Katiba kicheko vyama vyote

Katiba kicheko vyama vyote

Mwanzo mzuri, taratibu karibu tunaanza kuweka pembeni tofauti zetu za kiitikadi kwenye mambo muhimu ya Taifa. Hongereni wabunge na viongozi wa CDM, NCCR-Mageuzi na CUF kwa kuonyesha njia hata pale mlipotukanwa na kubezwa. Hongera JK kwa kuwa 'msikivu' anglau kwa hili la Katiba Mpya. Natumaini wabunge wa sisiemu na mawaziri hususan chikawe, wasira na lukuvi watakuwa wamejifunza kitu kutokana na hili. Nasi tunasubiri kuona na kusikia mlichojifunza na ukomavu wenu kuanzia Octoba 29 kule mjengoni.
 
hapo tutawaelewa ila bado bungeni hawa wabunge wao ni vigeugeu

Mkuu mimi sitaki kuwa mtabiri ila ukiwachunguza kwa Makini sura za wahusika wote walioshikana mikono kuna hali ya kutoaminiana kwa dhati ngoja tusubiri tuone...
 
Hakuna jipya lililojadiliwa wala hakuna litakalokuwa la maana JK amewaumbua wapinzani kuwa wao ni empty set.
 
Inahitaji uwe mwendawazimu kuishabikia masisiem!!

Nashauri watu wote wanaomwabudu Mungu na hasa wenye mapenzi ya kweli na nchi yetu,watu walioshiba uzalendo,kila mmoja kwa imani yake apige magoti kuiombea ccm na hasa wabunge wake ili yale mapepo yaliyowapagaa ya kudhani nchi hii ni mali ya ccm yawaondoke.Ile roho ya uzalendo iwarudie watambue nchi hii ni mali ya watanzania milioni 45 na kwamba katiba ni mali ya vizazi vijavyo pia.Naamini mapepo haya yakiwatoka,haya marekebisho ya katiba yanayorejeshwa bungeni kwa hisani ya wapinzani na Rais Kikwete,yatapita kwa asilimia 100.
 
Kweli rais Kikwete ana dhamira ya kweli.
Hiv hajatangaza mgogoro na bunge kama Chikawe alivyosema..?? Na kwa nini ameruhusu wapinzani kwenda tena Ikulu wakati Wasira alikataza..??? Kweli ngurumbili ndumila kuwili... Hakuna cha Ritz, wala Lizaboni
 
"Katiba bora inakuja Tanzania kwa sababu Rais Kikwete amesikiliza malalamiko ya vyama vya upinzani". Kweli?.

The draft constitution doomed to failure, before the Constitutional Review Commission (CRC) even start.

attachment.php

Viongozi wa vyama vya Siasa,(kushoto)Isaack Cheyo(UDP) Nancy Mrikaria(TLP) Fahmi Nassoro Dovutwa (UPDP),James Mbatia NCCR-Mageuzi,Profesa Ibrahim Lipumba(CUF),Philip Mangula(CCM) na Dk Willibrod Slaa(Chadema)wakiwa wameshikana mikono baada ya kikao cha pamoja jijini Dar es Salaam jana.

Yaani hii nchi rahisi kweli kuitawala kwa kweli. Hawa hawa walikataa mapendekezo haya haya mle bungeni, ambamo wamo wachache vile vile, na bado wanarudisha kule kule kujadiliwa, kwenye wingi wa wale wale waliofanya uhuni!
 
Back
Top Bottom