa akiwapeleka wanae Amani na Ali waliokuwa wakisoma kwao Karume (Malawi). Okelo ndie alikuwa Mwenyekiti wa BLM na alimuita Karume kuwa mtangazaji kufuatio kuwa na Kiswahili safi. Karume akamzunguka Okello na kwa kusaidiwa na Nyerere, Okello alishughulikiwa na Karume kuitwaa nafasi ya Mwenyekiti wa BLM!.Kwa vile Karume hakushiriki actively kwenye mapinduzi halisi, alikuwa na wasiwasi wakati wote kuwa wale makamanda wangemrudi!, thanks kwa ulinzi wa askari 300 wa Nyerere, vinginevyo hata hiyo 1971, asingefika!.

Mwezi Machi, 1964, Nyerere alizungumza na Karume kuhusu Muungano, Karume alikubali hapo hapo na kutaka Press Conference iitishwe siku hiyo hoyo watangaze kuwa wameshaungana na kuwa nchi moja, Nyerere Rais, Karume Makamo. Mwalimu alimgomea Karume na kumwambia afanye siri ili taratibu zifuatwe.

Mwanzoni mwa Aprili, Mwalimu alimuita AG waTanganyika, Rowland Brown na kumwambia aandae mkataba wa muungano na uwe siri. Kule Zanzibar, Karume akampa likizo AG wa Zanzibar, Wolfgang Dourado ili isitie kauzibe. Akatafutwa Mwanasheria wa Uganda, Daniel Wadada Nabudere (kakaye mwandishi mashuhuri, David Wadada Nabudere) kutoa ushauri kwa Karume kuhusu muungano.

Tarehe, 22 April, 1964 Nyerere aliyeandamana na Rashidi Kawawa, Oscar Kambona na Job Lusinde walitua ghafla Zanzibar na kwenda moja kwa moja Ikulu ya Zanzibar, wakiwa na hati za muungano na Karume alitakiwa azisaini. Wakati wa utiaji saini huo, ulishuhudiwa pia na Abdallah Kassim Hanga, Abdul-Aziz Ali Twala na Salim Rashidi.

Karume alitaka kumtumia mwanasheria huyo wa Uganda kusaini kwa niaba ya mwanasheria mkuu wa Zanzibar, ila Nabudere akakataa na kusisitiza lazima zisainiwe na Mwanasheria wa Zanzibar!. Ndipo Rowland Brown akatinga na Solicitor General wa Tanganyika, PRN Fifoot aliyesimama nafasi ya Dourado!. Hati za muungano zikasainiwa!. Baada ya hapo Nyerere na ujumbe wake wakawaa pipa lao na kurejea Dar!.

Mkumbuke mpaka Karume anasaini, hajaliambia chochote BLM, siku hiyo jioni Aboud Jumbe aliyekuwa Pemba, ndipo akaelezwa na Karume kilichotokea asubuhi, akashangaa sana!. Jambo kubwa kama hilo limefanyika vipi, BLM, hawajui kitu!.

Ni baada ya kusainiwa, Bunge la Tanganyika likatunga sheria ya Muungano, ili kuuthibitisha hati zile, 'ratification', na BLM nalo lilipaswa kukaa na kuridhia hati zile!.

Muungano Ulithibitishwa rasmi na Bunge la Tanganyika kwa kutungiwa sheria na na ikatolewa uthibitisho mwingine uliosainiwa na Fifffoot kuonyesha kuwa BLM liliketi na kuridhia, lakini kiukweli BLM halikukaa, kujadili, wala kupitisha chochote kule Zanzibar!. Kila kitu kilifanywa bara!.

Aprili 27, 1964 Nyerere na Karume, walitinga katika ukumbi wa Karimjee, jijini Dar es Dalaam kubadilishana hati za Muungano zilizosainiwa na Nyerere na Karume, na documents za ratification na tangu hapo Tanganyika na Zanzibar kuwa dola moja kwa misngi inayotambulika kimataifa. Baada ya kuungana, Mwalimu Nyerere alikuwa rais wa kwanza na Karume alikuwa makamu wa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Siku hiyo ya Aprili 27, 1964 ndio siku wajumbe saba wa Baraza la Mapinduzi waliapishwa kuwa wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano Watanganyika na Zanzibar ambao ni Amani Karume, Kassim Abdallah Hanga, Abdulrahman Babu, Hassan Nassor Moyo, Aboud Jumbe, Hasnu Makame na Idris Abdul Wakil. Kati yao, Aboud Jumbe na Hassan Nassor Moyo wangali hai. Baada ya hapo, Bunge la Muungano likakamata madaraka yote!.

5. Process ya Ratification kwa Upande wa Tanganyika.Process ya Ratification kwa Upande wa Zanzibar.
1.
Msingi mkuu wa ratification mkataba wa muungano ni kifungu hiki kwenye hati za muungano.

