KATIBA MPYA: Wakristo, masheikh wabishania dini zao,Mahakama ya Kadhi, OIC, Vatican zaibua mjadala

KATIBA MPYA: Wakristo, masheikh wabishania dini zao,Mahakama ya Kadhi, OIC, Vatican zaibua mjadala

nngu007

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2010
Posts
15,860
Reaction score
5,801
JUMAMOSI, JANUARI 12, 2013 09:04 GABRIEL MUSHI NA ARODIA PETER, DAR ES SALAAM


*Mahakama ya Kadhi, OIC, Vatican zaibua mjadala
*Washia wao wataka umri wa kupiga kura miaka 16

TUME ya Mabadiliko ya Katiba jana iliendelea na mikutano yake na wawakilishi wa makundi maalum katika jamii wakati ilipoendelea kukusanya maoni kutoka kwa viongozi wa kidini.


Mara baada ya mikutano hiyo iliyoendeshwa kwa nyakati na maeneo tofauti, viongozi wa kidini walikutana na kuzungumza na waandishi wa habari kueleza yale yaliyojiri katika vikao vyao hivyo.


Katika mazungumzo yao, kulionekana kuwapo kwa mvutano na ukinzani mkali wa hoja kati ya viongozi wa Kikristo na Kiislamu kuliko ilivyokuwa kwa watu wa imani tofauti.


Kubwa lililojitokeza na kuonekana kugusa hisia za viongozi wakuu wa dini hizo mbili halikuwa jingine zaidi ya kuendelea kuvutana kuhusu kuwapo ama kutokuwapo kwa Mahakama ya Kadhi hoja ambayo imeendelea kulitafuna taifa hili tangu mwaka 2005.


Mbali ya viongozi wa Kikristo kuendelea kusisitiza msimamo wao wa kupinga juhudi zozote za serikali kujihusisha katika uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi, kinyume ilivyosisitizwa na wenzao wa Kiislamu, hoja nyingine iliyoibua mjadala miongoni mwa wawakilishi wa dini hizo mbili ni ile ya Tanzania kuwa au kutokuwa mwanachama wa Nchi za Jumuiya ya Kiislamu Duniani (OIC).


Wakiwasilisha maoni yao, Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania (TEC), walisema Mahakama ya Kadhi haina maslahi kwa Watanzania wote bali ni kwa kikundi kinachotaka kuhodhi haki za watu wengine.


Makamu Rais wa TEC, Askofu Severine Niwemugizi alisema itakuwa kosa kama Katiba mpya itaruhusu kuwapo kwa mahakama hiyo, kwani itachochea uhasama.


"Mahakama ya Kadhi, kama chombo cha Kiislamu kina misingi, mamlaka na maamuzi yake, tutanataka isiwe ya kulazimishwa kuingizwa katika mifumo ya kiserikali


"Si vizuri, Serikali kuwa na dini. Tukiruhusu Mahakama ya Kadhi maana yake ni kwamba Serikali imejiingiza kwenye dini… dini imekuwepo kabla ya Serikali hivyo ziwe na taratibu zake na kamwe zisirasimishwe," alisema Niwemugizi.


Kuhusu OIC, Askofu Niwemugizi alisema kumekuwa na usiri mkubwa mno na itakuwa hatari kama itaruhusiwa kwa sababu ina lengo la kuua ukristo.


"Kuhusu OIC, bahati haya kwa kipindi kirefu sasa, mambo hayawekwi wazi, moja ya sheria za OIC ni kueneza uislamu na kufuta ukristo, kwa nchi wanachama mambo ambayo hayana maslahi kwa makundi mengine,


"Katika suala la Ubalozi wa Vatican nchini, si la Tanzania tu ni la kimataifa hivyo ni suala la mahusiano tu kwa kuwa kuna baadhi ya nchi za Kiislamu zenye uhusiano wa moja kwa moja na kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani Baba Mtakatifu,


"Haya yalikuwa ni makubaliano ya mwaka 1929,kati ya Vatican na Italia ambako ndipo yalipo makao makuu ya baba Mtakatifu.


