Katiba mpya: Tatizo si idadi ya serikali

Katiba mpya: Tatizo si idadi ya serikali

Baija Bolobi

JF-Expert Member
Joined
Feb 25, 2009
Posts
1,093
Reaction score
1,733
Wanabodi

Baada ya kusikiliza kwa makini maoni ya wanasiasa wa vyama vyote na pande zote mbili za Muungano, nashawishika kuamini kuwa kinachogomba si idadi ya serikali katika Muungano huu. Toka mapema katika hadidu za rejea kwa tume ya Warioba, ilipaswa wananchi waulizwe kama wanautaka Muungano ama hawautaki. Maoni ya wengi kama yangesema wanautaka, ndipo lingekuja swali la Muungano wa namna gani: serikali moja, mbili, tatu, au tano? Na kama wangejibu hawautaki, basi hapo tungeitaka tume ituandalie road map ya kuachana kwa amani. Kipindi cha miaka kama miwli kingetosha kugawana mbao, kuamua uraia mtu anaoutaka, na hapo katiba ya Tanganyika ingeandaliwa.

Sasa tuko kwenye vurugu tupu kwa sababu ya kuogopana kuulizana maswali magumu. Na ukiangalia kwa makini matokeo ya maoni ya wananchi yaliyokubaliwa na tume ya Warioba, utagundua logic ya ninachokisema kwamba;
-Wazanzibari wanaotaka Muungano wa mkataba, hawataki Muungano ila wanajificha ndani ya neno mkataba.
-Watanganyika wanaotaka serikali tatu, hawataki Muungano ila wanazunguka na kujificha ndani ya serikali tatu.
-Watanzania (pande zote mbili) wanaotaka serikali mbili, hawataki Muungano na wanajua haziwezekani kwa sasa ila
wanajificha ndani ya dola kulazimisha serikali mbili ili Muungano uvunjike.

Mwisho wa siku, tunahitaji kiongozi jasiri anayeshimu matakwa ya wananchi akubali wananchi waulizwe kama wanautaka Muungano au hawautaki. Hili ndilo swali la msingi, mengine ni kupotezeana muda
.
 
Wanabodi

Baada ya kusikiliza kwa makini maoni ya wanasiasa wa vyama vyote na pande zote mbili za Muungano, nashawishika kuamini kuwa kinachogomba si idadi ya serikali katika Muungano huu. Toka mapema katika hadidu za rejea kwa tume ya Warioba, ilipaswa wananchi waulizwe kama wanautaka Muungano ama hawautaki. Maoni ya wengi kama yangesema wanautaka, ndipo lingekuja swali la Muungano wa namna gani: serikali moja, mbili, tatu, au tano? Na kama wangejibu hawautaki, basi hapo tungeitaka tume ituandalie road map ya kuachana kwa amani. Kipindi cha miaka kama miwli kingetosha kugawana mbao, kuamua uraia mtu anaoutaka, na hapo katiba ya Tanganyika ingeandaliwa.

Sasa tuko kwenye vurugu tupu kwa sababu ya kuogopana kuulizana maswali magumu. Na ukiangalia kwa makini matokeo ya maoni ya wananchi yaliyokubaliwa na tume ya Warioba, utagundua logic ya ninachokisema kwamba;
-Wazanzibari wanaotaka Muungano wa mkataba, hawataki Muungano ila wanajificha ndani ya neno mkataba.
-Watanganyika wanaotaka serikali tatu, hawataki Muungano ila wanazunguka na kujificha ndani ya serikali tatu.
-Watanzania (pande zote mbili) wanaotaka serikali mbili, hawataki Muungano na wanajua haziwezekani kwa sasa ila
wanajificha ndani ya dola kulazimisha serikali mbili ili Muungano uvunjike.

Mwisho wa siku, tunahitaji kiongozi jasiri anayeshimu matakwa ya wananchi akubali wananchi waulizwe kama wanautaka Muungano au hawautaki. Hili ndilo swali la msingi, mengine ni kupotezeana muda
.

Naungana na wewe kwa uchambuzi wako, ila nadiriki kusema kuwa wanaotaka serikali tatu wanautaka Muungano kwa vile muda wote tulioungana tulikuwa na serikali mbili. Hawa wanaojifanya kutaka serikali tatu ni wazi mkuu hawautaki Muungano na sijui kwa nini wanajifanya wajasiri wa kuongea, lakini ujasiri wao unashindwa kuwafikisha kutamka wazi kuwa hawautaki muungano
 
Mkuu bado unausingizi kanawe uso kwanza umeandika vituko,
wenye akili fupi ndiyo hawajui faida za muungano lakini wenye akili pana wanajua umhimu wa muungano.
 
Kweli kunawatu wanahitaji vipimo vikubwa kama mleta mada huwezi kujua akili yake inawaza nini lakini ni madhara ya viroba na njaa.
 
Kweli kunawatu wanahitaji vipimo vikubwa kama mleta mada huwezi kujua akili yake inawaza nini lakini ni madhara ya viroba na njaa.
=======

Duh! Aliyelewa mkojo anamkosoa aliyelewa viroba! JF ina viroja.

 
Kwani muungano ni nini? Historia inatukumbusha tumekuwa na mashirikiano kati ya tanganyika na Z'bar tangu zama za mitume. Ndio maana kuna wanyakyusa, wangoni, Wamakonde nk kule Z'bar. N huku bara kuna waarabu, Wpemba, Watumbatu nk. Huu ulikuwa muungano wa dhati bila kujali serikali ngapi wala rasilimali zipi ziko wapi. Watu walifanya biashara, wtu wlioana, walitembeleana, walicheza pamoja nk. Shida ya ya sasa ni unafiki watu hawasemi ukweli kuhusu muungano, watu wana uchu wa madaraka, watu wana uchu wa kupora rasilimali za huku na kule ndo maana wanang'ng'ana na miungana yenye kulenga kuimarisha madaraka kwa manufaa binafsi. Napendekeza aina ya muungano uliokuwepo kabla kuingia wakoloni.
 
Back
Top Bottom