Karume hakusaini hati ya muungano

Karume hakusaini hati ya muungano

Mbona hizo barua za kiintelijenia hazioneshi kuwa Muungano haukusainiwa, bali zinaoshwa kuwa mkutano umeridhiwa na Karume na Barazza la Mapinduzi.

Nnachokiona kinachoashiria kuwa "order" ya muungano haijasainiwa ni hilo gazeti tu.

Well, its time Zanzibar au Tanzania Bara walete orijino document otherwise huu muungano una kila dalili za kuwa ni batili.
 
Halafu tunaambiwa muungano ulifanywa kwa maslahi ya wananchi. Jamani tuachiani tuamue sasa kipi kizuri kwetu na sio kwa faida ya viongozi waliopita!

Hata sasa hivi ukisikiliza kwa makini (between the lines) hoja za watawala kutetea muungano wa serikali mbili, haikuchukui dakika moja kugundua kuwa wanatetea maslahi yao kama kundi la watawala na kwa matarajio kuwa ni familia hizo hizo zitakazoendelea kutawala.
 
nakala halisi lazima itakuwa na contents za ovyo sana, ndio maana inafichwa kivile ili wananchi tusijue yaliyomo.
 
Kuna fact moja inarukwa na wanahistoria na waandishi wengi wa suala hili la muungano nalo ni kumzika mzee job lusinde akiwa hai. Job malecela lusinde(kaka wa j.s malecela) waziri wa mambo ya ndani na usalama wa taifa wa tanganyika by then ndiye mtanzania na mtanganyika pekee aliyeshiriki process ya utiwaji saini articles of union tangu na kabla ya tarehe 22.04.1964 ikiwa ni siku 4 kabla ya kuzaliwa kwa muungano huo tarehe 26.04.1964. Job lusinde yuko hai na ana nguvu kiasi na kumbukumbu za kutosha japo huwa hayuko tayari kueleza habari za muungano na maasi ya jeshi ya mwaka 1964. Akiwa mtanzania pekee aliyebaki anayejua drama nzima ilivyochezwa akiwa msiri mkubwa wa jk nyerere, mwana usalama waziri anajua the real truth than you can imagine. Basi aulizwe na atupe majibu kwani yeye na kambona walitangulizwa zanzibar kwa karume siku 2 kabla nyerere na bokhe munanka hawajatua zanzibar kumaliza mchezo mzima. Balozi lusinde moyo wake una siri nzito sana, yupo kilimani-dodoma
 
Hati ya Muungano haina utata. Tatizo ndugu zangu ni kwamba baadhi yetu hatuelewi utaratibu unaotumika wakati wa kutaka nyaraka za serikali kwa ajili ya rejea.

Hati yoyote ile ya serikali kama ilivyo hiyo ya Muungano inakuwa ni halali tu kama imetiwa saini na Katibu wa Bunge kwani ndiye mhifadhi wa nyaraka zote zile ikiwa ni pamoja na sheria zitumikazo katika mahakama.

Nyaraka hizo huwa hazina saini ya waliozisaini mwanzo bali zinakuwa na lakiri na saini ya Jatibu wa Bunge wa kipinfi husika. Waraka uliopelekwa katika kamati ya bunge maalum majuzi ilikuwa batili kwani haikutoka kwa Dkt Kashilila kama inavyotakiwa kisheria.

Kuhusu utaratibu na uhalali wa nyaraka za serikali wasiliana na Dkt Kashilila au Jaji Werema. Nyaraka zinazosambazwa na kufanyiwa tathmini si halali ni feki na zimetoka katika maktaba zetu za majumbani na si kopi ya serikali ambayo inatoka kwenye halisi iliyopo ofisini kwa Katibu wa Bunge.
 
Mjomba hizo ni habari tu za kintelijensia zilionyesha jinsi Muungano ulivyoanzia tena kwa maneno hapajakuwa na ushahidi hata mmoja wa kisheria, hizo document zote just ni intelligence information, wala sio mkataba wa Kisheria....
 
