Kati ya Mombasa na Nairobi wapi panamfaa mtafutaji?

Kati ya Mombasa na Nairobi wapi panamfaa mtafutaji?

Jamii forum kabla ya 2015 ilikuwa na vichwa sana na kulikuwa na mpaka viongozi wa serikal hakika ilikuwa ni home of great thinker ila kwasasa kuna vijana wa ovyo mno nimeamini kila lenye mwanzo halikosi kuwa na mwisho
kabisa, forum imevamiwa hadi na Wadada wa kazi, House Boy, na vijana wajinga wajinga. Forum hii sio ile ya enzi zile 2015 kurudi nyuma.
 
Jamii forum kabla ya 2015 ilikuwa na vichwa sana na kulikuwa na mpaka viongozi wa serikal hakika ilikuwa ni home of great thinker ila kwasasa kuna vijana wa ovyo mno nimeamini kila lenye mwanzo halikosi kuwa na mwisho
Huu ndio mfano halisi wa vijana wa kitanzania tulio nao.
Uwezo wa kufikiri mambo ya msingi na yenye tija ni mdogo sana.

Pia hali hii ya kudorora kwa jukwaa hili imechangiwa na utendaji wa hovyo wa Moderator wake.
Mabandiko ya kijinga kama haya enzi zile yalikuwa yanafutwa mara moja.
Inaonesha mods wa sasa ni group moja na hao wachafuzi.

MK254 hebu mpe kijana mwongozo wa hitaji lake.
 
kabisa, forum imevamiwa hadi na Wadada wa kazi, House Boy, na vijana wajinga wajinga. Forum hii sio ile ya enzi zile 2015 kurudi nyuma.
Kweli kabisa Mimi nimejiunga jforum mara ya kwanza 2012 Kwa ID nyingine ilikuwa fire sana,ila sasahivi Bora hata Facebook.
 
Jamaa kaomba ushauri mzuri sana ila amesahau jf ya Sasa imejaa wajinga wajinga sana, Bora angeomba hata kwenye comment kwenye post za watu maarufu Instagram
 
Habari ndugu zang Mlio wahi kusafiri East Africa hasa Kenya

Naomba kujua Mombasa na nairobi wapi pana mfaa mtafutaji?
Bila shaka asilimia kubwa ya wanaokujibu hapa hata Mombasa hawajawahi kufika ila tu wamesikia story tu. Wanavyojibu ni kama vile ukifika huko hata unaweza kubakwa... Story hazina ukweli wowote.
Jibu, naona Nairobi japo ni kugumu kuliko hata DSM.
 
Mkenya hapa, Kote kuzuri ila Nairobi fursa ni nyingi sana kwa mtu uliyejasiri kiutafutaji.
Mkuu inakuaje? Umewai kuishi Tanzania? Kiujumla kuna utofauti gani kimaisha kati ya hizi nchi mbili,Kenya na Tanzania kitamaduni na biashara pia?
 
Jamii forum kabla ya 2015 ilikuwa na vichwa sana na kulikuwa na mpaka viongozi wa serikal hakika ilikuwa ni home of great thinker ila kwasasa kuna vijana wa ovyo mno nimeamini kila lenye mwanzo halikosi kuwa na mwisho
Mi nishalalamika sana kuhusu hili ukienda kwenye Uzi complaints nimenadika. Mods inabidi wadhibiti hawa vijana. Kila jukwaa kwa Sasa piwe serious or not vijana ni kujibu mambo ya hovyo hovyo tu. Mtu kauliza kitu seriously wao wanaleta ujinga. Bwana Melo fanyeni mageuzi. Niliandika hapa nikajibiwa et utandawazi. Sasa hii inafanya JF isiwe Tena na mvuto. Now a days hata zile habari ambazo mods wanazirusha hata kwenye mitandao mingine ya kijamii 80% ni wao ndo wanazianzisha au zikianzishwa utakuta zina maana sana ila Sasa wacahngiaji mmmh utamshangaa. Jf inahitaji mageuzi
 
Mkuu inakuaje? Umewai kuishi Tanzania? Kiujumla kuna utofauti gani kimaisha kati ya hizi nchi mbili,Kenya na Tanzania kitamaduni na biashara pia?

Nimeishi mataifa kadhaa hapa EAC.....
Tofauti kubwa ya Dar na Nairobi ni kwamba, kwa Nairobi maisha ni ya mwendo kasi, yaani kila mtu yupo mbioni kusaka hela, fursa ni nyingi sema zinapaswa kwa mtu jasiri usiye mwoga mwoga au kuona aibu.
kasoro ya Nairobi ni kukosa ule mshikamano wa kijamii, yaani kila mtu yuko kivyake, kila mnapokutana asilimia kubwa ya mazungumzo yenu ni biashara tu.....kwa kweli japo mimi Mkenya ila hayo maisha kuna wakati huwa nayaona kama soul less, haipaswi tuwaze hela sana.

Kwa Dar, pia penyewe niliona pana kasi ya kiaina lakini sio balaa kama Nairobi, kuna mshikamano baina ya watu kwenye jamii.
 
