Kashfa ya Kontena la Vitunguu Saumu kutoka China: Badala ya kuchomwa vinarudishwa upya!

Kashfa ya Kontena la Vitunguu Saumu kutoka China: Badala ya kuchomwa vinarudishwa upya!

Ndio maana tuna idara za "Customs", "health", "TFDA", "TBS", "UWT" na zinginezo, kuhakikisha hatuingiziwi vibovu.

Nakuuliza, vitunguu vibovu bandarini vina husiana nini na Igunga?

Author anajaribu kukumbusha tu serikari hivi sasa akili ipo Igunga. Karibu wakuu wa Idara zote macho na akili zao ziko Igunga na kuwaacha wachina na mafisadi uchwara waingize takataka.

Samahani dada yangu FF hivi UWT nao wana nafasi kwenye uingizaji vyakula? ahaaaa ni wanawake wake wa CCM, Igunga vipi UWT hawakwenda? au ndo walioachiwa majukumu ya Bandari?
 
Author anajaribu kukumbusha tu serikari hivi sasa akili ipo Igunga. Karibu wakuu wa Idara zote macho na akili zao ziko Igunga na kuwaacha wachina na mafisadi uchwara waingize takataka.

Samahani dada yangu FF hivi UWT nao wana nafasi kwenye uingizaji vyakula? ahaaaa ni wanawake wake wa CCM, Igunga vipi UWT hawakwenda? au ndo walioachiwa majukumu ya Bandari?

Soma vizuri post. Asiyejuwa maana haambiwi maana, msitake kutubabaisha kwa maneno. Hata Usalama wa Taifa ni UWT na huko pia kuna wanawake. Igunga UWT wamekwenda au umesahau mlivyomvua hijab mwana mama wa UWT?
 
Soma vizuri post. Asiyejuwa maana haambiwi maana, msitake kutubabaisha kwa maneno. Hata Usalama wa Taifa ni UWT na huko pia kuna wanawake. Igunga UWT wamekwenda au umesahau mlivyomvua hijab mwana mama wa UWT?

Huyu hakuvuliwa hijab maana haukuwa na hijab. Huyu alivuliwa nguo aka mtandio.

By the way naomba namba yako nikutwangie, siamini kama wewe ni mzee kama wanavyo kusema. Nipe nafasi
 
Ahsante Nsiande, si i own hiyo label, hiyo label ni ya wateja wangu ambao tunawatengenezea nguo za pamba yenye ubora unaokubalika. Kama hizo nguo ukikuta ni za pamba na zimetengezwa Mauritius, kumbuka ni mimi nnae zisimamia kuanzia kupeleka pamba India ikafumwa mpaka kuifikisha Mauritius na kuhakikisha zinashonwa nguo kutokana na design na ubora autakao mwenye nembo ya "Cotton Club".

Naipenda sana, hongera mama jamani
 
Watu wengine wanajaribu kutenganisha yanayotokea kwenye ufisadi na matokeo yake kwa maisha ya wananchi. Kwamba kwa kuagiza au kuruhusu vitunguu saumu tunaua biashara yetu ya ndani sisi wenyewe na kuendelea kuwasukumiza watu kwenye kona ya umaskini wa kudumu.

Hapo nakubaliana na wewe Mwanakijiji, kwa nini Wachina walete vitunguu saumu wakati maeneo ya Iringa na sehemu za baridi kama Lushoto wanalima kwa wingi? Tujaribu kupanda mbegu nzuri ili kuimarisha uchumi wetu kwa kununua vitunguu vyetu.

Hivyo vya kichina kesho kutwa utasikia kuna mbolea fulani (xxx) ilitumika ambayo ina sumu kama vile ilivyokuwa kwa maziwa ya unga ya watoto.
 
sasa sie wapenzi wa vitunguu saumu ndio tumekwisha maana hivi lazima vitaingia tu sokoni.... ewe mola tuepushe na haya mabalaa kha!

Badala ya kitunguu saumu kuwa dawa sasa kitakupa tumbo la kuharisha.
 
Umekuja na habari nzuri sana para ya kwanza, kama ni ya kweli, halafu para ya mwisho ukamwaga pumba kama kawaida yako. Unanshangaza kwa kuiharibu habari kwa maswali yasiyo na msingi.

1. Kwa nini Tunashauriwa Tusfikir kwa Tumbo?

Jibu ni kwamba Unaweza kuwa na Vidonda vya Tumbo au unaweza kuwa na Njaa na Magonjwa mengine ya Tumbo kwa hiyo hata Fikra zako zitakuwa za kinjaanjaa tu.

