Katiba Mpya Haimpeleki Rais Ikulu

Katiba Mpya Haimpeleki Rais Ikulu

Filosofia ya Rorya

JF-Expert Member
Joined
Sep 20, 2021
Posts
3,211
Reaction score
3,611
Tusiyopenda kuyasikia kwenye Elimu ya Uraia.

Kimsingi madai ya Katiba mpya kwa minajili ya kushika nafasi ya urais naamini ni ndoto isiyotimia kwa vizazi vingi vijavyo. Uki-study historia mahala pengi utakubaliana nami kwamba madai ya Katiba mpya siyo kwa ajili ya wanaogombea urais kuingia Ikulu bali ni kwa ajili ya kuleta mfumo mzuri wa jamii imara iliyoshikamana kwa malengo maridhawa.

Katiba mpya imewaingiza wagombea wapya Ikulu kwa asilima ndogo sana sana isiyostahili wingi wa madai hayo na isiyoakisi gharama halisi za mchakato wa kuandika Katiba mpya hizo.

Kwa uelewa wangu, Rais hapelekwi Ikulu kwa Katiba mpya, Rais anapelekwa Ikulu kwa mfumo wa Dola (vetting ya dola), Katiba mpya na mfumo wa uchaguzi vinawapa tu wapigakura uwezo wa kuwapeleka wabunge Bungeni, Madiwani Halmashauri na Wenyeviti wa Serikali za Mitaa, Vitongoji na Vijiji basi. Katiba hata ikiwa mpya haiwapi wapigakura (wananchi) uwezo wa kumpeleka Rais Ikulu. Huu ndiyo uhalisia wa Afrika. Thought stirring discourse.
 
na huo mfumo wa dola inapatikana vipi wewe
Ni jinsi ya kumpata mgombea kupitia mchakato wa kidemokrasia wa Chama chake, kwa Katiba ya sasa ya JMT.

Ikiwa ni lazima kuwa na mgombea binafsi, Katiba (mpya) ielekeze jinsi ya kumpata huyo mgombea, kwa njia ya kidemokrasia.

Kwa njia yoyote, katika hizo mbili, msingi ni mgombea kuungwa mkono na idadi kubwa ya wapiga kura kabla ya uchaguzi. Kwa sababu hiyo, mgombea anayeungwa na chama, anakuwa na nafasi kubwa ya kuchaguliwa iwapo Chama kina wanachama na wafuasi wengi, na aliteuliwa kidemokrasia.
 
Tusiyopenda kuyasikia kwenye Elimu ya Uraia.

Kimsingi madai ya Katiba mpya kwa minajili ya kushika nafasi ya urais naamini ni ndoto isiyotimia kwa vizazi vingi vijavyo. Uki-study historia mahala pengi utakubaliana nami kwamba madai ya Katiba mpya siyo kwa ajili ya wanaogombea urais kuingia Ikulu bali ni kwa ajili ya kuleta mfumo mzuri wa jamii imara iliyoshikamana kwa malengo maridhawa.

Katiba mpya imewaingiza wagombea wapya Ikulu kwa asilima ndogo sana sana isiyostahili wingi wa madai hayo na isiyoakisi gharama halisi za mchakato wa kuandika Katiba mpya hizo.

Kwa uelewa wangu, Rais hapelekwi Ikulu kwa Katiba mpya, Rais anapelekwa Ikulu kwa mfumo wa Dola (vetting ya dola), Katiba mpya na mfumo wa uchaguzi vinawapa tu wapigakura uwezo wa kuwapeleka wabunge Bungeni, Madiwani Halmashauri na Wenyeviti wa Serikali za Mitaa, Vitongoji na Vijiji basi. Katiba hata ikiwa mpya haiwapi wapigakura (wananchi) uwezo wa kumpeleka Rais Ikulu. Huu ndiyo uhalisia wa Afrika. Thought stirring discourse.
Wanaodai katiba sio kwa ajili ya kuweka rais/chama madarakani. Sababu kubwa ya kudai katiba mpya ni ili kuweka mfumo mzuri utakaofuatwa na yeyote ambaye atapata nafasi ya kuongoza nchi yetu. Ndio maana kila siku mnalalamika kuwa aliyoanzisha magufuli yameachwa kwa kuwa tu una katiba inayojenga mtu badala ya mfumo. Kila kiongozi anajiamulia anavyotaka
 
