Omusolopogasi
JF-Expert Member
- Aug 31, 2017
- 7,101
- 18,051
Mustakabala huo hauwezi kuletwa na watawala madarakani katika wakati wowote. Kuwaomba, kuwalilia au kujaribu kuwalaumu kwa kutouridhia kwa wakati wowote ni kupoteza muda bure.
Wako madarakani kwa kura za kwenye vikapu. Katiba mpya ni mwiba. Hawataki kabisa kusikia (rejea swali la Kikeke kwa Samia). Hawawezi kutupa katiba mpya. Sisi tunaohitaji katiba mpya tuitafute. Tukisubiri tupewe kwenye kisahani, haitatokea. Hata Mbowe naye nadhani kauunga mkono juhudi baada ya kutoka Ikulu.
Sina la kuongeza. Ila najiuliza kwa nini Mbowe amekaa kimya baada ya kutoka Ikula na baada ya kikao cha Kamati Kuu? Maslahi ya nchi yanaweza kuwa yamezikwa kabisa ktk kikao hicho cha Ikulu.
Mbowe au Lissu kuunga juhudi? Hilo mbona litakuwa la mwisho kueleweka?
Baada ya kamati kuu Mbowe alikwenda Hai ambako pamoja na mengine alionana na nguli wengine wakiwamo kina Bobbi Wine.
Tokea huko kaonekana na kina Odinga.
Ninadhani yote ni katika uhamasishaji na kupata uzoefu.
Yote na yote katiba ni yetu ni lazima turejee kwenye harakati za kuidai kwa nguvu zetu zote.
Yaani CCM tumefikia hatua ya kuogopa sanduku la kura, badala yake sanduku letu la kura limekuwa TISS na Polisi? Kweli CCM tumefikia hali hii tuachoofia ni nini? Halafu tumeanzisha ujinga wa kupeana kura za asilimia mia! Mwenyekiti tulimpa 100%, Ndugai tulimpa 100%, Tulia 100%, juzi Kinana 100%. Hivi kweli mtu anawezaje kupata 100%? Au ni ujinga wetu tu?Hawa na chama chao hawanihusu. Sisi tunapigania demokrasia ya kweli na utawala wa sheria ndani ya chama chetu. Muda ndio huu wa kuhakikisha chama chetu kinatoka katika makucha ya sultani na genge lake. Kuendelea kuwa makondoo ndani ya chama ndo kunakosababisha mwenyekiti awe na kiburi cha kuamua lolote ndan ya chama.
Mwenyekiti tulimpa 100%, Ndugai tulimpa 100%, Tulia 100%, juzi Kinana 100%. Hivi kweli mtu anawezaje kupata 100%? Au ni ujinga wetu tu?
Mi najaribu kutoa ushabiki kwenye mawazo yangu. Najaribu kuwa neutral. Mbowe alitakiwa aendeleze madai mara tu baada ya kutoka jela. Leo 2022 wanaambiwa muda hautoshi. Sasa wakisubiri mpaka 2023, 2024... tutaipata kweli?
Nakubaliana na wewe kuwa maandamano ndio njia iliyobaki. Lakini maandamano hayatakuwa spontaneous. Lazima yawe organized. CHADEMA ina platform ya kufanya hivyo kama chama cha siasa. Watu ambao wanaweza kuongoza hili jambo bahati mbaya wako nje ya nchi. Serikali imekataa kuwahakikishia usalama wao kwa vile haitaki warudi.
Wewe unakubalina na hii strategy ya Mbowe ya kukaa kimya?
Tupee jina la hiyo team,Dudumizi 🤔Hawa na chama chao hawanihusu. Sisi tunapigania demokrasia ya kweli na utawala wa sheria ndani ya chama chetu. Muda ndio huu wa kuhakikisha chama chetu kinatoka katika makucha ya sultani na genge lake. Kuendelea kuwa makondoo ndani ya chama ndo kunakosababisha mwenyekiti awe na kiburi cha kuamua lolote ndan ya chama.
Hapo ulipo unakanyagwa kichwani lakini bado unawaza Chadema, una tatizo kichwani. pigania Katiba Mpya nawe uwe huru kutoka mikononi mwa kumsifia mwenyekiti wenu hata akiwatukana.Hata sisi huku kwetu tunapambana na genge la mwenyekiti ili kurudisha demokrasia ya kweli ndani ya chama chetu. Tunaomba chawa wa mwenyekiti na mwenyekiti mwenyewe watambue kuwa hiki chama ni cha wananchi na sio cha mtu binafsi.
Haiwezekani mwenyekiti atumie vipesa vyake alivyokusanya kupitia ruzuku mbali mbali kujimilikisha chama. Lengo la kukiita chama chetu "chama cha demokrasia na maendeleo" lilikuwa ni kutaka kuwaonesha wananchi na wanachama wetu kuwa chama chetu kinasimamia demokrasia ya kweli tofauti na sasa chama kimegeuzwa cha kisultani kinasimamia genge la mwenyekiti na familia yake.
Wenye maono ya kweli na chama wanazuiwa kupewa uongozi wa juu nk, huku ubadhilifu mkubwa wa mali za chama ukiendelea chini ya uongozi wa sultani na genge lake.
Mwaka huu tutahakikisha mwenyekiti na chawa wake wanaheshimu katiba ya chama iliyowekwa chini ya waasisi wetu kina mzee Mtei na hayati bob Makani, na tutarejesha demokrasia ya kweli ili kila mtanzania mwenye sifa zinazostahili kuongoza chama aweze kuongoza chama chetu kwa kipindi cha miaka mitano au kumi kama katiba yetu inavyosema.
Tushachoka kuwa chini ya uongozi wa kisultani. Chawa mnaruhusiwa kuja kwa wingi kunipinga kwa hoja.
View attachment 2173705
View attachment 2173706
Sasa hii akili au matope, unawezaje kufananisha chama kilicho hodhiwa na watu wachache dhidi ya hiki kinacho hodhiwa na mtu mmoja? Ina maana ccm wakifanya jambo lao na mwenyekiti wa chawa lazima aige? Chama chetu kinaitwa cha demokrasia na maendeleo lkn kiuhalisia ndan ya chama hakuna demokrasia wala maendeleo. Afu tukihoji chawa mnakuja kujaribu kukwepesha ukweli.Wewe MATAGA a.k.a mwana Lumumba mambo ya Chadema yanakuhusu vipi?
Mbona hushawishi kuondoa usultani ndani ya chama chako sisiemu ambamo kikundi cha watu wachache kimehodhi kila kitu miaka yote?