Kashfa ya Richmond: Lowassa, Karamagi na Dkt. Msabaha Wajiuzulu

One of the owners of Richmond is Rostam and he is the best buddy and financier of the Lowassa, so what do you think?

Kumbuka Rostam alikuwa mwekahazina wa ccm na hivyo ccm yote imeoza.Lowasa kakataa kuutumikia mfumo fisadi
 
Wanasubiri kampeni zianze ili kuchukua hatua uku kampeni zikiendelea

Hii ishu ya Edward Lowassa vs kinachoitwa ufisadi wake wa Richmond vs Mamlaka ya juu ambayo ni ofisi ya Rais ambaye tangu wakati huo mpaka leo ni huyu bwana anayeitwa Jakaya Mrisho Kikwete, ni ngumu na ni kaa la moto kwa maCCM!!

Watu tayari wanazo data za uchafu wote wa Ikulu chini ya huyu bwana (ambaye kiuhalisia yeye ndiye fisadi papa) mkononi na sidhani kama watatoka mwaka huu!!

Kama bado hujaelewa basi subiri tu walianzishe!!
 
Maelezo ktk mada na matamko ya Lowasa

1. Amesema kwa wenye ushahidi waende mahakami, na akasema kama kuvunja mkataba uliokuwa chini aliingiliwa na watu wa juu kwakila hatua aliyotaka kuchukua angefanyaje? aliyekuwa juu ya Waziri mkuu ni nani? Anaweza kuwa Shein? Obvously no; anaweza kuwa nani; jaza ndio maana watoto kwa sasa matajiri wa kutupwa

2. Mwakyembe anasema, kuna mengine hayamo ktk andiko la kamati ya bunge kwa sababu kama tungeyaweka hadharani nchi ingepasuka; hapa inadhihirisha tuhuma za lowasa ilikuwa kisingizio maana mkubwa wake alikuwa anajulikana na alijua nini kinaendelea hatua zote ila ilivyokuwa moto ikabidi kutoa kafara an yeye akakubali kikombe hicho; ubaya hakuwaambia mawakala wake akazidi kuwatumia vijana kumchafua lowasa wakiwemo akina nape na akinia makondoa kwa maslahi aonekane alijiuzuru kihalali na wengine wakapandishwa vyeo

Uchaguzi huu sasa tunampa mchawi kulea mtoto wetu kura zetu zote kwa Lowasa
 
hapo nawaza vp kama kwel upo?, na wahusika ni weng nao wakameza bomu kwamba mwaga mboga namwaga ugali?
 
Najiudhuru uwaziri mkuu kulinda serekali yangu na chama changu..Edward lowassa

Ukisoma post za kina miraj na ridhiwani utaona kuna uasama mbele ya lowassa,...

J.K ametumia nguvu zake zote kumtosa Lowassa,,Ila bado nguvu za wananchi..

Lowassa sio fisadi,lowassa ana ogopwa na mafisadi wanao itumia nchii kuvunia matumbo yao..wanataka kuendelea kuwala tu..

Historia ya nchi hii,itamsimulia lowassa kushinda viongozi wengi walio pita kwa ujasiri na uthubutu..

Wanasemaga siasa ni maisha,kama kijana nimejifunza katika maisha,hakuna kinacho weza kusitisha safari yako kama sio wewe mwenyewe.lowassa ametukanwa sana,wakubwa kwa wavijana,ila hajakata tamaa..

lowassa lowassa lowassa,october watanzania wata ishangaza dunia...
 
kitakacho.mponza lowassa kushindwa october ni kuendelea kukaa kimya badala ya kuyasema maovu ya richmond hadharani na waliohusika.
 
kitakacho.mponza lowassa kushindwa october ni kuendelea kukaa kimya badala ya kuyasema maovu ya richmond hadharani na waliohusika.
Tulia bado chakula hakijaiva, kampeni zikianza atatupakulia!
 
tusubir oct,mda mwngne naona kama plan hvi kwamba el awe rais maana friend wako akiona huku hupati anaweza kufanya njia ya kukuwezesha upande wa pili...kimficho kama hakupend hv,yan anakutupia kwa adui aliyekuwa tishio kwenu lakn ukienda ww adui anaridhka ...We unaonaje
 