Article VIII of the Articles of Union provides:" These Articles shall be subject to the enactment of laws by the Parliament of Tanganyika and by the Revolutionary Council of the Peoples Republic of Zanzibar in conjunction with the cabinet of ministers thereof, ratifying the same and providing for the Government of United Republic and of Zanzibar in accordance therewith2. Lengo la kifungu hicho, ni kwa vile muungano ni mkataba wa kimataifa, ili mkataba huo upate uhalali wa kisheria katika nchi husika, lazima mkataba huo uridhiwe na nchi husika, hivyo kifungu hicho kilimaanisha bunge la Tanganyika na Baraza la Mapinduzi, walipaswa waridhie mkataba huo kwa kuutungia sheria mahsusi ili kuuhalalisha kisheria ndani ya nchi zao!.

2. Kuridhia au kutoridhia, hakuondoi uhalali wa mkataba, bali unaondoa uhalali wa kisheria, pale yule ambaye alikosa uhalali wa kisheria pale mwanzo, akiamua hautaki tena ule mkataba, hawajibiki kuuvunja mkataba, but he can just walk away!.

3. Baada tuu ya hati za Muungano kutiwa saini ile Aprill 22 kule Zanzibar, Mwanasheria Mkuu Tanganyika enzi hizo, Rowland Brown aliandaa ratification na kupelekwa kwenye kikao cha bunge la Tanganyika, likapitisha ratification ile asubuhi ya Aprili 26, 1964 kwa kutunga sheria No. 243 ambayo ilitangazwa kwenye gazeti la serikali ya Tanganyika, GN No. hivyo kutimiza matakwa ya kile kifungu namba viii cha mkataba wa muungano.

4. Wakati hayo yakiendelea huku Tanganyika, Zanzibar nao kupitia Mwanasheria Wake Mkuu, Wolfgang Dourado, alipaswa kuandaa hiyo sheria ya ratification kule ikiitwa Decree, ili Baraza la Mapinduzi likae na kuipitisha hivyo kuutambua rasmi muungano kisheria. Hili halikufanyika lkwa sababu Dourado alipewa likizo ya siku 7 akapumzike nje ya nchi!. Aliporudi, seven day leter, akakuta game over!. Akaishia kulalamika kichini chini maana angetoa sauti, sijui kama hata unywele ungepatikana!. Ushahidi ni kauli ya Dourado Mwenyewe "I myself have been the Zanzibar Attorney General and Minster responsible for justice between 1984 and 1989. At that time I managed to peruse all the statute books of Zanzibar from 1964 and 1979 when the Revolutionary Council was acting as a legislative Assembly cum the Cabinet. No ratification law or any law to that effect is there. I was not myopic, but even if I was, the first Attorney General of Zanzibar after the Revolution had also testified the same that no law ratifying the Articles of unionexists on the Statute Books of Zanzibar." Dourado aliyasema hayo katika andiko lake la "The Consolidation of Union" alilowasilisha kwenye semina ya Tanhanyika Law Society, Julai 7, 1983 hapa jijini Dar es Salaam.

5. Mpaka Mungu amemuita Dourado mbele ya haki, msimamo wake ulikuwa "No law ratifying the Articles of the union of 1964 exists on the statute books of Zanzibar., I as a Principal Legal adviser to the Zanzibar government was not consulted ……… Zanzibar therefore did not have legal or constitutional advice from its Principal Legal adviser."

6. Badala yake, Solicitor General wa Tanganyika, PRN Fifoot ndiye alieandaa ratification document ya Zanzíbar ambayo aliisaini yeye na kumpatia Karume ile April, 27, 1964, Karume aiwasilishe kwenye bunge la Tanganyika ile siku Nyerere na Karume walibadilishana hati pale Karimjee. Hati ya aliyoiwasilisha Nyerere was a genuine ratified document iliyokuwa ratified na bunge la Tanganyika!. Hati aliyowasilisha Karume, was a fake one as if ni BLM ndilo nalo limefanya hiyo rafication kama lilivyofanya bunge la Tangayika!, It was just a make belive, kuizuga jumuiya ya kimataifa na hapo ndipo hata hao CIA na iteligensia yao wakaingizwa chaka na kubaki kupiga tarumbeta ya ratification kuwa ilifanyika!.

7. Hata kama Fifoot aliiandaa hiyo ratification ya Zanzibar, kwa nini hakumpa Douradau naibu wake, ili aisaini na kuipitisha kwenye kikao cha BLM ili angalau ionekane ilipitishwa Zanzibar?!.Kwa vile Zanzibar hawakuwa na bunge, Baraza la Mapinduzi ndilo lililokuwa Bunge, Baraza la Mawaziri na Mahakama, kwanini ile ratification iliyoandaliwa bara, isipelekwe tuu na kupigwa rubber stamp kwenye BLM ili kuipa uhalali kuwa ni kweli BLM waliridhia na kuratify?!.