Nimeishi mataifa kadhaa hapa EAC.....
Tofauti kubwa ya Dar na Nairobi ni kwamba, kwa Nairobi maisha ni ya mwendo kasi, yaani kila mtu yupo mbioni kusaka hela, fursa ni nyingi sema zinapaswa kwa mtu jasiri usiye mwoga mwoga au kuona aibu.
kasoro ya Nairobi ni kukosa ule mshikamano wa kijamii, yaani kila mtu yuko kivyake, kila mnapokutana asilimia kubwa ya mazungumzo yenu ni biashara tu.....kwa kweli japo mimi Mkenya ila hayo maisha kuna wakati huwa nayaona kama soul less, haipaswi tuwaze hela sana.

Kwa Dar, pia penyewe niliona pana kasi ya kiaina lakini sio balaa kama Nairobi, kuna mshikamano baina ya watu kwenye jamii.
Ahsante kwa maelezo mazuri mkuu, naomba niongeze swali jingine,ni stadi au fani zipi za kawaida ambazo vijana wa Nairobi wanafanya ili kujipatia kipato kwa wasio katika ajira rasmi au wasio na mitaji ya biashara? Mfano kwa dar unawezakuta vijana machinga wa mitaji midogo sana,au wanaowaremba wanawake cjuw urembo wa kucha n.k,je kwa huko hivyo vitu vipo pia?
 
Jamii forum kabla ya 2015 ilikuwa na vichwa sana na kulikuwa na mpaka viongozi wa serikal hakika ilikuwa ni home of great thinker ila kwasasa kuna vijana wa ovyo mno nimeamini kila lenye mwanzo halikosi kuwa na mwisho
Joined Feb_2023 alafu unazungumzia habari ya 2015 are you serious?
 
Nimeishi mataifa kadhaa hapa EAC.....
Tofauti kubwa ya Dar na Nairobi ni kwamba, kwa Nairobi maisha ni ya mwendo kasi, yaani kila mtu yupo mbioni kusaka hela, fursa ni nyingi sema zinapaswa kwa mtu jasiri usiye mwoga mwoga au kuona aibu.
kasoro ya Nairobi ni kukosa ule mshikamano wa kijamii, yaani kila mtu yuko kivyake, kila mnapokutana asilimia kubwa ya mazungumzo yenu ni biashara tu.....kwa kweli japo mimi Mkenya ila hayo maisha kuna wakati huwa nayaona kama soul less, haipaswi tuwaze hela sana.

Kwa Dar, pia penyewe niliona pana kasi ya kiaina lakini sio balaa kama Nairobi, kuna mshikamano baina ya watu kwenye jamii.
haipaswi tuwaze hela sana

ulianza vizuri ila hapo👆 umeharibu tunatakiwa tuwaze hela sana.

 
Ukisoma comment za mwanzo mwanzo unaweza ukahisi ukifika Mombasa automatically unajikuta huna bukta na umefungwa kamba.
 
Ahsante kwa maelezo mazuri mkuu, naomba niongeze swali jingine,ni stadi au fani zipi za kawaida ambazo vijana wa Nairobi wanafanya ili kujipatia kipato kwa wasio katika ajira rasmi au wasio na mitaji ya biashara? Mfano kwa dar unawezakuta vijana machinga wa mitaji midogo sana,au wanaowaremba wanawake cjuw urembo wa kucha n.k,je kwa huko hivyo vitu vipo pia?

Hivyo vitu vipo miji yote, yaani tena siku hizi naviona kote kote, nimekua naona Wanyarwanda wameshikilia biashara za kihivyo maeneo mengi Nairobi, jamaa ni wajasiri sana kwenye utafutaji, japo pia kuna Watanzania wengi tu ila wakutokea Kilimanjaro akina Mangi, huu mwezi wa Disemba huongozana kurudi kwao.
 
haipaswi tuwaze hela sana

ulianza vizuri ila hapo👆 umeharibu tunatakiwa tuwaze hela sana.

Ha ha ha!! hamnaa bana, haya maisha utazikwa uziache...kila kitu kwa wastani.
 
Hivyo vitu vipo miji yote, yaani tena siku hizi naviona kote kote, nimekua naona Wanyarwanda wameshikilia biashara za kihivyo maeneo mengi Nairobi, jamaa ni wajasiri sana kwenye utafutaji, japo pia kuna Watanzania wengi tu ila wakutokea Kilimanjaro akina Mangi, huu mwezi wa Disemba huongozana kurudi kwao.
Anhaa shukrani sana mkuu, pengine unaweza tutajia gharama za chumba Cha kuishi maeneo ya kawaida kwa mwezi ni shingapi ya kitanzania?
 
Ha ha ha!! hamnaa bana, haya maisha utazikwa uziache...kila kitu kwa wastani.
Bora uzikwe uziache kuliko uzikwe kapuku i mean masikini..... family yako inaweza ikanufaika nazo kwa namna moja ama nyingine.
 
Anhaa shukrani sana mkuu, pengine unaweza tutajia gharama za chumba Cha kuishi maeneo ya kawaida kwa mwezi ni shingapi ya kitanzania?

Vyumba vya kuishi ni kama Bongo tu, tofauti itakua ndogo sana, japo pia inategemea mtaa kwa mtaa
Kuanzia elfu tano za Kenya (Tshs 80,000)
Unaweza ukachukua chumba aina ya bedsitter, yaani chumba kimoja chenye choo ndani kwa 7,000 (Tshs 115,000)
Ni suala la kutafiti tu, kuna websites nyingi zenye taarifa
 
Back
Top Bottom