Uchaguzi wa mwaka huu kama kweli lowasa hajatumwa kuvuruga ukawa basi tutaskia siri nyingi kwenye kampeni ili kuchafuana
 

mi naona amemsaidia, unajua isingekuwa hv dr slaa /ukawa wangetumia hoja ya ufsad kumuangusha el...Ni kama cnema hvi
 
Imechapwa 21 July 2010



Chanzo: Mwanahalisi
 
 
Kinana: Lowassa safi, Nyalandu anazurura



"Mfano ni Waziri wa Maliasili na Utalii ambaye anafanya kazi ya kuzunguka nchi nzima na maeneo mengine wakati mizunguko yake haisaidii kuondoa matatizo ya wananchi." Kinana

Kwa ufupi


  • Katibu huyo wa CCM amwelezea kuwa ni mtu shupavu na mchapakazi
  • Waziri ajibu kuwa analijua tatizo la wananchi, litatuliwa wiki mbili zijazo

By Habel Chidawali, Mwananchi Kondoa/Monduli. Jana ilikuwa siku ya hisia tofauti kwa watu wawili wanaotajwa kwenye kinyang'anyiro cha urais, Edward Lowassa na Lazaro Nyalandu baada ya Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana kumsifu mmojawao na kumponda mwingine.

Akiwa Kondoa, Kinana alitumia muda mwingi kujibu kilio cha wananchi wanaosumbuliwa na askari wa wanyamapori kwa kumponda Waziri Nyalandu kuwa anazurura bila kushughulikia matatizo ya wananchi, lakini saa chache baada ya kuwasili Monduli alimsifu Lowassa kuwa ni kiongozi shupavu.

Tayari Nyalandu ameshatangaza nia ya kugombea urais, wakati Lowassa, mmoja wa wanachama wa CCM wanaotajwa sana kwenye kinyang'anyiro hicho, hajatangaza uamuzi wake lakini anatumikia adhabu ya chama chake kilichomfungia kujihusisha na harakati za uongozi pamoja na makada wengine watano.

Baada ya msafara wa Kinana kuwasili Monduli na kupokewa na viongozi wa chama hicho wa eneo, katibu huyo wa CCM, Kinana alipata nafasi ya kuzungumza machache kabla ya kuanza safari ya kukagua shughuli mbalimbali.

"Hatuna shaka na Monduli kwa kuwa yupo kiongozi shupavu, ndugu yetu Waziri Mkuu mstaafu na mjumbe wa (Halmashauri Kuu ya CCM) Nec," alisema Kinana akiwaelezea wananchi waliokuwapo eneo hilo.

"Wa Monduli mna kiongozi shupavu na mchapakazi. Hongera Bwana Lowassa."

Baadaye, Lowassa aliwakaribisha akisema: "Mmefanya kazi kubwa sana ya kukijenga chama chetu. Nawashukuru sana, karibuni."

Naye katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alisema: "Nafurahi kuwa katika jimbo la mzee wangu, rafiki yangu Edward Lowassa. Mapokezi mazuri, bila shaka Arusha mmeamka."

Kinana amekuwa akitumia sehemu kubwa ya ziara yake kushuhutumu viongozi wa Serikali na hasa mawaziri kwa kushindwa kuwatatulia wananchi matatizo yao na ilifikia wakati aliwataja mawaziri wanne aliowaita kuwa ni mizigo, tofauti na alivyofanya kwa waziri mkuu huyo wa zamani.

Lowassa alikuwa waziri mkuu wa kwanza wa Serikali ya Awamu ya Nne na anajulikana kama mtu aliye tayari kufanya uamuzi mgumu. Alilazimika kujiuzulu wadhifa huo mwaka 2008 baada ya kuibuka kwa kashfa ya Richmond.

Kinana alikuwa mtu tofauti wakati akijibu kero za wananchi mkoani Singida, ambako alimtaja moja kwa moja Waziri Nyalandu kuwa hashughulikii matatizo ya wananchi na badala yake amekuwa akizunguka bila msaada wowote.

Kinana alisema hayo juzi katika Kijiji cha Ikengwa, Kata ya Kinyasi wilayani Kondoa baada ya wananchi wa kijiji hicho kumchongea Nyalandu kwa Kinana kwamba wizara yake inawaua na kuwaumiza bila ya hatia, hivyo wamechoka.

Wananchi hao walisema mateso wanayoyapata kutoka kwa askari wa wanyamapori katika Pori la Mkungunero ni makubwa ambayo yanalenga kuondoa uhai wa watu.

