KATIBA MPYA: Wakristo, masheikh wabishania dini zao,Mahakama ya Kadhi, OIC, Vatican zaibua mjadala

hata hilo unalotaka halina tabu,ni kuweka wazi tu, ni mambo gani mnayotaka yashughulikiwe ndani ya dini husika,kwa mfano waislamu wao mambo yao ni matatu, mambo ya ndoa,miradhi,na kutoa maamuzi kama kuna tofauti kuhusu tafsiri za kuruani, sasa hapo matatizo yako wapi?
 
osokoni,kweli wewe ni usokoni,suala la kadhi kinachotakiwa ni serikali kutambua kwamba kuna Mahakama ya kadhi sio kuuda,kumbuka hata wewe unapooa mke unapata cheti na serikali inajua kwamba umeoa lakini aikusaidii kumlisha mke wako au kukuolea

Acha upumbavu wewe, waislamu wamekuwa wakidai serikali igharamie uanzishwaji wake ikiwa ni pamoja na kulipa wanasheria na mawakili na wafanyakazi wote wa mahakama! Kama ulisikiliza hotuba ya JK kwenye baraza la Idd(2011) aliweka wazi anashangaa kwa nini waislamu hawaanzishi hiyo mahakama ila akatahadharisha serikali haiwezi kujiingiza maana haina dini! Swala la kutambulika kuna chombo maalumu kinachoandikisha na kutambua taasisi za kidini lakini hili la kutaka liwekwe kwenye katiba ni big NO
 

Mgogoro sio kwamba serikali haitaki mahakama ya kadhi ianzishwe. Jamaa wanataka serikali igharamie huduma za uendeshaji wa hiyo mahakama, yaani pia wahudumu wake wapate pay-check kutoka serikalini.
Hawajui kuwa hata Katoliki wana mahakama zao za ndani ambazo wanatatua matatizo ya wanandoa na familia lakini husikii jopo la mapadre limeomba malipo serikalini au kuingizwa kwenye katiba.
 
Akiwasilisha maoni hayo, Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, Mohamed Dhilan alisema miaka 16 ni umri ambao unafaa kwa mwanamke kuolewa na kupiga kura kwa sababu viungo vyake vitakuwa vimekomaa.

Hawa nao wanawaza kubandua watoto wadogo tu.
 
OIC ni shirika linalotoa misaada ya kuendeleza dini ya kiislam,sasa tatizo likowapi,kama litakuwa linatoa misaada kwa waislam wa Tanzania kuendeleza na kukuza uislam?, sasa hawa wanaopinga awataki uislam uendelezwe?

kwani tanzania hakuna uisilamu? si watoe hiyo misaada, nani kawakataza? wamewahi kutoa msaada wowote wakagomewa?
 
kwani tanzania hakuna uisilamu? si watoe hiyo misaada, nani kawakataza? wamewahi kutoa msaada wowote wakagomewa?
nawasiwasi na elimu yako, maana wanaposema kujiunga na OIC inaitaji upate elimu,maana unachosema ni tofauti na unachofikiria.
 
kwa kuwa mimi ni muungwana nakubali matusi yako,na unavyotaka na iwe
 
kwa kuwa mimi ni muungwana nakubali matusi yako,na unavyotaka na iwe
kumbe mkuki kwa nguruwe? Angalia comment yako ya kwanza wewe ulisema mimi sio Osokoni ni Usokoni huo ni uungwana? better you keep quite stiff naked fool!
 
 
CCM ndio waliingiza swala hili la mahakama ya kadhi kwenye ilani yao ya mwaka 2005,ili kuwarubuni waislamu.Na wawe wa kwanza kuliondoa.La sivyo watakuwa chanzo cha udini Tanzania.
Naona pia kila siku sasa itakuja kuwa ya mapumziko sasa,kazi tunayo kupata katiba mpya!!!
 
Tuwe na mahakama moja itakayo tuhukumu kwa haki watanzania wote,tusingize mahakama za kidini.Kama mahakama zilizopo zina mapungufu tutoe maoni tuondoe hayo mapungufu,kama sivyo kuna siri nyuma yake.Natamani katiba mpya iwe na usawa isiwapendelee WAKRISTO wala WAISLAM.
 
:shut-mouth:Kam serikali ikikubali mahakama ya kadhi na tz kujiunga na OIC basi wakubali na kuanzisha mahakama za binafsi (private courts) kwa manufaa ya watu wasio na imani na serikali yao na wachache wasioamini katika mungu! Jamani ya ngoswe si aachiwe ngoswe? mahakama ya kadhi inamfaidi nini mkristo? tuache porojo! kama waislam wanataka mahakama hiyo waanzishe wenyewe na kuiendesha wenyewe kwa maslahi yao wenyewe. tusipeleke nchi kusikotamanika jamani, bado tunajipenda. Narudia; ikiwa serikali watakubali mahakama ya kadhi na mengineyo yenye udini basi tukubali tukatae tutakuwa tumeanzisha na mahakama bubu a.k.a mahakama binafsi huku mtaani ambako taaluma yake itakuwa bangi na unga kutolea hukumu kama maujai, ubakaji, uporaji maana navyo vina masilahi ya aina yake kwa watu wachache!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…