Katiba mpya ni lazima na siyo ombi

Katiba mpya ni lazima na siyo ombi

Mesaka

Member
Joined
Nov 5, 2010
Posts
31
Reaction score
2
Ndugu watazania na watanganyika suala la katiba mpya ni la lazima na wala sio ombi, kwani tayari Zanzibar wameshafanya mabadiliko. na hayo yameifanya kuikiuka katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo inasema Tanzania ni nchi moja yenye pande mbili, hivyo kuifanya zanzibar ni nchi ni kukiuka katiba ya Tanzinia, Hivyo mabadiliko ni lazima yafanyike kwa kuanzia na hilo pamoja na mengine mengi. Mara nyingi najiuliza ilikofia Tanganyika, kwani mbona siku ya uhuru wake tunasherehekea kwa picha ya Uhuru wa Tanzania wakati hakuna siku Tanzania ilipopata uhuru wake! Bendera inapandishwa ya Tanzania, Mgeni rasmi ni rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania! Ni lini nchi Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilipata uhuru wake na kutoka kwa nani?
 
Katiba Mbovu na viongozi wakle wabovu.

Hivi kweli kuna unaona kuna Rais wa Jamhuri ya Muungano af Kuna Rais wa Zanzibar

Swali la kizushi: wazanzibar wakiwa na tatizo juu ya Tanganyika nani wampelekee ili awasuluhishe iwapo Rais wa Jamhuri ni huyo huyo wa Tanganyika??

Kesi ya Mbweha na Digidigi unapeleka kwa Fisi.

Haya ndiyo madudu ya Katiba.

Katiba kubadilisha ni lazima si Ombo
 
Nadhan tuna mfano wa katiba na siyo katiba. Ukisoma katiba unaweza ukajiuliza hivi tanzania ktna watu kwel. Katiba inasema ni nchi ya kijamaa,wakati nchi inahalalisha ubinafsi,upumbavu huu! Tume inateuliwa na raisi aliye madarakan ambayo pia ni mgombea,ebu fikiria mwenyekiti wa tume atatenda kinyume cha matakwa ya bosi wake,haiwezekani!
 
Nadhan tuna mfano wa katiba na siyo katiba. Ukisoma katiba unaweza ukajiuliza hivi tanzania ktna watu kwel. Katiba inasema ni nchi ya kijamaa,wakati nchi inahalalisha ubinafsi,upumbavu huu! Tume inateuliwa na raisi aliye madarakan ambayo pia ni mgombea,ebu fikiria mwenyekiti wa tume atatenda kinyume cha matakwa ya bosi wake,haiwezekani!

Hapo nilipokupa Highlight nimekuunga mkono Mtweve.

Nimefurahi mmeking'oa kisiki cha Kimbulu
 
anaebisha afe!!! na wa kwanza atakua huyu mama Go........Kombani
 
katiba mpya ni lazima-na ili muungano uwepo inabidi tanganyika iwepo,tena iwe active sana,ifnaye mambo yake kwa utaratibu wake-pale kwenye mambo ya muungano ndo tuchangie viongozi kutoka tanganyika na zanzinbar-ila huku kwenye serikali ya tanganyika iuachwe watanganyika wenyewe-ikishindikana hii basi bora muungano ufe
 
Back
Top Bottom