Kashfa ya Richmond: Lowassa, Karamagi na Dkt. Msabaha Wajiuzulu

Anaandika Baba Askofu Rev.Dr.Benson Bagonza (PhD), Mkuu wa KKKT Dayosisi ya Karagwe.
___
Edward Ngoyai Lowasa ameondoka. Yuko mahali salama pasipo na mgao wa umeme wala usanii wa treni za umeme. Amepumzika baada ya kazi ngumu. Anapokufa mtu mzito kama Lowassa, kuna makundi matatu hujitokeza;
1. Wanaolia
2. Wanaofurahia
3. Wasiojua kama walie au wafurahie.

Makundi yote matatu tunayo katika kifo cha Edward Lowasa. Mimi sijui nipo kundi gani lakini niseme mambo manne ninayokumbuka:

1. Dola yetu ina mihimili mitatu: Bunge, serikali na mahakama. Lakini Lowassa alisababisha kuzaliwa kwa mihimili mitatu ndani ya mhimili wa bunge:
  • Wa kwanza ni Spika Samwel Sitta
  • Wa pili ni Wabunge mitume wakiongozwa na Mwakyembe
  • Mhimili wa 3 ulikua Edward Lowasa mwenyewe.
Hakika Bunge la 9 halitasahaulika kwa WEMA na UBAYA wake.

2. Alikuwa mtetezi asiye na mtetezi. Alikitetea chama chake, kikamtelekeza. Alimtetea Rais wake akamsaliti. Aliitetea nchi lakini nchi ikawatetea watesi wake.

3. Aliwapenda Wamasai, lakini Watesi wake wakamchonganisha na Wamasai. Wakahoji umasai wake na kudai Lowassa ni Mmeru. Lakini upendo wake kwa Wamasai ukawa na nguvu kuliko fitina za watesi wake. Akiwa hai na akiwa maiti Edward amebaki kuwa Mmasai.

4. Alisalitiwa na wengi aliowasaidia. Baada ya kumtumia kwa maslahi yao na kumtelekeza alibaki na Regina. Tujifunze kujali familia zetu. Mwisho wa yote, mzigo unabebwa na familia. Mambo ya “Pengo halitazibika” ni ulaghai mtupu. Kufa uone watakavyoziba pengo hata kabla ya mazishi.

LOWASSA KATIKA UBINADAMU WAKE:
A. Aliwaamini watu kuliko walivyomuamini.

B. Aliuchukia umaskini kwa vitendo. Watesi wake wakatumia hoja hii kumchonganisha na wananchi maskini. Wakasahau kuwa hata maskini wanauchukia umaskini wao na wanatamani kutoka.

C. Aliamini uzalendo si umaskini. Unaweza kuwa tajiri na ukawa mzalendo.

D. Alitumikia vyama 2 vikubwa. Vikamchafua na kumsafisha. Vikambeza na kumtukuza. Ameondoka akiwa mshindi kwa vyama vyote viwili.

E. Ameishi duniani miaka 70. Lakini Historia yake ni ndefu kuliko miaka yake. Ni mfupi wa umri lakini mrefu wa historia. Nenda Edward. Pole kwa Mama Regina, Watoto na wajukuu.!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Alionewa, issue hii ilipikwa kwa sababu za kisiasa.. Rais naye alitakiwa kujiuzuru kama ni hivyo
 
Nimeirudisha hapa kwa sababu naona part two ya hii movie imeanza,kuna watu bado wanamuona EL kama presidential material.Sijui tuko serious kiasi gani na hili taifa letu
Napingana na wewe mkuu
 
Nimeirudisha hapa kwa sababu naona part two ya hii movie imeanza,kuna watu bado wanamuona EL kama presidential material.Sijui tuko serious kiasi gani na hili taifa letu
Napingana na wewe mkuu
 
Nimeirudisha hapa kwa sababu naona part two ya hii movie imeanza,kuna watu bado wanamuona EL kama presidential material.Sijui tuko serious kiasi gani na hili taifa letu
Napingana na wewe mkuu
 
Augustoons said:
Hapo ndio haja ya kuwepo waziri asiye na wizara maaalum au naibu waziri mkuu inakuwepo. Ila ni washenzi tu hakuna haja ya kuweweseka nani aongoze shughuli za serikali bungeni Batilda Buriani si yupo? yeye si ndio mwakilishi wa waziri mkuu bunge?

Naam mi ndio maana hapa JF niliwahi kuwaambia kile kitabu cha UONGOZI WETU NA HATIMA YA TANZANIA alichoandika nyerere kina unabii mule,hakuna mtu anayekichambua lakini ipo siku,tusipoangalia mambo haya yalosemwa mule yatatimia.

Lowassa hana haja ya kusema hakupewa nafasi ya kujitetetea. Kamati haikuwa imemtuhumu mtu wala kuform chaji zozote,kamati ilialika watu kwenda mbele yake na kujieleza au kueleza lolote wanalolijua mbona hakwenda? Kisheria kujiuzulu kwa waziri mkuu hakutokani tu na kwamba yeye anahusika na hilo sakata bali ni ministerial responsibility, yeye kama kiranja wa baraza na mawaziri wake wameboronga bado alipaswa kujiuzulu hata kama asingehusika moja kwa moja.

Kama anadai hakupewa nafasi ya kujitetea ama kama anavyodai kuhojiwa? hakupaswa kuwasilisha barua ya kujiuzulu badala yake angewasilisha maelezo ya kujiteteta ili bunge lililomuidhinisha kuwa waziri mkuu lijadili utetezi wake na hatimaye litoe maamuzi,kwa nini kakimbilia kujiuzulu?

Afahamu kamati haikupendekeza aondoke ilimwambia atumie busara zake,sasa kama kujiuzulu na kulalamika ndio busara basi poa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…