Katavi: Wananchi Tanganyika walalamika kufyekewa mahindi hekari 60

Katavi: Wananchi Tanganyika walalamika kufyekewa mahindi hekari 60

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760

Baadhi ya Wananchi kijiji cha Kagunga Wilaya ya Tanganyika, Mkoa wa Katavi wamelalamika kufyekewa hekari 60 za mahindi jambo ambalo wamedai kuzorotesha ukuaji wa sekta kilimo na kujikwamua kiuchumi.

Tukio hilo la kufyekewa mahindi limetokea hivi karibuni kutokana na kile kinachotajwa ni uvamizi katika maeneo ya misitu ambayo inazuio la shughuli za binadamu.

Moja wa wahanga wa kufyekewa mahidi, Georgina Joseph mkazi wa kata ya Kasekese amedai kuwa suala la kufyekewa mahidi yao ni uonevu ambao haukubaliki kwa masirahi ya kupambana na umasikini.

Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika, Onesmo Buswelu amesema kuwa wilaya hiyo imetenga maeneo ya kilimo na uhifadhi hivyo idara ya maliasili imnekuwa imara kusimamia rasilimali ya misitu kwa kutumia sheria ili kuhifadhi misitu.

Pia soma ~ RC Mrindoko ufyekaji wa Mahindi kwa Wananchi wa Wilaya ya Tanganyika si maelekezo ya Serikali
 

Attachments

  • 2025-01-10 15-06-50.mp4
    73.6 MB
Baadhi ya Wananchi kijiji cha Kagunga Wilaya ya Tanganyika, Mkoa wa Katavi wamelalamika kufyekewa hekari 60 za mahindi jambo ambalo wamedai kuzorotesha ukuaji wa sekta kilimo na kujikwamua kiuchumi.

Tukio hilo la kufyekewa mahindi limetokea hivi karibuni kutokana na kile kinachotajwa ni uvamizi katika maeneo ya misitu ambayo inazuio la shughuli za binadamu.

Moja wa wahanga wa kufyekewa mahidi, Georgina Joseph mkazi wa kata ya Kasekese amedai kuwa suala la kufyekewa mahidi yao ni uonevu ambao haukubaliki kwa masirahi ya kupambana na umasikini.

Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika, Onesmo Buswelu amesema kuwa wilaya hiyo imetenga maeneo ya kilimo na uhifadhi hivyo idara ya maliasili imnekuwa imara kusimamia rasilimali ya misitu kwa kutumia sheria ili kuhifadhi misitu.
Wanaanda mashamba wanawaangalia,wanalima wanawaangalia,wanapanda wanawaangalia,yameota wanafyeka! Ubinadamu kazi.
 
Back
Top Bottom