Rais hapelekwi Ikulu kwa Katiba mpya, Rais anapelekwa Ikulu kwa mfumo wa Dola (vetting ya dola)
Hii yako inafanya kazi zaidi Urusi, Korea Kaskazini na Uchina ambako kuna vyama dola ila kwa nchi zenye mfumo unaotoa nguvu ya mpiga kura mtu yoyote mwenye kuweza kuongoza na anakubalika anaweza kuwa Raisi
 
Ndio sasa tunataka katiba mpya ili kama kura ya mwananchi ni maigizo tu basi katiba itamke!
 
Uko Afrika....

Hatuna elimu ya demokrasia ya nchi za MAGHARIBI ....

Halafu unayataka madaraka kwa kisingizio cha katiba mpya.....Khaaa 😳😳

Madaraka si jambo la kunywa chai na maandazi......🤣
 
Tusiyopenda kuyasikia kwenye Elimu ya Uraia.

Kimsingi madai ya Katiba mpya kwa minajili ya kushika nafasi ya urais naamini ni ndoto isiyotimia kwa vizazi vingi vijavyo. Uki-study historia mahala pengi utakubaliana nami kwamba madai ya Katiba mpya siyo kwa ajili ya wanaogombea urais kuingia Ikulu bali ni kwa ajili ya kuleta mfumo mzuri wa jamii imara iliyoshikamana kwa malengo maridhawa.

Katiba mpya imewaingiza wagombea wapya Ikulu kwa asilima ndogo sana sana isiyostahili wingi wa madai hayo na isiyoakisi gharama halisi za mchakato wa kuandika Katiba mpya hizo.

Kwa uelewa wangu, Rais hapelekwi Ikulu kwa Katiba mpya, Rais anapelekwa Ikulu kwa mfumo wa Dola (vetting ya dola), Katiba mpya na mfumo wa uchaguzi vinawapa tu wapigakura uwezo wa kuwapeleka wabunge Bungeni, Madiwani Halmashauri na Wenyeviti wa Serikali za Mitaa, Vitongoji na Vijiji basi. Katiba hata ikiwa mpya haiwapi wapigakura (wananchi) uwezo wa kumpeleka Rais Ikulu. Huu ndiyo uhalisia wa Afrika. Thought stirring discourse.
Duh, ila kwa kweli siku hizi JF imekuwa kimeo. Hoja zinakuja nyingi lakini more than 50% ni makapi.
Anyway sawa, ni uhuru wa mawazo
 
Tusiyopenda kuyasikia kwenye Elimu ya Uraia.

Kimsingi madai ya Katiba mpya kwa minajili ya kushika nafasi ya urais naamini ni ndoto isiyotimia kwa vizazi vingi vijavyo. Uki-study historia mahala pengi utakubaliana nami kwamba madai ya Katiba mpya siyo kwa ajili ya wanaogombea urais kuingia Ikulu bali ni kwa ajili ya kuleta mfumo mzuri wa jamii imara iliyoshikamana kwa malengo maridhawa.

Katiba mpya imewaingiza wagombea wapya Ikulu kwa asilima ndogo sana sana isiyostahili wingi wa madai hayo na isiyoakisi gharama halisi za mchakato wa kuandika Katiba mpya hizo.