8. Siku ile ya April 27, 1964, wakati Nyerere na Karume walipotinga ndani ya bunge la Tanganyika, kubadilishana hati za muungano zilizo kuwa ratified,Nyerere aliwasilisha hati halali ya muungano ilikuwa ratified kihalali na bunge la Tanganyika na kutangazwa rasmi kwenye gazeti la serikali, GN lakini Karume aliwasilisha ile hati iliyosainiwa na Fifoot alijifanya Dourado na kuziwasilisha hati za muungano kwenye bunge la Tanganyika as if ni kweli BLM lilikaa likajadili na kuridhia hizo hati za muungano, na Karume sio tuu amesaini hizo ratification bila kuzipitishia BLM, bali pia amezitungia Decree na kuitangaza katika GN hiyo hiyo ya Tanganyika japo kwenye GN ya Zanzibar sheria hiyo haipo!.

9. Kisheria, kwenye sheria ya mikataba, place of contact maters much as far as domestic laws are concerned, Ule mkataba wa muungano ni international contract, unaweza kusainiwa popote ndio maana Mwalimu Nyerere na time yake, walifunga safari kwenda Zanzibar. Process ya ratification sio international contact, ni domestic contact kutumia domestic laws (municipal) ambapo ratification hupaswa kufanywa na bunge husika likiwa nchi husika. Bunge la Tanganyika lilitimiza wajibu wake hivyo ratification ya Tanganyika ni legal. Kitendo cha ratification ya Zanzibar kuandaliwa na Fifoot wa Tanganyika na kusainiwa nae, halafu Karume kukabidhiwa sheria hiyo wakati sgeria za Zanzibar kwa wakati huo zilikuwa Decrees na kuiwasilisha bunge la Tanganyika, tangazo la ratification kutolewa kwenye GN ya Tanganyika na sio ya Zanzibar, ni mambo yanaifanya hiyo ratification kuwa voidable na sio void!


10. Hoja ya "privity' to contract na "capacity" to contract pia ipo kwa Karume kama Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, alikuwa na capacity to contact kama Karume kwenye zile articles of union, lakini kwenye Ratification, Karume hakuwa na Capacity ya kusaini sheria ambayo haikutungwa na BLM, na kusainiwa na Fifoot badala ya Dourado, na sheria hiyo kutopitishwa na BLM lakini akaiwasilisha as if imeridhiwa na BLM!, na Fifoot hakuwa na capacity to contract kwa niaba ya Dourado!, tena (ninahisi Fifoot alifanya "misrepresentation kujifanya Dourado ndio maana kuna uwezekano mkubwa, Karume hakupewa tena zile original documents!, alikuja mikono mitupu, na kurudi mikono mitupu ndio kule Zanzibar, hizo documents are no where to be seen!!). Emphasis mine!
11. Hata hivyo, kuna mabishano makubwa kati wanazuoni na wasomi mbalimbali wa sheria kuhusiana na hii issue ya ratification. Mwalimu wangu, Prof. Shivji amesema japo hakuna kumbukumbu zozote kuwa BLM liliridhia, kwa vile BLM limeipitisha sheria ya muungano, huko ndiko kuridhia kwenyewe!, kwa hiyo kwa Shivji, muungano uliridhiwa!.

12. Aliyekuwa kiongozi wa kambi ya upinzani kwenye BLW, Hon. Abubakar Khamis Bakary ambaye ndie aliyetoa posa ya ndoa na CCM kule BLW na kuunda SUK ambapo kama mshenga, amezawadiwa uwaziri wa sheria anapingana na Prof. Shivji kwa kusema kuwa sheria ambayo haikutungwa na BLM wala haikupitishwa na BLM, sio sheria halali kwa Zanzibar!.

13. Pamoja na Kutofautiana na Shivji kuhusu uhalali wa ratification, lakini Mhe. Bakari anakubaliana na Shivji kuwa muungano ni halali, kwa sababu, licha yakutokuwepo official ratification kutoka Zanzíbar, hakuna Wanzanzibari wowote waliochukua hatua zozote za kupinga au kulalamika, hivyo hiyo ni dalili kuwa Wanzanzibari wameukubali muungano impliedily not expressly!.

14. Mwanasheria mwingine wa Zanzibar, al maaruf, Ali Salehe, mwandishi na mtangazaji wa BBC, yeye anashikilia, kwa kwa vile muungano haukuridhiwa, lazima uridhiwe ili kuupa nguvu ya kisheria Zanzibar!. Hivyo anasema ratification ifanyike!. Na hapa ndipo na mimi niliposimamia kuwa Wanzanzibari wafanye ratification kama kweli hawautaki tena muungano, BLW likatae ku ratify ili mlango wa kutokea uwe wazi, wide open!.

