Kati ya mambo hayo, Kidedea na Kaole nani walibamba zaidi tasnia ya michezo ya kuigiza?

ilibidi kaole igizo lao liwe la muendelezo like tamthilia kama za isidingo, days of our lives, the bold and the beautiful. sijui walikwama wapi aisee sijui ITV waliwapa vikwazo hawa jamaa. Moja ya maigizo yao nayoyakubali hadi kesho ni Sayari, Jahazi, na tetemo
 
Jahazi daaah umenikumbusha mbali mkuu
 
Kaone ndio baba wa tamthilia hapa nchini. Kila msanii alitendea haki bafasi aliyopewa. Kwa kifupi kaole ndio imewatoa Joti na Mpaki, Bambo, Seki japo kwa sasa simsikii sana.
Mtu niliyekuwa na mkubali na bado namkubali sana na anacheza kiuhalisia sana ni bi star, mke wa Muhogo Mchungu.

Kwa kifupi kaole wapo juu japo sina uhakika kama bado wapo maana ivumayo haidumu
 
Joti, Mpoki na Seki wametokea Mambo hayo ya wale kina Bishanga na Richie. Bambo ni kweli ametokea kidedea. Makundi yote hayo kwa sasa hayapo tena imebaki story tu!
 
Kipindi kile sanaa ya vikundi vya maigizo ilikuwa hailipi sana watu walikuwa wanatafuta kuonyesha sura tu wakipata dili kwingine wanatoboa. Halafu I TV walikuwa wanawalipa pesa kidogo sana, halafu kulikuwa na jamaa anaitwa Chriss Muhenga ambae ndio alikuwa mtayarishaji na muongozaji wa vipindi vyote vya maigizo ITV enzi hizo. Huyu jamaa alilalamikiwa sana na wasanii kuwa anawanyonya.
 
Nafkiri alishafariki huyo jamaa
 
nakumbuka 2004 kaole walikua na igizo linaitwa Gharika ambayo masta kanumba alicheza na ray na johar,nafikir hata movie ya Johar yote walikopi ktk igizo hili..jumamosi moja saa tatu ucku tuliibiwa godoro jipya kutokana na nyumba nzima hadi ya jirani kuhamia sebureni kwetu bila kuwa na umakini na milango ya vyumba
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…