Katiba ya Tanzania na Mipaka ya Uhuru wa Kujieleza

Katiba ya Tanzania na Mipaka ya Uhuru wa Kujieleza

Nanyaro Ephata

JF-Expert Member
Joined
Jan 22, 2011
Posts
1,234
Reaction score
1,815

Ni kiwango kipi cha Uhuru kinakubalika na watawala kisiwe Uchochezi?​


Kama Taifa tumetoa Uhuru (Demokrasia) pana sana kwenye sekta ya uchumi hasa Ubinafsishaji wa bei ya kutupwa ya mali na mashirika ya umma. Lakini tumebana sana na kwa kiwango cha kutisha Uhuru na Demokrasia ya mawazo kisiasa.

Uhuru wa kujieleza ni biashara ya mawazo/fikra yenye soko kamili kama ilivyo bidhaa nyingine yoyote sokoni. Kamwe si jukumu la serikali wala la yeyote yule kuamua ni wazo lipi au ni fikra ipi au ni habari ipi iwe halali, bali ni soko la mawazo ndio huamua. Soko la mawazo/fikra litaamua ni wazo au fikra au habari ipi ni sahihi hivyo habari ya uongo itashindwa bila amri au shuruti ya Serikali.

Udhibiti wa habari au mawazo/fikra huru ni kinyume cha Ibara ya 18 ya Katiba yetu ya mwaka 1977, na kwa kuzingatia Ibara hii ya Katiba kile ambacho watawala wanakiita Uchochezi ndio Uhuru wenyewe wa kujieleza ambao unalindwa na ibara hii.

Ni nani mwenye haki ya kuamua uhalali wa maoni na aina ya uhuru wa mawazo/fikra ya mtu katika kutekeleza haki hiyo ya kikatiba?

Ni kiwango gani cha Uhuru kinakubalika na watawala ili kisiwe uchochezi?

Uhuru/demokrasia lazima izingatie vigezo vya kimataifa

Nanyaro EJ
 
Habari wakuu,

Kumekuwa na wimbi la watu wachache wanaokuja na hoja dhaifu eti uhuru wa kujieleza umebanwa.

Kwanza naomba niweke wazi kuwa watanzania wanataka maendeleo hawataki uhuru wa kujieleza kwani ukiwa na njaa kujieleza hakusaidii kitu chochote.Hii ndo sababu ya Libya kumkumbuka Gaddafi.

Embu nijikite kwenye hoja ya msingi kuwa, je wanaotaka uhuru wa kujieleza wanaelewa maana yake?

Je wao wanakubali mawazo yasiyoridhisha matakwa yao?

Tumeshuhudia hata humu ndani wale magwiji wa kuzungumzia kuwa uhuru wa kujieleza umegandamizwa wakiwatukana na kuwakebehi na kuwapa majina mbali mbali kama wachumia tumbo, wataka vyeo, wanajipendekeza na matusi kadhaa wale wasioendana nao kimawazo instead ya kuheshimu mawazo yao kama ulivyo muhimili mkubwa unaounda uhuru wa kuongea.

Pia tumeshuhudia mitandaoni wale wanaohuburi uhuru wa kuongea ndio mabingwa wa kublock watu wanaopingana nao kimawazo.

Je uhuru wao wa kuongea ni kuongea yale yanaowafuraisha?

Nimekuwa muhanga mkubwa wa maneno ya kebehi na matusi kuwa natumika naomba niweke wazi kuwa mimi nashabikia kile nachokiona sahihi na sifanyi kwa ajili ya kupata kitu fulani na sijawahi kupata kitu chochote.
 
Masenu K Msuya
Pole sana kama unaunga mkono yanayo endelea ndani ya tanzania.
Kingine ulitakiwa uzaliwe zamani siyo dunia ya sasa.
 
