Katiba kwanza uchaguzi baadaye

Katiba kwanza uchaguzi baadaye

chikub

Senior Member
Joined
Oct 15, 2015
Posts
110
Reaction score
28
Kama kuna kitu ambacho wapenda mabadiliko nchini wanapaswa kujitolea kwa nguvu zao zote ni upatikanaji wa katiba mpya ya nchi kwanza.

Katiba ndio ingini ya kuleta mabadiliko, huwezi kuleta mabadiliko nje ya katiba ya nchi. Katiba safi ya nchi ndo itakayozalisha tume safi ya uchaguzi, viongozi safi, uchumi safi, matumizi safi na maisha bora kwa kila mtu.

Wapinzani kukubali kushiriki kwenye uchaguzi kwa kutumia katiba ya zamani ni sawa na kukubali kushindwa uchaguzi kabla ya uchaguzi. Kushiriki uchaguzi kwa kutumia katiba hii ya zamani ni sawa na kuhalalisha wananchi kuwasindikiza watu wachache kupata ubunge na udiwani usiokuwa na tija kwa wanachi walio wengi.

Wabunge wa aina hii huwa wananufaika wao tu na familia zao kwakuwa hawawezi kuleta mabadiliko yenye manufaa mapana kwenye majimbo yao.

Wakijitahidi saaaana watawaletea wananchi wao bahashishi ndogo ndogo tu kama soda, madawati, computers mashuleni, kitanda kimoja labor ward, n.k. Kwa uchache wao hawawezi kuchangia kuinua hali za maisha ya wanajimbo hata kama wangekuwa na utashi wa kufanya hivyo. Hoja zao bungeni zinazimwa kama mshumaa unavyozimwa.

kushiriki uchaguzi kwa kutumia katiba mpya kunazalisha hasara kubwa kwa wananchi kuliko faida. Jasho la wananchi wanaoshiriki kuzalisha wabunge na madiwani wachache tu kwenye vyombo vya maamuzi huwa halirudi. Vyama vya upinzani acheni kuwatumia wananchi kama mitaji yenu na familia zenu huku mkifahamu katiba iliyoko haiwezi kuwapatia wananchi mabadiliko wanayoyataka.

Ni bora vyama vya siasa kuacha kushiriki chaguzi nchini ya katiba hii sasa ili kuepuka kuwatumia wananchi ambao makusudi yao ni tofauti na wanachokipata baada baada ya uchaguzi.
 
umezungumza kweli, ila kuna gharama sana ktk hili!!

hawawezi kuruhusu hilo litokeee!!
 
Mbowe na viongozi wa ukawa hii ni Kweli huu ndio uwe uchaguzi wenu wa mwisho kushiriki mpaka tuwe na katiba mpya na tume huru.
 
hii nchi ni zaidi ya katiba ukosefu wa elimu na ubora wa elimu inayopatikana kwa wananchi wengi na watoto wao hauwajengi katika fikra za kujitegemea,kujitambua wajibu wao kama wananchi,kuitambua thamani yao na kutambua ni wapi wametoka,wapi walipo, na wapi wanataka kwenda.
asilimia 80 ya wananchi wa hii nchi hata ukiwauliza malengo ya maisha yao ni wachache watakujibu. Jaribu kuuliza sasa hivi watu 10 walipokuwa watoto walitamani kuwa watu wa aina gani walitaka wafanye kazi gani? ukipata wanaoishi ndoto zao leo katika kumi sizani hata kama 3 wanafika. Elimu bora inatakiwa sio Elimu tu bali Elimu bora.
Ni kweli katiba mpya ndo itatutoa hapa tulipo ?
Jibu: Ndio ni kweli
Je mchakato mzima wa kuipata katiba mpya utakuwa huru wa haki na kila mwananchi atashiriki
jibu: Hapana
Kwenye mchakato wa katiba mmeona kilichotokea sote tu mashaidi namna CCM ilivyoubaka ule mchakato.
kama Leo watanzania wanaiamini CCM je watashindwa kuipigia kura katiba ambayo CCM itawashawishi waipe kura ya ndio au hapana.
Elimu bora inatakiwa. ukiwa na Taifa ambalo katika jimbo la watu 50000 watu 3000 wanaharibu kura ujue kazi si ndogo. watu 3000 waliamka wakaacha makazi yao, wakajipanga mstari kwenye mchakato wa kujiandikisha kwenye daftari tena kukiwa na misururu mirefu wakavumila hadi wakapata kadi za kura, ikafika siku ya kupiga kura wakaacha makaI yao, wakaacha shughuli zao,wakapanga mstari , alafu wakapiga kura ambazo zimeharibika watu 3000 hii inasikitisha ni zaidi ya msiba
 