"Kiongozi wa Vatican, ni kiongozi wa Kanisa Katoliki dunia nzima ana mchango mkubwa wa kijamii, hivyo si vibaya akawa na mwakilishi kila nchi.


"Kuufuta Ubalozi wa Vatican nchini ni sawa na kusema ufute ubalozi wa Iran, kwani nayo ni nchi ya Kiislamu na tunaendelea kuwa na uhusiano mazuri kama taifa pia kama ilivyo kwa Vatican," Askofu Niwemugizi.


CCT

Naye Mwenyekiti wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), Askofu Dk. Peter Kitula alisema si haki kuingi mambo ya dini kwenye Katiba ambayo inagusa wananchi wote.


"Na si Mahakama ya Kadhi tu, hata iwe ya mahakama ya kanisa hatuhitaji iingizwe kwenye mfumo wa kiserikali, tunataka Serikali iendelee kutekeleza mambo yake nje ya dini.


"Kama ilivyo katika ibara ya tatu, kipengele kidogo cha nne katika Katiba ya sasa, tunadhani hili libaki kwa kuwa litaendeleza umoja wa Watanzania,


Kuhusu suala la Muungano, CCT inapendekeza Serikali moja au ikishindikana ziwe Serikali tatu.


"Yaani pasiwepo na Serikali ya Zanzibar iliyo na bendera na wimbo wake, kama hii haiwezekani, namna nyingine ni kuwa na serikali tatu ambazo moja ya Zanzibar, Tanganyika na Muungano.


"Serikali hizi, zitaongozwa na mawaziri wakuu na zitakuwa na mambo yake kama nchi zinazojitegemea,Serikali ya Muungano itakuwa na wizara maalum ambazo zitashughulikia masuala ya muungano," alisema.


Katika hatua nyingine, makundi maalum yamependekeza kuwepo kwa Tume huru ya Uchaguzi, ambayo haitateuliwa na Rais kama ilivyo sasa, badala yake ipendekezwe na makundi mbalimbali ya kijamii.


MASHEIKH

Kwa upande wake, Amiri wa Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Mussa Kundecha alisema wamependekeza suala la Mahakama ya Kadhi lazima litambuliwe kama chombo kitakachosimamia sheria za jamii ya Waislamu wote.


Alisema hicho ndiyo chombo pekee, ambacho kinaweza kuwaunganisha Waislamu pindi wanapotaka kupata suluhu ya matatizo yao.


"Tunataka Mahakama ya Kadhi, iingie kwenye Katiba mpya ili mambo yetu tuweze kuyaendesha wenyewe, imani na uhuru wetu viwezi wazi,


"Katika hili, tunataka pia Katiba mpya itenge siku ya Ijumaa iwe maalum kwa asili ya kumpuzika kuazia saa 6:00 mchana ili kutoa fursa kwa wafanyakazi na wanafunzi wa Kiislamu kwenda kwenye ibada kama tunavyolekezwa na vitabu vya mwenyezi Mungu.


"Hii ni huduma ya kijamii, kwa sababu miongoni mwa matatizo yanayotupata ni kugombea mali... lakini mgawanyo huu umeelezwa vizuri katika taratibu za Kiislamu, unaepusha ugomvi au vita ya kugombea mali, baada ya mmiliki kuondoka.


"Hili si suala la mchezo kwa sababu isiwe kama mzaha huu, uliofanyika kipindi kilichopita... tunataka chombo kinachokubalika kisheria ambacho kitakuwa na mamlaka.


"Ni sawa na mgonjwa wa saratani anapopelekwa Muhimbili anahamishiwa hospitali ya Ocean Road… Waislamu hawataki sheikh mmoja ana midevu mingi, wanataka wanasheria wenye kujua sheria ya Kiislamu juu ya masuala ya mirathi ndoa na talaka, watengenezewe kama ilivyotengenezwa hosptali ya kutibu saratani.


