Uchaguzi 2020 Kasi ya Rais Magufuli imemshinda Abood, anaweza asipitishwe kugombea Morogoro Mjini

Uchaguzi 2020 Kasi ya Rais Magufuli imemshinda Abood, anaweza asipitishwe kugombea Morogoro Mjini

miketee

Member
Joined
Feb 17, 2020
Posts
38
Reaction score
23
Serikali ya Awamu ya 5 inajitahidi sana kufanya miradi mikubwa ya kimkakati ndani ya muda mfupi kwa gharama kubwa.

Miradi hii inatosha sana kuiuza Serikali na CCM kwa wananchi kama wawakilishi wake wangekuwa wanamsaidia vizuri Rais kuitangaza na kuifafanua kwa wananchi

Miongoni mwa miradi hiyo, ni mradi wa Reli ya Kisasa (SGR) ambayo inapita Morogoro. Fursa zake ni nyingi kwa wakazi wa mji huo uliopo katikati ya Dar es Salaam na Dodoma. Katikati ni kutamu

Cha ajabu, Mfanyabiashara Abdulazizi Abood ambaye ni Mbunge anayefahamika zaidi hapo Morogoro, ameshindwa kumsaidia Rais katika eneo hili.

Kwa maslahi ya chama na wananchi, Mbunge huyu ilibidi awe kinara wa kuzungumza bungeni kuhusu mradi huo ili wakazi wa jimbo lake lineemeke na fursa zilizopo. Kufanya hivyo kungekuwa na faida nyingi kwake, chama na kiongozi wake mkuu, Rais Magufuli.

Badala yake, mfanyabiashara huyu amekuwa bubu bungeni na jimboni. Wenzake wanahangaika, yeye hata wananchi wake hakutani nao. Hii inaleta taswira kuwa ni kiongozi mbinafsi na anautumia Ubunge au siasa kulinda maslahi ya biashara zake, sio kuhudumia wananchi.

Haya mambo kwa bahati mbaya hayaendani na falsafa za Magufuli. Yeye ashasema hataki mambo ya business as usual. Kasi yake inataka kila mmoja afanye anachofanya kwa maslahi ya wananchi kwanza.

Yapo madai kwamba, Abood amegeuka kuwa mfadhili wa viongozi wa chama na sio mbunge wa kupeleka matatizo ya wananchi Bungeni. Pia amekuwa akitoa misaada ya kilaghai pale linapozuka jambo jimboni.

Kama hayo ni kweli, ajiandae kustaafu siasa na jina lake kukatwa kwenye kura za maoni mwaka huu. Mzee Magufuli hatamuacha salama.
 
Kama ni hivyo wabunge wa ccm wanaongoza kwa kutochangia bungeni.

Tupeni orodha ya wabunge 50 wasio changia bungeni 98% ni wa ccm tunaomba tuwafahamu ili wasirudi tena awamu hii.
Sio kumlenga tu abood kwa maslai yako.
 
Watu wa Morogoro kwani mmeshalichoka basi lake la msiba?
 
Ningekuwa kamanda wa TAKUKURU Morogoro ningemkamata huyu aliyeanzisha uzi. Mpaka aseme yafuatayo:-
1. Kamtuma nani.
2. Kamlipa shilingi ngapi.
3. Je ni mmoja wa wanaotaka kugombea?. Kama ndiyo kwa nini kaanza kampeni za maji taka kabla ya muda.
4. Ni rafiki au ndugu wa mtia nia?. Kama ndiyo ana kosa la kujibu labda kama ni chadema la sivyo mashtaka yanamuhusu.
 
Abood anatoa Usafiri bure watu wakifiwa. Swali, kwa Hiyo anaombea watu wafe ili apate political millage??
 
Mbeya hatuna maendeleo pamoja na bla bla za Sugu
 
kuna kijana wa CCM hapo Morogoro anaitwa Melikiel..anaweza kumuangusha Abood kimzaha mzaha tu...
 
