singidadodoma
JF-Expert Member
- Nov 11, 2013
- 4,394
- 1,536
Napenda kuwasihi ndugu zangu wazanzibar ambapo binafsi nina undugu nao wa damu kabisa kwa upande wa mama yangu mzazi kuisoma vizuri kabisa, Katiba Inayopendekezwa, kifungu kwa kifungu ili kuepuka matukio ya upotoshaji unaofanywa kwa makusudi na wapinzani ambao wanataka kuficha ukweli kuhusu ubora wa katiba hiyo.
Karibia mambo yote yaliyokuwa kikwazo na kero kwa Wazanzibari kuhusiana na Muungano yamepatiwa ufumbuzi na kuwekwa sawa baada ya kutolewa ufafanuzi wa kina katika Katiba Inayopendekezwa.
Suala la ardhi ni miongoni mwa mambo yaliyofanyiwa ufafanuzi wa kina katika Katiba Inayopendekezwa lakini ukawa na wamekuwa wakipotosha suala hilo kwa makusudi kwa kudai kuwa "Ardhi ya Zanzibar imeuzwa Bara."
Katika sura ya Tatu, Ibara ya Katiba 23 hadi 26 katika Katiba Inayopendekezwa imeweka ufafanuzi mzuri wa matumizi ya ardhi kwa upande wa Bara na kwa upande wa Zanzibar na kutaja ardhi ndiyo rasilimali kubwa ya kukuza uchumi na maendeleo ya ustawi wa wananchi.
Kwa mujibu wa Katiba Pendekezwa, matumizi ya Ardhi kwa upande wa Tanzania Bara sheria zake zitatungwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati sheria za Ardhi na matumizi yake kwa upande wa Zanzibar zitatungwa na Baraza la Wawakilishi.
Katiba Inayopendekezwa imeondoa suala la Ardhi katika orodha ya mambo ya Muungano ambayo yapo 16 na kwamba hatua hiyo itaifanya Zanzibar kutumia rasilimali zake ikiwa ni pamoja na kuchimba rasilimali ya mafuta na gesi.
Katiba Inayopendekezwa imetoa fursa kubwa kwa Wazanzibari ambao sasa watakuwa na fursa ya kikatiba kutumia ardhi iliopo Tanzania kwa shughuli zao zote ikiwemo biashara na kilimo. Aidha wananchi wa Tanzania Bara waliopo Zanzibar nao wanayo fursa na haki ya kikatiba kutumia Ardhi iliopo Zanzibar kwa shughuli zao mbali mbali ikiwemo ujenzi wa nyumba za kudumu.
Ukawa na cuf kwa pamoja wamekuwa wakivusha kuwa ardhi ya Zanzibar imeuzwa Tanzania Bara, wanapaswa kuwapuuza kwa sababu katiba hii imetoa fursa kubwa kwa Wazanzibari kutumia ardhi iliopo Bara kwa matumizi yao mbalimbali bila ya bughudha ninaondoa kero zilizopo, kjiografia ukubwa wa ardhi iliopo katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo eneo la Bara lina ukubwa wa kilomita za mraba wastani zaidi laki tisa, wakati Ardhi iliopo Zanzibar ni kilomita za mraba 2,600 tu.
Kiuhalisia ardhi ya Zanzibar hata kwa matumizi ya Wazanzibari wenyewe ndiyo maana sehemu kubwa ya wananchi wa Zanzibar waliopo Tanzania Bara wanamiliki maeneo makubwa ya ardhi Tanzania bara bila matatizo wala ubaguzi wowote.
Wapinzani na UKAWA kwa makusudi wamekuwa wakifanya upotoshaji wa makusudi kinyume na misingi ya kiungwana baada ya kuona wanashindwa kujenga hoja za msingi za kuikosoa Katiba Inayopendekezwa wamebakia kutengeneza fitina za kuwachonganisha watu wa Bara na Zanzibar.
inashangaza kuona Cuf wanapinga Katiba Inayopendekezwa wakati ina mambo ambayo wao wenyewe waliyapendekeza wakati walipokuwa katika vikao vya Baraza la Wawakilishi, walipitisha azimio la kutaka masuala ya ardhi, mafuta na gesi kuondolewa katika orodha ya mambo ya Muungano, jambo ambalo limepitishwa na Katiba Inayopendekezwa lakini bila aibu wanaipinga Katiba hiyo.
Bunge la Katiba lilikubaliana na hoja hiyo na masuala ya gesi na mafuta yamepatiwa ufumbuzi na kuondolewa kwenye Muungano sasa wapinzania wanachopinga ni nini? Kitendo cha Ukawa kuisusia Katiba Inayopendekezwa na kuwashawishi wafuasi wao kutoipigia kura kinaonesha jinsi watu hao walivyokuwa hawana imani na uchungu wa wananchi wa Zanzibar ambao wanakabiliwa na matatizo mbalimbali ikiwemo suala la ajira kwa vijana.