WASABATO NA MISAADA

Nalo Kanisa la Waadventista wa Sabato, wametaka Katiba mpya itambue vikundi vidogo vidogo vya kidini ili visimezwe na makanisa makubwa.


"Tunataka fursa sawa katika uhuru wa kuabudu bila kukandamizwa, tunaamini tunafanya kazi siku sita, kama jumamosi tunakwenda kuabudu basi tufanye kazi jumapili na watoto wetu wasilazimishwe kufanya mitihani siku za jumamosi ili kuwatendea haki watu wote. "Suala la udini,lisipewe nafasi katika Katiba mpya, kwa maana kuwa masuala ya dini yasiingizwe katika mambo ya kiserikali ... mwenye uwezo wa kuongoza Serikali aangaliwe uwezo wake wala si dini au kabila lake," alisema Askofu Mkuu wa Jimbo la Mashariki mwa Tanzania, Mchungaji Mark Malekana.


WAASIA

Nao Muungano wa Jumuiya ya Khoja Shia Ithina-Asheri Jamaat ya Afrika, umeitaka Tume ya Mabadiliko ya Katiba kuhakikisha inaingiza kipengele kitakachorushu msichana mwenye umri wa miaka 16 kuolewa.

Akiwasilisha maoni hayo, Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, Mohamed Dhilan alisema miaka 16 ni umri ambao unafaa kwa mwanamke kuolewa na kupiga kura kwa sababu viungo vyake vitakuwa vimekomaa.

"Tunashauri katiba mpya ipige marufuku kugombea zaidi ya awamu mbili kwa sababu viongozi wengi wakikaa huko bungeni wanazoea hadi wanaota mizizi.

 

Napenda MAONI ya WATU wa DINI = DEMOKRASIA Safi
 
nimependa mapendekezo ya dini zote... ila uangalifu mkubwa unahitajika... mambo ya vatican na mahakama ya kadhi..
 
JUMAMOSI, JANUARI 12, 2013 09:04 GABRIEL MUSHI NA ARODIA PETER, DAR ES SALAAM


*Mahakama ya Kadhi, OIC, Vatican zaibua mjadala
*Washia wao wataka umri wa kupiga kura miaka 16

TUME ya Mabadiliko ya Katiba jana iliendelea na mikutano yake na wawakilishi wa makundi maalum katika jamii wakati ilipoendelea kukusanya maoni kutoka kwa viongozi wa kidini.


Mara baada ya mikutano hiyo iliyoendeshwa kwa nyakati na maeneo tofauti, viongozi wa kidini walikutana na kuzungumza na waandishi wa habari kueleza yale yaliyojiri katika vikao vyao hivyo.


Katika mazungumzo yao, kulionekana kuwapo kwa mvutano na ukinzani mkali wa hoja kati ya viongozi wa Kikristo na Kiislamu kuliko ilivyokuwa kwa watu wa imani tofauti.


Kubwa lililojitokeza na kuonekana kugusa hisia za viongozi wakuu wa dini hizo mbili halikuwa jingine zaidi ya kuendelea kuvutana kuhusu kuwapo ama kutokuwapo kwa Mahakama ya Kadhi hoja ambayo imeendelea kulitafuna taifa hili tangu mwaka 2005.


Mbali ya viongozi wa Kikristo kuendelea kusisitiza msimamo wao wa kupinga juhudi zozote za serikali kujihusisha katika uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi, kinyume ilivyosisitizwa na wenzao wa Kiislamu, hoja nyingine iliyoibua mjadala miongoni mwa wawakilishi wa dini hizo mbili ni ile ya Tanzania kuwa au kutokuwa mwanachama wa Nchi za Jumuiya ya Kiislamu Duniani (OIC).