Kwa uelewa wangu, Rais hapelekwi Ikulu kwa Katiba mpya, Rais anapelekwa Ikulu kwa mfumo wa Dola (vetting ya dola), Katiba mpya na mfumo wa uchaguzi vinawapa tu wapigakura uwezo wa kuwapeleka wabunge Bungeni, Madiwani Halmashauri na Wenyeviti wa Serikali za Mitaa, Vitongoji na Vijiji basi. Katiba hata ikiwa mpya haiwapi wapigakura (wananchi) uwezo wa kumpeleka Rais Ikulu. Huu ndiyo uhalisia wa Afrika. Thought stirring discourse.
Mhuu hili nalo wazo ingawa sikubaliani nalo kabisa, mimi naona si issue ya kumpeleka Rais ikulu ila cha msingi ni kurudisha nguvu za maamuzi kwa Wananchi wa Tanzania. Nionavyo mimi nguvu za wananchi zimepokwa na Serikali and Bunge ambalo halitetei tena maslahi ya wananchi . Pande zote tatu zimekubaliana na hili na mahakama nao wakipokwa uhuru wao. Watawala wanalijua hili vema nafikiri kuliko hata wananchi wenyewe pamoja na wapinzania. Kutawala kumebaki kwenye chama na sii serikali maana yake chama kimeshika hatamu kwani wanauwezo wa kumfukuza hata Rais mwenyewe. Kwenye nchi za kimagharibi vyama vyao vinakabidhi sera na malengo yake kwa Rais ili atekeleze kwa uhuru wake na hawaingilii mihimili ya nchi. Unaposema Katiba hampi wanamchi nguvu ya kumpeleka Rais ikulu nashindwa kukuelewa katiba italeta tume huru na uchaguzi huru hapo sasa ndipo nguvu ya mwananchi itakapo muingiza Rais ikulu. Tusigeneralise kwa kusingizia Africa no kuna nchi Africa zina tume huru na Viongozi wake wanachaguliwa na wananchi ingawa sio zote. Tusiache kubadili katiba kwa kisingizio cha kusema katiba haimuingizi Rais ikulu.
 
Tusiyopenda kuyasikia kwenye Elimu ya Uraia.

Kimsingi madai ya Katiba mpya kwa minajili ya kushika nafasi ya urais naamini ni ndoto isiyotimia kwa vizazi vingi vijavyo. Uki-study historia mahala pengi utakubaliana nami kwamba madai ya Katiba mpya siyo kwa ajili ya wanaogombea urais kuingia Ikulu bali ni kwa ajili ya kuleta mfumo mzuri wa jamii imara iliyoshikamana kwa malengo maridhawa.

Katiba mpya imewaingiza wagombea wapya Ikulu kwa asilima ndogo sana sana isiyostahili wingi wa madai hayo na isiyoakisi gharama halisi za mchakato wa kuandika Katiba mpya hizo.

Kwa uelewa wangu, Rais hapelekwi Ikulu kwa Katiba mpya, Rais anapelekwa Ikulu kwa mfumo wa Dola (vetting ya dola), Katiba mpya na mfumo wa uchaguzi vinawapa tu wapigakura uwezo wa kuwapeleka wabunge Bungeni, Madiwani Halmashauri na Wenyeviti wa Serikali za Mitaa, Vitongoji na Vijiji basi. Katiba hata ikiwa mpya haiwapi wapigakura (wananchi) uwezo wa kumpeleka Rais Ikulu. Huu ndiyo uhalisia wa Afrika. Thought stirring discourse.

Pamoja na yote woga wa nini kuihofia kiasi hicho?

Si kweli kuwa Hangaya kwa katiba inayoruhusu wizi wa wazi ana uhakika wa kujirejesha ikulu 2025?

Kwa mawazo yake si kuwa kipaumbele ni kukomaa na katiba hii hii lolote liwalo hadi baada ya 2025?
 
Ni swali zuri mkuu. Ni hivi:-

Kuwaza jambo ni jambo moja, kudai/kutaka jambo ni jambo moja, kutekeleza wazo na madai ni jambo moja pia, LAKINI kuyapewa hayo yote ni jambo jingine linalotegemea mifumo iliyowekwa tangu kuiasisi inatakaje? Je, wewe ulikuwa sehemu ya mchakato wa kuasisi mifumo hiyo? Dynasty kukuingiza Ikulu ni rahisi na ina nguvu kubwa sana kuliko Katiba mpya.

Zanzibar walirekebisha katiba. Maalim hakuingia Ikulu kama Rais bali kama Makamu Rais.