Ningekuwa kamanda wa takukuru morogoro ningemkamata huyu aliyeanzisha uzi. Mpaka aseme yafuatayo:-
1. Kamtuma nani.
2. Kamlipa shilingi ngapi.
3. Je ni mmoja wa wanaotaka kugombea?. Kama ndiyo kwa nini kaanza kampeni za maji taka kabla ya muda.
4. Ni rafiki au ndugu wa mtia nia?. Kama ndiyo ana kosa la kujibu labda kama ni chadema la sivyo mashtaka yanamuhusu.
Mtoa haoja aweza kuwa hajaandika bandiko lake kisayansi wala utafiti
ILA hii ya kusema Takukuru wamkamate kwa sababu ulizotaja ni PUMBA ZAIDI ni hayo tu povu ruksa
 
Moro hatuhitaji mbunge maskini!

Ebu tuambie mpaka sasa umeajili watu wangapi zaidi ya housegirl wako?
 
Moro hatuhitaji mbunge maskini!

Ebu tuambie mpaka sasa umeajili watu wangapi zaidi ya housegirl wako?

Unayafahamu majukumu na kazi za Mbunge lakini? Sidhani kama kigezo cha kuwa tajiri na kuajiri kama kipo. Nikupe tu pole, maana lolote linaweza kutokea.

Uombee tu siku hiyo ya uteuzi wa mgombea, Mwenyekiti aamke vizuri! au kati ya hao watia nia wa hilo Jimbo la Moro Mjini, asiwepo Mgombea mwenye shahada ya Uzamili au PhD! Akiwepo/wakiwepo, hakika jina la huyo Abood wako litakatwa na Mwenyekiti muda utakapowadia.

Hii awamu matajiri hasa wale wenye rangi kama ya huyo Abood, watapumulia mashine kwenye kinyang'anyiro cha ubunge maana Magufuli anawaogopa kama ukoma! kutokana na changamoto alizopitia kwenye uchaguzi uliopita.
 
Unayafahamu majukumu na kazi za Mbunge lakini? Sidhani kama kigezo cha kuwa tajiri na kuajiri kama kipo. Nikupe tu pole, maana lolote linaweza kutokea.

Uombee tu siku hiyo ya uteuzi wa mgombea, Mwenyekiti aamke vizuri! au kati ya hao watia nia wa hilo Jimbo la Moro Mjini, asiwepo Mgombea mwenye shahada ya Uzamili au PhD! Akiwepo/wakiwepo, hakika jina la huyo Abood wako litakatwa na Mwenyekiti muda utakapowadia.

Hii awamu matajiri hasa wale wenye rangi kama ya huyo Abood, watapumulia mashine kwenye kinyang'anyiro cha ubunge maana Magufuli anawaogopa kama ukoma! kutokana na changamoto alizopitia kwenye uchaguzi uliopita.
Kiongozi masikini anakuwa na mawazo yakimasikini masikini
 
CCM kwa uzandiki na fitna ni kwenu!! Yaani mtu asipoimba mapambio tayari hafai. Mtu anaanzaje kuwaambia wananchi kuhusu umuhimu wa mradi ambayo haujaisha na haujaanza kutumika. Mradi ambao CCM wenyewe walisema utaanza kazi Decemba 2019. Akiulizwa kwanini haujaanza atapaswa kutoa majibu wakati yeye si msimamizi, msemaji wa serikali wala mkandarasi!!

Hivi kuna mtu mpaka sasa hajui habari ya reli hiyo?? Hayo mnayotaka Aboud aseme ni yapi??
 
Usiwapigie ramli wapiga kura huwezi jua kama Abood anawagusa moja kwa moja hawo wapiga kura 'most of these people need poverty alleviation'
 
Kwa kipindi hiki ambacho TARURA wanajenga na kufukia vibarabara vyetu.Katika kipindi hiki ambacho madaktari unaowaona hospital ya morogoro nao huja zahanati za pembezoni na kutoa huduma bila shida.
katika kipindi hiki kuna mobile na online mahakama.
katika kipindi hiki morogoro tumeletewa kamshina wa ardhi na hati zinatolewa morogoro.
Katika kipindi hiki ambacho watoto wanaenda shule na kutufanya tukose wasichana wa kazi .Sioni hata umuhimu wa mbunge yeyote anafaa ila abood ameshatajirika na hana shida na hutusaidia sana kwenye mazishi ya ndugu zetu.kitu ambacho zaidi ya 90% hawafanyi majimboni mwao.
 
Back
Top Bottom