Mhh...mkuu kazi kweli kweli...tukifanya usanii na katiba mpya tu dalili hizi si nzuri
 
Njia nyingine rahisi ya kutafiti kuhusu nyaraka za kiserikali ni kupitia nyaraka zote zilizoandikwa katika kipindi husika. Je kuna mtu anaweza kuleta Nyaraka za Baraza la mapinduzi katika kipindi chote kuanzia Januari mwaka 1964 had November mwaka 1964 ambapo ndipo Jina la Tanzania lilipoanza kufanya kazi? At least tumeshaona waraka mmoja wa kutoka kwenye bunge la Tanganyika ukiwa na addendum ya articles of the Union na tumeshaona picha nyingi za Karume na Nyerere wakisaini makubaliano hayo. Hata kama huo waraka huo haupo, ni vizuri tunyeshwe nyaraka nyingine zilizofanyika hapo katikati kwa vile zitainyesha iwapo zilikuwa zinatambu muungano au vipi.
 
Kama haya ya kweli hivi wambunge wa CCM Zanzibar nani kawaronga au ni hizo laki 3 zimewakosesha uzalendo? wakati ndio huu tuweke kila kitu wazi, mpira urudishwe kwa wananchi kama tunataka Muungano au la na kama ndio ni Muungano wa serikali ngapi? Kama Taifa yatubidi tuanze upya tusiendelea kuweka uchafu uvunguni wa kapeti maana kwa sasa tuko uchi..
 
Njia nyingine rahisi ya kutafiti kuhusu nyaraka za kiserikali ni kupitia nyaraka zote zilizoandikwa katika kipindi husika. Je kuna mtu anaweza kuleta Nyaraka za Baraza la mapinduzi katika kipindi chote kuanzia Januari mwaka 1964 had November mwaka 1964 ambapo ndipo Jina la Tanzania lilipoanza kufanya kazi? At least tumeshaona waraka mmoja wa kutoka kwenye bunge la Tanganyika ukiwa na addendum ya articles of the Union na tumeshaona picha nyingi za Karume na Nyerere wakisaini makubaliano hayo. Hata kama huo waraka huo haupo, ni vizuri tunyeshwe nyaraka nyingine zilizofanyika hapo katikati kwa vile zitainyesha iwapo zilikuwa zinatambu muungano au vipi.

Kama haya ya kweli hivi wambunge wa CCM Zanzibar nani kawaronga au ni hizo laki 3 zimewakosesha uzalendo? wakati ndio huu tuweke kila kitu wazi, mpira urudishwe kwa wananchi kama tunataka Muungano au la na kama ndio ni Muungano wa serikali ngapi? Kama Taifa yatubidi tuanze upya tusiendelea kuweka uchafu uvunguni wa kapeti maana kwa sasa tuko uchi..

Pia upande wa pili tujiulize kwa nini Kalume aliuawa na kama taarifa zinavyoelezwa aliyefanya mauaji yale ni Comandoo Mahafudhi ambae tuliambiwa aliwekwa kizuizini na Nyerere na tutambue mauaji yale yalifanyika na Mtaalamu kwa kutumia Silaha bora zaidi. Mimi nahisi mauaji yale yalikuwa ya makusudi na lengo lilikuwa kupoteza mambo muhimu waliyokubaliana kati ya Nyerere na Kalume katika Muungano huu na ndio maana hadi leo Hii hatujasikia Hotuba za Kalume(R.I.P) pia hakuna huo mkataba uliosainiwa na pande hizi mbili kwa hiyo mauaji yale yalifanyika na Mkataba kuchomwa moto na hata Kiongozi aliyekuwepo wakati ule Aboud Jumbe kawekwa kizuizini kule Kigamboni na hili kuuficha udhalimu huu CCM imeamua kuibeba familia ya Kalume na kuhakikisha wanapewa nafasi yeyote ndani ya Serikali na Chama hata kama uwezo wa muhusika utakuwa mdogo kiasi gani mfano yule anayetembe na Kinana nimemsikiliza ni mtu mwenye uwelewa mdogo sana lakini nasikia aliwahi kuwa Barozi akiiwakilisha nchi.
 
Du ipo kazi kwelikweli, hata mimi wazo la kujua ni kwanini Karume aliuawa bado sijapata jibu lake! Japokuwa si mwisho wa kujua historia ila kwa waliopo kwa sasa kwenye bunge la katiba,
wanatakiwa kujadili zaid maslahi ya wananchi kwanza na si msimamo wa vyama vyao!
 