Wakiwasilisha maoni yao, Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania (TEC), walisema Mahakama ya Kadhi haina maslahi kwa Watanzania wote bali ni kwa kikundi kinachotaka kuhodhi haki za watu wengine.


Makamu Rais wa TEC, Askofu Severine Niwemugizi alisema itakuwa kosa kama Katiba mpya itaruhusu kuwapo kwa mahakama hiyo, kwani itachochea uhasama.


"Mahakama ya Kadhi, kama chombo cha Kiislamu kina misingi, mamlaka na maamuzi yake, tutanataka isiwe ya kulazimishwa kuingizwa katika mifumo ya kiserikali


"Si vizuri, Serikali kuwa na dini. Tukiruhusu Mahakama ya Kadhi maana yake ni kwamba Serikali imejiingiza kwenye dini… dini imekuwepo kabla ya Serikali hivyo ziwe na taratibu zake na kamwe zisirasimishwe," alisema Niwemugizi.


Kuhusu OIC, Askofu Niwemugizi alisema kumekuwa na usiri mkubwa mno na itakuwa hatari kama itaruhusiwa kwa sababu ina lengo la kuua ukristo.


"Kuhusu OIC, bahati haya kwa kipindi kirefu sasa, mambo hayawekwi wazi, moja ya sheria za OIC ni kueneza uislamu na kufuta ukristo, kwa nchi wanachama mambo ambayo hayana maslahi kwa makundi mengine,


"Katika suala la Ubalozi wa Vatican nchini, si la Tanzania tu ni la kimataifa hivyo ni suala la mahusiano tu kwa kuwa kuna baadhi ya nchi za Kiislamu zenye uhusiano wa moja kwa moja na kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani Baba Mtakatifu,


"Haya yalikuwa ni makubaliano ya mwaka 1929,kati ya Vatican na Italia ambako ndipo yalipo makao makuu ya baba Mtakatifu.


"Kiongozi wa Vatican, ni kiongozi wa Kanisa Katoliki dunia nzima ana mchango mkubwa wa kijamii, hivyo si vibaya akawa na mwakilishi kila nchi.


"Kuufuta Ubalozi wa Vatican nchini ni sawa na kusema ufute ubalozi wa Iran, kwani nayo ni nchi ya Kiislamu na tunaendelea kuwa na uhusiano mazuri kama taifa pia kama ilivyo kwa Vatican," Askofu Niwemugizi.


CCT

Naye Mwenyekiti wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), Askofu Dk. Peter Kitula alisema si haki kuingi mambo ya dini kwenye Katiba ambayo inagusa wananchi wote.


"Na si Mahakama ya Kadhi tu, hata iwe ya mahakama ya kanisa hatuhitaji iingizwe kwenye mfumo wa kiserikali, tunataka Serikali iendelee kutekeleza mambo yake nje ya dini.


"Kama ilivyo katika ibara ya tatu, kipengele kidogo cha nne katika Katiba ya sasa, tunadhani hili libaki kwa kuwa litaendeleza umoja wa Watanzania,


Kuhusu suala la Muungano, CCT inapendekeza Serikali moja au ikishindikana ziwe Serikali tatu.


"Yaani pasiwepo na Serikali ya Zanzibar iliyo na bendera na wimbo wake, kama hii haiwezekani, namna nyingine ni kuwa na serikali tatu ambazo moja ya Zanzibar, Tanganyika na Muungano.


"Serikali hizi, zitaongozwa na mawaziri wakuu na zitakuwa na mambo yake kama nchi zinazojitegemea,Serikali ya Muungano itakuwa na wizara maalum ambazo zitashughulikia masuala ya muungano," alisema.


Katika hatua nyingine, makundi maalum yamependekeza kuwepo kwa Tume huru ya Uchaguzi, ambayo haitateuliwa na Rais kama ilivyo sasa, badala yake ipendekezwe na makundi mbalimbali ya kijamii.