2. Kwa Tu nakatazwa kufikiria kwa Makalio?

Jibu ni kwamba Makalio ndiko iliko ile Kifaa ya Kunyea sasa unaweza kuwa umetoka Msalani halafu hujajiswafi Vizuri hapo ukitumia Makalio kufikiria Basi Fikra zako zitakuwa ki nnya nnya tu
 
Kuagiza biashara za nje hakuuwi biashara ya ndani bali kunasaidia kuikuza. Amma kwa kuweza kuonesha ubora wa bidhaa zetu amma udhaifu wa bidhaa zetu na kuchukua njia mbadala wa amma kuboresha bidhaa zetu amma kuziuza kwa ubora wake unaostahiki, mashindano ya kibiashara ndio njia pekee ya kukuza biashara, uelewa, elimu, viwango na hata "presentation" ya bidhaa. Na ikiwa tutaendelea kuogopa kuleta bidhaa za nje basi tukubali na matokeo ya kuzifunga fikra zetu na ziendelee kuwa pevu kama tunavyofikiri.

Biashara gani ya ndani tunayoikuza...?(non existent...!!!).., Ni kweli its all about supply and demand and through competition tunapata bidhaa ambazo ni bora zaidi kutokana na ushindani wa watu tofauti..., Ila how can you compete price wise, na bidhaa mbovu (rejects..) na zilizooza, if they can sell it for peanuts, in not so distance future viwanda vya nchini au wakulima wadogo watakufa a natural death kwa kushindwa kuuza bidhaa zao na hivyo kuwa bankrupt....

Something somewhere is terrible wrong bidhaa mbovu ambazo hazina soko pengine (rejects) na sababu ni rejects zinakuwa very cheap (na kama unavyojua hulka ya mbongo kitu kutoka nje ndio bora zaidi) zikiingia nchini zinaongeza supply hence kupunguza demand ya bidhaa za nchini (alafu kumbuka production wise hatuwezi kushindana na viwanda ambavyo ni mass production huo ndio ukweli..)

Hivyo basi ukiona kwamba hata vitu vinavyolimwa nchini (vitunguu n.k) havitoshelezi mpaka tunaagiza kutoka nje (au samaki..) basi ujue something has terrible gone wrong somewhere....

Toothpick; earbuds nazo tunaagiza.., bidhaa badala ya kuhakikisha tunaziongezea value na kuwa finished products nchini tunapeleka mali ghafi nje products zinakuwa processed na kurudishwa nchini...(hata nguo za wanajeshi na wanafunzi tungeweza kuzitengeneza hapa ili kukuza ajira..)

To make the long story short hakuna system in existence..., the all issue stinks... na kwa msaada wangeweza kuweka kodi kubwa kwa baadhi ya bidhaa zinazocompete na bidhaa za nchini ili kutokuwepo na utofauti wa bei..... Just imagine samaki wetu wazuri tunawasafirisha nje na sisi tunaletewa samaki ambao hawawezi kuuzwa pengine...
 
Vitunguu saumu ndivyo hivi vya kupikia pilau na vingine huwa naona ndugu zangu wa Singida wakiweka kwenye wale kuku wao wa kulimia ili wawe laini wakati wanachomwa au ni vingine? Ndivyo hivi ambavyo vinakosa soko kule Karatu na viunga vya jirani au vingine? Ndivyo hivi vinavyouzwa pale katiakoo kwa muuza viungo vya pilau au ni vitunguu saumu vingine? Mwanakijiji huenda kwenye kontena kuna madwa ya kichina na si vitunguu saumu. Siamini fanya utafiti mujarabu utujuze.

Kama kweli tumeagiza vitunguu saumu basi tena nchi yetu si riziki.
 
Huyu hakuvuliwa hijab maana haukuwa na hijab. Huyu alivuliwa nguo aka mtandio.

By the way naomba namba yako nikutwangie, siamini kama wewe ni mzee kama wanavyo kusema. Nipe nafasi
Amekula chumvi mwenzio, mwezi wa 8 alisherehekea miaka 30 ya ndoa yake, hapo hata kama aliolewa na ten yrs unadhani sahizi atakuwa na umri gani? Sijui kwa nini hataki kupumzika ale uzee wake kwa raha!..
 