Halafu tunaambiwa muungano ulifanywa kwa maslahi ya wananchi. Jamani tuachiani tuamue sasa kipi kizuri kwetu na sio kwa faida ya viongozi waliopita!


Muungano uko kwa ajili ya kushikishana adabu ndani ya CCM. Kama ukiwa na jeuri ndani ya CCM unakosa theluthi mbili toka Zanzibar ndani ya halmashauri kuu na mkutano mkuu wakati wa kugombea.
 
Mkuu Pasco,

Nakushukuru sana kwa darasa yako maridhawa ambayo kamwe sikutegemea kuipata kutoka kwako. Hata hivyo napenda nikiri kuwa kwa hakika nimekwazika na maelezo yako haya:

"Baada ya Karume, Aboud Jumbe akaukwaa urais. Dourado akamjulisha Jumbe kuhusu kukosekana kwan proper ratification na iliyopelekwa UN is fake!, wakaandaa document kuujulisha ulimwengu kuhusu hilo!Seif Sharif akamtonya Nyerere akashughulikiwa ipaswavyo, huku Dourado akaozea jela!.Tukatangaziwa "kuchafuka kwa hali ya hewa Zanzibar" bila kuelezwa kisa ni absence ya proper ratification !."

Naomba sana hapo nilipobold na red unifafanulie kwa uwazi kama ulivyofafanua sehemu nyengine muhimu. Nahisi nahitaji kuelewa kitu fulani kilichojificha ambacho naamini wewe unakifamu kwa nafasi yako. Huyu ni kiongozi wetu wa mpambano huu kuelekea ukombozi wa nchi yetu. Sasa inapotokea kutoa shutuma nzito kama hizi bila ya ufafanuzi unaweza kuleta sintofahamu katika jamii. Na kwa kadri nifahamuvyo mimi, lengo la JF sio kuchochea mifarakano lakini kujenga umoja,mshikamano, democrasia na uwazi kwa dhana ileile ya Freedom of expression.
 
Mkuu Pasco,

Nakushukuru sana kwa darasa yako maridhawa ambayo kamwe sikutegemea kuipata kutoka kwako. Hata hivyo napenda nikiri kuwa kwa hakika nimekwazika na maelezo yako haya:

"Baada ya Karume, Aboud Jumbe akaukwaa urais. Dourado akamjulisha Jumbe kuhusu kukosekana kwan proper ratification na iliyopelekwa UN is fake!, wakaandaa document kuujulisha ulimwengu kuhusu hilo!Seif Sharif akamtonya Nyerere akashughulikiwa ipaswavyo, huku Dourado akaozea jela!.Tukatangaziwa "kuchafuka kwa hali ya hewa Zanzibar" bila kuelezwa kisa ni absence ya proper ratification !."

Naomba sana hapo nilipobold na red unifafanulie kwa uwazi kama ulivyofafanua sehemu nyengine muhimu. Nahisi nahitaji kuelewa kitu fulani kilichojificha ambacho naamini wewe unakifamu kwa nafasi yako. Huyu ni kiongozi wetu wa mpambano huu kuelekea ukombozi wa nchi yetu. Sasa inapotokea kutoa shutuma nzito kama hizi bila ya ufafanuzi unaweza kuleta sintofahamu katika jamii. Na kwa kadri nifahamuvyo mimi, lengo la JF sio kuchochea mifarakano lakini kujenga umoja,mshikamano, democrasia na uwazi kwa dhana ileile ya Freedom of expression.
Mkuu Manyimbo,
Labda nikuulize, jee unajua chochote kuhusu kitu kinachoitwa Kuchafuka kwa hali ya hewa ya kisiasa Zanzibar?!.

Aboud Jumbe ndie rais aliyempokea Karume baada ya kuuwawa, nini kilimtokea?!. alifanya nini?!, na akafanywa nini?!.

Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, enzi hizo ilikuwa ni Wolfgang Dourado!, find out, aliandaa document gani, kuhusu muungano ambayo Jumbe alikuwa aipeleke UN, jee document hiyo ilikuwa na nini, na huyo Dourado nini kilimkuta?!.

Find out wakati wa mchafuko huo, Waziri Kiongozi wa SMZ alikuwa nani na alifanya nini?!.

Pasco
 
Back
Top Bottom