MASHEIKH

Kwa upande wake, Amiri wa Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Mussa Kundecha alisema wamependekeza suala la Mahakama ya Kadhi lazima litambuliwe kama chombo kitakachosimamia sheria za jamii ya Waislamu wote.


Alisema hicho ndiyo chombo pekee, ambacho kinaweza kuwaunganisha Waislamu pindi wanapotaka kupata suluhu ya matatizo yao.


"Tunataka Mahakama ya Kadhi, iingie kwenye Katiba mpya ili mambo yetu tuweze kuyaendesha wenyewe, imani na uhuru wetu viwezi wazi,


"Katika hili, tunataka pia Katiba mpya itenge siku ya Ijumaa iwe maalum kwa asili ya kumpuzika kuazia saa 6:00 mchana ili kutoa fursa kwa wafanyakazi na wanafunzi wa Kiislamu kwenda kwenye ibada kama tunavyolekezwa na vitabu vya mwenyezi Mungu.


"Hii ni huduma ya kijamii, kwa sababu miongoni mwa matatizo yanayotupata ni kugombea mali... lakini mgawanyo huu umeelezwa vizuri katika taratibu za Kiislamu, unaepusha ugomvi au vita ya kugombea mali, baada ya mmiliki kuondoka.


"Hili si suala la mchezo kwa sababu isiwe kama mzaha huu, uliofanyika kipindi kilichopita... tunataka chombo kinachokubalika kisheria ambacho kitakuwa na mamlaka.


"Ni sawa na mgonjwa wa saratani anapopelekwa Muhimbili anahamishiwa hospitali ya Ocean Road… Waislamu hawataki sheikh mmoja ana midevu mingi, wanataka wanasheria wenye kujua sheria ya Kiislamu juu ya masuala ya mirathi ndoa na talaka, watengenezewe kama ilivyotengenezwa hosptali ya kutibu saratani.


WASABATO NA MISAADA

Nalo Kanisa la Waadventista wa Sabato, wametaka Katiba mpya itambue vikundi vidogo vidogo vya kidini ili visimezwe na makanisa makubwa.


"Tunataka fursa sawa katika uhuru wa kuabudu bila kukandamizwa, tunaamini tunafanya kazi siku sita, kama jumamosi tunakwenda kuabudu basi tufanye kazi jumapili na watoto wetu wasilazimishwe kufanya mitihani siku za jumamosi ili kuwatendea haki watu wote. "Suala la udini,lisipewe nafasi katika Katiba mpya, kwa maana kuwa masuala ya dini yasiingizwe katika mambo ya kiserikali ... mwenye uwezo wa kuongoza Serikali aangaliwe uwezo wake wala si dini au kabila lake," alisema Askofu Mkuu wa Jimbo la Mashariki mwa Tanzania, Mchungaji Mark Malekana.


WAASIA

Nao Muungano wa Jumuiya ya Khoja Shia Ithina-Asheri Jamaat ya Afrika, umeitaka Tume ya Mabadiliko ya Katiba kuhakikisha inaingiza kipengele kitakachorushu msichana mwenye umri wa miaka 16 kuolewa.

Akiwasilisha maoni hayo, Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, Mohamed Dhilan alisema miaka 16 ni umri ambao unafaa kwa mwanamke kuolewa na kupiga kura kwa sababu viungo vyake vitakuwa vimekomaa.

