Katiba hii haifai na inaweza kutuletea matatizo hapo baadaye

Katiba hii haifai na inaweza kutuletea matatizo hapo baadaye

Wakusoma 12

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2017
Posts
4,035
Reaction score
11,462
Ndugu zangu bado tupo katika majonzi makubwa kama taifa ya kumpoteza kiongozi mkuu.

Yote juu ya yote Mungu atatusimamia nalo litapita.

Nachotaka kusema hapa ni huu utaratibu wa katiba kumtambua makamu wa Rais kama rais iwapo Rais aliyepo madarakani atafariki. Hii ni hatari kwani itatokea siku moja makamu asiye mwaminifu, lakini pia tunafahamu fika namna ilivyokuwa kazi ngumu kupata urais katika nchi za Kiafrika.

Hivyo kulingana na hali hii makamu wa Rais anaweza kutumiwa kama ngao na baaadhi ya watu wasio waaminifu na kumdhuru Rais ili kujitwalia madaraka. Hivyo kwa kutambua umuhimu wa nafasi nyeti ya urais ni bora makamu wa rais aruhusiwe tu kuwa Rais kama kipindi cha rais aliyekufa kitakuwa hakizidi mwaka mmoja na iwapo rais atafariki akiwa madarakani na muda wa uongozi wake utakuwani bado unazaidi ya mwaka mmoja mbele ili kukamilika basi, serikali ya mpito iundwe na kiongozi wake awe makamu wa Rais na ahitishe uchaguzi wa Rais ndani ya miezi 6.

Tunajifunza kutokana na makosa.
 
Kabla ya kulizungumza hili ni lazima pia ufahamu sababu zipi zilipelekea wakina Mzee Nyerere na Bomani kukubali kuweka nafasi ya mgombea mwenza kwenye katiba. Huu ni utaratibu mzuri tu na una mantiki kubwa kisheria kwasababu kwenye uchaguzi mkuu huwa tunachagua Raisi na Makamu wake kwa pamoja. Hivyo ni lazima uweke kichwani kwamba huyu mama alikuwa ni mgombea kama ambavyo Raisi Magufuli aligombea, na alipitishwa na chama kama ambavyo Raisi Magufuli alipitishwa.
 
Katiba ya Tanzania ni mbovu hilo liko wazi
 
Makamu wa Rais ni sawa na Rais na ndio maana akaitwa mgombea mwenza sifa zao wote zinafanana acha kelele piga kazi aseeee.
 
Munaona makosa kwa kuwa Makamu ni Mwanamke?
au kwa kuwa ni mzanzibari?
Au kwa kuwa Ni muislamu?
Au kwa kuwa Nyinyi watu wa Tanzania Bara Hamukutarajia kuwa sikumoja mutashika nafasi ya umakamu?
Munalo hilo ,sasa ni zamu yenu kushika mikasi na kuzindua makongamano.
Kikatiba makamo wa raisi amefanywa mtu wa kuzururza zurura tu huku na kule kuzindua na kufungua miradi.Ki kawaida Makamo wa Raisi hukabidhiwa Box la mikasi.
Najua wengi sasa wataibuka na Agenda ya Katiba Mpya ,ukiachilia wapinzani.
Too much Know mbele Kiza .
Wacha tuisome Namba kwanza ili tuthibitishe kuwa kuna umuhimu wa katiba Mpya kama Wananchi walivyopendekeza Kwenye Tume ya Warioba.
 
Katiba Mpya iseme iwapo Raisi atakapofariki wakiwa Ofisini kuwe na Uchaguzi mpya

Pia aseme kama Chama chochote kitakapofikisha asilimia 30 za kura kuwe na Serikali ya mseto

Huko Zanzibar inafanyika mpaka Damu imwagike

Haha mambo yanawezekana ni uamuzi na trust me Watanzania tutapendana zaidi
 
Ndugu zangu bado tupo katika majonzi makubwa kama taifa ya kumpoteza kiongozi mkuu.

Yote juu ya yote Mungu atatusimamia nalo litapita.

Nachotaka kusema hapa ni huu utaratibu wa katiba kumtambua makamu wa Rais kama rais iwapo Rais aliyepo madarakani atafariki. Hii ni hatari kwani itatokea siku moja makamu asiye mwaminifu, lakini pia tunafahamu fika namna ilivyokuwa kazi ngumu kupata urais katika nchi za Kiafrika.

Hivyo kulingana na hali hii makamu wa Rais anaweza kutumiwa kama ngao na baaadhi ya watu wasio waaminifu na kumdhuru Rais ili kujitwalia madaraka. Hivyo kwa kutambua umuhimu wa nafasi nyeti ya urais ni bora makamu wa rais aruhusiwe tu kuwa Rais kama kipindi cha rais aliyekufa kitakuwa hakizidi mwaka mmoja na iwapo rais atafariki akiwa madarakani na muda wa uongozi wake utakuwani bado unazaidi ya mwaka mmoja mbele ili kukamilika basi, serikali ya mpito iundwe na kiongozi wake awe makamu wa Rais na ahitishe uchaguzi wa Rais ndani ya miezi 6.

