Katiba Mpya Haimpeleki Rais Ikulu

Katiba Mpya Haimpeleki Rais Ikulu

Tusiyopenda kuyasikia kwenye Elimu ya Uraia.

Kimsingi madai ya Katiba mpya kwa minajili ya kushika nafasi ya urais naamini ni ndoto isiyotimia kwa vizazi vingi vijavyo. Uki-study historia mahala pengi utakubaliana nami kwamba madai ya Katiba mpya siyo kwa ajili ya wanaogombea urais kuingia Ikulu bali ni kwa ajili ya kuleta mfumo mzuri wa jamii imara iliyoshikamana kwa malengo maridhawa.

Katiba mpya imewaingiza wagombea wapya Ikulu kwa asilima ndogo sana sana isiyostahili wingi wa madai hayo na isiyoakisi gharama halisi za mchakato wa kuandika Katiba mpya hizo.

Kwa uelewa wangu, Rais hapelekwi Ikulu kwa Katiba mpya, Rais anapelekwa Ikulu kwa mfumo wa Dola (vetting ya dola), Katiba mpya na mfumo wa uchaguzi vinawapa tu wapigakura uwezo wa kuwapeleka wabunge Bungeni, Madiwani Halmashauri na Wenyeviti wa Serikali za Mitaa, Vitongoji na Vijiji basi. Katiba hata ikiwa mpya haiwapi wapigakura (wananchi) uwezo wa kumpeleka Rais Ikulu. Huu ndiyo uhalisia wa Afrika. Thought stirring discourse.
Unataka Tanzania iendelee na mfumo wa Rais kumchagua jaji mkuu na jaji mkuu anakwenda. kumuapisha Rais aliyemteua?
 
Is there any reason behind which makes you to use English instead of Swahili, since your main post was in Swahili. Or you think by using English I will consider you as an intellectual?
Dear Expert Member, get to comprehend the concept.
 
UONGO MTUPU, Electoral Votes zinapatikana kupitia Popular Votes. Kila jimbo Marekani lina idadi zake na sheria zake katika utoaji wa electoral votea. Mfano, California yenye Electoral Votes 55 mgombea yoyote wa Urais anaposhinda California hata kwa kura 1 anapewa electoral votes zote 55, ni kinyume cha katiba mjumbe wa electoral college kumpigia kura ya electoral vote mtu ambaye hajashinda Popular votes kwenye hilo jimbo.
Wajumbe wa Electoral College bila kujali vyama vyao ni lazima wapige kura kulingana na mshindi wa Popular votes katika majimbo yao.
Marekani ambayo ni Role Model ya Demokrasia kwenye sayari kura za wananchi hazimuingizi Rais Ikulu. Kuna Popular Votes (kura za wananchi) na Electoral College (kura za kundi dogo (niazime neno la Think Tank kufafanua) wanaodhaniwa kuwa ndiyo wana hatima ya Marekani kwenye brains na nyoyo zao, wanadhaniwa kuwa ni wazalendo wa damu, wanadhaniwa kuwa hawawezi kusaliti maslahi ya Marekani; ambao hawa ndiyo kura zao zinaamua nani awe rais kati ya wagombea, kwa Afrika hapa ndiyo tunaweza kuwafananisha kidogo na #Dola niliyosema kwamba ndiyo inamuingiza Rais Ikulu).

Hii Think Tank ya US baada ya kujaribiwa na Rais Trump kugoma kutoka Ikulu, waliona mantiki ya #Dola kutumika kumuingiza Rais Biden White House, #Dola ndiyo nchi, #Dola kumbe inawezajibadilisha na kuwa ndiyo Mamlaka Makuu ya Turufu kushinda hata Katiba wanayopaswa kuiheshimu na kuilinda. Katika historia ya Marekani ni mara tano sasa Rais aliyechaguliwa na Popular Votes kutochaguliwa na Electoral College. Kuna baadhi ya Majimbo waumini wa Popular Votes wameamua kuweka pingamizi kwa mfumo wa Electoral College kutumika kwenye Majimbo yao kwa sababu unachanganya na kuhujumu mfumo wa demokrasia ya haki.

Ni kwanini mahala pengi mhimili wa Mahakama ni ndugu ya Serikali kuliko Bunge. Mfumo wa Mahakama unatengenezwa na Serikali ambayo ndiyo inayomiliki #Dola. Katiba mpya ni nzuri ili kuweka mustakabali wa taifa lakini naamini haitoshi kumuingiza Rais Ikulu. IKUMBUKWE KUWA LENGO LA MSINGI LA CHAMA CHOCHOTE CHA SIASA DUNIANI NI KUSHIKA MADARAKA YA NCHI (Kuingia Ikulu). Mambo ni mengi inahitaji umakini.
 
Wanataka Katiba mpya ili kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi miongoni mwa mambo mengine, wanataka Tume Huru ya Uchaguzi ili washinde uchaguzi kwasababu LENGO LA MSINGI LA CHAMA CHOCHOTE CHA SIASA DUNIANI NI KUSHIKA MADARAKA YA NCHI (Kuingia Ikulu).
Na chama cha siasa ili kiweze kutekeleza sera zake lazima kiwe na madaraka.