"Tunashauri katiba mpya ipige marufuku kugombea zaidi ya awamu mbili kwa sababu viongozi wengi wakikaa huko bungeni wanazoea hadi wanaota mizizi.

kwa serikali hii ya ccm waislam wasahau kupata mahakama ya kadhi na kujiunga na OIC,kwa kuwa ccm awataki watu wapate mambo mema na kwakuwa hilo ni jambo jema ccm hawatakumbali,kwa waislam dawa ni kuing`oa ccm madarakani vinginevyo wasubiri kutumiwa kuiweka ccm madarakani
 
Vatican ni taifa na kiongozi wake ni papa, so kuwa na ubalozi hapa nchini ni sawa na na Jamhuri ya kiislamu ya Iran, Jamhuri ya kiislamu ya Saudia, na jamhuri nyingine zozote zilivo na ubalozi hapa nchi na pia ubalozi huu unahudiwa na Vatican kama mataifa mengine yanavohudumia balozi zao!
Mhakama ya kadhi waanzishe waislamu wenyewe na waiendeshe kwa gharama zao, serikali ikiridhia kuanzisha na kuhudumia mahakama hiyo basi wawe tayari pia kukubali na kusaidia kuanzisha mahakama ya kikatoliki, kilutheran, kiangalikana.kisabato na hata mahakama ya wapagani pia!
 
kwa serikali hii ya ccm waislam wasahau kupata mahakama ya kadhi na kujiunga na OIC,kwa kuwa ccm awataki watu wapate mambo mema na kwakuwa hilo ni jambo jema ccm hawatakumbali,kwa waislam dawa ni kuing`oa ccm madarakani vinginevyo wasubiri kutumiwa kuiweka ccm madarakani

Tutajiunga na OIC kwani sisi ni jamhuri ya kiislamu?? (OIC= Organization of Islamic Countries)
 
Habari imechakachuliwa kidogo,

Katika hgazeti la habari leo, Kuna kiongozi msaidizi wa wasabato ameelezea kufutwa kwa upelekaji wa pesa katika dini fulani tu kama ilivyo "MOU" sasa. na akapendekeza kama itabidi iwe basi kila dini lipate portion na isiwe serikali na dini fulani.
Nadhani hii haikupaswa kusahauliwa na mwandishi
 
Suala udini katika katiba kwangu binafsi na kwa kila mwenye akili na anaependa fairness sio sahihi.
tunafaham kua tanzania si nchi ya kidini. (sio uislam wala ukiristo wala dini nyingine yeyote)
kwa maana hii mtu yeyote anaeng'ang'ania kua dini fulani ingizwe kwne katiba ni m-dinmi, ni m-binafsi,
hana maslah kwa watu wasio wa dini yake (ambao ni watanzania)na suala la katiba ni la kitaifa sio kidini.
Mahakama ni taasisi kama taasisi nyingine, hivyo inapokua ya kidini iwekwe na dini yenyewe kwa ajili ya
kushughulikia kesi za kidini.
tanzania sio nchi ya kikiristo lakini mbona wakiristo hawajangangania nchi hii kutwaliwa kua ya kikiristo na
kuuondoa uslam?? waislam kungangania nchi kujiunga OIC sio ubinafsi?? sio kutaka kuwakandamiza kwa kutowatambua wakiristo na haki zao?? kama waislam wanataka mahakama ya kkadhi waiweke peke yao kwa hela zao ila sio ruzuku ya serikali.
Katiba ya nchii iendelee kuitambua nchi ka isiyo ya kidini.
Suala la kupumzika ijumaa: sio kua jumapli ni siku ya kupumzika kwa kua wakiristo (baadhi ya madhehebu) wanasali
ni kwa sababu ndio uaratibu wa kiserikali wa kupumzika. walichofanya wakiristo (baadhi ni kuchagua siku hyo ya jumapili
kusali kwani ndio siku watu wote wanakua na muda. kwa hyo solution sio ijumaa nayo kufanywa siku ya kupumzika bali labda wislam na madhehebu baadhi ya kikiristo wamue kusali jumapili.
 
kwa serikali hii ya ccm waislam wasahau kupata mahakama ya kadhi na kujiunga na OIC,kwa kuwa ccm awataki watu wapate mambo mema na kwakuwa hilo ni jambo jema ccm hawatakumbali,kwa waislam dawa ni kuing`oa ccm madarakani vinginevyo wasubiri kutumiwa kuiweka ccm madarakani

OIC... Kama ina NCHI na Inatuma MABALOZI wake kama VILE VATICAN sitaona sababu ya CCM kupinga OIC

Kuhusu MAHAKAMA ya KADHI Mimi sioni tatizo kama MASUALA yatakuwa ni kuhusu MASUALA ya NDOA na MIRATHI kwasababu hii ni TATIZO kweli kwa WaTanzania wa KIISLAMu wenye wake zaidi ya 3 na Watoto...

