Katiba Mpya: Heri Rais Samia akaruhusu mchakato, asisubiri mashinikizo

Katiba Mpya: Heri Rais Samia akaruhusu mchakato, asisubiri mashinikizo

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Suala la kuwapo au kutokuwapo kwa katiba mpya kwa sasa halina mbadala tena. Ni wazi kuwa watanzania walio wengi tunahitaji katiba mpya na iliyopo haitufai tena. Tofauti iliyopo ni kwenye viwango (extent) tu.

Ni dhahiri kuwa mchakato huu usiporuhusiwa kwa hiari, mashinikizo yatafuata. Huu ndiyo ulio ukweli mchungu.

Katiba mpya haizuiluki. Kwa hiari au kwa shuruti katiba mpya yaja. Kwa hiari, Mama ataibuka mshindi kwenye hili. Kwa shuruti, mama anajiweka matatani.

Chuki inazidi kumea baina ya watu na hata baina ya watu na serikali. Hali hii inahitaji ufumbuzi sasa na haiwezi tena kupuuzwa. Mzizi wa fitina ukiwa mapungufu ya wazi kwenye katiba iliyopo isiyokidhi mahitajio.

Mama Samia tunakuombea ukaione busara iliyoko katika jambo hili mapema na hatimaye ukaibuke kidedea.

Beberu hakukosea sana kusema: "Time time, before time times you."

Ninawasilisha.
 
Mkuu siyo Rahisi ni Hivyo, Ngoja tuone, maana CCM wanajua ya kwamba Katiba Mpya yenye tume huru ya Uchaguzi ndio Mwisho wao. Je wako tayari Kukabidhi nchi, kwa Maana Katiba Mpya Means CCM Kwa Kheri kama ilivyokuwa KANU ya Kenya.
 
Suala la kuwapo au kutokuwapo kwa katiba mpya kwa sasa halina mbadala tena. Ni wazi kuwa watanzania walio wengi tunahitaji katiba mpya na iliyopo haitufai tena. Tofauti iliyopo ni kwenye viwango (extent) tu.

Ni dhahiri kuwa mchakato huu usiporuhusiwa kwa hiari, mashinikizo yatafuata. Huu ndiyo ni ukweli ulio mchungu.
Barakoa mlililia akawapa..hii nyingine sahauni hadi mtakapokuwa nanyi wendazenu
 
Katiba sio kigezo cha kuitoa sisiemu madarakani. Sera thabiti na ushawishi kwa jamii kubwa ya wananchi(wapiga kura) ndo kitafanya vyama vya upinzani kushika madaraka.
 
Ngoja tuone, maana CCM wanajua ya kwamba Katiba Mpya yenye tume huru ya Uchaguzi ndio Mwisho wao.

Uzuri ni kuwa hata wao wanataka katiba mpya. Tatizo tu ni pale wanapoona katiba mpya itawanufaisha pia wengine wakiwamo Chadema.

Ukiwaweka Chadema pembeni, ufahamu kuwa hata Majaliwa anataka katiba mpya, pia Bashiru, Pole pole, Chalamila, Kigwangala, Gwajiboy nk wote CCM hao.

Hali ni hivyo hivyo hata kwa akina Shaka, Chongolo na wengi tu walioko huko.

Kwa mtaji huu bora mama angeliona hili akalitendea haki tu, wala hata si kufanya maamuzi magumu.
 
Hivi maamuzi ya Katiba ni swala la Raisi kuamua? Yaani Raisi ndio decision maker wa either review ya katiba ifanyike au la? Katiba ya sasa inasemaje kuhusu review ya katiba maana naona kila mtu anasema Raisi ndio aruhusu why yeye?
 
katiba sio kigezo cha kuitoa sisiemu madarakani. Sera thabiti na ushawishi kwa jamii kubwa ya wananchi(wapiga kura) ndo kitafanya vyama vya upinzani kushika madaraka.

Suala si kuitoa CCM madarakani. Bali kinachohitajika ni katiba mpya itakayo weka utangamano wa haki baina ya watu na baina ya watu na serikali.

Ni muhimu kuona tofauti ya mawili hayo.
 
Tusiishie kwenye mchakato, napenda sasa twende tukamalizie kile kipande kilichobaki toka kwa JK.
 
