Katiba mpya itatuletea matatizo haya 3 makubwa kwa nchi yetu

Katiba mpya itatuletea matatizo haya 3 makubwa kwa nchi yetu

Johnny Sack

JF-Expert Member
Joined
Jan 21, 2017
Posts
8,984
Reaction score
19,288
Nchi yetu sio ya demokrasia, hili tuliseme wazi bila kudanganya

Rais wa nchi hii anaamuliwa na kikao cha kamati kuu ya CCM na wazee, amboa ndio huamua nani akatwe jina na nani apitishwe kwenda kupigiwa kura na wajumbe wa chama

Akishapitishwa na wajumbe ndio tayari ameshakuwa rais, sababu mengine yanayofuata tunajua mwisho wake

Na katiba mpya inataka nchi hii iwe ya kidemokrasia, yaani Rais awe anaamuliwa na wananchi na sio kamati ya CCM

Hili nalipinga, Rais kuamuliwa na wananchi ni hatari, kwa sababu hizi

1. Wananchi wengi wa Tanzania ni wajinga, wananchi wajinga hawajui kutofautisha kati ya kiongozi mzuri na kiongozi asiyefaa, kiongozi mbaya ambaye atakuwa na uwezo wa kuhadaa wananchi wengi basi huyo ndio atakuwa Rais, hii ni hatari sana

2. Kuleta ukabila, tumeona katika miaka 5 iliyopita ukabila umeanza kumea Tanzania, lipo kundi la watu utasikia wakijidai sisi ndio tupo wengi Tanzania, sisi tunaweza kuamua Rais awe nani n.k, Rais akiwa anaamuliwa na wananchi itachochea zaidi ukabila kwa watu kupiga kura kikabila ili watoe Rais kwenye kabila lao

3. Rushwa na ufisadi kutamalaki, Rais akiwa anaamuliwa na wananchi inachangia viongozi kukwapua fedha za umma kwa ajili ya kuzitumia kwenye kampeni ya urais kuhakikisha wanashinda

Mfano Katika uchaguzi mkuu wa Kenya mwaka jana, Serikali ilikuwa ikitumia shilingi bilioni moja na nusu kila siku kwenye kampeni kuhakikisha mgombea wake Raila Odinga anashinda

Nini Cha kufanya?
Kuwaachia wazee wetu wastaafu pamoja na Chama kituamulie nani atakuwa Rais ni vizuri zaidi kuliko wananchi wasiojua lolote na wanaodanganyika kirahisi.

Nchi hii kwa sasa ipo chini ya Rais na wazee wenye busara ambao wataendelea kuhakikisha viongozi na wazee wajao wanakuwa na busara
 
Kati ya hivi ulivyovitaja kipi ambacho hakitokei kwa sasa hapa Tanzania?

Sasa kama hao wazee wameshindwa kutuletea watu ambao watayaondoa haya yote kwanini tusijaribu wananchi tuone kama unachokisema kipo sawa?

Unatawaliwa tu na fear of unknown ama wewe kwa sasa nimfaidika wa mfumo huu usio na check and balances, otherwise ndiyo ninyi mkitoka tu kwenye hiyo position ndiyo wakwanza kuja na mapendekezo against haya haya unayoya propagate for the time being.

Nchi inahitaji kutokuwa na mtu mmoja aliyejaziwa madaraka kama ya Mungu...Kuwe na urahisi wa wananchi kuwajibisha na kuwajibika kupitia mifumo na siyo kundi ama mtu fulani.
 
1.Kama wananchi wengi wa Tanzania ni wajinga kwa nini usiseme Rais achaguliwe na watu wenye elimu kuanzia Diploma kwenda juu tu kwa sababu hata katika hao wajumbe wa CCM wanaompitisha wajinga na vilaza wapo wengi tu

2.Kuhusu ukabila, hilo ni jambo rahisi sana kwa sababu katiba mpya inaweza kuweka mgombea ili ashinde urais lazima ashinde kwa zaidi 51% ya kura katika nusu ya mikoa yote ya nchi.

3.Unasemaje kuhusu Rushwa na ufisadi uliotamalaki nchini kwa miaka mingi wakati hatuna Katiba mpya? Escrow, EPA, rada ya BAE, ndege ya Rais, Meremeta, 1.5T, Plea bargain n.k mbona vimekuwepo tu pasipo uwepo wa katiba mpya?
 
Kama wananchi wengi w Tanzania ni wajinga kwa nini usiseme Rais achaguliwe na watu wenye elimu kuanzia Diploma kwenda juu tu?
Sasa hili ndio wazo, sasa tutalitekelezaje?
 