Kuna habari za kuaminika sana kuwa kuna kontena la futi 40 (karibu tani 30) na limeingie nchini kwa karibu wiki mbili sasa ambalo limejaa vitunguu saumu ambalo linajaribiwa kuingizwa nchini na kundi la Wachina. Sasa wakaguzi wa pale bandari wakagundua kuwa vitunguu vinaoneshwa (kwenye mifuko yake) kuwa vimeexpire tangu 2009. Sasa jana Wachina wetu walienda TFDA ili kupata kibali cha kuingiza vitunguu hivyo nchini. Lakini ilikuwa vikitoka hapo viende kutiwa moto - chanzo toka bandarini - kinadokeza kuwa hivyo vitunguu vimekomaa kiasi kwamba ukivipasua "unaweza kupata kizunguzungu au kupaliwa".

Sasa Wachina hawako tayari kuingia hasara. Nasikia wametembeza mlungula wa kitu kidogo kuanzia TFDA, Kilimo, TRA na kwa vile sijafuatilia leo tangu hili sakata lianze jana walikuwa waende na TBS. Sasa uwezekano wa vitunguu hivyo kuingizwa sokoni ni mkubwa hasa kama haitawezekana kuvirudisha China. Sasa hivi vimehifadhiwa katika mafriji ya bandari pale na jamaa hawataki ifanyike "manual" inspection wanataka "scanning". Jamaa wametembeza karibu dola 5000 ili kurahisisha utoaji wa vitunguu hivyo; kuanzia TFDA kwenyewe kilimo na TRA.

Sijui ni mazao gani yanalimwa huko Igunga (najaribu kukumbuka kama kuna maeneo ya Tabora wanalima Vitunguu saumu) lakini vyovyote vile ilivyo taifa lnapofikia kuagiza hata vigunguu saumu basi tuna hali mbaya sana. Ndio nimebakia kusema kuwa kuna kashfa nyingine ni za kijinga.

Tumekula samaki wa nyuklia sembuse vitunguu vilivyo expire?
 
Vitunguu saumu ndivyo hivi vya kupikia pilau na vingine huwa naona ndugu zangu wa Singida wakiweka kwenye wale kuku wao wa kulimia ili wawe laini wakati wanachomwa au ni vingine? Ndivyo hivi ambavyo vinakosa soko kule Karatu na viunga vya jirani au vingine? Ndivyo hivi vinavyouzwa pale katiakoo kwa muuza viungo vya pilau au ni vitunguu saumu vingine? Mwanakijiji huenda kwenye kontena kuna madwa ya kichina na si vitunguu saumu. Siamini fanya utafiti mujarabu utujuze.

Kama kweli tumeagiza vitunguu saumu basi tena nchi yetu si riziki.

Mkuu ukimsoma vizuri mwanakiji utaona kuna mahali amesema wachina hawataki physical check up wanalazimisha ifanyike scanning, hujiulizi kwa nini? Stuka!

Pembe za ndovu zimeenda bara Asia mara ngapi huku documents zikisema ni magogo ama plastics?

Huajona sukari kule mkoani mara inavuka kwenda kenya malori na malori huku juu wakiwa wametandaza magodoro? Bongo full magumashi!
 
Jamani habari, hoja ya vitunguu saumu ni muhimu kuiangalia kwa makini hayou ya siasa mimi sita yaongelea kwa sasa.
Kama uwezo wa kulima vitunguu saumu vya kawaida (vile tulivyo zoea siku zote).
Kuna haja gani ya serikali kuruhusu kuingiza(import), kwanza vitunguu vyeupe (genetically modified products)

pili, mkulima wa kawaida wa vitunguu hivi analindwa je na nguvu ya soko na madhara yake kwenye bei (au anaachwa kama mtoto wa mtaani)?
Yamkini mimi ndio sielewi sera ya biashara kubwa, lakini nafikiri haya yana waangusha wa kulima wa kitanzania ambao wengi ni wadogo (kimitaji na pia kiuzalishaji)

Kama forum yetu ina mjuzi wa economic planning na anaye elewa vyema sera na mipango anijuze, huenda kuna jema katika yanayofanywa
 
Nna uhakika hujawahi kufanya biashara wala huielewi biashara, kuagiza biashara za nje hakuuwi biashara ya ndani bali kunasaidia kuikuza. Amma kwa kuweza kuonesha ubora wa bidhaa zetu amma udhaifu wa bidhaa zetu na kuchukua njia mbadala wa amma kuboresha bidhaa zetu amma kuziuza kwa ubora wake unaostahiki, mashindano ya kibiashara ndio njia pekee ya kukuza biashara, uelewa, elimu, viwango na hata "presentation" ya bidhaa. Na ikiwa tutaendelea kuogopa kuleta bidhaa za nje basi tukubali na matokeo ya kuzifunga fikra zetu na ziendelee kuwa pevu kama tunavyofikiri. Au tukubali kuwa na fikra changa zenye uwezo wa kufikiri mapya kwa kujifunza mapya mengi kutoka kwa wenzetu waliokubali kuwa hakuna fikra pevu utakayoifundisha ikaelewa (try to teach an old dog new tricks). Kuwa na fikra pevu ni ufinyu wa kufikiri.