Hivi maamuzi ya Katiba ni swala la Raisi kuamua? Yaani Raisi ndio decision maker wa either review ya katiba ifanyike au la? Katiba ya sasa inasemaje kuhusu review ya katiba maana naona kila mtu anasema Raisi ndio aruhusu why yeye?

Rais hana maamuzi ya nini cha kufanya na katiba au lini, bali kuridhia kwake ni muhimu kwa ajili ya amani na utulivu.

Ila anaweza kushurutishwa au anaweza ku preempt kwa kutoa ridhaa mapema. Ku preempt kwake ndiyo ulio msingi wa mada kwa kuzingatia hapa tulipo sasa.
 
Barakoa mlililia akawapa..hii nyingine sahauni hadi mtakapokuwa nanyi wendazenu

Mkuu kwani wewe huyaoni mapungufu ya katiba yaliyopo? Kama Majaliwa, Bashiru, nk wakiwamo wabunge hawa walio wanufaika wakuu wa katiba iliyopo nao wana taabu nayo:



Wewe utakuwa nani kuwa nje?

Ila mama ajue ikibidi, safari hii tumedhamiria kweli kweli. Siyo siri tuko tayari kwenda zetu kwa kesho bora zaidi ya watoto na watoto wa watoto wetu.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Haiheshimiwi na ndiyo sababu katika katiba mpya lazima kuwepo na vipengele mbali mbali vya kuwapa adhabu kubwa wote watakaohusika kuvunja katiba ya nchi kwa namna moja au nyingine. Kwa mfano Rais anaposhiriki kuvunja katiba Watanzania wawe na uwezo wa kumshtaki, yeye na wote alioshirikiana nao kuvunja katiba, mahakamani na adhabu yake ianzie kifungo cha miaka 10 na kuendelea.

Hii katiba tuliyonayo inaheshimiwa kwanza kabla ya kudai hiyo mpya?
 
Hii katiba tuliyonayo inaheshimiwa kwanza kabla ya kudai hiyo mpya?

Katiba tuliyo nayo haiheshimiwi na baadhi ya watu kwa sababu ya mapungufu na mianya ya wazi iliyomo.

Inahitajika mpya itakayo hakikishwa kuwa haiachi mianya kama ilivyopo.

Mfano: kwanini wawepo watu wasioweza kushitakiwa kwa mapungufu yao yoyote kwa mujibu wa katiba?

Itaheshimiwa katiba vipi kwenye mazingira kama haya?
 
Haahaha mtu hajawahi ridhika.

Uzuri ni kuwa hata yeye Samia asiyekuwa Rais anaihitaji katiba mpya.

Kwamba binadamu hatosheki? Si kwa katiba hii ambayo msingi wake ni wa serikali ya chama kimoja iliyo asisiwa miaka 44 iliyopita.
 
Suala la kuwapo au kutokuwapo kwa katiba mpya kwa sasa halina mbadala tena. Ni wazi kuwa watanzania walio wengi tunahitaji katiba mpya na iliyopo haitufai tena. Tofauti iliyopo ni kwenye viwango (extent) tu.

Ni dhahiri kuwa mchakato huu usiporuhusiwa kwa hiari, mashinikizo yatafuata. Huu ndiyo ulio ukweli mchungu.

Katiba mpya haizuiluki. Kwa hiari au kwa shuruti katiba mpya yaja. Kwa hiari, Mama ataibuka mshindi kwenye hili. Kwa shuruti, mama anajiweka matatani.

Chuki inazidi kumea baina ya watu na hata baina ya watu na serikali. Hali hii inahitaji ufumbuzi sasa na haiwezi tena kupuuzwa. Mzizi wa fitina ukiwa mapungufu ya wazi kwenye katiba iliyopo isiyokidhi mahitajio.

Mama Samia tunakuombea ukaione busara iliyoko katika jambo hili mapema na hatimaye ukaibuke kidedea.

Beberu hakukosea sana kusema: "Time time, before time times you."