JK: Mwenyekiti wa CCM ana nguvu kubwa sana
Huo ndiyo ukweli, laiti hata kungekuwa na mwenyekiti separate from Rais, lakini mtu huyo huyo unamkuta huku ukikwazana naye unamkuta na upande wa pili, waliotofauti naye kimawazo watayapeleka kwa nani?

Katika makosa aliyoyafanya Mwl Baba yetu, alale mahala pema ni kushindwa kutuachia katiba nzuri baada ya yeye kung'atuka...Tanzania leo tungekuwa nchi ya mfano kama 1995 tungeingia vyama vingi huku tukiwa na katiba mpya
 
Kati ya hivi ulivyovitaja kipi ambacho hakitokei kwa sasa hapa Tanzania?

Sasa kama hao wazee wameshindwa kutuletea watu ambao watayaondoa haya yote kwanini tusijaribu wananchi tuone kama unachokisema kipo sawa?

Unatawaliwa tu na fear of unknown ama wewe kwa sasa nimfaidika wa mfumo huu usio na check and balances, otherwise ndiyo ninyi mkitoka tu kwenye hiyo position ndiyo wakwanza kuja na mapendekezo against haya haya unayoya propagate for the time being...

Nchi inahitaji kutokuwa na mtu mmoja aliyejaziwa madaraka kama ya Mungu...Kuwe na urahisi wa wananchi kuwajibisha na kuwajibika kupitia mifumo na siyo kundi ama mtu fulanj
Tanzania ni nchi inyosifika sana kwa kutokua na ukabila, kiwango cha chini cha ufisadi kuliko hata hizo nchi zenye katiba nzuri
 
3. Rushwa na ufisadi kutamalaki, Rais akiwa anaamuliwa na wananchi inachangia viongozi kukwapua fedha za umma kwa ajili ya kuzitumia kwenye kampeni ya urais kuhakikisha wanashinda
Katiba ya sasa ndio kichaka cha wala rushwa. Katiba ya Warioba inataka rais aliye madarakani ashitakiwe kwa makosa anayoyafanya. Hili ni pigo kwa CCM kwani wao ndio wataathirika kwa makosa ya rushwa na ufisadi
 
Katiba ya sasa ndio kichaka cha wala rushwa. Katiba ya Warioba inataka rais aliye madarakani ashitakiwe kwa makosa anayoyafanya. Hili ni pigo kwa CCM kwani wao ndio wataathirika kwa makosa ya rushwa na ufisadi
Kenya Rais anashatikiwa kwa rushwa kabla au baada ya kustaafu, je hilo limeondoa rushwa? Hapana, tena sisi tuna afadhali


Afrika Kusini Rais anashatakiwa na hata kuondolewa madarakani, je hilo limeondoa rushwa? Tena wanatuzidi
 
Wewe ni moja ya wanufaika wa huu mfumo mbovu.
Eti Wananchi wengi ni wajinga!
Wewe mwenyewe ni mjinga sababu umetoa hoja za kijinga sana.
Wananchi ukiwapa kanga na pilau si tayari kura unazo?
 
Kenya Rais anashatikiwa kwa rushwa kabla au baada ya kustaafu, je hilo limeondoa rushwa? Hapana, tena sisi tuna afadhali


Afrika Kusini Rais anashatakiwa na hata kuondolewa madarakani, je hilo limeondoa rushwa? Tena wanatuzidi
Kenya uchumi wake kwa ukubwa ukoje ukilinganisha na Tanzania?
 
Nini Cha kufanya?
Kuwaachia wazee wetu wastaafu pamoja na Chama kituamulie nani atakuwa Rais ni vizuri zaidi kuliko wananchi wasiojua lolote na wanaodanganyika kirahisi.
Matunda ya mfumo wa Elimu yetu ya Kipuuzi!
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Nchi yetu sio ya demokrasia, hili tuliseme wazi bila kudanganya

Rais wa nchi hii anaamuliwa na kikao cha kamati kuu ya CCM na wazee, amboa ndio huamua nani akatwe jina na nani apitishwe kwenda kupigiwa kura na wajumbe wa chama

Akishapitishwa na wajumbe ndio tayari ameshakuwa rais, sababu mengine yanayofuata tunajua mwisho wake

Na katiba mpya inataka nchi hii iwe ya kidemokrasia, yaani Rais awe anaamuliwa na wananchi na sio kamati ya CCM

Hili nalipinga, Rais kuamuliwa na wananchi ni hatari, kwa sababu hizi

1. Wananchi wengi wa Tanzania ni wajinga, wananchi wajinga hawajui kutofautisha kati ya kiongozi mzuri na kiongozi asiyefaa, kiongozi mbaya ambaye atakuwa na uwezo wa kuhadaa wananchi wengi basi huyo ndio atakuwa Rais, hii ni hatari sana