Katibu wa CCM wa Kata ya Inyasi, Jusberi Jumanne aliyesoma risala ya malalamiko hayo, alisema wanaishi ndani ya kijiji chao na kufanya shughuli zao za kilimo, lakini kila wakati wanachomewa nyumba, mazao yao kufyekwa na hata kuwasababishia ulemavu na vifo.

"Mheshimiwa katibu mkuu, hapa ni kijiji halali kilichosajiliwa 1974 na kupewa hati 398, lakini hifadhi hiyo ilikuja kuweka mipaka yao mwaka 2006, jambo hili sisi tunaona ni uonevu ambao tunafanyiwa bila ya kushirikishwa na kuambiwa tuhame kwa nguvu na hatujui mahali pa kwenda," alisema.

Akijibu hoja hiyo Kinana alionekana kukerwa na namna maisha ya watu wa maeneo hayo yasivyoshughulikiwa ili nao waishi kama Watanzania wengine.

"Ni jambo la aibu kwa Waziri wa Maliasili na Utalii kusikia migogoro lakini yeye akawa kimya,"alisema Kinana.

"Nyalandu awaeleza Watanzania kama kuna mahali amefanikiwa kumaliza kabisa migogoro walau 10 kwani amekuwa ni bingwa wa maneno na matembezi."

Kinana alisema ni lazima Nyalandu abebe msalaba huo kwani roho za binadamu zina thamani… ni heri roho ya binadamu kuliko mnyama ingawa alizuia wanyama wasiuawe.

"Hawa mawaziri lazima waje, na nina wasihi waje haraka, yaani Waziri wa Maliasili na Utalii na mwenzake wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi," alisema.

"Mfano ni Waziri wa Maliasili na Utalii ambaye anafanya kazi ya kuzunguka nchi nzima na maeneo mengine wakati mizunguko yake haisaidii kuondoa matatizo ya wananchi."

Kinana alitaka kamatakamata ya wananchi isimamishwe kwanza hadi ufumbuzi kuhusu mipaka ya pori hilo itakapoangaliwa upya. Alipoulizwa kuhusu tuhuma hizo, Waziri Nyalandu alisema anakubaliana na alichosema Kinana, lakini akataka watu wajjue kuwa mgogoro huo ni wa muda mrefu.

"Mgogoro huo ni wa siku nyingi, hivyo busara inahitajika sana kulinda watu, mali zao na maliasili. Niliunda kamati ambayo yumo Mkuu wa Wilaya ya Dodoma na Manyara, Ma-RAS (maofisa utawala wa mikoa) wao na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii ambayo imefanya uchunguzi pamoja na kuongea na wananchi," alisema.

"Kamati inatarajiwa kumaliza kazi wiki hii na itanikabidhi kwa kuwa mimi ndiye niliyeiunda. Nimepanga kwamba ndani ya hizi wiki mbili za Bunge, mimi na Waziri wa Ardhi tutatangaza suluhisho la tatizo hili. Tutaenda pamoja Mkungunero kuongea na wananchi."

Katika mkutano huo, Mbunge wa Kondoa Kaskazini, Zabein Mhita alisema kuwa katika kata hiyo na maeneo mengine kumekuwa na kelele zinazotishia amani na tayari kwa baadhi ya watu wameshapoteza maisha.

Walimkabidhi Kinana maganda ya risasi pamoja na rundo la mabaki ya nguo zilizochomwa moto na askari wa wanyamapori.
 
mbona mnaahangaika jamani mara ooh mtt wake anamiliki nyumba mbele mara ooh sijui nn na nn ....mtakonda bure mafuriko hayazuiliki kwa kiganja
 

JK: Lowasa jembe


Kwa ufupi


  • Mnaweza kuchafuana leo, kesho mkapata mgombea mwenye nundu nyingi na mabandeji kila mahala, halafu mkapata shida kumnadi.

By Waandishi Wetu Dodoma/Dar es Salaam. Rais Jakaya Kikwete amemwagia sifa Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa hatua ambayo inaweza kutafsiri mengi katika medani ya siasa nchini.

Akizungumza na wabunge wa CCM kwenye Ukumbi wa White House Dodoma juzi, Rais Kikwete ambaye pia mwenyekiti wa chama hicho, alisema nguvu za Lowassa pekee zinatosha kushinda uchaguzi mdogo wa kiti cha udiwani Kata ya Makuyuni kilichoko wilayani Monduli.

