Kati ya Fuso Tandamu na Scania Kipisi ipi ni gari nzuri kwa mtu anayeiingia kwa mara ya kwanza kwenye biashara ya usafirishaji?

Kati ya Fuso Tandamu na Scania Kipisi ipi ni gari nzuri kwa mtu anayeiingia kwa mara ya kwanza kwenye biashara ya usafirishaji?

Sibishani na wewe kwani sio mashindano.
Nadhani ungekua umeweka kila gari hapo juu inabeba kiasi gani ungekua vema. Yaani unashangaa gari kubeba tani 30??? Really? Sidhani kama ulikua serious na ukisemacho.

Sikushangaa gari kubeba Tani 30 kuna sehemu(Sio Bongo) Chuma zinavuta mpaka Tan 50 na kuna kipindi cha nyuma Tulikua tunatwisha mpaka 35-40 hapa hapa

Nilitaka uwe precise tu na kama ulivyosema hapo chini na Danpol nilikuelewa vibaya

Mimi nilikua nimefocus kwenye swali la mtoa mada wewe uliongelea Trucks zote kwa ujumla

Pamoja sana mkuu
 
Nafikiri anza na Fuso ili kuweza kukomaa kwa kuexperience vitu kadha wa kadha ili utakapo fikia levels za Scania usisumbuke sana. Sababu pia hata gharama ya vipuli Scania iko juu sana.

Ukiweza agiza kabisa Japan ila kama ukichukua used hapa basi hakikisha unapata yenye mileage ndogo vinginevyo ni majuto.

NB:Ukitaka kuwin biashara ya usafirishaji kuwa smart kwa kununua gari(haswa ya kuagiza nje) itumie mpaka pale utakapo ona imerudisha mtaji wako kabla haija anza kusumbua uza ile ndiyo itakuwa faida yako then agiza tena, Hivyo hivyo hapo utaipenda hii biashara la sivyo utaichukiana kuanza kuwaza ushirikina.
Kwa uzoefu wako zile SCANIA kama zakubebea mbao Iringa,huchukua muda Gani kurudisha Fedha ya mtaji?..
 
Kwa uzoefu wako zile SCANIA kama zakubebea mbao Iringa,huchukua muda Gani kurudisha Fedha ya mtaji?..
Miezi nane nane hivi kama linapiga kazi mara mbili kila mwezi.
 
Back
Top Bottom