Pole sana kama unaunga mkono yanayo endelea ndani ya tanzania.
Kingine ulitakiwa uzaliwe zamani siyo dunia ya sasa.
Mkuu kwenye katiba kuna uhuru wa uchaguzi na wenye akili wote wanaunga mkono juhudi kubwa za maendeleo angalia historia ya nchi zilizoendelea
 
Mkuu kwenye katiba kuna uhuru wa uchaguzi na wenye akili wote wanaunga mkono juhudi kubwa za maendeleo angalia historia ya nchi zilizoendelea
Wenye akili ni wapi mkuu na wasiyo na akili ni akina nani?
 
Mkuu kwenye katiba kuna uhuru wa uchaguzi na wenye akili wote wanaunga mkono juhudi kubwa za maendeleo angalia historia ya nchi zilizoendelea
Maendeleo na Uhuru wa kujieleza vinahusiana na kutofautiani vipi? Uli kingine kiwepo lazima kingine kisiwepo? Au kukiwa na uhuru wa kuongea kunashikilia pesa ya maendeleo?

Hii ni sawa na kutembea na kuongea hivi ili utembee inabidi usiongee?
 
Uluposema watanzania wanahitaji maendeleo sio uhuru wa kujieleza nikaacha kusoma...upeo wako na kuelewa maendeleo bado ni mdogo...hujui maana ya maendeleo.!
 
Ni sawa na kumruhusu aliyefiwa kulia. Ndio Uhuru Wa kujieleza, ila akisema ndio aliyeua ruksa kumkamata au next ni nani , kuongea kuropoka hakuzuii serikali kutimiza malengo yake.
 
Wenye akili ni wapi mkuu na wasiyo na akili ni akina nani?
Kwako ww ccm ndio wenye haki ya kufanya mikutano kila siku tunamuona polepole akifanya mikutano ya hadhara na ya ndani lkn vyama vingine vikifanya mikutana polisi wanaiingilia kwahiyo ww hapo huoni tatizo kila siku mkuu yupo kwenye shughuli za kiselikari anafanya siasa anapokea wanasiasa kwahiyo ccm ndio watanzania zaidi ya watu wavyama vingine jaribu kuushughulisha ubongo wako kidogo utaona kuna kadouble standard ambako nika baya kwa nchi yetu
 
Soma katiba na sheria ya vyama vya siasa mheshimiwa
 
Kwako ww ccm ndio wenye haki ya kufanya mikutano kila siku tunamuona polepole akifanya mikutano ya hadhara na ya ndani lkn vyama vingine vikifanya mikutana polisi wanaiingilia kwahiyo ww hapo huoni tatizo kila siku mkuu yupo kwenye shughuli za kiselikari anafanya siasa anapokea wanasiasa kwahiyo ccm ndio watanzania zaidi ya watu wavyama vingine jaribu kuushughulisha ubongo wako kidogo utaona kuna kadouble standard ambako nika baya kwa nchi yetu
Umekosea kuni replay au vipi?
 
Wewe una
Masenu K Msuya

Wewe una akili zaidi ya Maaskofu 32 wa RC na 27 wa KKKT.

Hongera sana.

Wao kwa upeo wao finyu, wameona hivyo lakini wewe unakataa. Bahati nzuri wewe ni Verified User. Usiwe na shaka, watakuona kweye uDC.
 
Mkuu kwenye katiba kuna uhuru wa uchaguzi na wenye akili wote wanaunga mkono juhudi kubwa za maendeleo angalia historia ya nchi zilizoendelea
Mkuu nikatubu kwa kosa gani je ni dhambi kutofautiana mawazo na wewe embu heshimu uhuru wangu wa kujieleza
Ooh kumbe sasa umejuwa maana ya uhuru wa kujieleza na kutofautiana kimawazo lkn kwa nchi yetu kwasasa ukitofautiana na serikali unapata vitisho mala unalewa tra,polisi na uhamiji nyumbani kwako mifano ni mingi askofu niwemugizi,
 