Kenya waliandika katiba mpya. Raila Odinga hajaingia Ikulu.

Uganda walirekebisha katiba. Robert Kyagulanyi hajaingia Ikulu.

Zimbabwe waliandika katiba mpya. Morgan Tsvangirai hakuingia Ikulu. Mugabe hakuondolewa na Katiba mpya bali aliondolewa na #Dola.

DR Congo marehemu Étienne Tshisekedi alishinda uchaguzi na bado hakuingia Ikulu licha katiba ya DR Congo kurekebishwa kabla ya uchaguzi. Joseph Kabila alikuja kuondolewa Ikulu kwa shinikizo la Kanisa Katoliki likishirikiana na #Dola.

Ivory Coast Laurent Gbagbo alishindwa kwenye masanduku ya kura lakini akaendelea kuwa Rais siyo kwa nguvu za Tume ya Uchaguzi au kura za wananchi bali kwa nguvu za #Dola. Alassane Quattara aliyetambuliwa na Tume ya Uchaguzi, ECOWAS, AU, UN na Watazamaji wa Uchaguzi kama mshindi wa urais bado hakuingia Ikulu hadi pale #Dola ilipokubali kumutii kama Amiri Jeshi Mkuu hata kama ni kwa shinikizo.

Malawi ni #Dola (kupitia mkono wake wa Mahakama) ilikubali kufanyakazi na Rais Lazarus Chakwera badala ya Mutharika ambaye #Dola hiyohiyo ndiyo iliendelea kumtambua kama Rais.

Katiba mpya na kura pekee havitoshi kumuingiza Rais Ikulu (na wala siyo vigezo muhimu).

Dynasty imewaingiza wengi Ikulu Afrika.
 
Mhuu hili nalo wazo ingawa sikubaliani nalo kabisa, mimi naona si issue ya kumpeleka Rais ikulu ila cha msingi ni kurudisha nguvu za maamuzi kwa Wananchi wa Tanzania. Nionavyo mimi nguvu za wananchi zimepokwa na Serikali and Bunge ambalo halitetei tena maslahi ya wananchi . Pande zote tatu zimekubaliana na hili na mahakama nao wakipokwa uhuru wao. Watawala wanalijua hili vema nafikiri kuliko hata wananchi wenyewe pamoja na wapinzania. Kutawala kumebaki kwenye chama na sii serikali maana yake chama kimeshika hatamu kwani wanauwezo wa kumfukuza hata Rais mwenyewe. Kwenye nchi za kimagharibi vyama vyao vinakabidhi sera na malengo yake kwa Rais ili atekeleze kwa uhuru wake na hawaingilii mihimili ya nchi. Unaposema Katiba hampi wanamchi nguvu ya kumpeleka Rais ikulu nashindwa kukuelewa katiba italeta tume huru na uchaguzi huru hapo sasa ndipo nguvu ya mwananchi itakapo muingiza Rais ikulu. Tusigeneralise kwa kusingizia Africa no kuna nchi Africa zina tume huru na Viongozi wake wanachaguliwa na wananchi ingawa sio zote. Tusiache kubadili katiba kwa kisingizio cha kusema katiba haimuingizi Rais ikulu.

Ni mawazo duni sana kufungamanisha urais au chaguzi tu na katiba.

Yote unayoyaona ni kutapatapa kwa waimba mapambio wale wale. Lengo ni kutoridhia hoja yoyote ya katiba mpya angalau kabla ya 2025.
 
Ni swali zuri mkuu. Ni hivi:-

Kuwaza jambo ni jambo moja, kudai/kutaka jambo ni jambo moja, kutekeleza wazo na madai ni jambo moja pia, LAKINI kuyapewa hayo yote ni jambo jingine linalotegemea mifumo iliyowekwa tangu kuiasisi inatakaje? Je, wewe ulikuwa sehemu ya mchakato wa kuasisi mifumo hiyo? Dynasty kukuingiza Ikulu ni rahisi na ina nguvu kubwa sana kuliko Katiba mpya.