Lakini kama ITAJIHUSISHA na MASUALA ya KITAIFA kama WIZI; Unyang'anyi na kuweka SHERIA kali kama ile ya SUDAN ya kukata kiwiko MWIZI - hapo SIUNGI MKONO...
 

OIC... Kama ina NCHI na Inatuma MABALOZI wake kama VILE VATICAN sitaona sababu ya CCM kupinga OIC

Kuhusu MAHAKAMA ya KADHI Mimi sioni tatizo kama MASUALA yatakuwa ni kuhusu MASUALA ya NDOA na MIRATHI kwasababu hii ni TATIZO kweli kwa WaTanzania wa KIISLAMu wenye wake zaidi ya 3 na Watoto...

Lakini kama ITAJIHUSISHA na MASUALA ya KITAIFA kama WIZI; Unyang'anyi na kuweka SHERIA kali kama ile ya SUDAN ya kukata kiwiko MWIZI - hapo SIUNGI MKONO...
kama umekubali kwa kadhi sawa,na uliyosema kwa upande wa kadhi ndivyo ilivyo.labda nikuelimishekuhusu OIC hili ni shirika la kiislamu linalotoa misaada,kama ilivyo worldbank,sasa tatizo liko wapi kama watu watapewa misaada tena misaada nafuu
 
Ikitokea wakubali kuwa iwepo mahakama ya Kadhi humu nchini, basi kifungu hicho kifafanue bayana kuwa kila dhehebu la dini litakalotaka kuwa na mahakama yake kulingana na msahafu wa dini hiyo, linaruhusiwa na Serikali itatambua mahakama hiyo na kuihudumia. Wasipofanya hivyo, watakuwa wagawa wananchi. Niafadhali kuweka msimamo kuwa Serikali haitajihusisha na masuala ya dini yoyote wala bunge lisiburuzwe kujadili mambo ya dini moja na kutaka kuyapa hadhi ya kitaifa!
 
Vatican ni taifa na kiongozi wake ni papa, so kuwa na ubalozi hapa nchini ni sawa na na Jamhuri ya kiislamu ya Iran, Jamhuri ya kiislamu ya Saudia, na jamhuri nyingine zozote zilivo na ubalozi hapa nchi na pia ubalozi huu unahudiwa na Vatican kama mataifa mengine yanavohudumia balozi zao!
Mhakama ya kadhi waanzishe waislamu wenyewe na waiendeshe kwa gharama zao, serikali ikiridhia kuanzisha na kuhudumia mahakama hiyo basi wawe tayari pia kukubali na kusaidia kuanzisha mahakama ya kikatoliki, kilutheran, kiangalikana.kisabato na hata mahakama ya wapagani pia!
osokoni,kweli wewe ni usokoni,suala la kadhi kinachotakiwa ni serikali kutambua kwamba kuna Mahakama ya kadhi sio kuuda,kumbuka hata wewe unapooa mke unapata cheti na serikali inajua kwamba umeoa lakini aikusaidii kumlisha mke wako au kukuolea
 
kama umekubali kwa kadhi sawa,na uliyosema kwa upande wa kadhi ndivyo ilivyo.labda nikuelimishekuhusu OIC hili ni shirika la kiislamu linalotoa misaada,kama ilivyo worldbank,sasa tatizo liko wapi kama watu watapewa misaada tena misaada nafuu

