Kashfa kwa Vatikan na kwa kanisa la Romani Katoliki

Kashfa kwa Vatikan na kwa kanisa la Romani Katoliki

mbenge

JF-Expert Member
Joined
May 15, 2019
Posts
4,864
Reaction score
10,483
Yametukia matukio mbalimbali fedheha na udhalilishaji wa kijinsia yenye kuwahusisha viongozi wa kidini wa kanisa Katoliki la Roma. Matukio haya ya aibu kubwa na ya kashfa za kingono yanawahusu vijana na watoto wenye umri wa chini ya miaka 18, wote wa kike na wa kiume yakiambatana na vitendo vya ubakaji ambayo yalianza kuibuliwa toka miaka ya 1950.

Baada ya kuwepo kwa ukimya wa muda mrefu kutoka kwa viongozi wa juu wa kanisa hili kubwa ulimwenguni kote, bado kuliendelea kuwepo kwa malalamiko na mashauri mengi ya kijinai yaliyokwisha kufunguliwa na familia za wahanga. Pamoja na hayo yote kutokea, bado mamlaka ya juu wa kanisa hili ulichokwisha kukijifanya ni kuomba tu msamaha wa jumla kwa wahanga pasipo hata kutaka kuwawajibisha wahusika ama kuonyesha nia ya kuwalipa fidia wahanga.

Leo imetolewa ripoti nchini Ufaransa kuhusu wahanga wapatao 330, 000 ambao waliathirika, ambao wanalihusisha dhehebu hili kubwa la Kikristo na lenye maarufu ulimwenguni kote.

Je! Mamlaka ya Vatikano inaguswa kwa dhati na kashfa hii ama itaweza kuja na kauli gani yenye kushawishi na kuweka mambo sawa?

Je! Hii kashfa kwa nini isiwe sababu ya kutengua kanuni za useja ili mapadri nao waruhusiwe kuoa ili kuepuka tamaa za kingono?
 
This is a global issue! Imani ni suala la mtu binafsi na Yesu Kristo kama Bwana na Mwokozi. Juzi KKKT (equivalent) Marekani wamesimika askofu shoga;

Anglican ndio usiseme. Hata kwa ma mdogo nako ni balaa tupu! Zikitolewa ripoti hapatakalika. Linda moyo wako kuliko vyote ulindavyo ndugu.
 
This is a global issue! Imani ni suala la mtu binafsi na Yesu Kristo kama Bwana na Mwokozi. Juzi KKKT Marekani wamesimika askofu shoga; Anglican ndio usiseme. Hata kwa ma mdogo nako ni balaa tupu! Zikitolewa ripoti hapatakalika. Linda moyo wako kuliko vyote ulindavyo ndugu.
Mkuu Dudus, ukubwa ni jalala, lakini umaarufu ni kudumisha enzi.
 
bcoz the end of false religions is near, na haya yatatokea na kuendelea kutokea zaid na zaid, maana mwisho u karbu, na ili ufike hayana budi kutokea ili kuudhihirisha umma wa mtu mweusi ubaya wa izo iman za kigeni, haya mambo yalishatabiliwa ktk maandiko ya kweli(achana na hayo mauongo yenu yaliyokopiwa mnaita biblia).

huyo mrumi pamoja na wadogo zake wakina Islamic, ruthelan, morevaian,wasabato, wangrikana, walokole na takataka zote zilizojipa malmaka ya dini&imani tokea kwa mama yao Catholic lazma zfike mwsho, na mwsho wao mbaya na hauzuiliki ndiomaana huon nguvu za papa na wapumbv wenzake wakihangaika kuzuia, sababu kwenye mapango yao ya vitabu vya sili walivyoiba afrika, yanaonesha tabili juu ya haya yatokeayo na yatakayotokea, hayana mpinzani lazma yatokee.

shida ni kwa wew mtu mweusi kung'ang'ania kuusafisha ukatoric wako, uislam wako, ama ukristo wako kwakuleta visingizio vya maandiko, ijapokuwa unaona mapungufu ya imani yako, hutak kubadirika, unakaza shingo.

niwaambie ukwel, wale woote wanaopinga mafundisho ya kuurudia ukuu wa afrika na imani za kwel za afrika(sio mizimu), hawa wote ndyo watahukumiwa pamoja na shetan kwa mujibu wa biblia zenu mnavyomuita, pia mtatupwa ktk shimo la usahaulifu(jehanamu ya moto kwa mujibu wafundisho yenu ya uongo).

hakuna moto wala jehanamu, ukwel mchungu, na ndio ujue kwanzia sasa,

dini sio Mpango wa Muumba kuwepo,.ndiomaana zmejawa mikanganyiko, na uongo mwngi, pia hivyo vitabu vyenu, si Neno la Mungu maana vimejawa stori za uongo na mikanganyiko ya kujipinga vyenyewe, anaebisha na abishe lkn naweza mpa swali hapa akachemka na akenda mpka kwa kiongoz wake wa dini kitaifa na kidunia kamwe hatokupa majibu sahih ya mikanganyiko zaid ya kuleta vitisho kuwa Mambo ya Mungu hayachunguziki.

amkeni waafrik dini hazina maana kwako, hazina mchango kwako wala ukomboz, ile raha unayofeel ukiw kanisani na kujiona mwema, ile ni demonic feeling unapata baada ya kuamini uwepo wa nguvu zao huko makanisani, ili kukutrick usitoke ktk uo uongo wa dini.

