Katiba Inayopendekezwa si ya CCM

Katiba Inayopendekezwa si ya CCM

Kwani majina ya mtu yanakuwa kwenye paji ya uso wake, shati zake na suruali zake? Tunaweza kutambua ni katiba ya viongozi tawala kwa sababu ndio walioondoa maadili ya viongozi: (1) uadilifu, (2) uwajibikaji na (3) uwazi. Wangewezaje kuyaingiza hayo wakati wameharibu? Kesi ya ngedere anapelekewa nyani!!

Ndio hao wenye akaunti nje zenye pesa chafu wakiongozwa na mzee wa vijisenti. Kuhusu zuio la kuweka pesa ng'ambo ya nchi wanasema: Sheria zitatungwa za namna ya kuweka fedha nje. Kwani ni watanzania wangapi wa kawaida wanaweza kuweka fedha nje ya nchi? Hao wanaokula mlo mmoja?

Tuache ushabiki, nchi hii ni yetu sote.
naona umeandika vitu usivyovijua wala kuvisoma, eti maadili wameondoa, uadilifu, uwajibikaji na uwazi, Hivi nkuulize wewe umesoma Katiba ya wapi ukaona kuwa hivo vitu vimeondoloewa? Sasa huko ndo kupotosha watanzania, kwanza unaonekana hujaisoma hiyo katiba pili unaonekana kuwa wewe ni bendera fuata upepo, sasa kwa taarifa yako Hakuna kitu kilichoondolewa kati ya hivo vyote ulivyotaja hapo juu, kasome IBARA YA 28-31 utaona uwongo wako na dhamira itakusuta kwa uwongp uloanika hapo juu. Hanisi mkubwa
 
Back
Top Bottom