Tatizo la OIC... lina SHARTI MOJA kuwa Pamoja na MISAADA inayoitoa kwenye KATIBA yake inasema hiyo MISAADA sio ya BURE; Inatakiwa pia wawe na UWEZO wa kuzidisha IDADI ya WAISLAMU kwenye HIZO SEHEMU MISAADA inapotolewa

SHERIA za OIC
To protect and defend the true image of Islam, to combat defamation of Islam and encourage dialogue among civilizations and religions;

to foster noble Islamic values concerning moderation, tolerance, respect fordiversity, preservation of Islamic symbols and common heritage and to defend the universality of Islamic religion;

to advance the acquisition and popularization of knowledge in consonance
with the lofty ideals of Islam to achieve intellectual excellence;

to support the struggle of the Palestinian people, who are presently under foreign occupation, and to empower them to attain their inalienable rights, including the right to self-determination, and to establish their sovereign state with Al-Quds Al-Sharif as its capital, while safeguarding its historic and Islamic character, and the holy places therein;

to create conducive conditions for sound upbringing of Muslim children and youth, and to inculcate in them Islamic values through education for
strengthening their cultural, social, moral and ethical ideals;

Any State, member of the United Nations, having Muslim majority and
abiding by the Charter, which submits an application for membership may
join the Organisation if approved by consensus only by the Council of Foreign Ministers on the basis of the agreed criteria adopted by the Council of Foreign Ministers.
 
Habari imechakachuliwa kidogo,

Katika hgazeti la habari leo, Kuna kiongozi msaidizi wa wasabato ameelezea kufutwa kwa upelekaji wa pesa katika dini fulani tu kama ilivyo "MOU" sasa. na akapendekeza kama itabidi iwe basi kila dini lipate portion na isiwe serikali na dini fulani.
Nadhani hii haikupaswa kusahauliwa na mwandishi

HahahaaAaaaa hilo kwa wenye agreement halitaonekana
 
kwa serikali hii ya ccm waislam wasahau kupata mahakama ya kadhi na kujiunga na OIC,kwa kuwa ccm awataki watu wapate mambo mema na kwakuwa hilo ni jambo jema ccm hawatakumbali,kwa waislam dawa ni kuing`oa ccm madarakani vinginevyo wasubiri kutumiwa kuiweka ccm madarakani

mambo gani mema ndani ya OIC?
 
labda nikuelimishekuhusu OIC hili ni shirika la kiislamu linalotoa misaada,kama ilivyo worldbank,sasa tatizo liko wapi kama watu watapewa misaada tena misaada nafuu[/QUOTE]
Ndivyo eeh... Basi watakua wamechelewa sana kuzisaidia nchi wanachama kama Somalia ambazo hata chakula wanaombeleza kwa kila mwenye rehema kwao. Ama kule 'mission is complete?' (kwani >99% ni dini moja, no more converts)
I believe more in open trade than misaada

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
mambo gani mema ndani ya OIC?
OIC ni shirika linalotoa misaada ya kuendeleza dini ya kiislam,sasa tatizo likowapi,kama litakuwa linatoa misaada kwa waislam wa Tanzania kuendeleza na kukuza uislam?, sasa hawa wanaopinga awataki uislam uendelezwe?
 
labda nikuelimishekuhusu OIC hili ni shirika la kiislamu linalotoa misaada,kama ilivyo worldbank,sasa tatizo liko wapi kama watu watapewa misaada tena misaada nafuu
Ndivyo eeh... Basi watakua wamechelewa sana kuzisaidia nchi wanachama kama Somalia ambazo hata chakula wanaombeleza kwa kila mwenye rehema kwao. Ama kule 'mission is complete?' (kwani >99% ni dini moja, no more converts)
I believe more in open trade than misaada

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums[/QUOTE]
OIC wanatoa fedha sio chakula
 
Back
Top Bottom