Kwa sababu ikiwa Katiba Inayopendekezwa itapigiwa kura ya ndio kwa wingi itatoa fursa na nafasi kwa Zanzibar kuanza kuchimba mafuta na gesi kwa ajili ya kujenga mazingira mazuri ya kiuchumi na ustawi wa jamii kwa wananchi wake. Anafahamisha kuwa juhudi zimeanza kuchukuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibair ikiwemo kuwasomesha vijana mbali mbali katika fani ya mafuta na gesi.
Karibia mambo yote yaliyokuwa kikwazo na kero kwa Wazanzibari kuhusiana na Muungano yamepatiwa ufumbuzi na kuwekwa sawa baada ya kutolewa ufafanuzi wa kina katika Katiba Inayopendekezwa.
Suala la ardhi ni miongoni mwa mambo yaliyofanyiwa ufafanuzi wa kina katika Katiba Inayopendekezwa lakini ukawa na wamekuwa wakipotosha suala hilo kwa makusudi kwa kudai kuwa "Ardhi ya Zanzibar imeuzwa Bara."
Katika sura ya Tatu, Ibara ya Katiba 23 hadi 26 katika Katiba Inayopendekezwa imeweka ufafanuzi mzuri wa matumizi ya ardhi kwa upande wa Bara na kwa upande wa Zanzibar na kutaja ardhi ndiyo rasilimali kubwa ya kukuza uchumi na maendeleo ya ustawi wa wananchi.
Kwa mujibu wa Katiba Pendekezwa, matumizi ya Ardhi kwa upande wa Tanzania Bara sheria zake zitatungwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati sheria za Ardhi na matumizi yake kwa upande wa Zanzibar zitatungwa na Baraza la Wawakilishi.
Katiba Inayopendekezwa imeondoa suala la Ardhi katika orodha ya mambo ya Muungano ambayo yapo 16 na kwamba hatua hiyo itaifanya Zanzibar kutumia rasilimali zake ikiwa ni pamoja na kuchimba rasilimali ya mafuta na gesi.
Katiba Inayopendekezwa imetoa fursa kubwa kwa Wazanzibari ambao sasa watakuwa na fursa ya kikatiba kutumia ardhi iliopo Tanzania kwa shughuli zao zote ikiwemo biashara na kilimo. Aidha wananchi wa Tanzania Bara waliopo Zanzibar nao wanayo fursa na haki ya kikatiba kutumia Ardhi iliopo Zanzibar kwa shughuli zao mbali mbali ikiwemo ujenzi wa nyumba za kudumu.
Ukawa na cuf kwa pamoja wamekuwa wakivusha kuwa ardhi ya Zanzibar imeuzwa Tanzania Bara, wanapaswa kuwapuuza kwa sababu katiba hii imetoa fursa kubwa kwa Wazanzibari kutumia ardhi iliopo Bara kwa matumizi yao mbalimbali bila ya bughudha ninaondoa kero zilizopo, kjiografia ukubwa wa ardhi iliopo katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo eneo la Bara lina ukubwa wa kilomita za mraba wastani zaidi laki tisa, wakati Ardhi iliopo Zanzibar ni kilomita za mraba 2,600 tu.
Kiuhalisia ardhi ya Zanzibar hata kwa matumizi ya Wazanzibari wenyewe ndiyo maana sehemu kubwa ya wananchi wa Zanzibar waliopo Tanzania Bara wanamiliki maeneo makubwa ya ardhi Tanzania bara bila matatizo wala ubaguzi wowote.
Wapinzani na UKAWA kwa makusudi wamekuwa wakifanya upotoshaji wa makusudi kinyume na misingi ya kiungwana baada ya kuona wanashindwa kujenga hoja za msingi za kuikosoa Katiba Inayopendekezwa wamebakia kutengeneza fitina za kuwachonganisha watu wa Bara na Zanzibar.
inashangaza kuona Cuf wanapinga Katiba Inayopendekezwa wakati ina mambo ambayo wao wenyewe waliyapendekeza wakati walipokuwa katika vikao vya Baraza la Wawakilishi, walipitisha azimio la kutaka masuala ya ardhi, mafuta na gesi kuondolewa katika orodha ya mambo ya Muungano, jambo ambalo limepitishwa na Katiba Inayopendekezwa lakini bila aibu wanaipinga Katiba hiyo.
Bunge la Katiba lilikubaliana na hoja hiyo na masuala ya gesi na mafuta yamepatiwa ufumbuzi na kuondolewa kwenye Muungano sasa wapinzania wanachopinga ni nini? Kitendo cha Ukawa kuisusia Katiba Inayopendekezwa na kuwashawishi wafuasi wao kutoipigia kura kinaonesha jinsi watu hao walivyokuwa hawana imani na uchungu wa wananchi wa Zanzibar ambao wanakabiliwa na matatizo mbalimbali ikiwemo suala la ajira kwa vijana.
Kwa sababu ikiwa Katiba Inayopendekezwa itapigiwa kura ya ndio kwa wingi itatoa fursa na nafasi kwa Zanzibar kuanza kuchimba mafuta na gesi kwa ajili ya kujenga mazingira mazuri ya kiuchumi na ustawi wa jamii kwa wananchi wake. Anafahamisha kuwa juhudi zimeanza kuchukuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibair ikiwemo kuwasomesha vijana mbali mbali katika fani ya mafuta na gesi.