Kata ya Makuyuni iko wilayani Monduli, ambako Lowassa amekuwa mbunge wake tangu mwaka 1995.

Habari za kutoka ndani ya kikao hicho zinaeleza kuwa Rais Kikwete alitoa kauli hiyo kuhusu kampeni za uchaguzi huo wa Makuyuni, baada ya kuwa ametoa ruksa kwa makada wa chama hicho wanaotaka urais kuanza kujipitisha pitisha miongoni mwa wanachama wa chama hicho. Lowassa anatajwa kuwa miongoni mwa wanaCCM wanaotaka kumrithi Rais Kikwete kwenye Uchaguzi Mkuu mwaka 2010.

"Sina tatizo na pale Makuyuni, najua muscles (misuli) za Mzee Lowassa zinatosha kutupa ushindi; au vipi mzee?" alidokeza mmoja wa wabunge wa CCM akimnukuu Rais Kikwete.

Uchaguzi wa Udiwani Kata ya Makuyuni unaotarajiwa kufanyika Juni 16, mwaka huu, utakuwa wa ushindani mkali kati ya CCM na Chadema ambao historia yao kisiasa mkoani Arusha ni ya uhasama.

Katika uchaguzi huo, unaofanyika baada ya kifo cha Abdillah Warsama (CCM), chama hicho kitatetea nafasi yake kwa kumsimamisha Godluck Lerunya na Chadema ni Japhet Sironga.

Mbali na Kata ya Makuyuni, uchaguzi wa udiwani mkoani Arusha utafanyika pia katika Kata za Kaloleni, Themi, Kimandolu na Elerai, kutokana na waliokuwa madiwani wa kata hizo (Chadema), kufukuzwa na chama chao.

"Mnaweza kuchafuana leo, kesho mkapata mgombea mwenye nundu nyingi na mabandeji kila mahala, halafu mkapata shida kumnadi," alisema.

Siyo mara ya kwanza kwa Kikwete kumsifia Lowassa kwani aliwahi kufanya hivyo mwaka jana huko Longido wakati akikabidhi ng'ombe.

Pia aliwahi kumsifia wakati wa kampeni za uchaguzi za mwaka 2010 wakati Kikwete alipomwelezea Lowassa kama Mbunge makini na kuwaomba watu wa Monduli kumchagua tena.

Hata hivyo, alipoulizwa kama baada ya kuruhusiwa kuanza kujipitisha kwa wanaCCM kama anataka kuwania urais, Lowassa alijibu kupitia watu wake wa karibuni kuwa asingependa kuzungumzia suala hilo hasa baada ya Rais kutoa kauli hiyo.



Kutangaza nia ruksa

Rais Kikwete aliwaeleza wabunge hao kuwa si kosa kwa watu kutangaza nia ya kugombea nafasi mbalimbali za uongozi ikiwamo urais mwaka 2015.

"Wabunge na mawaziri wenye nia ya kutangaza nia ya kugombea urais wawe huru, kwani hiyo ni haki yao, isipokuwa wafanye kwa wema bila kukivuruga chama na kuwagawa wanaCCM katika makundi. Sioni tatizo watu kujipitisha. Sisi sote hapa tulijipitisha. Lakini tufanye hivyo kistaarabu bila kuvurugana."

Aliwaagiza wabunge wa chama hicho kwenda majimboni mwao kusikiliza kero za wananchi badala ya kusubiri wakati wa uchaguzi.



Membe

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe ambaye naye anatajwa kuwa miongoni mwa wagombea amewataka waandishi waache kuandika kila siku habari za urais na badala yake waandike mambo ya maendeleo.

Akizungumza na waandishi wa habari jana baada ya kukutana na mabalozi wa nchi zinazoendelea kuhusu Mkutano wa Smart Partnership, unaotarajiwa kufanyika nchini, Membe alisema ni vizuri yakaandikwa mambo ya maendeleo na si kila wakati kuandika mambo ya urais.

"Mkutano kama huu nchi kama Kenya watauripoti vizuri na kwa undani hivyo mfanye hivyo si kila kitu urais 2015," alisema Membe. Mkutano huo utaanza Mei 28, hadi Juni Mosi na utajadili jinsi gani sayansi na teknolojia vinaweza kutumika kuzikwamua kiuchumi.

Imeandikwa na Kizitto Noya, Habel Chidawali na Boniface Meena.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…