Kwani ni kosa chama cha siasa kutaka madaraka ?
 
Is there any reason behind which makes you to use English instead of Swahili, since your main post was in Swahili. Or you think by using English I will consider you as an intellectual?
JF is bilingual.
 
Na chama cha siasa ili kiweze kutekeleza sera zake lazima kiwe na madaraka.

Kwani ni kosa chama cha siasa kutaka madaraka ?
Siyo kosa kabisa mkuu.

Charles Njonjo alipotaka kumng'oa mzee Jomo Kenyatta akaenda kum-consult babake kwanza. Babake akamwambia ebu fungua jokofu hilo hapo, chukuwa kipande cha nyama mpe paka, Charles akafanya hivyo, paka alivyoanza kukila mzee Njonjo akamwambia Charles ebu sasa mnyang'anye paka hicho kipande cha nyama kabla hajakimaliza, Charles akasema haiwezekani, mzee Njonjo akamuuliza kwanini haiwezekani, Charles akajibu paka atanidhuru. Mzee Njonjo akamwambia Charles sawasawa kabisa kumbe umeelewa somo, sasa ukitaka kumnyang'anya mzee Jomo Kenyatta urais jiandae kudhuriwa. Mimi simo! Charles akapanda ndege kurudi London akaghairi mpango huo. Nimefafanua kifasihi zaidi.
 
Siyo kosa kabisa mkuu.

Charles Njonjo alipotaka kumng'oa mzee Jomo Kenyatta akaenda kum-consult babake kwanza. Babake akamwambia ebu fungua jokofu hilo hapo, chukuwa kipande cha nyama mpe paka, Charles akafanya hivyo, paka alivyoanza kukila mzee Njonjo akamwambia Charles ebu sasa mnyang'anye paka hicho kipande cha nyama kabla hajakimaliza, Charles akasema haiwezekani, mzee Njonjo akamuuliza kwanini haiwezekani, Charles akajibu paka atanidhuru. Mzee Njonjo akamwambia Charles sawasawa kabisa kumbe umeelewa somo, sasa ukitaka kumnyang'anya mzee Jomo Kenyatta urais jiandae kudhuriwa. Mimi simo! Charles akapanda ndege kurudi London akaghairi mpango huo. Nimefafanua kifasihi zaidi.
Kwahiyo hamtaki katiba mpya ili kulinda madaraka ?

Kama nilielewa vizuri thesis yako ilikuwa ni kwamba katiba haiwezi kukupeleka ikulu kwa maana ya kukupa madaraka.

Sasa kama thesis yako ni hiyo mbona jibu lako hili ni contradictory ?
 
Sasa kama hivyo ndivyo, hii hoja kuwa Chadema wanataka katiba mpya ili waingie ikulu inatoka wapi?
Nyuma ya madai ya CHADEMA ya Katiba mpya (mwendelezo wa madai ya viongozi wa vyama vya upinzani) ni dhana yao potofu kuwa vyama vya upinzani vinashindwa kuongoza Dola, kwa maana ya mgombea wao kutokuchaguliwa Rais kwa sababu ya Tume ya Uchaguzi siyo huru. Lakini hawajawahi kutathmini ni kwa nini wagombea wao wa Urais hawapati kura za kutosha.

Kwa kuwa njia ya kuelekea kuongoza Dola inaonekana ni ndefu, kwa Vyama vya Upinzani, viongozi wake wana dhana nyingine (potofu) ya kutaka wigo wa nafasi za kuongoza nchi hii upanuliwe, kwa kudai Muungano wa Serikali Tatu (3). Ikiwa hivyo, wanaamini wengi wao (viongozi wa upinzani) watapata nafasi za madaraka serikalini.
 
Nyuma ya madai ya CHADEMA ya Katiba mpya (mwendelezo wa madai ya viongozi wa vyama vya upinzani) ni dhana yao potofu kuwa vyama vya upinzani vinashindwa kuongoza Dola, kwa maana ya mgombea wao kutokuchaguliwa Rais kwa sababu ya Tume ya Uchaguzi siyo huru. Lakini hawajawahi kutathmini ni kwa nini wagombea wao wa Urais hawapati kura za kutosha.

Kwa kuwa njia ya kuelekea kuongoza Dola inaonekana ni ndefu, kwa Vyama vya Upinzani, viongozi wake wana dhana nyingine (potofu) ya kutaka wigo wa nafasi za kuongoza nchi hii upanuliwe, kwa kudai Muungano wa Serikali Tatu (3). Ikiwa hivyo, wanaamini wengi wao (viongozi wa upinzani) watapata nafasi za madaraka serikalini.
Ulisoma wapi mkuu.
Una elimu gani?
 
Sikwenda shule ila nina elimu ya ufahamu na kujitambua
Ni kweli hujakwenda shule. Na kama umeenda basi ni shule za kata na kusoma vyuo kama CBE, MWALIMU NYERERE na vingine vya mfano huo
 
Back
Top Bottom