Wakudadavuwa
JF-Expert Member
- Feb 17, 2016
- 17,506
- 16,003
Mantiki ya andiko inakosa maana. Sioni umuhimu wa kuandika wewe ni CHADEMA au CCM.
Jenga hoja yako. Katiba tunayoongekea ni ya nchi. Siyo ya CCM wala CHADEMA. Kwa fikra zako unaamini kuwa CHADEMA wote wanataka katuba mpya, na CCM wote hawataki katiba mpya?
Wananchi walio wengi, webye vyama na wasio na vyama, wanataja katiba mpya. Hilo lilidhihirishwa kwa data, na tume ya Warioba. Kwa sasa, zaidi kinachogomba miongoni mwa wananchi, ni timing.
Kumbe hata rasimu ya pili ya Warioba ilikuwa haifai.
Swala la mbunge kuhama chama na ubunge wake halifai. Hiyo rasimu ingepita nadhani kipindi kile cha hamahama cha wabunge wangeweza kuhama bila hata kununuliwa kwa bei kubwa, wangepozwa kwa hela kidogo tu ya mboga na kuhama chama.
So binafsi hiyo rasimu ya Warioba ilikuwa haifai pia, japo CHADEMA walisusia mchakato kwa hoja dhaifu ila kumbe subconciously walifanya la maana sana. Mambo gani ya mtu kuhama chama anahama na ubunge wake? Huko ni kuwasaliti wananchi. Wananchi walimpa ubunge kutokana na sera za chama chake hivyo anapohama chama anaenda kinyume na makubaliano ya wapiga kura wake.
Chadema hakuna ruzuku, wanatafuta mwanya wa kupiga hela kupitia bunge la katiba. Raisi Samia achana nao hawa wachumia tumbo wa kisiasa.
Kwa hiyo wewe unataka kusema kila alitakalo Lissu ndilo lafaa kuwa kwenye Katiba?
CCM pamejaa wajinga sana.Chadema hakuna ruzuku, wanatafuta mwanya wa kupiga hela kupitia bunge la katiba. Raisi Samia achana nao hawa wachumia tumbo wa kisiasa.
Sasa hoja ya Serikali Tatu kama ilikuwa haina msingi kwa maelezo yako inakuwaje tena iharibu mchakato wa kupata katiba nzima?.Naitaka katiba mpya . lakini hapa mkuu unahoja kubwa. Lile liumoja lao ukawa lilisababisha mkwamo wa katiba. Cuf walikuwa lazima wasikilizwe na ukawa wenzao kuhusu mamlaka ya Zanzibar. Ndio maana hoja ya serikaki tatu isiyo na msingi wowote ikavuruga mchakato
Eti mimi ni chadema [emoji3][emoji3] jamaa jinga sana
Ivi nyie kipindi hicho mlikuwa watoto? Chukua rasmu ya warioba ambayo ndio maoni ya wananchi halisi na chukua Katiba pendekezwa Soma between the lines utuambie hazifanani kwa kiasi gani na utuambie kilicho andikwa kwenye Katiba pendekezwa ni nini na walipata hizo baraka wapi? Ni wehu tu na waganga njaa wanaweza kukubali na kubaki bungeni kwa kilicho fanywa na bunge la katiba
Je, huoni kuwa ni Zanzibar ni nchi , ina katiba, ina bunge lake, ina rais wake, ina wimbl waje wa taifa? xHii Zanzibar iliungana na nani mpaka tukapata Tanzania? Hiyo nchi iko wapi?Kwan nn faida na harasa ya serikali 3 na zipi faida na harasa za serikali 2? Wenda kila upande ulikuwa unajaribu kujitengenezea mazingira ya upataji kiurahis ndio maana hawakuona vitu vingne zaid ya hilo.
Wewe siyo Chadema bali Kadema!Habari za usiku wanajukwaa. Ni muda mrefu sijachangia chochpte humu wala kuweka bandiko lolote humu zaidi tu ya kusoma mawazo yenu.
Naomba nieleweke kwamba mimi ni mfuasi mtiifu wa chadema na nitaendelea kukitii siku zote.na niweke wazi kwamba sijawahi kukihujumu chama wala sifikirii kufanya hivyo. Nije kwenye mada sasa. CHADEMA tunataka katiba mpya lakini kiukweli suala la katiba mpya haliwezekani.
Kwanini nasema haliwezekani? Kwasababu wakati wa kuitengeneza Rasimu ya pili ya warioba 2014 ili iwe the proposed constitution hawahawa viongozi wetu walikuwa ni wajumbe pale bungeni lakini walishindwa kuendelea kukaa pale bungeni na wenzao wengine kwa sababu tu ya suala la serikali mbili na serikali tatu. Wakabishana weeee hadi kufikia kuiambia serikali ilete hati ya muungano.
Ukiangalia hilo suala la muungano halikuwa na athari yoyote lakini wao wakasusa na kukimbia pale bungeni wakiongozwa na lipumba ambaye leo wanamuona sio mpinzani.ndani ya ile rasimu kuna mambo mengi ya muhimu sana wangeweza kuyapambania ambayo kama wangesusa kwa sababu ya hayo tungewaona ni mashujaa.