Muumba wa kwel haabudiwi ktk makanisa, maana uwepo wa nguvu zake ni kila sehemu, na haitaji dini ili umjue, naishia hapa.
FB_IMG_16295005485734736.jpg
 
Nakuelewa sana..ila wapi tutapata muongozo wa dini zetu za kiafrika...ili tuweze zifuata na kuziabudu.

#MaendeleoHayanaChama
... akikujibu ni-tag Mkuu! Afrika hii hii watemi wakifa walikuwa wanazikwa na vijana walio hai? Akasome historia ya Shaka Zulu aone mambo ya ajabu alyofanya dhidi ya watu wake; hao ndio viongozi wa kiafrika socially, politically, and spiritually!
 
Mimi naamini safari ya mwanadamu kuutafuta ukweli bado haija tamatika, tena tunawezaku kusema ndio kwanza inaanza.

Katika harakati hizo ndizo zilizo dini na huko kwenye dini kusingiziwa na mengine ndiyo ikawa tiketi ya kupotea njia kwa binadamu ya kuitafuta ukweli.

Vile mwanadamu hapendi kushindwa ndivyo yupo tena katika harakati za kuutafuta ukweli na naamini ipo siku utajulikana, na itakua nje ya dini.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yametukia matukio mbalimbali fedheha na udhalilishaji wa kijinsia yenye kuwahusisha viongozi wa kidini wa kanisa Katoliki la Roma...
Kwani waliooa huwa hawadhalilishi watoto? Wote waliopatikana na hatia ya kunyanyasa watoto kingono ni makasisi tu.

Useja ndiyo upadre na useja ukimshinda Padre anakaa pembeni. Kosa halibadili kanuni na sheria. Acha hizo
 
This is a global issue! Imani ni suala la mtu binafsi na Yesu Kristo kama Bwana na Mwokozi. Juzi KKKT Marekani wamesimika askofu shoga; Anglican ndio usiseme. Hata kwa ma mdogo nako ni balaa tupu! Zikitolewa ripoti hapatakalika. Linda moyo wako kuliko vyote ulindavyo ndugu.
Hakuna cha global issue, hapa issue ni mapadri, maaskofu na makadnari wa kanisa katoliki kulawiti watoto na vijana wadogo wa kanisani.

Imani ni jambo la mtu binafsi kweli ila watu ambao wanaaminika kupewa watoto ili kuwalinda na kuwakuza kiimani wanawageuza nyuma na kuwalawiti hao ni watu wa aina gani?

Halafu hii sio Ulaya tu, ni Duniani kote mapadri na maaskofu katoliki wanalawiti vijana. Huku afrika ambako hakuna uchuguzi wa wazi, siku mambo yakiwa wazi itakua balaa.

Uchunguzi unasema zaidi ya 80% ya mapadri katoliki ni mashoga

Makanisa mengine ni ya kufuta kabisa.
 
This is a global issue! Imani ni suala la mtu binafsi na Yesu Kristo kama Bwana na Mwokozi. Juzi KKKT Marekani wamesimika askofu shoga; Anglican ndio usiseme. Hata kwa ma mdogo nako ni balaa tupu! Zikitolewa ripoti hapatakalika. Linda moyo wako kuliko vyote ulindavyo ndugu.
Hizi dini bana zimejaa ujinga tu then tunaenda kuwapigia magoti Mapadri na Wachungaji na unakuta wengine mashoga Kama hao Ili watuondolee zambi dah.
 
bcoz the end of false religions is near, na haya yatatokea na kuendelea kutokea zaid na zaid, maana mwisho u karbu, na ili ufike hayana budi kutokea...
Daaah, mkuu, wewe huna dini? Shimo la usahaulifu maana yake nini? Na maandiko hayo umeyapata wapi? Ina maana mkuu huamini kama biblia ni mkusanyiko wa historia ya mambo yaliyotokea kwa watu walioishi nyakati za agano la kale (kabla ya kuzaliwa Kristo) na habari za agano jipya (baada ya kizaliwa Kristo)?

Je, habari zilizoongelewa katika biblia, za watu mashuhuri kama manabii, unahisi nazo ni uzushi? Lakini mbaya zaidi hata Yesu Kristo humuamini? Mbona tunawasoma akina mtume Paulo wanamshuhudia katika kazi alizotumwa kufanya hapa duniani mpaka mwisho wake? Lakini pia shuhuda za mambo hayo bado zipo, na watu wanaoenda kuhiji wanatuthibishia.

Nikufahamishe tu kuwa dini ni daraja lililopo (lililowekwa) kati yetu na Mungu wetu. Hiyo ndio njia ya mahusiano kati yetu na Mungu.
 
Back
Top Bottom