2. Kuleta ukabila, tumeona katika miaka 5 iliyopita ukabila umeanza kumea Tanzania, lipo kundi la watu utasikia wakijidai sisi ndio tupo wengi Tanzania, sisi tunaweza kuamua Rais awe nani n.k, Rais akiwa anaamuliwa na wananchi itachochea zaidi ukabila kwa watu kupiga kura kikabila ili watoe Rais kwenye kabila lao

3. Rushwa na ufisadi kutamalaki, Rais akiwa anaamuliwa na wananchi inachangia viongozi kukwapua fedha za umma kwa ajili ya kuzitumia kwenye kampeni ya urais kuhakikisha wanashinda

Mfano Katika uchaguzi mkuu wa Kenya mwaka jana, Serikali ilikuwa ikitumia shilingi bilioni moja na nusu kila siku kwenye kampeni kuhakikisha mgombea wake Raila Odinga anashinda

Nini Cha kufanya?
Kuwaachia wazee wetu wastaafu pamoja na Chama kituamulie nani atakuwa Rais ni vizuri zaidi kuliko wananchi wasiojua lolote na wanaodanganyika kirahisi.

Nchi hii kwa sasa ipo chini ya Rais na wazee wenye busara ambao wataendelea kuhakikisha viongozi na wazee wajao wanakuwa na busara
Kwanza, inabidi uwaombe Watanzania msamaha kwa kuwatukana kuwa nbi wajinga. Ina maana ni wewe TZ una akili. Pili, nini maana ya vyama vingi, kama unataka wazee wa CCM wawaamulie TZ raisi awe nani. Jinsi, CCM ina nafasi ya kuteua mgombea ndivyo hivyo itakuwa kwa vyama vingine. Siasi na uchaguzi ni "very complicated". Kumpigia mgombea kura kunategemea vigezo vingi ambavyo huwezi kuviepuka, na wakati mwingine inabidi mpiga kura a"prioritize" vigezo na saa nyingine vigezo vinapingana. Hivi vigezo vinatumika hata kwa sasa. Hivi vigezo vipo nchi zote. Watu wanaweza kumpigia mtu kura kwa sababu nyingi, lakini naona wewe umeona kabila tu.

Hakuna kitu hatari kama nepotism iliyopo CCM. Nchi imekuwa ya wazee wachache. Ndiyo maana ulimsikia Nnauye, Makamba, Malima, Mwingi, na wengineo ukiwa kichanga na sasa una miaka 70 au 80 bado hayo majina bado yapo. Hii nepotism katika siasa na nchi ndiyo inayofanya tusiwe na mabadiliko, maana nyoka hawezi kuzaa chura au mjusi, na inbreeding ni hatari kwa kuiendelea uwepo wa binadaam maana mnapoana ndugu mwisho wenu ni kuteketea. Hata wafugaji wanajuwa pia mbegu lazima itoke nje. Lakini sisi tunang'ang'ania CCM iliyo chini ya koo. Wewe unafikiri koo zina fikra mbadala. Wewe unafikiri kwa nini Magufuli aliuawa. Magufuli hakuwa katika koo teule za CCM.

Wewe unafikiri watu kama Kinana wataleta mabadiliko gani zaidi ya kutetea biashara zake za meli ambazo hazilipi kodi. Makamba atatetea nini zaidi kuishukuru CCM tokana ni kifungo kikubwa kilichokuwa kinamkabili akiwa mwalimu na sasa aqnastarehe na anataka mtoto wake aliyeibia mtihani na kufutiwa matokea kurejea katika kilele. Wizi wa mitihani ni kosa la jinai, lakini kwa CCM ni kigezo cha kupokewa kwenye "inner circle" maana watu kama hao wanatakiwa. Wewe unafikiri ni bure TANESCO kumuongezea mkandarasi wa bwawa la Nyerere mwaka mmoja na Makamba akatupamo mwaka mmoja wa kwake na kuwa miaka minne. Wewe unadhania ni bure Bunge kuagiza Waziri makamba na Wenzake waanze kumkata pesa mkandarasi pesa kwa kuchelewesha mradi lakini Makamba na wenzake wamegoma na hakuna kitakachofanyika. Yaani mnategemea Makamba na wenzake wamchukulie hatua mkndarasa, alafu wakale wapi. Makamba kaajiriwa na Samia/Kikwete/Baba yake na anawajibika kwao, siyo kwa Bunge. NCHI INALIWA nadiyo maana baada ya kufariki Magufuli walirudishwa wapiga deal wabobevu. Sasa nchi inaliwa kila upande.
 
Back
Top Bottom