Ninawasilisha.
Hao "Watanzania wengi" ulikutana nao lini wakaazimia uyasemayo?
Katiba mpya ama ya zamani siyo muarobaini wa Matatizo yanayowakabili wananchi kwa sasa.
Kenya ilijinasibu kuwa na Katiba mpya na tume huru ya uchaguzi, lakini bado figisu figisu za kutoaminiana zinazidi kupamba moto, sababu..waliopo madarakani wanaonekana wanafaidi zaidi keki ya taifa, na wasio chama madarakani wanaona salama yao bado haijapatikana!
Kuna nchi duniani haina hata katiba, lakini wanaendelea na maisha yao kwa raha mustarehe.
Usirubunike kwa ghirba za wanasiasa wachumia tumbo...Kaza mkwiju kwa kufanya kazi za halali kwa nguvu na bidii zote ili ujikwamue kiuchumi kwani hilo ndilo litakalokuokoa wewe na familia yako na utaishi vizuri hata kama kuna katiba mpya, ya zamani, ama bila katiba.
 
Hao "Watanzania wengi" ulikutana nao lini wakaazimia uyasemayo?
Katiba mpya ama ya zamani siyo muarobaini wa Matatizo yanayowakabili wananchi kwa sasa.
Kenya ilijinasibu kuwa na Katiba mpya na tume huru ya uchaguzi, lakini bado figisu figisu za kutoaminiana zinazidi kupamba moto, sababu..waliopo madarakani wanaonekana wanafaidi zaidi keki ya taifa, na wasio chama madarakani wanaona salama yao bado haijapatikana!
Kuna nchi duniani haina hata katiba, lakini wanaendelea na maisha yao kwa raha mustarehe.
Usirubunike kwa ghirba za wanasiasa wachumia tumbo...Kaza mkwiju kwa kufanya kazi za halali kwa nguvu na bidii zote ili ujikwamue kiuchumi kwani hilo ndilo litakalokuokoa wewe na familia yako na utaishi vizuri hata kama kuna katiba mpya, ya zamani, ama bila katiba.
Chizi wew, jiulize mwenyewe kwanini
 
Hao "Watanzania wengi" ulikutana nao lini wakaazimia uyasemayo?
Katiba mpya ama ya zamani siyo muarobaini wa Matatizo yanayowakabili wananchi kwa sasa.
Kenya ilijinasibu kuwa na Katiba mpya na tume huru ya uchaguzi, lakini bado figisu figisu za kutoaminiana zinazidi kupamba moto, sababu..waliopo madarakani wanaonekana wanafaidi zaidi keki ya taifa, na wasio chama madarakani wanaona salama yao bado haijapatikana!
Kuna nchi duniani haina hata katiba, lakini wanaendelea na maisha yao kwa raha mustarehe.
Usirubunike kwa ghirba za wanasiasa wachumia tumbo...Kaza mkwiju kwa kufanya kazi za halali kwa nguvu na bidii zote ili ujikwamue kiuchumi kwani hilo ndilo litakalokuokoa wewe na familia yako na utaishi vizuri hata kama kuna katiba mpya, ya zamani, ama bila katiba.

Hao watanzania wengi nimekutana nao kote nchini. Ndiyo maana nimekuorodheshea hawa uone walivyotapakaa:

Majaliwa, Bashiru, Polepole, Chalamila nk wakiwamo hata wabunge wanaoona malipo yao hayatoshi.

Wengine ni wote wanaolilia tume huru ya uchaguzi, wasiokuwa na ajira, wafanyakazi wanaonung'unikia mishahara midogo kila leo nk.

Inafahamika kuwa wapo wabinafsi wachache ambao ni wanufaika wa moja kwa moja wa katiba iliyopo na wale wasiojua kuwa ni waaathirika wa katiba hii kwa kukosa elimu tu.

Wewe upo kundi gani hapo mkuu?
 
Kuna mambo lazima uzibe masikio kama husikii vile...

Kwa upepo unavyovuma, hali ya uwanja ilivyo na watu nao walivyo dhamiria, Mama mbona kawafungua macho wengi?

Wasiotaka kurejea tulikokuwa si wachache. Wanahitaji kesho ya uhakika. Inaeleweka kuwa inawezekana lakini si bila katiba sahihi.

Mola amjalie Mama kuiona busara iliko. Urais si lelemama hakuna kulala.

La Katiba mpya liko njiani linakuja. Uchaguzi ni kwake. Kusubiri mashinikizo au kuwahi na kujizatiti kileleni.
 
Back
Top Bottom