15. Prof. Haroub Othman ametofautiana na Shivji kwa kusema wajumbe wawili wa BLM, Abrahman Mohamed Babu na Khamis Abudulah Ameir, walimweleza kuwa BLM walijadilili hati za muungano na kuridhia! (bila maandishi wala kumbukumbu?). Prof. Haroub anadai siku anaelezwa hayo walikuwa club ya YASU akiwa anacheza na katoto fulani ambacho kalikuwa bado hata hajabalehe, kakiitwa Ali Juma Shamhuna!.

16. Kufuatia uwepo wa document ya ratification huku bara, na Zanzibar kimataifa ilikufa rasmi siku ile ya April, 26, 1964, hakuna tena anaejali kama hizo ratification documents zili fojiwa huku bara, ndio maana hata tume ya Nyalali, ilizihalalisha na kimataifa everthing is ok na humo humo ndimo hao majasusi wa Marekani, walikolalia na wote wanaoamini muungano uliridhiwa, japo ni kweli kwa bara muungano uliridhiwa kwa kauli na matendo, kwa Zanzibar, uliridhiwa kwa kauli bila matendo!, na sasa tunasikia kauli za kupinga na matendo ya akufukuzaye!.

17. Kiukweli Karume aliliendesha BLM kibabe sana, yeye kama Rais, Jaji Mkuu na Spika, wale wote waliopingana naye, hakuna ajuaye kilichowakuta ili walishughulikiwa kimya kimya na hata miili yao haikubahatika kuonekena (inasemekana walining'inizwa jiwe shingoni na kutoswa baharini!. Kina Babu kuona hivyo, wakajitimkia zao kabla ya kuwakuta, hayajawakuta. Uvumilivu ulipowashinda waliobaki, nao wakamshughulikia Karume!. (Naamini inteligensia ya Mwalimu alishauona mwelekeo wa Karume kwenye majaaliwa ya muungano, hivyo nae akaacha ya kumkuta yamkute, muungano udumu!.

18. Baada ya Karume, Aboud Jumbe akaukwaa urais. Dourado akamjulisha Jumbe kuhusu kukosekana kwan proper ratification na iliyopelekwa UN is fake!, wakaandaa document kuujulisha ulimwengu kuhusu hilo!. Seif Sharif akamtonya Nyerere, Jumbe akashughulikiwa ipaswavyo, huku Dourado akaozea jela!.Tukatangaziwa "kuchafuka kwa hali ya hewa Zanzibar" bila kuelezwa kisa ni absence ya proper ratification!.

19. Wanzanzibar ni watu wazito sana kujifunza, licha ya kujua kilichomkuta Jumbe kilihusu kuutishia muungano, Dr. Salmini nae akataka kucheza karata yake zile siku zake za mwisho mwisho alinukuliwa akisema, wao wanayatambua yale mambo 11 tuu ndio ya halali, hivyo akajenga hoja kubadili katiba aongeze kipindi cha tatu ili ayashughulikie!. Tiss ilimshughulikia yeye na timu yake yote wakatupwa kando!. Hamshaghai kwa nini Salmin baada ya kustaafu hakuitwa popote kuwa mgeni rasmi kwenye shughuli rasmi?, na yule dada yetu naye akaporwa!.

20.Kupitia hoja hizo na nyingine ambazo sikuzitaja, Mimi Pasco wa JF, kwa Mamlaka niliopewa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Chini ya Kifungu cha "Freedom of Expressions", Sasa Natamka Wazi kuwa Muungano Kati ya Tanganyika na Zanzibar, Haukuwa Ratified Properly in Zanzibar!. Ila pia Nasisitiza, Muungano Huu ni Halali, japo ulikosa uhalali kwa njia ya Expressly in Zanzibar, umepata uhalali huo Impliedly!.


Angalizo.
Unaruhusiwa kucoment chochote wakati mada hii ikiteremka, just coments tuu ila naomba sana, maswali juu ya kuhusu hii mada kabla sijafika mwisho, maana sitakujibu mpaka nimalise, ila nikishamaliza sura zote kumi, nitapokea maswali, maoni au mapendekezo. Endepo uliuliza swali kabla sijafika mwisho, na hatimaye ulikuja jibu la swali lako kwenye mada za mbele, sitakujibu upya bali nitakurefer kwenye majibu ya swali lako.

Hii mada siyo accademic paper, naishusha kwa level ya mwananchi wa kawaida wa Tanzania ambaye ni darasa la saba!. Hata hivyo kwa faida ya wasomi ambao wangependa kuzama deep, mwisho, nitawawekea, references za kusoma zaidi.

Natanguliza shukrani.

Pasco.​
 
Back
Top Bottom