Kasoro kubwa nilizoziona katika ujenzi wa uwanja wa KMC Complex

Kasoro kubwa nilizoziona katika ujenzi wa uwanja wa KMC Complex

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975
Pamoja na wazo jema la ujenzi wa uwanja wa KMC Complex, naomba nijikite kutoa kasoro kadhaa nilizoziona katika mradi huu.

Kasoro zangu zitajikita katika maeneo yafuatayo:
1. Design
2. Gharama za matumizi
3. Ufinyu wa nafasi

SEHEMU YA 1: DESIGN
Ukiangalia design ya ujenzi wa uwanja huo umekaa zaidi kama uwanja wa mazoezi kuliko uwanja wa mashindano. Hapa nitatolea mfano uzio mrefu uliojengwa kutenganisha sehemu ya kuchezea na mashabiki.

Ule uzio unaondoa ladha ya kuangalia mechi maana unalazimika kuangalia mpira kupitia kwenye zile nyavu. Hii hitilafu niliiona pia uwanja mpya wa Amaan ingawa level zinazoathirika kwenye uwanja ule ni chache za chini.

Kama ilishindikana kuweka majukwaa yaliyo juu maana ingehitaji kuweka platform ya cement, ilitakiwa kuwa na uzio mfupi halafu watumiaji wa uwanja watakiwe kuweka wahudumu kuzunguka uwanja kudhibiti mashabiki. Hii ingesaidia kuepuka hii adha.

Kasoro nyingine katika design ni kushindwa kuweka viti vya plastiki vya mtu mmoja mmoja na kuamua kuweka mabenchi. Pamoja na kwamba mabenchi yanadumu zaidi ila hii imekuja na changamoto zake.

Kwanza ni kushindwa kucontrol uingiaji wa mashabiki maana hata kama unaweza kukadiria watu watakaaje kwenye mabenchi, waswahili tunajua tunavyoweza kujibana. Hii inaondoa comfortability na burudani uliyoilipia na kuifuata.

Tungefanya mambo kisomi, tungeweka viti vya plastiki halafu hii gharama ingewekwa katika malipo ya matumizi ya uwanja. Yaani, unasema kwa mfano kila kiti kimegharimu 50,000 kukiweka. Basi katika bei za tiketi, kuna shilingi 500 inawekwa kama rejesho la gharama za kuweka kila viti. Utaona haifiki mwaka gharama za hivyo viti inakuwa imesharudi na viti standard vinaweza kukaa si chini ya miaka 5 kabla ya kuanza kuchakaa na kuharibika.

Sehemu ya 2 na 3 zinafuata...
 
SEHEMU YA 2: Gharama za matumizi

Kwenye hili kwanza sijaelewa inakuwaje unazipa vipaumbele timu zisiyo na makazi katika Manispaa ziutumie halafu timu za hapo hapo bado wanasema wanazifikiria kisa hazipo ligi kuu? Hapa naona kuna shida. Kuna umuhimu wa kubalance utoaji huduma na biashara. Nilishawahi kusema huu uwanja ni level ya ligi daraja la kwanza na shule za sekondari na ndiyo wateja wakubwa ambao wangetafutwa.

Wanasema gharama za kukodi kwa mechi ni milioni 6, mazoezi ni 300K, shughuli nyingine 200K. Tofauti ya bei ya mazoezi na mechi ni kubwa sana. Wangeenda deep zaidi kwenye kuset hizi bei badala ya kuangalia tu kigezo cha kusema hii ni mechi na hii ni mazoezi kwa kuangalia uwepo wa mashabiki.

Wajifunze jinsi ya kufanya hiyo biashara kwa weledi, wasifanye mambo kiserikali. Simba wamecheza hapo bila mashabiki hali kadhalika Yanga, kibiashara unazichaji vipi timu hizo kubwa na zenye uwezo 300K tu kutumua uwanja kucheza mechi hata kama hakuna mashabiki wanaoingia?

Sehemu ya 3 inafuata........
 
halafu watumiaji wa uwanja watakiwe kuweka wahudumu kuzunguka uwanja kudhibiti mashabiki.
Walichokikimbia ni hii gharama ya kuwalipa Hawa Watu maana hawatosimama bure na kingine ule uwanja umewekewa vile kwa ajili ya Security zaidi kwa wachezaji na pia km hujaangalia sio uwanja huo tu hata uwanja wa Azam Complex nao una hizo Waya zamani kipindi cha nyuma hazikuwepo Ila sasa wamezungusha Waya hizo, sababu ni Usalama wa wachezaji kuna mashabiki wengine ni Vichaa
 
Kwa nyongeza kuhusu issue ya viti, ukosefu wa viti (na ikichangiwa na udogo wa uwanja) unaturudisha kwa makomandoo wa milangoni na chaka la walinzi wa milangoni kujikusanyia pesa za milangoni ambazo haziingii katika mifuko ya klabu husika. Kuna watu wengi wanaangalia mechi za Simba pale KMC bila kulipia tiketi.

