Katiba mpya: Kosa la CCM ni lipi.?

Katiba mpya: Kosa la CCM ni lipi.?

Kaka mwisho

JF-Expert Member
Joined
Dec 19, 2011
Posts
407
Reaction score
178
Tukielekea kwenye kuunda katiba mpya ya jamhuri wa muungano pamekuwa na mjadala mkubwa sana kuhusu aina ya muungano, kuna watu wanaotaka serikali 1, 2 au 3 na kuna vyama tayari vimetoa misimamo yao mfano mzuri ni CHADEMA, CUF na NCCR Mageuzi vimeungana pamoja na kutaka serikali 3.

CCM ilipotangaza kuwa msimamo wake ni serikali 2 imekuwa nongwa. Kosa la CCM ni lipi ikiwa kila vyama vimetoa misimamo yake kuhusu muundo wa muungano.

Presha ya wapinzani na watu wanaotaka serikali 3 inatoka wapi ikiwa siku ya mwisho wananchi ndio tutakaoamua kwa kura ya maoni.

Demokrasia ni mashindano ya hoja na kura, tushindane kwa hoja na siku ya mwisho wajumbe wataamua kwa kura zao pale bungeni.

Ama kweli kunya anye kuku akinya bata kaharisha.
 
kwa mujibu wa tume ya Warioba ni kuwa zaidi ya asilimia 60 ya walio toa maoni yao wanataka serekali 3 ikumbukwe hata CCM walitoa maoni yao sasa CCM ni Nani mpaka ipingane na maoni ya asilimia 60 walikuwa wapi kabla bunge halijaanza! ikumbukwe kuwa kazi ya bunge la katiba si kubadilisha maoni ya wa TZ ila kuiboresha ,CCM jifunzeni kuwatumikia wanainchi mnakera sana
 
kwa mujibu wa tume ya Warioba ni kuwa zaidi ya asilimia 60 ya walio toa maoni yao wanataka serekali 3 ikumbukwe hata CCM walitoa maoni yao sasa CCM ni Nani mpaka ipingane na maoni ya asilimia 60 walikuwa wapi kabla bunge halijaanza! ikumbukwe kuwa kazi ya bunge la katiba si kubadilisha maoni ya wa TZ ila kuiboresha ,CCM jifunzeni kuwatumikia wanainchi mnakera sana

Kimsingi hicho kinachofanywa ama kuhubiriwa na akina Nape ni msimamo wa watu wachache ndani ya CCM wanaotaka kubaka maoni na matakwa ya Watanzania kwa faida zao binafsi. Walifanya jitihada kubwa kuvuruga hata uundwaji wa mabaraza ya kata kwenye ngazi ya wilaya ili waweze kupenyeza ajenda zao mfu na baada ya kuona jitihada zao zimegonga mwamba wanajitahidi kuingilia hata BUNGE MAALUM LA KATIBA.

Hakika jitihada zao mfu na potofu zitashindwa na mwisho wa siku aibu itakuwa kwao. EE MWENYEZI MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
Kosa la ccm na akina nape wake wanasemea huo msimamo wao dodoma, kumbe inatakiwa waende uwanja wa kibandamaiti zanzibar waitishe mkutano wa hadhara waseme huo msimamo wao , mbona nape hafanyi hivo? Kakazania tu serikali 2 akiwa dodoma , aende na zanzibar akaseme hizo serikali zake mbili
 
Kama kweli wanataka serikali mbili kama sasa, mbona viongozi wa kitaifa kama Rais wa Jamhuri, Makamu wa Rais au Waziri Mkuu hawafanyi ziara Zanzibar kuhimiza maendeleo au kufungua miradi? Kwanini hawaendi kama kweli tupo kwenye muungano!
 
Ina maana Rais wa Muungano huwa hawajibiki ipasavyo kwa upande wa Zanzibar?
 
katiba ya Zanzibar inaitambua kama nchi,Kikwete akienda kule yeye ni mgeni jamani hamuelewi protocal nini,ya kule yanamalizwa na Raisi wao,JK anachughulikia yale ya muungano tu...
Haki za Raia ya Zanzibar zilizo ainishwa kwenye katiba yao ni kulinda maslahi yao ya Kiuchimi,Kijamii na Kisiasa...
 
kwa mujibu wa tume ya Warioba ni kuwa zaidi ya asilimia 60 ya walio toa maoni yao wanataka serekali 3 ikumbukwe hata CCM walitoa maoni yao sasa CCM ni Nani mpaka ipingane na maoni ya asilimia 60 walikuwa wapi kabla bunge halijaanza! ikumbukwe kuwa kazi ya bunge la katiba si kubadilisha maoni ya wa TZ ila kuiboresha ,CCM jifunzeni kuwatumikia wanainchi mnakera sana

watu waliohojiwa na tume ya Warioba hawazidi hata elfu 50, wakati tupo zaidi ya milion 46. Tusubiri kura ya maoni ndio suluhisho.
 
Acha ujinga!
Kosa la Miccm wenzio ni kujazana mule bengeni!
Ikipita kura, ni lazima miccm itashinda kwa vile imejazana mle!
 
Back
Top Bottom