Zanzibar walirekebisha katiba. Maalim hakuingia Ikulu kama Rais bali kama Makamu Rais.

Kenya waliandika katiba mpya. Raila Odinga hajaingia Ikulu.

Uganda walirekebisha katiba. Robert Kyagulanyi hajaingia Ikulu.

Zimbabwe waliandika katiba mpya. Morgan Tsvangirai hakuingia Ikulu. Mugabe hakuondolewa na Katiba mpya bali aliondolewa na #Dola.

DR Congo marehemu Étienne Tshisekedi alishinda uchaguzi na bado hakuingia Ikulu licha katiba ya DR Congo kurekebishwa kabla ya uchaguzi. Joseph Kabila alikuja kuondolewa Ikulu kwa shinikizo la Kanisa Katoliki likishirikiana na #Dola.

Ivory Coast Laurent Gbagbo alishindwa kwenye masanduku ya kura lakini akaendelea kuwa Rais siyo kwa nguvu za Tume ya Uchaguzi au kura za wananchi bali kwa nguvu za #Dola. Alassane Quattara aliyetambuliwa na Tume ya Uchaguzi, ECOWAS, AU, UN na Watazamaji wa Uchaguzi kama mshindi wa urais bado hakuingia Ikulu hadi pale #Dola ilipokubali kumutii kama Amiri Jeshi Mkuu hata kama ni kwa shinikizo.

Malawi ni #Dola (kupitia mkono wake wa Mahakama) ilikubali kufanyakazi na Rais Lazarus Chakwera badala ya Mutharika ambaye #Dola hiyohiyo ndiyo iliendelea kumtambua kama Rais.

Katiba mpya na kura pekee havitoshi kumuingiza Rais Ikulu (na wala siyo vigezo muhimu).

Dynasty imewaingiza wengi Ikulu Afrika.
Katiba ikisema matokeo ya Urais yanapingwa mahakamani kwa uhuru, wakati huohuo mahakama zetu zikawa huru kutoka kwenye mikono ya wanasiasa na zinalindwa na katiba bila kuingiliwa, majeshi yote yakajitenga na siasa( hapa kwetu RPC anakadi ya chama na anatembea na katiba na ilani ya chama). Itakuwaje hapo?
 
Sasa kama hivyo ndivyo, hii hoja kuwa Chadema wanataka katiba mpya ili waingie ikulu inatoka wapi?

Mhuu hili nalo wazo ingawa sikubaliani nalo kabisa, mimi naona si issue ya kumpeleka Rais ikulu ila cha msingi ni kurudisha nguvu za maamuzi kwa Wananchi wa Tanzania. Nionavyo mimi nguvu za wananchi zimepokwa na Serikali and Bunge ambalo halitetei tena maslahi ya wananchi . Pande zote tatu zimekubaliana na hili na mahakama nao wakipokwa uhuru wao. Watawala wanalijua hili vema nafikiri kuliko hata wananchi wenyewe pamoja na wapinzania. Kutawala kumebaki kwenye chama na sii serikali maana yake chama kimeshika hatamu kwani wanauwezo wa kumfukuza hata Rais mwenyewe. Kwenye nchi za kimagharibi vyama vyao vinakabidhi sera na malengo yake kwa Rais ili atekeleze kwa uhuru wake na hawaingilii mihimili ya nchi. Unaposema Katiba hampi wanamchi nguvu ya kumpeleka Rais ikulu nashindwa kukuelewa katiba italeta tume huru na uchaguzi huru hapo sasa ndipo nguvu ya mwananchi itakapo muingiza Rais ikulu. Tusigeneralise kwa kusingizia Africa no kuna nchi Africa zina tume huru na Viongozi wake wanachaguliwa na wananchi ingawa sio zote. Tusiache kubadili katiba kwa kisingizio cha kusema katiba haimuingizi Rais ikulu.
Marekani ambayo ni Role Model ya Demokrasia kwenye sayari kura za wananchi hazimuingizi Rais Ikulu. Kuna Popular Votes (kura za wananchi) na Electoral College (kura za kundi dogo (niazime neno la Think Tank kufafanua) wanaodhaniwa kuwa ndiyo wana hatima ya Marekani kwenye brains na nyoyo zao, wanadhaniwa kuwa ni wazalendo wa damu, wanadhaniwa kuwa hawawezi kusaliti maslahi ya Marekani; ambao hawa ndiyo kura zao zinaamua nani awe rais kati ya wagombea, kwa Afrika hapa ndiyo tunaweza kuwafananisha kidogo na #Dola niliyosema kwamba ndiyo inamuingiza Rais Ikulu).