Leo kweli mtu haswa mwenye fikra za kimaendeleo anakwambia usiagize bidhaa za nje kwani zinauwa biashara yetu ya ndani? Inashangaza sana.

Halafu uhusishe mambo kibao na uagizaji wa vitunguu?

Hivi huwa unatafuta njia za kupakaza kila unapoweza au ndio upevu wa fikra zako umefikia ukomo wa kufikiri?

Faiza Fox

amna mtu mwenye haki ya kukulazimisha where you pledge your political loyalty, lakini inabidi huwe na chembe ya utaifa hata kidogo. Wewe ina maana nchi maskini kama tanzania ambayo bado watu wengi wana-rely on agricultural, you think its right for the government to allow importation of the things we can locally produce to improve peoples life chances.

Kwa mtaji huo ndio maana tunalalamikia capitalism kwa uozo wa mkullo na wenzake for crying out loud hata huyo capitalist ana kitu anaita comparative advantage, si kila kitu kiingie sokoni kirahisi rahisi tu. Kama tuna upungufu wa garlic serikali ilitakiwa kusubsidize wakulima walime. Lakini kama tupo kwenye point ya kusema tunaagiza basi amna tutakachoweza fanya wenyewe kamwe na tutalaumu capitalism kwa ajili ya kuikariri na si kuilewa.
 
Watu wengine wanajaribu kutenganisha yanayotokea kwenye ufisadi na matokeo yake kwa maisha ya wananchi. Kwamba kwa kuagiza au kuruhusu vitunguu saumu tunaua biashara yetu ya ndani sisi wenyewe na kuendelea kuwasukumiza watu kwenye kona ya umaskini wa kudumu.

Mwanakiji

kama watu hawajui hata kitendo cha kuuza wanayama hai kwenda kwenye mazoo nje ni kusabatoge utalii na biashara na uwekezaji wa utalii hapa kwetu wa seriali na wananchi Sasa watalionaje hilo kwenye vitunguu swaumu. anavyolima mzee amabye hawana hata data zake. TRA watakuambia bora huyu mchina wana TIN no. kwao ni smhiko tu ndio muhimu.

Kama hata ofisi ya mbunge , ofisi ya RC, ofisi ya DC sofa na viti vyote vinayotumika ni vya kutoka china . hata meza na viti vya wageni. watachochea ajira vipi nchini. Watakuzeje uuifu na teknoljia za ndani. wenye majukwa ni rahisi kusema laini ni ngumu hata wenyewe kuishi maneno yao. jibu rahisi la CAG na TAKUKURU watakuambia taratibu za tender zilifuatwa. Angalia hata kwenye ofisi za wabunge kweye majimbo yenye mbao wawe ni wa upinzani au wa CCM.

Ulizia pale ikulu katika sanamu na vinayago vilivyomo mule kuna kazi ya mtanzania? Je uzio ikulu umepakwa kwa rangi ya kampuni gani? Utaambiwa cha muhimu tender na taratibu zinafuatwa .Mtazamaji akshidna tender yeye anakwenda china. Tender na taratibu amabazo hazjaribu kuwaweba watanzania mhhhh .Utenzi mwingine ni kuwa vya watanzaia havina viwango bora.

Wangejua hata wachina wamefikia walipo sababu ya uzalendo ya kupenda vyao kwanza.
 
Mie nadhani wako ndio uliolala, Igunga kuna limwa nini inahusiana nini na vitunguu vya bandarini? halafu kuna kosa lipi kuagiza vitunguu saumu kutoka nje? mradi vitengo vya afya viruhusu, sioni uhusiano wa biashara na Igunga na Bandarini. Nadhani mpaka sasa utajuwa ni ubongo wa nani uliokufa. Nakupa pole sana.

Kwenye red umeonyesha uwezo mdogo sana wa kufikiri kuhusu uchumi wa nchi, na soko la ndani na nje. Huwezi ukaangiza vitu vinavyopatika nchi mwako nje kirahisi hivyo, huko ni kuuwa uchumi wa wananchi wako na nchi kwa ujumla. Mbaya zaidi unaletewa vitunguu saumu vilivyoexpire, lazima uwe kichaa na muuaji wa wanachi wako ndo utakubali kuviingiza nchini mwako.
 
Back
Top Bottom