Tunajifunza kutokana na makosa.
Lumumba mnakumbuka shuka asubuhi 🤣
 
Kweli kabisa,hii katiba inaweza pelekea makamu akampiga kipapai Rais mteule ili yeye awe Rais. Mleta mada anahoja ya msingi sana.Lazima tuwe na katiba isoyotoa mwanya wa makamu kumsaliti Rais mteule. Huwezi jua maana pesa ndio iliyosababisha Yuda msaliti Yesu.Sizani km mleta mada anahofu na Rais kuwa mwanamke au Mzanzibari.

Afterall,Rais awe Me,Ke, Mzanzibari au Mtanganyika sizani km kuna mtu atakayegawana nae mshahara au posho zake. Posho na mshahara wake atakula na familia yake.
 
Ndugu zangu bado tupo katika majonzi makubwa kama taifa ya kumpoteza kiongozi mkuu.

Yote juu ya yote Mungu atatusimamia nalo litapita.

Nachotaka kusema hapa ni huu utaratibu wa katiba kumtambua makamu wa Rais kama rais iwapo Rais aliyepo madarakani atafariki. Hii ni hatari kwani itatokea siku moja makamu asiye mwaminifu, lakini pia tunafahamu fika namna ilivyokuwa kazi ngumu kupata urais katika nchi za Kiafrika.

Hivyo kulingana na hali hii makamu wa Rais anaweza kutumiwa kama ngao na baaadhi ya watu wasio waaminifu na kumdhuru Rais ili kujitwalia madaraka. Hivyo kwa kutambua umuhimu wa nafasi nyeti ya urais ni bora makamu wa rais aruhusiwe tu kuwa Rais kama kipindi cha rais aliyekufa kitakuwa hakizidi mwaka mmoja na iwapo rais atafariki akiwa madarakani na muda wa uongozi wake utakuwani bado unazaidi ya mwaka mmoja mbele ili kukamilika basi, serikali ya mpito iundwe na kiongozi wake awe makamu wa Rais na ahitishe uchaguzi wa Rais ndani ya miezi 6.

Tunajifunza kutokana na makosa.
Makamu asiye muaminifu anawezaje kukubalika na chama na mgombea na akapigiwa kura na wananchi?

Nchi ikiweza kumchagua mtu asiye muaminifu kuwa makamu wa rais hivyo, ina tatizo kubwa kuliko makamu wa rais kuwa rais.
 
Chakukusaidia wewe mleta mada,si rahisi kama unavyofikiri.naukiwa na mawazo hayo hautoishia hapo tu baadae utasema walinzi wakiwa na tamaa watachukua nchi na pia utaendelea kwa wakuu wa vyombo vya usalama nk
 
Kwani uzuri wa katiba unaangalia kipengele kimoja tu?
 
Munaona makosa kwa kuwa Makamu ni Mwanamke?
au kwa kuwa ni mzanzibari?
Au kwa kuwa Ni muislamu?
Au kwa kuwa Nyinyi watu wa Tanzania Bara Hamukutarajia kuwa sikumoja mutashika nafasi ya umakamu?
Munalo hilo ,sasa ni zamu yenu kushika mikasi na kuzindua makongamano.
Kikatiba makamo wa raisi amefanywa mtu wa kuzururza zurura tu huku na kule kuzindua na kufungua miradi.Ki kawaida Makamo wa Raisi hukabidhiwa Box la mikasi.
Najua wengi sasa wataibuka na Agenda ya Katiba Mpya ,ukiachilia wapinzani.
Too much Know mbele Kiza .
Wacha tuisome Namba kwanza ili tuthibitishe kuwa kuna umuhimu wa katiba Mpya kama Wananchi walivyopendekeza Kwenye Tume ya Warioba.
Katiba mpya inasemaje inapotokea rais wa jmt anapofarik baada ya kutumikia miez sita baada ya kiapo???
 
Katiba Mpya iseme iwapo Raisi atakapofariki wakiwa Ofisini kuwe na Uchaguzi mpya

Pia aseme kama Chama chochote kitakapofikisha asilimia 30 za kura kuwe na Serikali ya mseto

Huko Zanzibar inafanyika mpaka Damu imwagike

Haha mambo yanawezekana ni uamuzi na trust me Watanzania tutapendana zaidi
Na lazima katiba hiyo mpya iseme kipind tunasubir uchaguz mpya ni nan atakayekaim huo urais
 
Makamu asiye muaminifu anawezaje kukubalika na chama na mgombea na akapigiwa kura na wananchi?

Nchi ikiweza kumchagua mtu asiye muaminifu kuwa makamu wa rais hivyo, ina tatizo kubwa kuliko makamu wa rais kuwa rais.


Kuna makundi yanamtaja Nchimbi awe VP
Imagine that
 
Back
Top Bottom