Japokuwa kwa kiasi fulani takwimu hizo zinaweza kuwa zimekuzwa na ukweli kwamba watu wengi sasa wana ufahamu na wanakwenda kupima Kisukari, na pia vipimo vimekuwa vinapatikana sehemu mbali mbali...basi takwimu lazima zipande. Hata hivyo, huo ndio ukweli wenyewe..kuwa maisha tunayoishi sasa yanatuongezea hatari za kupata tatizo hili, tubadilikeni jamani..tujali tunachokula, na tuwe na utaratibu wa kufanya mazoezi mara kwa mara.
Lingine ni watoto wetu...siku hizi yaani idadi ya watoto wenye vitambi ni kubwa hasa ukienda kwenye shule hizi za Saint nini sijui..watoto wa kike kwa wa kiume wamefura mafuta hatari, na wazazi wanachukulia kama jambo la kawaida tu, na wengine wanaona ni sifa kuwa watoto eti ndio wana afya...si kweli, si afya ile! Tunawaexpose watoto kwenye life style hatarishi tangu umri mdogo, ndio hawa wanakuja kuishia kuwa na kisukari na high blood pressure katika umri mdogo..and its not their fault, ni fault yetu sisi kama wazazi kuwabambikiza maisha hatarishi watoto wanakuja athirika baadae!