Ccm mnachofanya mungu atawahukumu
 
hii nchi ni zaidi ya katiba ukosefu wa elimu na ubora wa elimu inayopatikana kwa wananchi wengi na watoto wao hauwajengi katika fikra za kujitegemea,kujitambua wajibu wao kama wananchi,kuitambua thamani yao na kutambua ni wapi wametoka,wapi walipo, na wapi wanataka kwenda.
asilimia 80 ya wananchi wa hii nchi hata ukiwauliza malengo ya maisha yao ni wachache watakujibu. Jaribu kuuliza sasa hivi watu 10 walipokuwa watoto walitamani kuwa watu wa aina gani walitaka wafanye kazi gani? ukipata wanaoishi ndoto zao leo katika kumi sizani hata kama 3 wanafika. Elimu bora inatakiwa sio Elimu tu bali Elimu bora.
Ni kweli katiba mpya ndo itatutoa hapa tulipo ?
Jibu: Ndio ni kweli
Je mchakato mzima wa kuipata katiba mpya utakuwa huru wa haki na kila mwananchi atashiriki
jibu: Hapana
Kwenye mchakato wa katiba mmeona kilichotokea sote tu mashaidi namna CCM ilivyoubaka ule mchakato.
kama Leo watanzania wanaiamini CCM je watashindwa kuipigia kura katiba ambayo CCM itawashawishi waipe kura ya ndio au hapana.
Elimu bora inatakiwa. ukiwa na Taifa ambalo katika jimbo la watu 50000 watu 3000 wanaharibu kura ujue kazi si ndogo. watu 3000 waliamka wakaacha makazi yao, wakajipanga mstari kwenye mchakato wa kujiandikisha kwenye daftari tena kukiwa na misururu mirefu wakavumila hadi wakapata kadi za kura, ikafika siku ya kupiga kura wakaacha makaI yao, wakaacha shughuli zao,wakapanga mstari , alafu wakapiga kura ambazo zimeharibika watu 3000 hii inasikitisha ni zaidi ya msiba

kaka tokea nianze kuisoma jf 2010 wewe unaakili kuliko dr slaa na mwanakijiji katika kuchambua na kuuelewesha uma
 
hii nchi ni zaidi ya katiba ukosefu wa elimu na ubora wa elimu inayopatikana kwa wananchi wengi na watoto wao hauwajengi katika fikra za kujitegemea,kujitambua wajibu wao kama wananchi,kuitambua thamani yao na kutambua ni wapi wametoka,wapi walipo, na wapi wanataka kwenda.
asilimia 80 ya wananchi wa hii nchi hata ukiwauliza malengo ya maisha yao ni wachache watakujibu. Jaribu kuuliza sasa hivi watu 10 walipokuwa watoto walitamani kuwa watu wa aina gani walitaka wafanye kazi gani? ukipata wanaoishi ndoto zao leo katika kumi sizani hata kama 3 wanafika. Elimu bora inatakiwa sio Elimu tu bali Elimu bora.
Ni kweli katiba mpya ndo itatutoa hapa tulipo ?
Jibu: Ndio ni kweli
Je mchakato mzima wa kuipata katiba mpya utakuwa huru wa haki na kila mwananchi atashiriki
jibu: Hapana
Kwenye mchakato wa katiba mmeona kilichotokea sote tu mashaidi namna CCM ilivyoubaka ule mchakato.
kama Leo watanzania wanaiamini CCM je watashindwa kuipigia kura katiba ambayo CCM itawashawishi waipe kura ya ndio au hapana.
Elimu bora inatakiwa. ukiwa na Taifa ambalo katika jimbo la watu 50000 watu 3000 wanaharibu kura ujue kazi si ndogo. watu 3000 waliamka wakaacha makazi yao, wakajipanga mstari kwenye mchakato wa kujiandikisha kwenye daftari tena kukiwa na misururu mirefu wakavumila hadi wakapata kadi za kura, ikafika siku ya kupiga kura wakaacha makaI yao, wakaacha shughuli zao,wakapanga mstari , alafu wakapiga kura ambazo zimeharibika watu 3000 hii inasikitisha ni zaidi ya msiba
Umesema vema, lakini hata katiba pendekezwa ya CCM mliyoisusia ninyi UKAWA ilikuwa na unafuu kwenye masuala ya uchaguzi kuliko hii ya sasa iliyotumika. Bora mngeikubali kwanza hii pendekezwa kisha mngejua nini chakufanya mkishafika Ikulu (win-win, lose-lose) badala ya lose-win mliyoichagua UKAWA.
 
binafsi sidhani kama kuna haja ya kuingia garama mpya ya uandikaji wa katiba. tuanzie tu pale rasimu ya warioba ilipoishia tumalizie. sioni tatizo kubwa kwenye ile rasimu ya jaji warioba na wenzake.
 
Umesema vema, lakini hata katiba pendekezwa ya CCM mliyoisusia ninyi UKAWA ilikuwa na unafuu kwenye masuala ya uchaguzi kuliko hii ya sasa iliyotumika. Bora mngeikubali kwanza hii pendekezwa kisha mngejua nini chakufanya mkishafika Ikulu (win-win, lose-lose) badala ya lose-win mliyoichagua UKAWA.

Katiba pendekezwa imesusiwaje wakati kura ya maoni haikupigwa? When one door is closed another one will open.
 
Back
Top Bottom