Hii Think Tank ya US baada ya kujaribiwa na Rais Trump kugoma kutoka Ikulu, waliona mantiki ya #Dola kutumika kumuingiza Rais Biden White House, #Dola ndiyo nchi, #Dola kumbe inawezajibadilisha na kuwa ndiyo Mamlaka Makuu ya Turufu kushinda hata Katiba wanayopaswa kuiheshimu na kuilinda. Ndiyo maana #Dola ikichukuwa nchi kwa mapinduzi huwa hatua ya kwanza ni ku-suspend katiba au wanaifanya kuwa junior. Katika historia ya Marekani ni mara tano sasa Rais aliyechaguliwa na Popular Votes kutochaguliwa na Electoral College. Kuna baadhi ya Majimbo waumini wa Popular Votes wameamua kuweka pingamizi kwa mfumo wa Electoral College kutumika kwenye Majimbo yao kwa sababu unachanganya na kuhujumu mfumo wa demokrasia ya haki.

Ni kwanini mahala pengi mhimili wa Mahakama ni ndugu ya Serikali kuliko Bunge. Mfumo wa Mahakama unatengenezwa na Serikali ambayo ndiyo inayomiliki #Dola. Katiba mpya ni nzuri ili kuweka mustakabali wa taifa lakini naamini haitoshi kumuingiza Rais Ikulu. IKUMBUKWE KUWA LENGO LA MSINGI LA CHAMA CHOCHOTE CHA SIASA DUNIANI NI KUSHIKA MADARAKA YA NCHI (Kuingia Ikulu). Mambo ni mengi inahitaji umakini.
 
Marekani ambayo ni Role Model ya Demokrasia kwenye sayari kura za wananchi hazimuingizi rais Ikulu. Kuna Popular Votes (kura za wananchi) na Electoral College (kura za kundi dogo (niazime neno la Think Tank kufafanua) wanaodhaniwa kuwa ndiyo wana hatima ya Marekani kwenye brains na nyoyo zao, wanadhaniwa kuwa ni wazalendo wa damu, wanadhaniwa kuwa hawawezi kusaliti maslahi ya Marekani; ambao hawa ndiyo kura zao zinaamua nani awe rais kati ya wagombea, kwa Afrika hapa ndiyo tunaweza kuwafananisha kidogo na #Dola niliyosema kwamba ndiyo inamuingiza Rais Ikulu).

Hii Think Tank ya US baada ya kujaribiwa na Rais Trump kugoma kutoka Ikulu, waliona mantiki ya #Dola kutumika kumuingiza Rais Biden White House, #Dola ndiyo nchi, #Dola kumbe inawezajibadilisha na kuwa ndiyo Mamlaka Makuu ya Turufu kushinda hata Katiba wanayopaswa kuiheshimu na kuilinda. Katika historia ya Marekani ni mara tano sasa Rais aliyechaguliwa na Popular Votes kutochaguliwa na Electoral College. Kuna baadhi ya Majimbo waumini wa Popular Votes wameamua kuweka pingamizi kwa mfumo wa Electoral College kutumika kwenye Majimbo yao kwa sababu unachanganya na kuhujumu mfumo wa demokrasia ya haki.