Mfano suala la Wabunge kuongoza miaka 10. Waziri na spika kutokuwa wabunge, matokeo ya raisi, wabunge na madiwani kuhojiwa mahakamani, tume huru ya uchaguzi, Mamlaka ya Rais kupunguzwa, mgombea binafsi, mbunge anapofariki basi aliyeshika nafasi ya pili wakati wa uchaguzi basi anakuwa mbunge na wananchi kuwawajibisha wabunge wavivu, mbunge akihama chama basi anahama na ubunge wake na sio mambo ya by election. Mengine nadhani kama ulibahatisha kuyaona kama ulisoma ile draft.
Sasa, ukiangalia kilichowafanya wakasusa ni kitu kidogo na kisicho na maana yoyote ile kwa wananchi.
Binafsi nahisi Rais Samia ameshagundua kwamba hata akisema mchakato urudi upya mambo yatakuwa ni yaleyale business as usual. Yaani CCM watataka serikali mbili huku CHADEMA wakitaka serikali tatu na mwisho hawataelewana na mchakato utakwama tena na hivyo kodi za wananchi zitakwenda bure Maana kumbuka walikuwa wanakula posho daily Tsh laki 3. Hivyo Rais sidhani kama atakubali huu mchakato urudiwe maana mambo yatajirudia ni yaleyale tu. Itakuwa ni uharibifu wa fedha..ni vizuri wang’ang’anie tu hii iliyopo ifanyiwe amendments baadhi ya vipengele lakini suala la katiba mpya hilo I’m sure halitafanikiwa.
Kitu kingine wanachohitaji viongozi wetu ni political rallies kuruhusiwa ni kweli hilo sio hisani bali ni takwa la kikatiba iliyopo lakini kuhusu hilo nadhani mheshimiwa Rais ashalitolea ufafanuzi tayari.kwamba tusubiri kwanza ajenge uchumi wawekezaji waje wakute nchi ikiwa tulivu haina labshalabsha zozote ndipo turudi majukwaani (angalau huyu katoa sababu zenye mashiko kidogo kuliko mwendazake).
Maana usisubiri hadi Raisi aongee direct kwamba “jamani utawala ulopita nilikuwa nikimshauri hiki na kile mwenzangu hakuwa akinisikiliza ndio Maana uchumi umeyumba”kwa sababu hakuna asiyejua kwamba Mzee alikuwa hashauriki.sasa Mama hawezi kuanza kumkandia na kuanza kujitetea.
Mimi nadhani tuwe watulivu tukisubiri huo uchumi unaojengwa then tukiona labda miaka miwili au mmoja unakata tunaweza kurudi kumkumbusha.lakini kwa style kama ya kuwapa vipaza watu kama mdude halafu kwa kauli kama zile kiukweli haipendezi na mwisho tutampa hasira Raisi asije akawa kama mwendazake tuanze kubambikiwa makesi na kufurushwa hata kwenye mikutano ya ndani.
Chadema chama langu waelewe tu upinzani upo ndani ya damu. Kumbuka Magufuli alipiga ban mikutano na kufunga wanasiasa na kununua wabunge na madiwani ila ilipofika wakati wa uchaguzi bado alisumbuka sana kuona nyomi la Chadema mwisho akapora uchaguzi kwa nguvu(nilisimamia uchaguzi so niliona ujinga uliofanyika) niwatakie siku njema na niwaase mfanye kazi kwa bidii na kama wewe ni mwanafunzi basi soma kwa bidiii.na msisahau kumuabudu mwenyezi Mungu.
Mwaka 2010 chadema walisema uchaguzi haukuwa huru na wa haki, lakini kwa vile Mbowe na genge lake walishinda katika uchaguzi ule na kuwa na uhakika wa kuingiza ruzuku ndan ya chama kwa kila kichwa kimoja, basi waliingia bungeni na wakawa wanashiriki vikao vya bunge. Mwaka 2015 pia chadema wakaja na kilio kile kile cha kususia matokea ya uchaguzi kwa madai kwamba uchaguzi ule haukuwa huru na wa haki, lakini kwa vile Mbowe na genge lake walishinda ubunge tena katika majimbo yao na kupata uhakika wa ruzuku kupitia vichwa vyao basi walikubali kuingia bungeni na kushiriki vikao vya bunge kama kawa. Mwaka 2020 baada ya mwenyekiti na genge lake kuangukia pua ndo wanakuja na porojo ya kususia bunge kwa madai yale yale ambayo wao yaliwaingiza bungeni kwa zaidi ya miaka 10. Mbowe na genge lake wanafikiria kuwa kila mtanzania ni poyoyo kam ilivyo misukule yake. Mwambie akumbuke haya maneno ya kingereza "You can fool some people sometimes, but you can't fool all the people all the time" - Bob Marley. Mwambieni atafute vyanzo vingine vya kupata pesa za kuwalipa kina Mmawia, hizi propaganda zake za kutaka kupiga hela kupitia mchakato wa katiba wenye akili tushaugundua na hautamsaidia.Hawana ruzuku ama wamegomea ruzuku haramu?