Mashabiki wengine wanalipia tiketi wanabaki kujibanza kwenye korido kwa sababu ya kukosa sehemu katika mabenchi ya kukaa au wanazuiwa kwa sababu ya uwanja "kujaa".

Matatizo mengi nchi hii ni "ripple effect" ya kasoro fulani ambayo ilikuwa "overlooked".
 
Kwa nyongeza kuhusu issue ya viti, ukosefu wa viti (na ikichangiwa na udogo wa uwanja) unaturudisha kwa makomandoo wa milangoni na chaka la walinzi wa milangoni kujikusanyia pesa za milangoni ambazo haziingii katika mifuko ya klabu husika. Kuna watu wengi wanaangalia mechi za Simba pale KMC bila kulipia tiketi.

Mashabiki wengine wanalipia tiketi wanabaki kujibanza kwenye korido kwa sababu ya kukosa sehemu katika mabenchi ya kukaa au wanazuiwa kwa sababu ya uwanja "kujaa".

Matatizo mengi nchi hii ni "ripple effect" ya kasoro fulani ambayo ilikuwa "overlooked".
Kijiwe cha pool table toka lini kikawa na washangiliaji wengi?
 
Walichokikimbia ni hii gharama ya kuwalipa Hawa Watu maana hawatosimama bure na kingine ule uwanja umewekewa vile kwa ajili ya Security zaidi kwa wachezaji na pia km hujaangalia sio uwanja huo tu hata uwanja wa Azam Complex nao una hizo Waya zamani kipindi cha nyuma hazikuwepo Ila sasa wamezungusha Waya hizo, sababu ni Usalama wa wachezaji kuna mashabiki wengine ni Vichaa
Tunarudi kule kule, kasoro hapo ni ya design. Ukiweka majukwaa ya juu, hata ukiweka uzio wa waya hauzuii mashabiki kuona mpira
vizuri, mfano ni uwanja wa Mkapa. Kwa kuwa wameweka majukwaa temporary kwa maana ya kushindwa kuweka platform ya zege ili majukwaa yawe juu, basi wangelazimika kufupisha zile nyaya.
 
Viwanja Vingi katika kama Italia, Brazil, Argentina na nchi nyingi za America ya kusini huwa wanaangalia na nyavu zao uwanjani
Sio utaratibu mzuri ndio maana kwenye mashindano makubwa hukuti hizo nyavu.
 
SEHEMU YA 2: Gharama za matumizi

Kwenye hili kwanza sijaelewa inakuwaje unazipa vipaumbele timu zisiyo na makazi katika Manispaa ziutumie halafu timu za hapo hapo bado wanasema wanazifikiria kisa hazipo ligi kuu? Hapa naona kuna shida. Kuna umuhimu wa kubalance utoaji huduma na biashara. Nilishawahi kusema huu uwanja ni level ya ligi daraja la kwanza na shule za sekondari na ndiyo wateja wakubwa ambao wangetafutwa.

Wanasema gharama za kukodi kwa mechi ni milioni 6, mazoezi ni 300K, shughuli nyingine 200K. Tofauti ya bei ya mazoezi na mechi ni kubwa sana. Wangeenda deep zaidi kwenye kuset hizi bei badala ya kuangalia tu kigezo cha kusema hii ni mechi na hii ni mazoezi kwa kuangalia uwepo wa mashabiki.

Wajifunze jinsi ya kufanya hiyo biashara kwa weledi, wasifanye mambo kiserikali. Simba wamecheza hapo bila mashabiki hali kadhalika Yanga, kibiashara unazichaji vipi timu hizo kubwa na zenye uwezo 300K tu kutumua uwanja kucheza mechi hata kama hakuna mashabiki wanaoingia?

Sehemu ya 3 inafuata........
Simba pale bunju wana kapeti nzuri tu ni swala la kusimika tu hata jukwaa la mabua nimeuangalia uwanja wa Jkt na huo wa kino boys tofauti na ule wa bunju ni mafundi welding kuingia mzigoni😂😂😂😂
 
Mkuu you are better than that. Mbona jamaa anatoa ushauri positive sana, nini tatizo?
Achana naye huyo. Hawa ndiyo wageni wa mitandao wanajenga chuki na wivu dhidi ya mtu wasiyemjua, wanabaki kumfuata kila wanapomuona. Wala asikuumize kichwa, ameshakula tofali lake saaafi mwache akafie mberee
 
Achana naye huyo. Hawa ndiyo wageni wa mitandao wanajenga chuki na wivu dhidi ya mtu, wanabaki kumfuata kila wanapomuona. Wala asikuumize kichwa, ameshakula tofali lake saaafi mwache akafie mberee
Jenga wa kwako shida nini kwani kukuambia ujenge wa kwako ndio kukuonea wivu kweli umechanganyikiwa
 
Back
Top Bottom