Ni kwanini mahala pengi mhimili wa Mahakama ni ndugu ya Serikali kuliko Bunge. Mfumo wa Mahakama unatengenezwa na Serikali ambayo ndiyo inayomiliki #Dola. Katiba mpya ni nzuri ili kuweka mustakabali wa taifa lakini naamini haitoshi kumuingiza Rais Ikulu. IKUMBUKWE KUWA LENGO LA MSINGI LA CHAMA CHOCHOTE CHA SIASA DUNIANI NI KUSHIKA MADARAKA YA NCHI (Kuingia Ikulu). Mambo ni mengi inahitaji umakini.
Hoja yako unataka kuhalalisha nini ?

Kwani wanaodai katiba mpya wamekwambia wanataka waende ikulu ?
 
Tusiyopenda kuyasikia kwenye Elimu ya Uraia.

Kimsingi madai ya Katiba mpya kwa minajili ya kushika nafasi ya urais naamini ni ndoto isiyotimia kwa vizazi vingi vijavyo. Uki-study historia mahala pengi utakubaliana nami kwamba madai ya Katiba mpya siyo kwa ajili ya wanaogombea urais kuingia Ikulu bali ni kwa ajili ya kuleta mfumo mzuri wa jamii imara iliyoshikamana kwa malengo maridhawa.

Katiba mpya imewaingiza wagombea wapya Ikulu kwa asilima ndogo sana sana isiyostahili wingi wa madai hayo na isiyoakisi gharama halisi za mchakato wa kuandika Katiba mpya hizo.

Kwa uelewa wangu, Rais hapelekwi Ikulu kwa Katiba mpya, Rais anapelekwa Ikulu kwa mfumo wa Dola (vetting ya dola), Katiba mpya na mfumo wa uchaguzi vinawapa tu wapigakura uwezo wa kuwapeleka wabunge Bungeni, Madiwani Halmashauri na Wenyeviti wa Serikali za Mitaa, Vitongoji na Vijiji basi. Katiba hata ikiwa mpya haiwapi wapigakura (wananchi) uwezo wa kumpeleka Rais Ikulu. Huu ndiyo uhalisia wa Afrika. Thought stirring discourse.
Kama hiyo katiba mpya haitamtoa rais wako madarakani, hofu ya nini kwenye kupatikana hiyo katiba mpya?
 
Mhuu hili nalo wazo ingawa sikubaliani nalo kabisa, mimi naona si issue ya kumpeleka Rais ikulu ila cha msingi ni kurudisha nguvu za maamuzi kwa Wananchi wa Tanzania. Nionavyo mimi nguvu za wananchi zimepokwa na Serikali and Bunge ambalo halitetei tena maslahi ya wananchi . Pande zote tatu zimekubaliana na hili na mahakama nao wakipokwa uhuru wao. Watawala wanalijua hili vema nafikiri kuliko hata wananchi wenyewe pamoja na wapinzania. Kutawala kumebaki kwenye chama na sii serikali maana yake chama kimeshika hatamu kwani wanauwezo wa kumfukuza hata Rais mwenyewe. Kwenye nchi za kimagharibi vyama vyao vinakabidhi sera na malengo yake kwa Rais ili atekeleze kwa uhuru wake na hawaingilii mihimili ya nchi. Unaposema Katiba hampi wanamchi nguvu ya kumpeleka Rais ikulu nashindwa kukuelewa katiba italeta tume huru na uchaguzi huru hapo sasa ndipo nguvu ya mwananchi itakapo muingiza Rais ikulu. Tusigeneralise kwa kusingizia Africa no kuna nchi Africa zina tume huru na Viongozi wake wanachaguliwa na wananchi ingawa sio zote. Tusiache kubadili katiba kwa kisingizio cha kusema katiba haimuingizi Rais ikulu.

Hoja yako unataka kuhalalisha nini ?

Kwani wanaodai katiba mpya wamekwambia wanataka waende ikulu ?
Wanataka Katiba mpya ili kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi miongoni mwa mambo mengine, wanataka Tume Huru ya Uchaguzi ili washinde uchaguzi kwasababu LENGO LA MSINGI LA CHAMA CHOCHOTE CHA SIASA DUNIANI NI KUSHIKA MADARAKA YA NCHI (Kuingia Ikulu).
 
Back
Top Bottom