Kassim Majaliwa: Namuagiza Naibu Waziri Mkuu kushughulikia suala la uhaba wa mafuta nchini

Hivi shida kubwa kutoka Kwa wadau wa mafuta wanasema ni nini? Maana Kwa maelezo ya Waziri mkuu Kuna uhaba wa mafuta lakini ewura wanasema mafuta yapo,Je Ewura wanadanganya?
 
Ndugu Wananchi tunaomba utulivu kidogo, Mheshimiwa Naibu Waziri Mkuu anashauriana na Waziri wa Nishati kuona ni jinsi gani hili suala linashughulikiwa!
 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amemuagiza Naibu Waziri Mkuu, Dk Dotto Biteko kukaa na wadau wa mafuta ili washughulikie changamoto ya upatikanaji ndani ya siku saba.

Majaliwa ametoa kauli hiyo leo Alhamisi Septemba 7, 2023 alipokuwa anajibu maswali ya papo kwa hapo kutoka kwa wabunge katika kipindi cha asubuhi.

Katika swali la msingi, Mbunge wa Lushoto (CCM) Rashid Shangazi alitaka kujua Serikali inaweka mkakati gani kuhakikisha upatikanaji wa mafuta unakuwa ni mzuri nchini.

Mbunge huyo amesema kumekuwa na sintofahamu kuhusu suala la mafuta kwani licha ya bei zinazopanda kila wakati lakini mafuta hayo huwa hayapatikani kila inapofika jumatano ya kwanza ya mwezi ambayo ni siku ya kutangaza bei mpya ya bidhaa hiyo.

“Nikiri tunayochangamoto ya mafuta nchini, lakini zipo jitihada mbalimbali ambazo zinachukuliwa na Serikali kuondokana na tatizo hilo kwani nishati hiyo ndiyo injini ya uchumi,” amesema Majaliwa.

Waziri Mkuu amesema tayari Rais alishamteua Naibu Waziri Mkuu ambaye ni Waziri wa Nishati pia ambaye ameanza kushughulikia jambo hilo kwa kukaa na wadau mbalimbali.

“Niendelee kumuagiza Naibu Waziri Mkuu aendelee kushughulikia hili ndani ya wiki moja tuwe na majibu na katika hilo wapanue wigo kwa waagiza mafuta ili tuwe na mafuta ya kutosha na suala la bei tutaangalia huko mbeleni,” amesema Majaliwa.

Mjadala huo umeibuka ikiwa ni siku moja tu tangu Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura) kutangaza bei mpya za mafuta zitakazotumika Septemba ambazo zimepaa ikilinganishwa na Agosti.

Katika taarifa kwa umma iliyotolewa jana Jumanne Septemba 5, 2023 saa 4 usiku na Mkurugenzi Mkuu wa mamlaka hiyo, Dk James Mwainyakule imeonesha kuwa kuanzia Jumatano Septemba 6 jijini Dar es Salaam petroli itauzwa Sh3,213 na dizeli itauzwa kwa Sh3,259.

Bei hizo zinamaanisha kuwa katika Mkoa wa Dar es Salaam petroli imeongezeka kwa Sh14 kutoka Sh3,199 ya Agosti huku dizeli ikiongezeka zaidi kwa Sh324.

MWANANCHI
 
Upatikananji wa umeme wa uhakika na upatikanaji wa mafuta wa uhakika kwa siku za karibuni umekuwa changamoto kubwa. Vyote viko chini ya Biteko. Je, atatatua changamoto hizi? Au zitamtatua? Acha tuone.
 
Kiswaswadu anafurukuta
 
Hii ni Kaole
 
Hivi bei haiwezi kuwa moja ,Nchi nzima? Km bidhaa zingine
 
DUUU
 
Hizi Sinema za Mafuta na Umeme, Serikali yenyewe ndiyo inazijua. Kwa maana inaonekana wanakula pamoja na hao Waagizaji.

Juzi majira ya saa 2 usiku nilienda kujaza Petrol kwenye gari yangu, ajabu waliniambia Mafuta hayapo. Jana majira ya saa 3 asubuhi Kituo hicho hicho cha Mafuta wakaniuzia Petrol waliyosema haipo Jana yake ila kwa bei ya Juu kidogo ya shilingi 3,302 kwa lita.

Miaka ya nyuma kulikuwa na Hadithi inasema "Nani atamfunga Paka Kengele"?

Wacha Wananchi tuendelee kuteseka hadi akili zikiturudia.
 
Yeye mwenyewe, wiki moja ya ripoti ya kuungua kwa soko la kariakoo imeisha?
 
Hivi bei haiwezi kuwa moja ,Nchi nzima? Km bidhaa zingine
Inashangaza sana.
Bidhaa kama soda, vocha, umeme, bia nk bei ni moja nchi nzima.
Mafuta bei tofauti lkn Latra wanatangaza nauli moja nchi nzima wakati bei za mafuta hazilingani.
Kwa sababu ya mafuta, tulio mbali na Dar; kila kitu bei juu.
Angalia bei za mkoa wa Kagera.
Utadhani serikali haitaki waendeshe magari na pikipiki.
Ewura pangeni bei moja kama mlivyofanya kwa umeme.
Mungu ibariki Tanzania.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…