Ooh kumbe sasa umejuwa maana ya uhuru wa kujieleza na kutofautiana kimawazo lkn kwa nchi yetu kwasasa ukitofautiana na serikali unapata vitisho mala unalewa tra,polisi na uhamiji nyumbani kwako mifano ni mingi askofu niwemugizi,
Sasa unaogopa tra kama unalipa kodi au unaogopa uhamiaji kama wewe ni raia
 
Masenu K Msuya

Nnachokusifu ni kuwa unatamani kuwa katika kundi la emerging writers, sio mbaya. Tatizo scope ya source ya argument yako (including your own exposure) ni ndogo sana. Kwa mfano nani kakwambia waLibya wote wanaregret? Kwa taarifa wapo wanaoventilate sasa hivi kwa kupata uwezo wa kuchangia kwenye mustakabali wa nchi yao. Ni kweli the country is now unstable lakini ni transitional situation ambayo will ultimately be corrected. Lakini watakuwa wamepata uhuru walinyanganywa kwa kiini macho cha prosperity iliyokuwa under rulership ya mtu mmoja.
Hii hoja nyingine ya kuwa banned huko kwenye forum za watu inaonyesha wazi huna nidhamu ukiwa kwenye hizo fora wakati unazijua rule. Remedy ya hili kaanzishe forum yako na wewe uwaban.
Umekuja na mada yenye heading ya kufikirisha halafu ulichokiweka ni Libya na walivokuban halafu unataka kuwa emerging writer much less a great thinker kwa kukurupuka huku.
You got more surprises coming dude.
 
Wewe una

Wewe una akili zaidi ya Maaskofu 32 wa RC na 27 wa KKKT.

Hongera sana.

Wao kwa upeo wao finyu, wameona hivyo lakini wewe unakataa. Bahati nzuri wewe ni Verified User. Usiwe na shaka, watakuona kweye uDC.
Hupati Maaskofu kwa sababu Wana akili kuzidi kondoo zao. Hata wakifika 1000. Haimaanishi wanaakili kubwa. Chunguza kwa makini ....maaskofu wengi ni zero brain katika mambo mengi sana. Ndiyo maana wamewekewa wasaidizi na mashemasi. Matamko yao hujipinda Pinda daima. Kwa sababu hawajui ni kipi. Mfano Ngwajima aliapia Lowasa , leo hii ana kunywa chai kwa Magu. Kama siyo uongo na unafiki kwenye matamko yao , itakuwa nini? Hawako kufanya iliyo hakika na kweli.
 
Hupati Maaskofu kwa sababu Wana akili kuzidi kondoo zao. Hata wakifika 1000. Haimaanishi wanaakili kubwa. Chunguza kwa makini ....maaskofu wengi ni zero brain katika mambo mengi sana. Ndiyo maana wamewekewa wasaidizi na mashemasi. Matamko yao hujipinda Pinda daima. Kwa sababu hawajui ni kipi. Mfano Ngwajima aliapia Lowasa , leo hii ana kunywa chai kwa Magu. Kama siyo uongo na unafiki kwenye matamko yao , itakuwa nini? Hawako kufanya iliyo hakika na kweli.
Unalinganisha Bishops wa RC/KKKT na Bishops calibre ya Gwajima ?

You are not serious.

Gwajima au Lusekelo wanao angalau Maaskofu watano wa kukaa na kuandika waraka kama huo?
 
Dogo nshakwaambia haumo kwenye List ya Watakaoteuliwa kuwa DCs! Ni Bora ukaendelea ku develop Web zako uweze kwenda chooni! Hii thread inaonesha Ni namna gani hujui hata unachokieleza! Wewe mwenyewe usietaka Uhuru wa Kujieleza unajieleza, au huutaki kwa kundi Fulani la watu ila kundi jingine liwe na huo Uhuru?
 
Back
Top Bottom